Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

120
The University of Dodoma University of Dodoma Institutional Repository http://repository.udom.ac.tz Humanities Master Dissertations 2020 Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka vitendawili vya Kiswahili Ngatungwa, Felista J. The University of Dodoma Ngatungwa, F. J. (2020). Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka vitendawili vya Kiswahili (Tasnifu ya Umahiri). Chuo Kikuu cha Dodoma, Dodoma. http://hdl.handle.net/20.500.12661/2919 Downloaded from UDOM Institutional Repository at The University of Dodoma, an open access institutional repository.

Transcript of Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

Page 1: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

The University of Dodoma

University of Dodoma Institutional Repository http://repository.udom.ac.tz

Humanities Master Dissertations

2020

Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika

semi: mifano kutoka vitendawili vya Kiswahili

Ngatungwa, Felista J.

The University of Dodoma

Ngatungwa, F. J. (2020). Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka vitendawili

vya Kiswahili (Tasnifu ya Umahiri). Chuo Kikuu cha Dodoma, Dodoma.

http://hdl.handle.net/20.500.12661/2919

Downloaded from UDOM Institutional Repository at The University of Dodoma, an open access institutional repository.

Page 2: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

USAWIRI WA FALSAFA YA KIAFRIKA KATIKA SEMI:

MIFANO KUTOKA VITENDAWILI VYA KISWAHILI

FELISTA J. NGATUNGWA

SHAHADA YA UMAHIRI KATIKA FASIHI YA

KISWAHILI CHUO KIKUU CHA DODOMA

DISEMBA, 2020

Page 3: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

USAWIRI WA FALSAFA YA KIAFRIKA KATIKA SEMI:

MIFANO KUTOKA VITENDAWILI VYA KISWAHILI

NA

FELISTA J. NGATUNGWA

TASNIFU KWA AJILI YA KUKAMILISHA MAHITAJI YA

SHAHADA YA UMAHIRI KATIKA FASIHI YA KISWAHILI

CHUO KIKUU CHA DODOMA

DISEMBA, 2020

Page 4: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

i

IKIRARI NA HAKIMILIKI

Mimi, Felista Juma Ngatungwa, ninathibitisha kuwa tasnifu hii ni kazi yangu halisi

na haijawahi kuwasilishwa katika Chuo Kikuu kingine chochote ndani na nje ya nchi

kwa minajili ya kutunukiwa shahada inayofanana na hii au nyingine yoyote.

Saini

Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kupiga chapa au kusambaza

sehemu yoyote ya tasnifu hii bila idhini ya mwandishi au Chuo Kikuu cha Dodoma.

Page 5: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

ii

ITHIBATI YA MSIMAMIZI

Aliyetia saini hapa chini anathibitisha kwamba, ameisoma tasnifu hii iitwayo

“Usawiri wa Falsafa ya Kiafrika katika Semi: Mifano kutoka Vitendawili vya

Kiswahili” na anapendekeza kuwa inafaa kukubaliwa na Chuo Kikuu cha Dodoma

kwa ajili ya kutunukiwa Shahada ya Umahiri katika fasihi ya Kiswahili ya Chuo

Kikuu cha Dodoma.

Page 6: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

iii

TABARUKU

Naitabaruku kazi hii kwa wazazi wangu wapendwa, Bw. Juma Ngatungwa na Bi

Tulelia Madenge kwa malezi na jitihada zao katika kunisomesha na kuniombea siku

zote ili niweze kufanikiwa katika masomo yangu. Pia, naitabaruku kwa mume wangu

kipenzi, Bw Braison Paul Mkiwa na watoto wangu wapendwa, Ivan Braison na

Edrick Braison kwa uvumilivu wao katika kipindi chote nikiwa masomoni. Sina cha

kuwalipa zaidi ya upendo wangu wa dhati kwao. Nawaombea nyote Mwenyezi

Mungu awabariki na kuwajazia pale mlipopunguza kwa ajili yangu.

Page 7: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

iv

SHUKURANI

Kwanza, ninamshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kuniwezesha

kufanya kazi hii na kuikamilisha nikiwa mzima wa afya njema. Bila yeye

nisingeweza kufanya chochote.

Pili, ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa msimamizi wangu wa utafiti na

mwalimu wangu Dkt. Stella Faustine. Licha ya kuwa na majukumu mengi hakusita

kuwa bega kwa bega nami katika kunielekeza, kuniongoza na kunishauri kwa kila

hatua mpaka ninakamilisha utafiti huu. Mungu ambariki na kumlipa kila lenye kheri.

Tatu, ninapenda kuwashukuru wahadhiri wangu wa Chuo Kikuu cha Dodoma kwa

kunifundisha na kunipa miongozo mbalimbali iliyosaidia wakati wa masomo yangu.

Nao ni Dkt. Athuman Ponera, Dkt Stella Faustine, Dkt. Zuhura Badru, Dkt.

Abdumalik Feruzi na Dkt. Aginiwe Sanga. Mwingine kwa umuhimu ni Bw. Adrian

Fuluge kwa ushauri na mchango wake wa kimawazo ambao kimsingi umeijenga kazi

hii.

Mwisho, ninawashukuru wanafunzi wenzangu wa umahiri katika fasihi ya Kiswahili

mwaka 2018-2020 kwa ushirikiano wao tangu tulipoanza masomo mpaka

tulipomaliza. Mwenyezi Mungu awabariki.

Page 8: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

v

IKISIRI

Tasnifu hii inayoitwa “Usawiri wa Falsafa ya Kiafrika katika Semi: Mifano kutoka

Vitendawili vya Kiswahili” iliongozwa na malengo mahsusi matatu. Nayo ni, mosi,

kubainisha vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni. Pili,

kujadili falsafa ya Kiafrika kama inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili na

tatu, kutathmini athari ya falsafa ya Kiafrika kwa jamii kama inavyosawiriwa katika

vitendawili vya Kiswahili. Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Kisosholojia

kupitia misingi yake kama ilivyofafanuliwa katika utafiti huu. Nadharia hii ilitumika

katika michakato ya ukusanyaji wa data, uchambuzi na uwasilishaji wa matokeo ya

utafiti.

Utafiti huu ni wa kitaamuli, umetumia usanifu wa kifenomenolojia katika ukusanyaji

na uchanganuzi wa data. Utafiti huu ulifanywa uwandani na maktabani. Data

zilikusanywa kwa kutumia mbinu za mahojiano, mijadala ya vikundi lengwa na

udurusu wa nyaraka. Eneo la utafiti lilihusisha mikoa ya Kagera na Dodoma.

Sampuli ya utafiti iligawiwa katika makundi matatu. Nayo ni wanafunzi wa shule ya

msingi na sekondari, wanajamii wenye umri kuanzia miaka hamsini na tano na

kuendelea na maandiko kuhusu vitendawili vya Kiswahili na falsafa ya Kiafrika.

Sampuli ilipatikana kwa kutumia mbinu ya sampuli lengwa ya mpokezo na wa

kutegemea fursa.

Matokeo ya utafiti yameonesha kuwa falsafa ya Kiafrika hudhihirika kupitia mambo

mbalimbali yanayojitokeza katika maisha ya mwanadamu. Mambo hayo ni suala la

umoja na ushirikiano, ndoa na uzazi, “uchawi na ushirikina”, uhai na kifo, uduara,

maadili na suala la imani katika Mungu na mizimu. Aidha, kupitia mifano

mbalimbali ya vitendawili vya Kiswahili, utafiti umebaini kuwa, utanzu wa

vitendawili una hazina kubwa katika kuhifadhi na kutunza maarifa ya falsafa ya

Kiafrika na pia falsafa hiyo ina athari kubwa katika maisha ya jamii ya Kiafrika.

Utafiti umependekeza kuwa bado kuna haja ya tafiti nyingi zaidi kufanyika katika

uga wa fasihi simulizi, ili kubaini ni kwa namna gani tanzu za fasihi hiyo zinaweza

kutumika kama darasa la kufunza na kuhifadhi maarifa ya kifalsafa ya jamii za

Waafrika.

Page 9: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

vi

YALIYOMO

IKIRARI NA HAKIMILIKI......................................................................................... i

ITHIBATI YA MSIMAMIZI.......................................................................................ii

TABARUKU............................................................................................................... iii

SHUKURANI..............................................................................................................iv

IKISIRI......................................................................................................................... v

YALIYOMO............................................................................................................... vi

ORODHA YA VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA.......................................................x

SURA YA KWANZA................................................................................................. 1

UTANGULIZI.............................................................................................................1

1.1 Utangulizi kwa Jumla............................................................................................. 1

1.2 Ufafanuzi wa Istilahi Muhimu................................................................................1

1.2.1 Falsafa..................................................................................................................1

1.2.2 Falsafa ya Kiafrika...............................................................................................2

1.2.3 Utamaduni............................................................................................................2

1.2.4 Vitendawili.......................................................................................................... 2

1.3 Usuli wa Tatizo la Utafiti....................................................................................... 3

1.4 Tamko la Tatizo la Utafiti.......................................................................................5

1.5 Malengo ya Utafiti..................................................................................................5

1.5.1 Lengo Kuu........................................................................................................... 5

1.5.2 Malengo Mahsusi.................................................................................................5

1.6 Maswali ya Utafiti.................................................................................................. 6

1.7 Manufaa ya Utafiti..................................................................................................6

1.8 Mawanda ya Utafiti................................................................................................ 6

1.9 Muhtasari wa Sura ya Kwanza............................................................................... 7

SURA YA PILI........................................................................................................... 8

KIUNZI CHA NADHARIA NA MAPITIO YA MAANDIKO.............................. 8

2.1 Utangulizi............................................................................................................... 8

2.2 Kiunzi cha Nadharia............................................................................................... 8

2.3 Mapitio ya Maandiko..............................................................................................9

2.3.1 Mapitio Kuhusu Falsafa ya Kiafrika....................................................................9

Page 10: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

vii

2.3.2 Mapitio ya Maandiko Kuhusu Falsafa ya Kiafrika na Fasihi............................ 14

2.3.3 Mapitio ya Maandiko kuhusu Vitendawili vya Kiswahili.................................19

2.4 Mapengo Yanayojitokeza..................................................................................... 22

2.5 Muhtasari wa Sura ya Pili.....................................................................................23

SURA YA TATU.......................................................................................................24

METHODOLOJIA YA UTAFITI.......................................................................... 24

3.1 Utangulizi............................................................................................................. 24

3.2 Usanifu wa Utafiti.................................................................................................24

3.3 Mkabala wa Utafiti............................................................................................... 24

3.4 Eneo la Utafiti.......................................................................................................25

3.5 Walengwa wa Utafiti............................................................................................ 25

3.5.1 Jamii Tafitiwa.................................................................................................... 26

3.5.2 Sampuli na Usampulishaji Wake.......................................................................26

3.5.2.1 Sampuli ya Utafiti...........................................................................................27

3.6 Ukusanyaji wa Data..............................................................................................28

3.6.1 Njia na Zana za Ukusanyaji wa Data.................................................................28

3.6.1.1 Mahojiano....................................................................................................... 28

3.6.1.2 Mjadala wa Vikundi Lengwa..........................................................................29

3.6.1.3 Udurusu wa Nyaraka...................................................................................... 29

3.6.2 Mchakato wa Ukusanyaji Data na Udhibiti wake............................................. 29

3.7 Uchanganuzi wa Data........................................................................................... 30

3.8 Itikeli za Utafiti.....................................................................................................30

3.9 Uhalali na Uthabiti wa Matokeo ya Utafiti...........................................................31

3.10 Changamoto Zilizojitokeza Wakati wa Utafiti na Utatuzi wake........................ 31

3.11 Muhtasari wa Sura ya Tatu................................................................................. 32

SURA YA NNE......................................................................................................... 33

UWASILISHAJI NA MJADALAWAMATOKEO YA UTAFITI.................... 33

4.1 Utangulizi............................................................................................................. 33

4.2 Vijenzi vya Falsafa ya Kiafrika katika Muktadha wa Kitamaduni.......................33

4.2.1 Suala la Umoja na Ushirikiano.......................................................................... 33

4.2.2 Suala la Maadili katika Jamii.............................................................................35

Page 11: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

viii

4.2.3 Suala la Uhai na Kifo.........................................................................................37

4.2.4 Dhana ya Uduara............................................................................................... 38

4.2.5 Suala la Imani katika Mungu na Mizimu.......................................................... 41

4.2.6 Suala la Uchawi na Ushirikina.......................................................................... 43

4.2.7 Dhana ya Ndoa na Uzazi................................................................................... 45

4.3 Falsafa ya Kiafrika katika Vitendawili vya Kiswahili..........................................47

4.3.1 Falsafa ya Umoja na Ushirikiano...................................................................... 48

4.3.2 Falsafa ya Umuhimu wa Maadili Katika Jamii................................................. 52

4.3.3 Falsafa ya Uhai na Kifo..................................................................................... 55

4.3.4 Falsafa ya Uduara.............................................................................................. 58

4.3.5 Falsafa ya Imani katika Mungu na Mizimu.......................................................62

4.3.6 Falsafa ya Uchawi na Ushirikina.......................................................................65

4.3.7 Falsafa ya Uzazi na Malezi................................................................................68

4.4 Athari za Falsafa ya Kiafrika kwa Jamii Kama Inavyosawiriwa katika

vitendawili vya Kiswahili....................................................................................71

4.4.1 Athari Chanya za Falsafa ya Kiafrika kwa Jamii.............................................. 72

4.4.1.1 Inasaidia Kudumisha Umoja na Mshikamano................................................72

4.4.1.2 Inasaidia Kulinda Maadili ya Jamii................................................................ 74

4.4.1.3 Inasaidia Kutambulisha Jamii ya Waafrika Ndani na Nje ya Afrika..............76

4.4.1.4 Inasaidia Kuhifadhi na Kurithisha Amali za Kitamaduni za jamii.................77

4.4.1.5 Inasaidia wanajamii kushika imani ya dini.....................................................78

4.4.2 Athari Hasi za Falsafa ya Kiafrika kwa Jamii................................................... 78

4.4.2.1 Kuchochea Vitendo vya Uvunjifu wa Amani katika Jamii............................ 79

4.4.2.2 Kukwamisha Maendeleo ya Jamii.................................................................. 80

4.4.2.3 Inasababisha Hofu na Mashaka kwa Wanajamii............................................ 80

4.5 Muhtasari wa Sura ya Nne....................................................................................81

SURA YA TANO...................................................................................................... 83

MUHTASARI, HITIMISHO NAMAPENDEKEZO........................................... 83

5.1 Utangulizi............................................................................................................. 83

5.2 Muhtasari wa Tasinifu.......................................................................................... 83

5.3 Hitimisho.............................................................................................................. 85

5.3.1 Mchango Mpya wa Utafiti.................................................................................85

Page 12: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

ix

5.3.2 Utoshelevu wa Nadharia....................................................................................86

5.4 Maoni na Mapendekezo kwa Tafiti Zijazo...........................................................86

5.5 Muhtasari wa Sura ya Tano.................................................................................. 87

MAREJELEO........................................................................................................... 88

VIAMBATANISHO................................................................................................. 94

Page 13: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

x

ORODHA YA VIFUPISHO VILIVYOTUMIKA

BAKITA Baraza la Kiswahili Tanzania

Bi. Bibi

Bw. Bwana

Dkt. Daktari

Hm Hakuna mwaka

K.h.j Keshatajwa hapo juu

Ltd Limited

Prof. Profesa

TUKI Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili

Uk. Ukurasa

Wah. Wahariri

WWW World Wide Web

Page 14: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

1

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI

1.1 Utangulizi kwa Jumla

Sura hii inabeba utangulizi wa tasnifu yetu. Katika sura hii, istilahi muhimu

zilizotumika katika tasnifu hii zimefafanuliwa. Mambo mengine yaliyojitokeza ni

pamoja na; usuli wa tatizo la utafiti, tamko la tatizo la utafiti, malengo ya utafiti,

maswali ya utafiti, manufaa ya utafiti na mawanda ya utafiti.

1.2 Ufafanuzi wa Istilahi Muhimu

Istilahi muhimu zinazohusiana na utafiti huu ni falsafa, falsafa ya Kiafrika,

utamaduni na vitendawili. Katika kufafanua istilahi hizi, mtafiti amefafanua kwa

mujibu wa wataalamu mbalimbali na kisha kutoa maana ya jumla kama ilivyotumika

katika utafiti huu.

1.2.1 Falsafa

Kwa mujibu wa Wizara ya Elimu na Utamaduni (1992) falsafa ni taaluma

inayojishughulisha na kutafuta ukweli wa jambo kwa njia ya kutafakari. Maelezo

haya yanathibitisha kuwa, falsafa ni mtazamo alio nao mwanadamu katika kufikiria

mambo yanayotokea. Mawanda ya fasili hii yanabainisha kuwa, falsafa ni taaluma

inayoweza kusomwa au kufundishwa kama taaluma nyingine. Fasili inayofanana na

hiyo imetolewa na Chuachua (2010). Yeye anafafanua kuwa, falsafa ni taaluma ya

kutafuta ukweli kwa njia ya kutafakari kwa kina. Kwa hiyo, kutafakari kwa kina

kuhusu ukweli wa jambo fulani kunasaidia kubaini maarifa ya jamii kupitia mambo

mbalimbali yanayojenga maarifa hayo. Aidha, Wamitila (2010) anakwenda mbali

zaidi ya hapo kwa kufafanua kuwa, falsafa ni istilahi inayotumiwa kuelezea wazo au

mawazo anayoyaamini mtu, mwandishi au mtunzi kuwa yale anayoyaandika yana

ukweli unaotawala misingi ya maisha. Kwa mtazamo wa mtaalamu huyu, falsafa ni

jumla ya imani na mawazo aliyo nayo mtu juu ya jambo fulani kuwa ni kweli

kulingana na maisha halisi ya jamii. Hivyo basi, falsafa inaweza kufafanuliwa kuwa

ni taaluma au elimu ya kutafuta uhakika wa mambo fulani katika maisha kwa njia ya

kuutafakari ulimwengu. Falsafa hujishughulisha na kudadisi hali halisi ya maisha ya

binadamu katika jamii yake kwa kuzingatia imani, mila, desturi pamoja na mienendo

aliyo nayo binadamu.

Page 15: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

2

1.2.2 Falsafa ya Kiafrika

Simchimba (2012) anafafanua kuwa, falsafa ya Kiafrika ni jumla ya mitazamo,

mielekeo na misimamo waliyo nayo Waafrika juu ya mambo yanayowazunguka na

yanayowatofautisha kati yao na jamii nyingine. Maana inayokaribiana na ya

Simchimba inatolewa na Faustine (2017) ambaye amefafanua zaidi kuwa falsafa ya

Waafrika ni fikra au mitazamo mbalimbali inayoeleza masuala mahususi ya kimaisha

yanayohusiana na jamii ya Waafrika (Wabantu). Fikra au mitazamo hiyo ndiyo

inayowawezesha kuutafakari ulimwengu wao kwa kuuhusisha na vitu vilivyomo na

hatimaye, kuutilia maana. Kwa jumla, falsafa ya Kiafrika inaweza kuelezwa kuwa ni

jumla ya fikra, mienendo, ukweli na matendo yanayohusu Waafrika (Wabantu)

ambayo wanayaamini na kuyazingatia katika nyanja mbalimbali za maisha yao.

1.2.3 Utamaduni

Stanley (2008) anafafanua kuwa, utamaduni ni jinsi binadamu wanavyoyakabili

maisha katika mazingira yao ikijumuisha ujuzi, imani, sanaa, maadili, sheria na

desturi. Hujumuisha namna wanavyovaa, mila zao za ndoa, lugha, maisha ya

kifamilia na sherehe zao za dini. Utamaduni wa Waswahili hautofautiani sana kati ya

jamii moja na nyingine zinazopatikana katika nchi ya Tanzania. Ufafanuzi huo

unaonesha kuwa utamaduni hujumuisha kanuni zote za maadili na hudhihirika katika

shughuli za kijamii, lugha na katika mlolongo mzima wa maisha. Aidha, fasili ya

mtaalamu huyu inakaribiana na ile iliyotolewa na Hoppenau na wenzake (2009).

Hawa wanafafanua kuwa, utamaduni ni mfumo wa pamoja wa kiimani, maadili,

desturi, tabia na kazi za sanaa ambao hutumiwa na wanajamii katika kukabiliana na

dunia. Mfumo huo hurithishwa kutoka kizazi hadi kizazi kwa njia ya kujifunza.

Fasili hii inafafanua kwamba, utamaduni humwezesha mwanadamu kuifahamu,

kutafsiri na kuielewa dunia inayomzunguka kwa namna mbalimbali. Hivyo, kwa

jumla tunaweza kusema kuwa utamaduni ni jumla ya mambo yote yanayofanywa

katika jamii kwa kuzingatia mila na desturi za jamii hiyo na huweza kurithishwa

kutoka kizazi kimoja kwenda kingine kwa njia ya mapokeo.

1.2.4 Vitendawili

Wamitila (2003) anafafanua kuwa, kitendawili ni aina ya semi ambayo huwa

imefumbwa na hutolewa kwa mwanahadhira ili aifumbue. Swali la fumbo hilo na

jawabu lake hufahamika katika jamii fulani inayohusika. Upekee wa fasili hii upo

Page 16: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

3

katika matumizi ya sitiari katika utegaji wa vitendawili ambayo ndiyo sifa kuu ya

vitendawili. Maana inayofanana na hii inaelezwa na Mulokozi (2017) ambaye

anafafanua kuwa, kitendawili ni usemi wenye fumbo; ni swali ambalo huulizwa kwa

hadhira ili ilipatie ufumbuzi. Maelezo ya wataalamu hawa yanathibitisha kuwa,

vitendawili ni fumbo ambalo hutolewa kwa hadhira kama swali ili iweze kulifumbua.

Kwa jumla, vitendawili vinaelezwa kuwa ni semi zenye mafumbo ambazo hutolewa

kwa hadhira kwa kutumia sitiari ili kuifanya hadhira yake kufikiria kwa kina katika

kutoa majibu. Hata hivyo, vitendawili vinaweza kutofautiana kati ya jamii moja na

nyingine kutokana na tofauti za kimazingira na mabadiliko yanayotokea katika jamii

hizo kufuatia maendeleo ya sayansi na teknolojia.

1.3 Usuli wa Tatizo la Utafiti

Katika ulimwengu tunaoishi, kila jamii ina namna yake ya kuuelewa, kuuthamini na

kuutathmini utamaduni wake. Matendo na kila akifanyacho mwanadamu akiamini

kuwa ni kweli kulingana na matakwa ya jamii yake ndiyo falsafa ya jamii hiyo.

Aidha, kila jamii huishi kulingana na taratibu au miongozo inayokitwa ndani ya

falsafa yake ambayo huifanya jamii moja kutofautiana na jamii nyingine.

Mshiu na Wenzake (2007) kama wanavyonukuliwa na Makame (2016) wanaeleza

kuwa neno falsafa linatokana na maneno mawili yenye asili ya Ki- Giriki; “philos”

na “sophia” yakiwa na maana ya “love” au “kutafuta” busara na hekima. Maelezo

hayo yanabainisha kuwa, falsafa hujihusisha na kuchunguza na kutafakari kwa kina

juu ya asili ya vitu, sababu na maana ya vitu na kuyapatia ufumbuzi kwa kutumia

busara na hekima. Kwa hiyo, maelezo hayo yanafafanua kuwa, mwanafalsafa

afikiriapo kufanya jambo, fikra hizo lazima zitawaliwe na busara na hekima pamoja

na kuupata ufumbuzi wa jambo fulani lililojichomoza ndani ya jamii.

Historia inaeleza kuwa, uchunguzi kuhusu kuwepo kwa falsafa ulibaini kwamba,

falsafa ilianza mnamo karne ya kumi na sita katika maeneo mbalimbali. Hii

inathibitishwa na Mshiu na wenzake (2007), kama wanavyonukuliwa na Makame

(2016). Wanasema kuwa;

Page 17: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

4

By its origin philosophy started in the sixteenth 16th century in Asiaand Europe. This can be proved by many documents present inEurope and Asia and other parts of the world such as Africa (uk.14).

Kwa asili yake falsafa ilianza katika karne ya 16 katika Afrika naUlaya. Hii inathibitishwa kwa maandiko mengi yapatikanayo Ulayana Asia na katika sehemu nyingine duniani kama vile Afrika (tafsiriya mtafiti).

Maneno haya yanabainisha kuwepo kwa falsafa katika jamii mbalimbali

ulimwenguni. Hii ni kwa sababu, hakuna jamii inayoishi kiholela pasipo kuwa na

misingi au miongozo fulani inayojikita katika utamaduni wao. Kwa hiyo, falsafa ya

Kiafrika inajumuisha mambo yote ambayo Waafrika wanayaamini kuwa ni ya kweli

na wanayatenda katika nyanja zote za maisha yao.

Kwa vile falsafa ya jamii fulani hujifungamanisha na maisha ya jamii hiyo, fasihi

nayo kama sehemu ya jamii, hujinasibisha kwa namna ya moja kwa moja na falsafa

ya jamii hiyo. Hii inatokana na sababu kuwa, fasihi ni zao la jamii na hutumika kama

jukwaa la kuelezea uzoefu, kaida, mila na desturi za jamii husika. Pia, fasihi kama

tawi mojawapo la sanaa, hutumika kudhihirisha falsafa ya jamii husika. Kwa maana

hiyo, hatuwezi kuitenganisha au kuondoa fasihi ya jamii husika katika kuchunguza

falsafa ya jamii hiyo kwa sababu falsafa hubebwa na misingi ya vipera vya fasihi

inayotawala na kutumika katika jamii hiyo. Kwa kutambua hilo, tumeona ni vema

kuchunguza usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili.

Baadhi ya watafiti na wataalamu wa fasihi wamefanya uchunguzi kuhusiana na

falsafa ya Kiafrika. Watafiti kama vile Simchimba (2012), Duwe (2016), Faustine

(2017) na Mlelwa (2017) wamefanya tafiti zao kuhusu Falsafa ya Kiafrika

inavyosawiriwa katika kazi za fasihi andishi na fasihi Simulizi (methali, sanaa za

maonyesho na hadithi). Hata hivyo, uchunguzi wa falsafa ya Kiafrika katika

vitendawili haujafanyika kwa kina. Baadhi ya wataalamu waliotafiti kuhusu

vitendawili kama vile Khumalo (1974), Stefanova (2003), Gwaravanda na Masaka

(2008), Badru (2012; 2015) hawakuhusisha uchunguzi wa vitendawili na falsafa ya

Kiafrika. Jambo hili linasababisha jamii kutokuwa na uelewa mkubwa kuhusu

vitendawili kama amali muhimu katika kuhifadhi na kufunza maarifa ya jamii.

Utafiti huu ulikusudiwa kuziba pengo hilo kwa kuangalia namna vitendawili vya

Page 18: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

5

Kiafrika vinavyoweza kusawiri falsafa ya Kiafrika pamoja na athari za falsafa ya

Kiafrika kwa jamii.

1.4 Tamko la Tatizo la Utafiti

Wataalamu kadhaa wamefanya tafiti zao kuonesha namna falsafa ya Kiafrika

inavyosawiriwa katika tanzu mbalimbali za fasihi. Miongoni mwao ni Mbiti (1969),

Balisidya (1973), Hussein (1976), Mulokozi (1983), Senkoro (1996), Simchimba

(2012), Duwe (2016), Faustine (2017) na Mlelwa (2017). Hata hivyo, wengi wa

wataalamu hawa tafiti zao zimekitwa katika fasihi andishi. Kwa wale

walioshughulikia fasihi simulizi mahususi katika kipera cha vitendawili kama vile

Amana (2013), Badru (2015) na Mshana (2015) kwa kuwataja baadhi, hawajahusisha

tafiti zao na jinsi vitendawili vinavyoweza kubeba falsafa ya Kiafrika. Hali hii

inasababisha vitendawili kama kipera cha fasihi kutoeleweka na kupewa hadhi sawa

kama ilivyo kwa vipera vingine vya fasihi katika ufunzaji na utunzaji wa maarifa ya

falsafa ya Kiafrika. Utafiti huu umekusudia kuziba pengo hilo kwa kuchunguza

usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili na kubainisha athari

zake kwa jamii.

1.5 Malengo ya Utafiti

Utafiti huu uliongozwa na malengo ya aina mbili, ambayo ni lengo kuu na malengo

mahsusi.

1.5.1 Lengo Kuu

Lengo kuu la utafiti huu ni kuchunguza usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika

vitendawili vya Kiswahili.

1.5.2 Malengo Mahsusi

Utafiti huu uliongozwa na malengo mahsusi matatu ambayo ni;

a) Kubainisha vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni,

b) Kujadili namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika vitendawili vya

Kiswahili,

c) Kutathmini athari ya falsafa ya Kiafrika kwa jamii kama inavyosawiriwa

katika vitendawili vya Kiswahili.

Page 19: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

6

1.6 Maswali ya Utafiti

a) Je, ni vijenzi vipi vinavyobainisha falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa

kitamaduni kwa jamii ya Waafrika?

b) Ni kwa namna gani falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika vitendawili vya

Kiswahili?

c) Je, falsafa ya Waafrika kama inavyosawiriwa katika vitendawili vya

Kiswahili ina athari gani kwa jamii ya Waafrika?

1.7 Manufaa ya Utafiti

Matokeo ya utafiti huu yana manufaa yafuatayo; Mosi, kusaidia katika kupanua wigo

wa ufahamu juu ya uhusiano wa fasihi na falsafa ya jamii husika. Pili, kutoa

mwongozo kwa wasomi na watafiti wa baadae ambao watahitaji kufanya utafiti

katika uga wa falsafa ya Kiafrika. Tatu, kutoa nafasi kwa watafiti wengine kutumia

taaluma hii ya falsafa katika kuzichambua kazi nyingine za fasihi simulizi kama

hadithi, nyimbo na ngoma na kazi za fasihi andishi. Nne, utafiti huu utaiendeleza na

kuisheheneza fasihi simulizi ya Kiswahili kwa kuonesha umuhimu wake katika

kuhifadhi na kufunza maarifa ya kifalsafa ya jamii ya Waafrika.

1.8 Mawanda ya Utafiti

Utafiti huu umechunguza usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka

vitendawili vya Kiswahili. Malengo mahsusi ya utafiti huu yalikuwa ni matatu. Nayo

ni mosi, kubainisha vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni.

Pili, kujadili namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika vitendawili vya

Kiswahili. Tatu, kutathmini athari ya falsafa ya Kiafrika kwa jamii kama

inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili. Kwa jumla, utafiti huu umeitazama

falsafa ya Waafrika katika muktadha wa utamaduni tu na sio katika nyanja

nyinginezo. Aidha, utafiti huu unawaangalia Waafrika kwa kujiegemeza katika jamii

ya Wabantu. Hii inatokana na utambuzi kuwa, Waafrika wamegawanyika katika

makundi makubwa matatu, yaani Wabantu, Wakushi na Wanilo. Tumechagua

Wabantu kwa sababu, kwa mujibu wa Chuachua (2016:2) na Faustine (2017),

Wabantu ndiyo jamii kubwa zaidi Afrika yenye mfumo wa lugha unaofanana. Hivyo,

ni rahisi kuelewa mawazo na mitazamo ya kifalsafa ya Waafrika kupitia lugha zao

zaidi ya makundi mengine. Zaidi ya kuwa na kiungo cha lugha wanaunganishwa na

mila, desturi na falsafa ambazo zinashabihiana sana.

Page 20: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

7

Aidha, vitendawili vilivyotumika vilikusanywa kutoka kwa wanafunzi wa shule za

msingi na sekondari wa wilaya ya Bukoba na vile vilivyopatikana katika matini

mbalimbali za kifasihi zinazohusu vitendawili vya Kiswahili. Data zilizokusanywa

na mtafiti zilichambuliwa na kuwasilishwa kwa kuzingatia malengo ya utafiti huu tu

na si vinginevyo.

1.9 Muhtasari wa Sura ya Kwanza

Sura hii imefafanua vipengele mbalimbali ikiwemo utangulizi, usuli wa tatizo la

utafiti, tamko la tatizo la utafiti, malengo ya utafiti, maswali ya utafiti, manufaa ya

utafiti pamoja na mawanda ya utafiti. Vipengele hivyo vimefafanuliwa kwa

kuzingatia mada ya utafiti huu. Sura inayofuata imefafanua kuhusu nadharia

iliyotuongoza katika utafiti huu pamoja na mapitio ya maandiko mbalimbali kuhusu

falsafa ya Kiafrika kwa jumla, falsafa ya Kiafrika katika fasihi na maandiko kuhusu

vitendawili vya Kiswahili.

Page 21: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

8

SURA YA PILI

KIUNZI CHA NADHARIA NA MAPITIO YA MAANDIKO

2.1 Utangulizi

Sura hii imefafanua kuhusu mambo makuu mawili. Mosi, kiunzi cha nadharia

iliyotumika katika utafiti huu. Pili, maandiko mbalimbali yaliyopitiwa

yanayohusiana na mada ya utafiti. Katika mapitio yanayohusiana na mada hii tuna

vipengele vitatu ambavyo ni; mapitio kuhusiana na falsafa ya Kiafrika kwa jumla,

mapitio kuhusu falsafa ya Kiafrika katika fasihi na mapitio kuhusu vitendawili vya

Kiswahili. Aidha, kutokana na mapitio hayo, mapengo ya utafiti yamebainishwa.

2.2 Kiunzi cha Nadharia

Utafiti huu uliongozwa na nadharia ya Kisosholojia. Nadharia hii iliasisiwa na

mtaalamu wa Kifaransa Hippolyte Taine (1828-1893). Taine aliangalia kazi ya fasihi

kama taswira ya kijiografia, kitamaduni na kimazingira iliyochimbuka kutoka katika

jamii husika. Akifafanua kuhusu nadharia hii anasema kuwa kazi ya kifasihi

inatakiwa kuchukuliwa kama taarifa ya kweli inayohusu maisha halisi ya watu. Kwa

hiyo, nadharia hii inajishughulisha na kazi yeyote ya sanaa kulingana na hali ya jamii

ambayo sanaa hiyo imechipuka na kukuzwa. Pia, hutumika katika kuchunguza

uhusiano uliopo baina ya kazi ya sanaa, jamii na namna jamii hiyo ilivyoundwa.

Wananadharia wa Kisosholojia wanazingatia mambo makuu mawili ambayo ni,

namna gani jamii inahusiana na fasihi na namna ambavyo fasihi inafanya kazi katika

jamii.

Burke (1941) anaona kuwa kazi ya sanaa ikiwa ni pamoja na fasihi inatumia mbinu

mbalimbali ambazo zinamsaidia mwanajamii kuelewa vizuri na kuongeza uwezo wa

kujiongoza juu ya jamii yake. Wahakiki wa Kisosholojia wanaweka mkazo zaidi

katika utendaji na msisitizo juu ya dhima ya fasihi katika jamii. Wanaona kuwa

fasihi ina dhima kubwa ambazo ni kuelimisha, kuburudisha na kuonya jamii.

Utafiti huu umetumia mihimili miwili ya nadharia hii kama ifuatavyo;

a) Fasihi haiwezi kujitenga na jamii ambayo fasihi hiyo imetengenezwa

kutoka kwenye jamii hiyo (Taine, 1873 na Narizvi, 1982). Mhimili huu

umetusaidia kujadili namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika

vitendawili vya Kiswahili. Hii ni kwa sababu fasihi ya jamii fulani ina

Page 22: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

9

mfungamano na maisha ya jamii husika. Kwa hiyo, vitendawili vya

Kiswahili vilivyotumika katika utafiti huu ambavyo vimesawiri falsafa ya

Kiafrika vimetokana na jamii na vinahusu maisha halisi ya jamii ya

Waafrika.

b) Kazi ya kifasihi ni taswira ya kijiografia, kimazingira na kiutamaduni

ambamo kazi hiyo imechimbuka kutoka katika jamii husika (Mungah,

1999). Mhimili huu umesaidia katika uchambuzi wa data ili kukamilisha

lengo la kwanza, la pili na la tatu. Malengo hayo yanahusu kubainisha

vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni, namna

falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili na

athari zake kwa jamii ya Waafrika. Hii ni kwa sababu, vitendawili hivyo

vinaakisi maisha halisi ya jamii ya Waafrika na hivyo, vimemwezesha

mtafiti kupata picha halisi ya maisha ya Waafrika wanavyoishi katika

mazingira yao. Kwa hiyo, kupitia hayo, athari za imani na mitazamo yao

imeweza kubainika.

Hivyo, nadharia hii inahusiana na utafiti huu ambao unachunguza usawiri wa falsafa

ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili. Hii ni kwa sababu nadharia

inachunguza jamii mahsusi na mihimili yake inaweka mkazo fasihi kuendana na

miktadha ya maisha ya jamii husika. Kwa hiyo, nadharia hii imesaidia kukamilisha

malengo ya utafiti huu ambayo yamejikita katika kuchunguza jamii mahsusi ya

Waafrika (Wabantu) katika vitendawili vya Kiswahili kama yalivyobainishwa katika

mihimili hapo juu.

2.3 Mapitio ya Maandiko

Sehemu hii inahusu mapitio mbalimbali yaliyotumika katika utafiti huu. Mapitio

hayo yamegawanyika katika vipengele vitatu. Navyo ni, mapitio kuhusu falsafa ya

Kiafrika, mapitio kuhusu falsafa ya Kiafrika na fasihi na mapitio kuhusu vitendawili

vya Kiswahili.

2.3.1 Mapitio Kuhusu Falsafa ya Kiafrika

Katika kuifafanua falsafa ya Kiafrika, kumekuwa na mzozo miongoni mwa

wataalamu juu ya kuwapo ama kutokuwapo kwa falsafa ya Kiafrika. Kutokana na

mzozo huo zimeibuliwa hoja mbili kinzani. Wapo wataalamu wanaosema kuwa

Page 23: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

10

falsafa sharti iwe katika maandishi; na kwa kuwa falsafa ya Kiafrika haikuandikwa

basi hakuna falsafa hiyo (Kaponda, 2018). Naye Chuachua (2016) anamtaja

Bodunlin (1981) anayekubaliana na mtazamo huu kuwa, falsafa ya Kiafrika imekuwa

ikitawaliwa na mgogoro wa fikra kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwa falsafa ya

Kiafrika. Anaeleza kuwa mgongano huo wa hoja unakwenda mbali zaidi na kutaka

kujua kama falsafa ya Kiafrika ipo, ni ipi hiyo? Kwa mtazamo huu, Waafrika kama

watu ambao hapo awali falsafa yao haikuwekwa katika maandishi, walitazamwa

kama watu wasio na falsafa yao. Hivyo, tunakubaliana na Duwe (2016) anayeona

kuwa, mtazamo huu umejikita katika fikra za wataalamu wa Kimagharibi wenye

lengo la kuwadhihaki na kuwadhalilisha Waafrika.

Duwe (2016) anataja baadhi ya wataalamu wanaodai kuwa Waafrika hawana falsafa

kuwa ni: Muller, 1873; Spencer, 1851 na Bruhi, 1978. Sababu ya madai yao ni

kwamba, hakuna maandishi au vielelezo vyovyote vinavyofafanua suala la kuwapo

kwa falsafa ya Kiafrika. Wataalamu wengine wanakwenda mbali zaidi na kusema

kuwa, falsafa ya Waafrika haijitoshelezi kwani wanafalsafa wa Kiafrika wamechota

mbinu za wanafalsafa wa Kimagharibi katika kufafanua na kuelezea falsafa yao. Pia,

uchunguzi uliofanywa na waandishi wa Kiafrika unachukuliwa kuwa chanzo chake

ni katika nchi za Magharibi, (Hontondji 2004). Andiko la mtaalamu huyu

limemsaidia mtafiti kupata mawazo ya jumla kuhusu mtazamo wa wataalamu wa

Kimagharibi wenye lengo la kuwadhalilisha Waafrika kuwa hawana falsafa. Utafiti

huu unapingana na mawazo ya wataalamu hao kwa kuthibitisha kuwa Waafrika wana

falsafa yao inayodhihirika katika vitendawili vya Kiswahili.

Kwa upande mwingine, wapo wataalamu ambao wametafiti juu ya falsafa ya

Kiafrika na kugundua kuwa Waafrika wana falsafa yao inayojidhihirisha kutokana na

namna wanavyoishi, uzoefu, mila na desturi zao. Baadhi ya wataalamu hao ni kama

Temples, 1959; na Mbiti, 1969. Kwa mujibu wa wataalamu hawa falsafa sio lazima

iandikwe na kila jamii ina miongozo yake inayoaminika na kufuatwa kwa lengo la

kuendesha maisha ya jamii. Wataalamu hawa wanakubaliana kuwa Waafrika wana

falsafa yao ila kuja kwa wageni kumeiathiri falsafa ya Kiafrika. Mawazo ya

wataalamu hawa kuhusu falsafa ya Kiafrika ni kama ifuatavyo:

Page 24: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

11

Temples (1959) anaeleza kuwa mtu yeyote anayedai kuwa Waafrika hawana falsafa

anawaondoa katika kundi la wanadamu. Waafrika wana uwezo wa kufikiri na

kutenda kutokana na misingi ya jamii zao. Fikra za Waafrika zimetawaliwa na vitu

viwili ambavyo ni uhai na kifo. Waafrika wanaamini kuwa mtu akiumwa nguvu za

uhai zinapungua hivyo anaamini atakufa. Anataja vipengele mbalimbali

vinavyodhihirisha falsafa ya Waafrika kama dini, “uchawi na ushirikina”, uganga,

uduara, matambiko. Kuhusu uduara, anasema kuwa maisha ya Waafrika

yametawaliwa na wazo la duara, yaani maisha yana sifa ya uzuri. Mambo hayo

huonekana katika vitu kama vile viti (vigoda), vyungu, vinu, nyungo na hata baadhi

ya nyumba huonekana katika umbo la duara. Andiko hilo lina mchango katika utafiti

huu kwani limesaidia kubainisha vipengele mbalimbali ambavyo kwavyo, maarifa ya

kifalsafa huibuka ndani yake. Hata hivyo, andiko hilo halijajikita katika utanzu

wowote mahsusi ma kuonesha ni kwa namna gani falsafa ya Kiafrika inavyoweza

kusawiriwa katika fasihi simulizi. Ili kuziba pengo hilo, utafiti huu umechunguza

usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili.

Mbiti (1969) amefanya kazi nyingi zinazohusiana na falsafa ya Kiafrika. Katika kazi

hizo amebainisha mambo yanayofanywa na Waafrika ambayo yanaipambanua

falsafa ya Waafrika. Baadhi ya mambo hayo ni kama suala la umoja na ushirikiano.

Anasema kuwa Waafrika wanaishi kwa kushirikiana katika mambo mbalimbali. Hii

inathibitika pale anaposema:

Whatever happens to the individual happens to the whole group,and whatever happens to the whole group happens to the individual.The individual can only say, “I am because we are: and since weare therefore, I am” (uk. 106)

Kila kinachomtokea mtu binafsi kinakuwa kimetokea kwa kundizima, na kila kinachotokea katika kundi zima kinakuwakimemtokea mtu binafsi. Mtu anaweza kusema” nipo kwa sababutupo na kwa kuwa tupo basi nipo” (Tafsiri ya mtafiti)

Maelezo hayo yanathibitisha wazi kuwa, Waafrika wanaishi kwa kutegemeana. Mtu

akipata tatizo jamii nzima huchukulia tatizo hilo kama ni lao wote. Jambo hili

linawafanya kuishi kwa ushirikiano mkubwa miongoni mwao. Masuala mengine

yanayojitokeza katika falsafa ya Kiafrika kama inavyofafanuliwa na Mbiti (1969) ni

suala la imani katika dini za asili, matambiko na suala la wakati. Kuhusu suala la

Page 25: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

12

wakati anasema kuwa, Waafrika wanaishi katika sasa na hawana kesho. Andiko hilo

ni la msingi katika utafiti wetu kwani limedokeza kuwa, Waafrika walikuwa na dini

zao na utamaduni wao ambao ndio hubainisha falsafa yao na hivyo kutoa msukumo

kwa mtafiti kuchunguza namna falsafa hiyo inavyoweza kusawiriwa katika

vitendawili vya Kiswahili. Hata hivyo, pamoja na umuhimu huo, andiko hilo

limeacha mwanya wa kutafiti kwa kuwa halijabainisha vijenzi vya falsafa ya

Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni. Utafiti huu umeziba pengo hilo kwa

kubainisha vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni.

Aidha, Mbiti (1975) anaeleza kuhusu dhana ya roho kama kipengele cha falsafa ya

Kiafrika. Mtaalamu huyu anaona kwamba, kuna aina mbili za roho ambazo ni roho

asilia na roho ya binadamu. Katika maeneo hayo inaaminiwa kuwa, kuna kani uhai

inayoongoza kuwepo kwa roho asilia ambayo huhusisha vitu kama anga, nyota na

maumbile ya asili kama maji na milima. Vile vile, kwa upande wa roho za binadamu,

huhusisha zile za watu waliokufa kipindi cha vizazi vinne au vitano vilivyopita. Hii

inathibitishwa pale anaposema:

They are considered to be part of their families. They are believed tolive close to their homes where hey lived when they were human being.They show interest in their surviving families, and inturn theirfamilies remember them by pouring out parts of their drinks andleaving beats of food for time to time. The living dead may also visittheir surviving relatives in dreams or vision or even openly and maketheir wishes known. (Uk 72-73)

Wanachukuliwa kama ni sehemu za familia zao. Wanaaminiwakuendelea kuishi jirani na makazi yao ambayo waliishi wakati wakiwahai. Wanaonesha kuvutiwa na ndugu zao wanafamilia wanaoishi, nafamilia zao pia zinaendelea kuwakumbuka kwa kumwaga sehemu zavinywaji vyao na kuacha chakula mara kwa mara. Pia wahengahuwatembelea ndugu zao walio hai katika ndoto au maono au hatakwa wazi na kutoa matarajio yao. (Tafsiri ya mtafiti)

Maelezo katika nukuu hiyo yanaonesha kuwa, kwa Waafrika roho za binadamu

zinahusisha pia zile za watu waliokwisha kufariki katika kipindi fulani. Hii inatokana

na sababu kwamba, watu walio hai hufanya vitu mbalimbali kuonesha kuwakumbuka

wahenga hao na kuwaomba katika shida zao. Wahenga hao pia huwatokea walio hai

kwa njia ya ndoto au maono na kujibu maombi yao. Mtaalamu huyu anatuambia

kuwa mtu akifariki roho yake inaendelea kuwepo karibu na walio hai na

Page 26: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

13

kuwatembelea mara kwa mara. Andiko hili limemsaidia mtafiti katika kuelewa

dhana ya roho kama kipengele kimojawapo cha falsafa ya Kiafrika. Licha ya

manufaa hayo, andiko hilo halijabainisha mambo ambayo kupitia kwayo falsafa ya

Kiafrika inajipambanua katika vitendawili vya Kiswahili. Pengo hilo ndilo

limeshughulikiwa na mtafiti kwa kubainisha vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika

muktadha wa kitamaduni.

Jengo na Wenzake, (1982) katika andiko lao wanashadidia uwepo wa falsafa ya

Kiafrika katika jamii za Kiafrika. Fikra za wataalamu hawa zinatia hamasa katika

kujitambua na kulinda heshima ya Waafrika kwa kuwa Waafrika ni binadamu wenye

utashi kama walivyo wengine. Wanaeleza kuwa uchambuzi wa falsafa yoyote lazima

utokane na mfumo wa jamii uliopo wakati falsafa hiyo inatokea. Madai haya ni

muhimu kwa kuwa ili kubaini falsafa ya jamii ni vema kuchunguza msingi ulioijenga

falsafa hiyo hasa kwa kuzingatia ethnofilosofia ya jamii husika. Fikra hizi

zimemsaidia mtafiti katika kuthibitisha kuwa kila jamii ina falsafa yake kutokana na

uzoefu wanaoupata wanajamii kwa kuishi katika mazingira yao kwa muda mrefu.

Hata hivyo, andiko hili limeacha pengo la kutafiti kwa kuwa, halikufafanua namna

falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika fasihi simulizi. Pengo hilo

limeshughulikiwa katika utafiti huu kwa kujadili namna falsafa ya Kiafrika

inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili.

Pia, Menkiti (1984) anakubaliana na mawazo ya John Mbiti katika andiko lake

linalohusisha dhana ya mtu na jumuia. Katika andiko hilo, anafafanua kuhusu mila

na desturi za Waafrika. Anaeleza kuwa, Waafrika wanaamini kifo sio Mwisho wa

uhai bali ni mwanzo wa maisha mengine. Haya yanathibitika pale anaposema:

Following John Mbiti, we can call the inhabitants of the ancestralcommunity by the name of the living dead. For the ancenstral deadare not dead in the world of spirits nor are they dead in the memory ofthe living men and women who continue to remember them, and whoincessantly ask their help through various acts of libation andsacrificial offering. (uk.174)

Page 27: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

14

Kwa kufuatia mawazo ya John Mbiti, tunaweza kuwaita wakazi wajumuiya ya wahenga kwa jina la wafu wanaoishi. Wahenga haohawajafa katika ulimwengu wa kiroho. Kadhalika, hawajafa katikakumbukumbu za waliohai, wake kwa waume ambao wanaendeleakuwakumbuka na huendelea kuomba msaada wao kupitia matendombalimbali ya matambiko na kutoa sadaka. (Tafsiri ya mtafiti)

Katika andiko hili, Menkiti amefafanua juu ya imani za Waafrika katika kifo ambapo

anaona kuwa mtu akifa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine wa kiroho.

Hii ina maana kuwa mwili ndio unaotengana na roho lakini roho inaendelea kuwepo

na kuwatembelea waliohai. Fikra hizi zinashabihiana kwa kiasi kikubwa na Stumph

na Fierser (2008) ambao wanaona kuwa roho ya binadamu ni muunganiko wa mwili

na roho. Baada ya mwili na roho kutengana kutokana na kifo, roho husambazwa kwa

binadamu wengine mmoja baada ya mwingine na kuwa roho hizi haziteketei kwa

kuwa hurudi kuungana na roho za dunia. Maelezo haya yamemsaidia mtafiti katika

kubaini kuwa kifo na uhai ni kipengele kimojawapo cha falsafa ya Kiafrika kwa

kuwa, kinajaribu kujibu maswali ya msingi ya kifalsafa. Maswali hayo pengine

yasingeweza kujibiwa kwa taaluma nyingine. Andiko la mtaalamu huyu limeacha

pengo la kutafiti kwani andiko hilo halikufafanua kwa kina kuhusiana na namna

falsafa hiyo inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili. Utafiti huu umeziba

pengo hilo kwa kujadili namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika vitendawili

vya Kiswahili.

2.3.2 Mapitio ya Maandiko Kuhusu Falsafa ya Kiafrika na Fasihi

Wapo watafiti mbalimbali waliofanya tafiti zao kuhusu usawiri wa falsafa ya

Kiafrika katika fasihi yaani fasihi simulizi na fasihi andishi. Mawazo ya wataalamu

hawa kuhusu falsafa ya Kiafrika ni kama ifuatavyo;

Hussein (1976) katika kitabu chake cha Kinjekitile, ameonesha kuhusu falsafa ya

Kiafrika inayohusu imani za “uchawi” na “ushirikina”. Dhana hii imejitokeza katika

harakati za kupambana na kupinga ukoloni nchini Tanzania. Kinjekitile anatumia

uchawi kwa kukaa ndani ya maji kutwa nzima jambo ambalo kwa hali ya kawaida

haliwezekani, na anapoibuka anatoka na dawa ya maji. Dawa hiyo inaaminika kuwa

kinga kwa wapiganaji na imani kuwa risasi ikipigwa itageuka maji na haitamdhuru

mtu yeyeote aliyekunywa dawa hiyo. Jambo hili linaonesha nguvu asilia alizonazo

Kinjekitile. Nguvu hizo zinazomwezesha kutenda mambo yasiyo ya kawaida ambayo

Page 28: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

15

mtu mwingine hawezi kutenda, ndizo zinabainisha falsafa ya Kiafrika katika masuala

ya imani. Kazi hii ni miongoni mwa kazi nyingi za fasihi zinazotambulisha imani za

Kiafrika na hivyo kubainisha falsafa yao. Andiko hili limemsaidia mtafiti kutambua

kuwa, suala la “uchawi” na “ushirikina” ni mojawapo ya amali ya kifalsafa ya

Waafrika ambayo pia mtafiti amelijadili kuonesha namna linavyojitokeza katika

vitendawili vya Kiswahili. Pengo lililoachwa katika andiko hilo ni kuwa, mtaalamu

huyu amefafanua kuhusu kipengele kimoja cha falsafa ya Kiafrika na kuacha

vipengele vingine vikiwa bado havijafafanuliwa kwa kina. Pengo hilo limezibwa na

mtafiti katika utafiti huu kwa kujadili kuhusu vipengele vingine vya falsafa ya

Kiafrika kama umoja na ushirikiano, uzazi na ulezi na uduara na kuona namna

vinavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili.

Gyekye (1987) ameongelea kuhusu dhana ya mizimu ambayo ni kipengele

kimojawapo cha falsafa ya Waafrika. Katika kazi yake, Gyekye amechambua kuhusu

dhana ya kuwepo na sababu za kuwepo kwa jamii ya Waakani. Katika uchambuzi

wake amebainisha kuwa, Waakani wanatofautisha kati ya mizimu na roho. Kwake

mizimu ni dhana inayorejelea kitu kisichojulikana. Aidha, anaongeza kuwa, mizimu

ni mtu anayemithilishwa kuwa na uhusianao kati ya “mwili” na “roho” kwa kutenda

matendo ya mtu aliyehai. Kwake anaona visawe hivi viwili yaani; mizimu na roho

wakati fulani huingiliana katika matumizi na sifa zake. Utafiti wake umemsaidia

mtafiti kuelewa vema dhana ya imani katika mizimu ambayo pia mtafiti katika utafiti

huu, ameibainisha namna inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili. Pengo

lililobainika katika utafiti wake ni kuwa, utafiti huo haujafafanua kuhusu namna

suala la imani katika mizimu linavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili.

Utafiti huu umeziba pengo hilo kwa kujadili namna falsafa hii ya imani katika

mizimu inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili.

Katamba (2011) amechunguza kuhusu suala la utoaji majina kwa watoto kama

kipengele kimojawapo cha falsafa ya Kiafrika. Katika tasnifu yake iliyolenga

kuchunguza utamaduni wa kutoa majina wa jamii ya Wanyakyusa. Amebainisha juu

ya asili na chimbuko la majina ya jamii ya Wanyakyusa, kuchunguza juu ya

visababishi vya utoaji wa majina hayo na maana mbalimbali za majina katika jamii

hiyo. Katika utafiti huo alibaini kuwa, kuna sababu mbalimbali zinazosababisha

majina kutolewa. Sababu hizo ni kama vile matatizo ya kifamilia na sababu za

Page 29: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

16

kihistoria zinazoambatana na matukio yaliyotokea wakati mtoto anazaliwa. Hata

hivyo, kila jina linalotolewa huwa na maana na hakuna jina ambalo hutolewa

kiholela bila kuwa na maana. Andiko hili ni muhimu kwani linabainisha mila na

desturi za Watanzania katika muktadha wa kitamaduni ambazo kwazo maarifa ya

kifalsafa ya Waafrika huibuliwa ndani yake. Hata hivyo, utafiti huo umeacha pengo

la kutafiti katika kufafanua athari ya utamaduni huo kwa jamii kama inavyosawiriwa

katika vitendawili vya Kiswahili. Pengo hilo limezibwa na utafiti huu kwa

kutathmini athari ya falsafa ya Waafrika kwa jamii kama inavyojitokeza katika

vitendawili vya Kiswahili.

Simchimba (2012) amefanya utafiti wake uliojikita katika kuchunguza falsafa ya

Kiafrika katika methali za Kiswahili. Anasema methali ni kipengele muhimu cha

lugha kinachogusa kwa kiasi kikubwa maisha ya watu. Kupitia methali za Kiswahili

aliweza kuthibitisha kuwepo kwa falsafa ya Kiafrika. Katika utafiti huo anataja

baadhi ya vipendele vya falsafa ya Kiafrika vinavyojitokeza katika methali hizo

kuwa ni falsafa ya umoja, ukweli na maana, hekima na busara, masuala ya ndoa,

falsafa ya uzazi na sanaa jadi. Utafiti huo una mchango mkubwa katika utafiti wetu

kwani umeonesha kupitia methali namna Waafrika wanavyofikiri na kutenda mambo

mbalimbali katika jamii na hivyo kutambulisha falsafa yao. Hata hivyo, vitendawili

kama kipera kimojawapo cha fasihi simulizi hakikushughulikiwa katika utafiti huo,

na hivyo kutoa mwanya kwa mtafiti kuchunguza namna vitendawili vya Kiswahili

vinavyoweza kusawiri falsafa ya Waafrika.

Duwe (2016) amefanya utafiti wake juu ya mdhihiriko wa falsafa ya Uduara katika

sanaa za maonyesho za jamii ya Wangoni. Katika utafiti huo, alibainisha miktadha

mbalimbali ambayo kwayo falsafa ya uduara inadhihirika katika jamii ya Wangoni.

Anafafanua baadhi ya miktadha hiyo kuwa ni katika mkao wa kula, katika miktadha

ya ngoma zao, katika shughuli za mazishi (misiba) na katika sherehe zao za kikabila.

Pia anaeleza kuwa baadhi ya vitu vyao wanavyovitumia kama vile vigoda na nyungo

ni za umbo la duara. Andiko hili linadhihirisha kuwa Waafrika wana falsafa ya

uduara. Andiko hili lilimwezesha mtafiti kuongeza maarifa kwa kubaini kuwa, dhana

ya uduara ni kipengele muhimu katika uibuaji wa maarifa ya falsafa ya Waafrika.

Hata hivyo, licha ya umuhimu huo, andiko hilo halijaonesha chochote kuhusu namna

vitendawili vya Kiswahili vinavyoweza kutumika kudhihirisha falsafa ya uduara kwa

Page 30: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

17

kuwa halikuwa lengo lake la utafiti. Utafiti huu umeziba pengo hilo kwa kuonesha

namna falsafa ya Kiafrika ikiwemo uduara inavyodhihirika katika vitendawili vya

Kiswahili.

Naye Makame, (2016) amefafanua dhana ya Usihiri kama inavyojitokeza katika

riwaya za Kiswahili. Katika utafiti wake amechunguza miktadha ambayo usihiri

huelekezwa katika riwaya teule, sababu zinazochangia kutokea kwa falsafa ya usihiri

katika riwaya na kutathmini athari za matumizi ya falsafa ya usihiri kwa jamii na

wasomaji wa riwaya. Utafiti wake ulibaini kuwa sababu zichangiazo kutokea kwa

falsafa ya usihiri katika riwaya ni shughuli za kisiasa, shughuli za kiutamaduni,

shughuli za kiuchumi na sababu za kitajriba au mazoea. Aidha, amefafanua athari

chanya za falsafa ya usihiri kama kuimarisha mapenzi, ufahari na ulinzi na athari

hasi ni kusababisha kuleta ugomvi ndani ya jamii na kujenga maadili mabaya. Utafiti

wake umemsaidia mtafiti katika kubaini kuwa, usihiri ni kipengele kimojawapo

kinachodhihirisha falsafa ya Waafrika. Kwa kuwa utafiti huo umeshughulikia

kipengele kimoja cha falsafa ya Waafrika, umeacha pengo kwa upande wa vipengele

vingine vya falsafa ya Kiafrika kama vinavyojitokeza katika vitendawili vya

Kiswahili. Pia, kipengele hicho kimejadiliwa kwa kuonesha namna kinavyojitokeza

katika riwaya za Kiswahili. Hivyo, hakijajadiliwa kwa upande wa vitendawili ili

kuona namna dhana ya usihiri inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili.

Pengo hilo limezibwa na utafiti huu kwa kujadili namna vipengele mbalimbali vya

falsafa ya Kiafrika vinavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili.

Faustine (2017) alifanya utafiti wake kuhusu falsafa ya Waafrika na ujenzi wa

mtindo wa uhalisiaajabu katika riwaya ya Kiswahili. Katika utafiti huo alibainisha

namna falsafa ya Waafrika inavyosawiriwa katika riwaya teule za Kiswahili za

kihalisiajabu. Pia alijadili namna falsafa ya Waafrika inavyojitokeza kama kijenzi

cha mtindo wa uhalisiajabu katika riwaya teule za Kiswahili za kihasiajabu.

Akifafanua kuhusu falsafa ya Waafrika anasema kuwa Waafrika wanaamini katika

nguvu-hai ambazo zimepangwa kidarajia kwa maana kuwa Mwenyezi Mungu ndiye

mmiliki mkuu wa nguvu-hai wakifuatia wahenga, mababu, wazazi na kadhalika. Hii

ina maana kuwa wahenga wana nguvu kubwa kuliko mababu na mababu wana

nguvu kuliko wazazi na hivyo hivyo mpaka katika ngazi ya chini. Katika hili

anasema kuwa;

Page 31: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

18

Kwa Waafrika, mfumo wa kidarajia ndio unaoweka msingi wamaadili ambao umekitwa katika nguvu-hai. Kwa maana hiyo,kuwatii wahenga na mababu ni chanzo cha baraka kubwa aunguvu-hai kubwa kuliko wazazi. Kinyume chake, ni kuitafuta laanainayotokana na upungufu wa nguvu hiyo. Falsafa mbalimbalizinazoijenga falsafa jumuifu ya Waafrika kama vile uzazi na ulezi,uchawi, maisha baada ya kifo, busara na hekima, umoja naushirikiano na dhana ya uduara zinajengwa katika msingi wafalsafa kuu ya kuwapo kwa nguvu-hai.

Maelezo ya mtaalamu huyu yanathibitisha kuwa, Waafrika wana falsafa yao ambayo

imekitwa katika nguvu-hai. Waafrika wanaamini kuwa, mtu akiumwa nguvu hai

zake zinapungua kwa hiyo atakufa na mchawi ndiye anayeweza kupunguza nguvu-

uhai za mtu. Vile vile, wenye uwezo wa kuongeza nguvu-hai wanaoelezwa na

Faustine kuwa ni Mungu – mizimu – wahenga – mababu – wazazi. Andiko la

mtaalamu huyu limemsaidia mtafiti kuelewa falsafa ya Kiafrika katika mawanda

mapana ya kazi za fasihi za kihalisiajabu. Hata hivyo, utafiti wake ulijikita katika

kufafanua namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza kama kijenzi cha mtindo wa

uhalisiajabu katika riwaya teule za kihalisiajabu. Kwa kuwa, andiko hili halijatoa

ufafanuzi kuhusu namna falsafa hiyo inavyosawiriwa katika vitendawili vya

Kiswahili na wala kubainisha athari za falsafa hiyo kwa jamii kwa sababu suala hilo

halikuwa lengo la mtaalamu huyu. Hali hii ndiyo imemfanya mtafiti kuamua

kulishughulikia ilio kuziba pengo hilo kwa kujadili namna falsafa ya Waafrika

inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili pamoja na athari za falsafa hiyo kwa

jamii.

Mlelwa, (2017) alifanya utafiti wake kuhusu falsafa ya Kiafrika katika vitabu teule

vya fasihi ya Kiswahili: Ngoma ya Ng’wanamalundi na Dunia Uwanja wa Fujo.

Katika utafiti wake amebainisha vipengele vya falsafa ya Kiafrika vinavyojitokeza

katika kazi teule pamoja na kulinganisha na kulinganua namna waandishi wa kazi

hizo walivyotumia vipengele vya falsafa ya Kiafrika katika kusuka simulizi na

kuumba wahusika wao. Baadhi ya vipengele hivyo ni kama vile uchawi na ulozi,

uhai na kifo, hekima na busara, umoja na ushirikiano, uzuri, wakati, maadili, uganga

na uongozi. Utafiti wake umekuwa na umuhimu mkubwa katika utafiti huu kwani

umepanua mawanda ya uelewa wetu kuhusu vipengele vinavyodhihirisha falsafa ya

Kiafrika. Andiko hilo halijafafanua athari ya falsafa ya Kiafrika kwa jamii kama

inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili kwa kuwa lilikuwa nje ya malengo

Page 32: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

19

yake. Hivyo, pengo hilo limezibwa na utafiti huu kwa kutathmini athari ya falsafa ya

Kiafrika kwa jamii kama inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili.

Kaponda (2018) amefanya uchunguzi kuhusu Ontolojia ya Kiafrika katika mbolezi

za Wanyasa. Amebainisha aina za mbolezi zinazopatikana katika jamii ya Wanyasa

na vipengele vya ontolojia ya Kiafrika katika mbolezi za Wanyasa. Pia, ametoa

tathmini juu ya umuhimu wa ontolojia ya Kiafrika kwa jamii na Waafrika kwa

ujumla. Baadhi ya vipengele vya ontolojia ya Waafrika vilivyodhihirika kupitia

mbolezi za Wanyasa ni ardhi, Mungu, kifo, roho, utu, na wahenga au mizimu.

Anaendelea kueleza kuwa, katika jamii ya Wanyasa fasihi ambayo yamkini ni zao la

jamii imetumika ili kufikisha mawazo ya kifalsafa ambayo ni matokeo ya uzoefu wa

wanajamii katika mazingira yao. Katika utafiti wake ametathmini nafasi ya ontolojia

ya Kiafrika kwa jamii. Baadhi ya faida zinazoelezwa na mtafiti ni kama vile

kudumisha umoja na mshikamano, kujadili masuala muhimu ya jamii, kurithisha

amali za jamii na kulinda maadili. Utafiti wake umekuwa na umuhimu mkubwa

kwani umetusaidia kujua kuwa, fasihi ya jamii ndiyo hutumika kufikisha mawazo ya

kifalsafa ya jamii husika. Hata hivyo, andiko hilo halikugusia chochote kuhusu

falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili kwa sababu suala hilo halikuwa

lengo lake la utafiti wake. Hivyo, ili kuziba pengo hilo, mtafiti ameona ni vema

utafiti huu kujengewa hoja kuhusu usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi

hususani vitendawili vya Kiswahili.

2.3.3 Mapitio ya Maandiko kuhusu Vitendawili vya Kiswahili

Mng’aruti (2008) anafasili vitendawili kuwa ni maneno yanayoficha maana ya kitu

ili kisijulikane kwa urahisi. Maneno ya kawaida, vitu au hali mbalimbali za kawaida

huelezwa kimafumbo au kisanaa ili wafumbuzi wayafumbue. Fasili hii ni pana sana

kwani inajumuisha vitu vyote ambavyo hutolewa kwa njia ya mafumbo kuingia

katika kundi la vitendawili ambavyo kiuhalisia sio vitendawili. Vijitanzu kama nahau,

mafumbo na methali pia hutumia mafumbo lakini sio vitendawili. Pamoja na

mapungufu ya fasili hii bado inatupa mwanga juu ya sifa muhimu ya vitendawili ya

hali ya ufiche ambayo hueleza jambo kwa hali za kawaida zilizozoeleka kisanaa au

kimafumbo. Aidha, anaona kuwa vitendawili vina umuhimu mkubwa kama ilivyo

kwa methali. Kwa hiyo, andiko hili limekuwa na umuhimu katika utafiti wetu kwani

limepanua wigo wa ufahamu wetu kuhusu umuhimu wa vitendawili kwa jamii. Licha

Page 33: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

20

ya kuwa na umuhimu huo, andiko hili halijaeleza kama vitendawili vinaweza

kutumika kudhihirisha amali za kifalsafa za jamii ya Waafrika. Ili kuziba pengo hilo,

mtafiti ameona ni vema utafiti huu kujengewa hoja juu ya usawiri wa falsafa ya

Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili.

Amana, (2013) anaeleza kuhusu dhana ya vitendawili kuwa ni swali la kisitiari

ambapo sehemu moja ya ulinganishi uliopo inadokezwa tu ilhali ya pili inabakia ya

kukisiwa. Kama sanaa, vitendawili hutegemea uwezo alionao mtu kutambua,

kuhusisha na kulinganisha vitu vya aina tofauti katika mazingira yake. Hii ni sanaa

inayotendwa na inayosimama kivyake tofauti na sanaa tegemezi au elekezi kama

methali. Vitendawili hulenga maisha ya jamii na shughuli wafanyazo. Vitendawili

vingi hushughulikia mambo tofauti yanayomhusu binadamu kama kifo, uhai, chakula,

maisha na mazingira. Pia akielezea kuhusu asili ya vitendawili anasema vitendawili

vinatokana na mahitaji ya kisanaa, mahitaji ya matumizi, mahitaji ya kueleza

mazingira na maendeleo na misemo ya kimtaa. Anataja sifa za vitendawili na

muundo wake.

Katika andiko lake Amana, (2013), amefafanua pia kuwa vitendawili vina umuhimu

mkubwa kwa jamii. Kwa kutaja baadhi ya faida hizo ni kama vile, husaidia kuhifadhi

historia na utamaduni wa jamii, huwa msingi wa kuyachambua maisha ya jamii,

kuonesha hisia za wanajamii kuhusu mtu au kitu fulani, kuelimisha kuhusu

mazingira, imani, amali, mavazi na historia. Pia, vitendawili huchochea kufikiria kwa

wanajamii kwa njia ya kupevusha kukabiliana na maisha yao na kudhihaki au

kukejeli sifa na tabia zisizofaa. Andiko hili limekuwa na umuhimu mkubwa katika

utafiti wetu kwani limevielezea vitendawili katika mawanda mapana ya kimaudhui

na hivyo kumpatia mtafiti nafasi ya kuvielewa vitendawili kwa upana. Pengo

lililoachwa katika utafiti huo ni kuwa, utafiti wake haujatambulisha vitendawili kama

amali ya kifalsafa ya Kiafrika. Kutoshughulikiwa kwa kipengele hicho katika andiko

hili ndio kumemfanya mtafiti kutaka kujua zaidi vitendawili kama amali za

kitamaduni vinavyoweza kusawiri falsafa ya Kiafrika. Hivyo, utafiti huu

unachunguza usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili.

Gwaravanda na Masaka (2008) wananukuliwa na Badru (2015) katika utafiti wao wa

vitendawili vya jamii ya Washona wa Zimbabwe. Wanashadidia umuhimu wa

Page 34: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

21

vitendawili kwa kueleza kuwa vitendawili ndicho kiini cha mfumo wa elimu ya jamii

hiyo. Utafiti wao unaonesha kuwa dhima kubwa ya vitendawili ni kuelimisha na sio

kuburudisha tu kama ilivyoelezwa na watu walio wengi. Vitendawili vinafundisha

vijana masuala yanayohusu mila, desturi, uzoefu wao, miiko na tamaduni katika

mazingira yao. Utafiti huu unaosisitiza umuhimu wa vitendawili umetupa hamasa ya

kutaka kuchunguza zaidi katika utanzu huu ambao kwa baadhi ya watafiti haupewi

kipaumbele ili kubaini uchomozi wa falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya

Kiswahili. Pengo lililojitokeza katika andiko hilo ni kuwa, andiko hilo limefafanua

dhima ya vitendawili kwa jumla bila kutathmini athari ya falsafa ya Kiafrika kwa

jamii kama inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili. Utafiti huu umeziba

pengo hilo kwa kutathmini athari ya falsafa ya Kiafrika kwa jamii kama

inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili.

Naye Badru (2015) amefanya utafiti wake kuhusiana na taswira na ubainishaji wa

mabadiliko ya kiujumi katika vitendawili vya Kiswahili. Katika utafiti wake

amefafanua dhima za vitendawili nakukanusha madai ya baadhi ya wataalmu

wanaoona kuwa vitendawili ni sanaa ya watoto na haina umuhimu wowote kwa jamii

zaidi ya kuburudisha watoto. Amefafanua dhima za vitendawili kiuchumi, kijamii na

kiutamaduni. Utafiti huu ni muhimu kwani umesaidia katika kutoa mwongozo mzuri

katika kufafanua ujumi wa Kiafrika katika vitendawili. Hata hivyo, andiko hilo

halikuzungumzia chochote kuhusu namna vitendawili vya Kiswahili vinavyoweza

kutumika kuhakiki falsafa ya Kiafrika. Pia, halijatathmini athari ya falsafa ya

Kiafrika kwa jamii kama inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili. Ili kuziba

pengo hilo, utafiti huu unakwenda zaidi ya hapo kwa kuchunguza vipengele vya

falsafa ya Kiafrika vinavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili na kutathmini

athari ya falsafa hiyo kwa jamii.

Mtaalamu mwingine ambaye amefanya uchunguzi wa vitendawili ni Damka (2015).

Yeye alichunguza dhima ya vitendawili vya jamii ya Wanyisanzu wa Iramba Singida.

Katika andiko hilo alitafiti kuhusu chanzo cha mabadiliko ya dhima za vitendawili

vya jamii ya Wanyisanzu na vipengele vya fani vinavyosababishwa na mabadiliko ya

utegaji vitendawili. Anaeleza kuwa vitendawili vilikuwa na dhima kubwa kabla ya

uhuru wa Tanganyika na hata sasa katika jamii yetu. Miongoni mwa dhima

zinazotajwa ni kama kuelimisha jamii kuhusu mambo ya kiuchumi, kiutamaduni na

Page 35: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

22

kijamii, kuhifadhi na kuendeleza mila na desturi za jamii inayohusika, kufundishia

msamiati mpya shuleni na kutangaza biashara za watu ili bidhaa zao ziweze

kununuliwa kwa wingi. Andiko hili limekuwa na umuhimu katika utafiti wetu kwani

limetuongoza katika kubaini umuhimu wa vitendawili katika jamii. Hata hivyo,

andiko hili limeacha pengo lililotakiwa kuzibwa na utafiti huu kwani halijafafanua

namna vitendawili vya Kiswahili vinavyoweza kusawiri falsafa ya Kiafrika. Utafiti

huu umeziba pengo hilo kwa kujadili namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza

katika vitendawili vya Kiswahili.

Vilevile, Mshana (2015) amefanya utafiti wake ambapo amechunguza usawiri

chanya wa mwanamke katika vitendawili vya jamii ya Wanyiha. Katika utafiti huo,

alitathmini usawiri chanya wa mwanamke katika vitendawili vya jamii ya Wanyiha

na kuchunguza ujumbe unaopatikana katika vitendawili. Utafiti wake ulibaini kuwa

mwanamke anasawiriwa kama mama na mlezi wa watoto katika jamii. Akitolea

mfano wa kitendawili cha “mama anatembea na kibyongo” ambacho jibu lake ni

“konokono”, mtafiti alieleza kuwa, kitendawili hiki kinamsawiri mwanamke na

mtoto wake tangu akiwa tumboni, kuzaliwa kwake akiwa katika hali ya uchanga

anamlea mwanae hadi anapokufa na hata akifa uhusiano wa mama na mwana

huendelea kwenye ndoto, dua na mizimu. Vitendawili vinamsawiri mwanamke kama

kiumbe mvumilivu na mchapakazi katika jamii. Andiko hili limemsaidia mtafiti

kupanua uelewa wake kuhusu dhima kubwa ya vitendawili katika jamii. Hata hivyo,

utafiti huo haujagusia chochote kuhusu usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika

vitendawili vya Kiswahili. Hivyo, ili kuziba pengo hilo, utafiti huu umechunguza

usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili.

2.4 Mapengo Yanayojitokeza

Wakati wa kupitia maandiko mbalimbali ya watafiti na wahakiki wa kazi za fasihi,

falsafa ya Waafrika na vitendawili vya Kiswahili, tumebaini mapengo yafuatayo;

Mosi, watafiti hawa hawajabainisha na kueleza kwa kina vijenzi vya falsafa ya

Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni. Pili, tafiti nyingi hazijashughulikia suala la

falsafa ya Kiafrika kama inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili. Tatu, kazi

hizo hazijachunguza kwa kina kuhusu athari ya falsafa ya Kiafrika kama

inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili. Hivyo, utafiti huu umeshughulikia

Page 36: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

23

mapengo hayo yaliyoachwa na watafiti waliotangulia kwa kupitia malengo mahsusi

matatu yaliyotuongoza katika utafiti huu.

2.5 Muhtasari wa Sura ya Pili

Sura hii imefafanua kuhusu kiunzi cha nadharia iliyotumika katika kufafanua na

kuchanganua data za utafiti na maandiko mbalimbali ambayo mtafiti aliyapitia. Kwa

ujumla mapitio hayo yamebeba mawazo na mitazamo mbalimbali ya wataalamu na

wanazuoni kuhusu falsafa ya Kiafrika kwa ujumla wake, falsafa ya Kiafrika katika

fasihi na mitazamo mbalimbali kuhusu vitendawili vya Kiswahili. Hivyo, sura

inayofuata inafafanua kuhusiana na methodolojia iliyotumika katika mchakato

mzima wa kukusanya na kuchambua data za utafiti huu.

Page 37: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

24

SURA YA TATU

METHODOLOJIA YA UTAFITI

3.1 Utangulizi

Sura hii imefafanua kuhusu methodolojia iliyotumika katika kufanikisha utafiti huu.

Vipengele vilivyoshughulikiwa katika sehemu hii ni usanifu wa utafiti, mkabala wa

utafiti, eneo la utafiti, walengwa na sampuli ya utafiti, mbinu za ukusanyaji na

uchanganuzi wa data. Vipengele vingine ni vifaa mbalimbali vilivyotumika katika

kukusanya data, itikeli za utafiti, uhalali na uthabiti wa data. Aidha, mtafiti ameeleza

baadhi ya changamoto mbalimbali alizokutana nazo wakati wa kukusanya data na

namna alivyozitatua.

3.2 Usanifu wa Utafiti

Utafiti huu ulitumia usanifu wa fenomenolojia katika kukusanya data na

kuchanganua data za utafiti huu. Kwa mujibu wa Kothari (2004) usanifu wa utafiti ni

uamuzi kuhusu nini, wapi, lini, kwa kiwango gani na namna gani utafiti utafanyika.

Hii ina maana kuwa usanifu wa utafiti ni mpangilio maalumu wa kanuni za

kukusanya data na uchanganuzi wake ili kufikia uyakinifu wa malengo ya utafiti kwa

kuzingatia muda, mahali pa utafiti na hali ya uchumi iliyopo katika kuikamilisha

mada ya utafiti. Utafiti huu ulijikita katika ufafanuzi wa taarifa zilizokusanywa na

kuchambuliwa kwa njia ya maelezo yaliyoakisi mtazamo wa wahojiwa kulingana na

walivyoielewa falsafa ya Kiafrika. Hivyo, ilichukuana na usanifu wa

kifenomenolojia kwa sababu data zilikusanywa kwa kujigeza katika uelewa,

mitazamo, na tajiriba za watafitiwa kuhusiana na falsafa yao. Fenomenolojia

hujihusisha na maisha ya binadamu na namna ya kuufahamu ulimwengu kulingana

na uzoefu wa maisha ya watu hao kuhusiana na jambo fulani. Hivyo, usanifu huu

ulifaa sana katika utafiti huu kwani ulihusiana na maisha halisi ya watu katika

mitazamo yao, na hivyo, kusaidia kumwongoza mtafiti kuchunguza mawazo na

tajiriba za watafitiwa kuhusu falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili.

3.3 Mkabala wa Utafiti

Utafiti huu ulitumia mkabala wa kitaamuli katika ukusanyaji, uchanganuzi wa data

pamoja na kutoa matokeo ya utafiti. Ponera (2016) anaeleza kuwa utaamuli ni aina

mojawapo ya mikabala ya kufanyia utafiti, ambao hutumia zaidi tafakuri katika

kuhusisha taarifa mbalimbali za kitafiti. Pia huhusisha ufafanuzi wa jambo kwa

Page 38: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

25

kuzingatia misingi ya nadharia husika, pamoja na ithibati bayana zipatikanazo

maskanini au uwandani. Kwa hiyo, mkabala huu umekuwa na manufaa katika utafiti

huu kwa sababu, data zinazohusiana na falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya

Kiswahili zilizopatikana uwandani na maktabani zimechanganuliwa na kufafanuliwa

kwa njia ya maelezo. Data hizo zimesadifu usanifu wa utafiti huu kwa sababu

zilikusanywa na kuchambuliwa kwa njia ya maelezo yaliyoakisi mitazamo ya

watafitiwa kulingana na walivyoielewa falsafa yao.

3.4 Eneo la Utafiti

Utafiti huu ulifanyika uwandani na maktabani. Maeneo yaliyohusishwa ni Mikoa ya

Dodoma na Kagera. Katika mkoa wa Dodoma, sehemu zilizotumika ni wilaya ya

Dodoma mjini. Eneo hili lilichaguliwa kwa sababu ya uwepo wa maktaba za Chuo

Kikuu cha Dodoma na maktaba ya Mkoa wa Dodoma. Maktaba hizo zilitumika

kudurusu nyaraka mbalimbali zinazohusiana na mada huzika. Mkoa wa Kagera,

utafiti ulifanyika wilaya ya Bukoba ambapo mtafiti aliweza kuwapata walengwa wa

utafiti wake walioshiriki kutoa data za uwandani. Nao ni wanafunzi wa shule za

msingi na sekondari wa Bukoba pamoja na wanajamii wa wilaya ya Bukoba. Eneo

hili lilichaguliwa kutokana na sababu kuwa mazingira na wenyeji wa eneo hilo ni

miongoni mwa jamii za Kiafrika wanaotumia lugha ya Kiswahili ambao mtafiti

aliwakusudia. Pia, sehemu hii hakuna mwingiliano mkubwa wa makabila na, ni

mojawapo ya watu ambao hawajaacha mila na desturi zao kwa kiasi kikubwa. Hivyo,

ilikuwa rahisi kwa mtafiti kupata taarifa sahihi kutoka kwa watafitiwa. Taarifa hizo

zilihusiana na vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni, falsafa

ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili na athari za falsafa hiyo kwa jamii kama

inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili.

3.5 Walengwa wa Utafiti

Kwa mujibu wa Kombo na Tromp (2006), walengwa wa utafiti ni kundi la watu, vitu

au elementi ambazo mtafiti amekusudia kuvitumia katika utafiti wake. Kipengele

hiki cha walengwa wa utafiti kimehusisha makundi mawili ambayo ni jamii tafitiwa

na sampuli iliyoshughulikiwa.

Page 39: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

26

3.5.1 Jamii Tafitiwa

Faustine (2012) anaeleza kuwa jamii tafitiwa ni jumla ya vitu vyote ambavyo mtafiti

anaweza kuvitumia kwa ajili ya kupata data za utafiti wake. Vitu hivyo huweza kuwa

kundi la watu, eneo fulani la kijiografia au maandiko yanayohusiana na mada husika.

Katika utafiti huu, jamii tafitiwa ilijumuisha:

a) Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za wilaya ya Bukoba. Kundi hili

liliteuliwa kwa sababu mtafiti alikusudia kupata vitendawili vingi

iwezekanavyo kwani ni katika kiwango hiki cha elimu ambapo wanafunzi

hujifunza vitendawili kwa kiasi kikubwa.

b) Wanajamii wa wilaya ya Bukoba mkoani Kagera. Kundi hili liliteuliwa

kutokana na sababu kuwa, mada ya utafiti inamtaka mtafiti kutumia watu

wenye ujuzi au uzoefu wa moja kwa moja juu ya falsafa yao huku akihusisha

na uhalisi wa maisha yao. Wanajamii hawa wametumiwa kama kiwakilishi

tu cha jamii za Kiafrika wanaotumia lugha ya Kiswahili. Hata hivyo, mtafiti

angeweza kuwatumia wanajamii kutoka katika jamii nyingine tofauti na hii,

lakini, kutokana na rasilimali alizokuwa nazo hasa muda na fedha

zilisababisha kuteua walengwa hao kama kiwakilishi cha jamii nyingine za

Kiafrika. Kundi hili limesaidia kupata data kuhusu vijenzi vya falsafa ya

Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni na kufafanua athari za falsafa hiyo

kwa jamii kama inavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili.

c) Matini mbalimbali za kifasihi zilizohusu semi hasa vitendawili na maandiko

yanayohusu falsafa ya Kiafrika. Matini hayo yamesaidia kupatikana kwa

data zinazohusu vitendawili vya Kiswahili na falsafa ya Kiafrika kwa jumla.

3.5.2 Sampuli na Usampulishaji Wake

Ponera (2019) anasema usampulishaji ni kitendo cha kuteua sehemu ya wango ili

itumiwe na mtafiti katika kuchunguza na kupata majibu ya tatizo lake la utafiti.

Usampulishaji ni kitendo cha mtafiti kuteua sehemu ya watu, dhana au vitu ambavyo

vimechaguliwa kutoka katika kundi au jamii fulani ili kuwakilisha kutoa taarifa

zitakazokuwa kiwakilishi cha jamii nzima. Utafiti huu umetumia usampulishaji

lengwa katika kupata sampuli ya watafitiwa. Katika mbinu hii mtafiti hulenga kundi

fulani la watu, vitu au dhana zinazoaminika kuwa na uhakika juu ya utafiti husika

(Kombo na Tromp 2006).

Page 40: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

27

Utafiti huu umetumia usampulishaji lengwa wa aina mbili; tajwa na wa kutumia

fursa. Mosi, mtafiti ametumia usampulishaji lengwa wa kutegemea fursa katika

kuwapata wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ambao kimsingi walipatikana

kutegemeana na fursa ya muda huo. Hawa walisaidia kupatikana kwa vitendawili

vya Kiswahili wanavyovitumia katika mazingira yao na namna vitendawili hivyo

vinasawiri falsafa ya Kiafrika. Pili, utafiti huu ulitumia usampulishaji lengwa wa

kupokezana au tajwa katika kuwapata wanajamii. Hawa walieleza kuhusu vijenzi vya

falsafa ya Kiafrika na kufafanua athari ya falsafa hiyo kwa jamii kama

inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili. Aidha, matini mbalimbali

zilizotumika pia zimetumia usampulishaji lengwa kwani zimechaguliwa kwa

kuzingatia maarifa yanayopatikana kuhusiana na mada ya utafiti. Hivyo,

usampulishaji huu umerahisisha kupata taarifa za kina kuhusu falsafa ya Kiafrika

inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili, vijenzi vya falsafa ya Kiafrika

kama vinavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili na athari ya falsafa ya

Kiafrika kwa jamii.

3.5.2.1 Sampuli ya Utafiti

Kwa mujibu wa Gay (1987) sampuli ni sehemu ndogo ya kundi lengwa

iliyochaguliwa kushiriki katika kutoa data za utafiti. Utafiti huu ni wa kitaamuli

ambao huhusisha maelezo katika kutafsiri data. Idadi ya watafitiwa katika tarakimu

haina athari yoyote ya kitafiti bali imewekwa kama mwongozo wa kupata ramani ya

makadirio ya bajeti na muda wa utafiti. Sampuli iliyolengwa katika kutoa taarifa za

utafiti huu ilijumuisha; wanafunzi ishirini (20) kutoka shule za msingi za Wilaya ya

Bukoba. Hawa walishiriki katika kutoa taarifa zinazohusiana na vitendawili vya

Kiswahili. Pia, wanafunzi kumi (10) kutoka shule za sekondari za wilaya ya Bukoba.

Kundi hili lilishiriki katika kutoa taarifa zinazohusiana na vitendawili na kueleza

namna vitendawili vinavyosawiri masuala ya mila, desturi, uzoefu na kaida za jamii

ambavyo kwa jumla vinaunda falsafa ya Kiafrika. Pia wanajamii ishirini na watano

(25) wa wilaya ya Bukoba mkoani Kagera. Hawa walishiriki katika kutoa taarifa

zilizohusiana na vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni,

falsafa ya Kiafrika katika vitendawili na athari ya falsafa hiyo kwa jamii. Matini

nane (8) za falsafa na vitendawili vya Kiswahili zenye maudhui yanayohusiana na

mada yetu. Matini hizi zilisaidia katika kupatikana kwa maudhui yanayohusu

Page 41: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

28

vitendawili vya Kiswahili na falsafa ya Kiafrika kwa jumla. Mtafiti alitumia idadi

hiyo ya watafitiwa kutokana na aina ya utafiti wa kitaamuli ambao unaeleza kuwa

idadi ya watafitiwa wanaweza kuwa kuanzia watatu hadi thelathini kutegemeana na

miktadha mingine inayozungukia utafiti wenyewe (Ponera, 2019).

3.6 Ukusanyaji wa Data

Sehemu hii inaelezea njia na zana zilizotumika katika ukusanyaji wa data. Pia,

sehemu hii imefafanua jinsi mchakato wa ukusanyaji data ulivyofanyika.

3.6.1 Njia na Zana za Ukusanyaji wa Data

Njia zilizotumika katika ukusanyaji wa data za utafiti huu ni tatu, nazo ni mahojiano,

mjadala wa vikundi lengwa na udurusu wa nyaraka. Mtafiti ametumia njia za

kukusanyia data zaidi ya moja ili kuongeza kiwango cha uthabiti wa data za utafiti.

Kama anavyoeleza Ponera (2019) kuwa, kutumia mseto wa njia za kukusanyia data

huongeza uwezekano wa kuwa na kiwango kikubwa cha uthabiti. Hii ni kwa sababu

huondoa uwezekano wa kuwapo kwa hitilafu za kiutafiti zinazoweza kuletwa na

watafitiwa au mtafiti. Zana zilizotumika katika ukusanyaji wa taarifa ni simu, shajara,

kalamu. Zana nyingine ni mwongozo wa mahojiano, mwongozo wa mjadala wa

vikundi na mwongozo wa udurusu. Zana hizo zimeakisi vema njia zilizotumika

katika kukusanya taarifa. Ufafanuzi kuhusu njia za ukusanyaji data zilizotumika ni

kama ifuatavyo;

3.6.1.1 Mahojiano

Kothari (2009) anaeleza kuwa mahojiano ni majibizano ya ana kwa ana au ya simu

yanayofanywa na watu wawili au zaidi kwa lengo la kukusanya taarifa au maoni

kuhusu suala fulani la kiutafiti. Mtafiti ametumia mahojiano ya ana kwa ana na

wanajamii wa wilaya ya Bukoba katika kupata vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika

muktadha wa kitamaduni na kueleza athari za falsafa hiyo kwa jamii. Sababu ya

kutumia njia hii ni kuwa, katika mahojiano mtafitiwa anakuwa yuko huru kutoa data

zenye usahihi. Pia, ni njia rahisi inayompa fursa ya kuuliza maswali pale

panapohitajika na hivyo kupata data za kina. Mtafiti alitumia mwongozo wa

mahojiano uliohusu vitendawili vya Kiswahili na falsafa ya Kiafrika ili kupata data

zilizohitajika.

Page 42: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

29

3.6.1.2 Mjadala wa Vikundi Lengwa

Hii ni njia ya kukusanya taarifa inayohusisha mazungumzo baina ya mtafiti na

watafitiwa wakiwa katika vikundi juu ya mambo anayotaka kuyapata (Ponera 2019).

Mtafiti ametumia mjadala wa vikundi lengwa kwa wanafunzi wa shule za msingi na

sekondari ili kupata vitendawili vya Kiswahili vinavyotumika katika jamii. Hivi

vimemsaidia mtafiti kubaini namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza kutoka katika

vitendawili hivyo. Mtafiti aliamua kutumia njia hii kwa kuwa watafitiwa wake ni

watoto hivyo yawezekana wasiwe huru zaidi kutoa ushirikiano wao wakiwa mmoja

kuliko wakiwa katika kundi.

3.6.1.3 Udurusu wa Nyaraka

Kothari (2004) anaeleza kuwa udurusu wa nyaraka ni njia ya kukusanya data kutoka

katika vitabu, makala na matini za kielektroniki kwa lengo la kuzifanyia uchambuzi.

Anaendelea kueleza kwamba data zinazokusanywa kutoka vyanzo hivyo huitwa data

fuatizi. Mtafiti ameitumia mbinu hii kwa kusoma vitabu, makala na tovuti

mbalimbali zilizohusiana na utafiti huu. Hizi zilimsaidia kupata data zilizohusiana na

vijenzi vya falsafa ya Kiafrika, vitendawili vya Kiswahili na namna vitendawili

hivyo vinavyosawiri falsafa ya Kiafrika.

3.6.2 Mchakato wa Ukusanyaji Data na Udhibiti wake

Ili kupata data zilizohitajika kutoka kwa watafitiwa, mtafiti alianza kukusanya taarifa

zake kutoka kwa wanafunzi. Katika mjadala wa vikundi, mtafiti aliwagawa

watafitiwa wake katika idadi ya wanafunzi watano watano kwa wanafunzi wa shule

za sekondari na watoto kumi kumi kwa wanafunzi wa shule za msingi. Katika

makundi hayo mtafiti aliwafafanulia maswali yanayotakiwa kujibiwa na watafitiwa

katika mjadala na kuwaacha waeleze maoni yao. Mtafiti aliandika katika shajara

yake maoni ya watafitiwa hao. Kwa upande wa wanafunzi wa sekondari, aliwagawia

karatasi walizotumia kuorodhesha vitendawili vya Kiswahili na kisha kujadili kwa

pamoja kuhusu amali za kijamii zinazojitokeza katika vitendawili hivyo. Muda

uliotumika katika mijadala ni dakika themanini (80). Mbinu nyingine iliyotumika ni

mahojiano. Mtafiti aliwahoji watafitiwa wake maswali yaliyohusiana na lengo husika

na kisha kunukuu maelezo ya mahojiano hayo katika shajara yake. Muda uliotumika

kwa kila mhojiwa ni kuanzia dakika arobaini na tano hadi dakika sitini. Mbinu ya

mwisho ilikuwa ni udurusu wa nyaraka. Mtafiti alikusanya nyaraka zinazohusiana na

Page 43: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

30

mada ya utafiti kutoka katika vitabu, majarida, makala na tovuti mtandaoni. Mtafiti

alichambua kwa kina maudhui ya nyaraka hizo huku akihusisha na malengo ya

utafiti wake na hivyo kurahisisha upatikaji wa taarifa kutoka katika vyanzo hivyo.

Kwa jumla mchakato huo umesaidia kupatikana data za kutosha kuhusiana na

usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili.

3.7 Uchanganuzi wa Data

Ponera (2019) anafafanua kuwa, kuchanganua data ni mchakato wa kuzishughulikia

taarifa za utafiti zilizokusanywa ili kupata maana au mantiki pamoja na kupata

taarifa ua data chache zinazohitajika. Utafiti huu umefanywa kwa kutumia mkabala

wa kitaamuli, yaani mkabala usio wa kitakwimu. Enon (1998) anaeleza kuwa utafiti

wa kitaamuli ni utafiti ambao data zake huelezwa na kufafanuliwa kwa njia ya

maelezo. Mtafiti alichagua mkabala huu kwa sababu mada ya utafiti ni ya kifasihi

inayohitaji ufafanuzi wa mawazo na mtazamo juu ya dhana husika.

Katika uchanganuzi wa data za utafiti huu, mtafiti ametumia mbinu ya usimbishaji

wa maudhui. Ponera (2019) anaeleza kuwa hii ni mbinu inayofaa sana kwenye data

zenye uchangamani mkubwa wa dhana. Anamnukuu Masele (2016) anayefafanua

kuwa, mbinu hii hufafanua ujuzi, tajiriba, maana na uhalisi wa watafitiwa. Utafiti

huu ulihusisha ufafanuzi kuhusu ujuzi na mitazamo ya watafitiwa kuhusiana na

falsafa yao hivyo, imesaidia kuchanganua tabia, uzoefu na tajiriba za jamii kuhusu

maisha yao pamoja na mifumo yao ya maisha ili kubaini falsafa yao. Mtafiti alianza

kwa kuzichambua na kuzipanga data kulingana na muoano wa data hizo kimaudhui.

Hii ilifanyika kwa kuziweka data pamoja ili zilingane na malengo ya utafiti pamoja

na kuangalia uhusiano wa data alizozikusanya. Kwa hiyo, data zilizokusanywa kwa

njia ya mahojiano na mijadala ya vikundi lengwa zilichanganuliwa kwa kuwianisha

na njia ya udurusu wa nyaraka. Kwa kuongozwa na nadharia ya Kisosholojia, data

hizo zilifafanuliwa na kuwasilishwa kama matokeo ya utafiti.

3.8 Itikeli za Utafiti

Katika kuendesha mchakato wa utafiti huu, mtafiti alizingatia taratibu zote muhimu

za kimaadili wakati wote wa utafiti kuanzia hatua ya ukusanyaji data, uchanganuzi

wa data za utafiti na uandishi wa ripoti ya utafiti. Taratibu zilizozingatiwa ni pamoja

na:

Page 44: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

31

a) Kupata kibali kutoka katika Chuo Kikuu cha Dodoma. Mtafiti alichukua

barua ya utambulisho kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma iliyomtambulisha

katika maeneo husika aliyoenda kukusanya data za utafiti. Pia, aliwasilisha

barua au kibali hicho katika maeneo husika ya utafiti wake ambayo ni mkoa

wa Kagera na Dodoma.

b) Vilevile mtafiti aliwaomba ridhaa watafitiwa ili kuwafanyia utafiti. Aidha,

aliwafafanulia watafitiwa malengo na umuhimu wa utafiti huu. Watafitiwa

walihiari kuhojiwa na mtafiti alinukuu maelezo yao katika shajara yake.

c) Mtafiti aliwaeleza watafitiwa haki zao za msingi kama kuwa huru kuuliza

maswali pindi wanapoona kuna jambo halijaeleweka vema. Pia aliwaeleza

kuwa taarifa zilizotolewa zitakuwa ni siri na zitatumika kwa shughuli ya

utafiti tu. Hivyo, mtafiti alitunza siri za taarifa za watafitiwa wake ambao

baadhi hawakutaka kupigwa picha na kujulikana kwa watu wengine kama

wao walishiriki kutoa taarifa hizo.

d) Kihaiba, mtafiti alionekana katika mwonekano unaokidhi tamaduni za jamii

husika. Katika hii, mtafiti alivaa mavazi ya heshima yaliyoendana na maadili

na itikeli za jamii ya watafitiwa sambamba na kufuata mila na desturi za

mazingira yao.

3.9 Uhalali na Uthabiti wa Matokeo ya Utafiti

Kothari (2009) anaeleza kuwa, uhalali wa utafiti ni hali ya utafiti kuwa na uwezo wa

kupima mambo yaliyotakiwa kupimwa au kutafitiwa. Pia, kwa upande wa uthabiti

anaeleza kuwa ni hali ya utafiti kuweza kutoa matokeo yanayofanana au kuwiana

ikiwa utafiti utafanyika wakati mwingine, mahali pengine au na mtu mwingine.

Hivyo, mtafiti alizingatia uwazi wa malengo ya utafiti ili yaweze kueleweka kwa

urahisi kwa watafitiwa wake. Pia, mtafiti aliwafafanulia watafitiwa wake kuwa

taarifa watakazozitoa zitakuwa ni siri na zitatumika kwa malengo ya utafiti tu. Hii

ilisaidia watafitiwa kutoa taarifa sahihi kwa uhuru zaidi bila kuhofia. Vilevile, mtafiti

alitumia lugha nyepesi isiyoleta mkanganyiko pamoja na kueleza bayana mipaka ya

utafiti huu.

3.10 Changamoto Zilizojitokeza Wakati wa Utafiti na Utatuzi wake

Changamoto mbalimbali zilijitokeza wakati wa kuendesha zoezi la utafiti huu hasa

katika wakati wa kukusanya data. Baadhi ya changamoto hizo ziliweza kupatiwa

Page 45: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

32

ufumbuzi na mtafiti na hatimaye kufanikisha zoezi hili. Changamoto hizo ni kama

vile:

Watafitiwa kusitasita kutoa ushirikiano wao moja kwa moja katika mahojiano na

baadhi yao kukataa kutoa taarifa. Changamoto hii ilitokana na mitazamo hasi ya

baadhi ya watafitiwa kwa sababu jamii haina uelewa wa kina kuhusu umuhimu wa

utafiti unaofanywa katika maeneo yao na kuogopa kwamba huenda kuna mambo

mengine tofauti yanafanywa na mtafiti. Hii ilitokana na ugeni wa mtafiti katika

mazingira yao. Changamoto hii ilitatuliwa baada ya mtafiti kuwafafanulia malengo

ya utafiti na kuwaeleza kuwa taarifa watakazozitoa zitabaki kuwa siri kati ya

mtafitiwa na mtafiti na zitatumika kwa malengo ya utafiti tu

Gharama za kuendesha shughuli za utafiti kuwa juu kuliko makadirio ya bajeti ya

utafiti. Hii ilitokana na ukweli kwamba, gharama hizo zilimhusu mtafiti mwenyewe

kwa kuwa hakuwa na udhamini wowote. Hivyo, kuna wakati ilimuwia vigumu

kusafiri kwenda kukusanya data kwa wakati hivyo alilazimika kusubiri mpaka hali

ya uchumi iwe sawa ndipo asafiri na hivyo ikasababisha kutokukusanya data kwa

wakati aliokusudia.

Kucheleweshwa kwa mchakato wa utoaji vibali vya kukusanya data kutoka katika

taasisi husika. Kuna wakati ambapo mtafiti alicheleweshwa kutokana na sababu za

kimfumo kutokuwa sawa hivyo kusubirishwa mpaka pale mfumo uliporekebishwa.

Tukio hilo lilichukua takribani majuma matatu ambayo hakuwa na budi kusubiria ili

kukamilisha taratibu za kupatiwa kibali cha kukusanya data.

3.11 Muhtasari wa Sura ya Tatu

Sura hii imefafanua kuhusu methodolojia ya utafiti na mchakato mzima uliofanywa

na mtafiti wakati wa kukusanya data. Sura imeelezea usanifu wa utafiti, mkabala wa

utafiti, eneo la utafiti, walengwa wa utafiti na ukusanyaji wa data. Aidha, njia na

zana za ukusanyaji wa data pamoja na mchakato wa ukusanyaji data zimefafanuliwa.

Vipengele vingine vilivyofafanuliwa ni uchanganuzi wa data, itikeli za utafiti, uhalali

na uthabiti wa matokeo ya utafiti. Pia, mtafiti amebainisha changamoto alizokutana

nazo wakati wa ukusanyaji wa data na namna zilivyotatuliwa. Sura inayofuata

inafafanua kuhusu mjadala wa matokeo ya utafiti.

Page 46: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

33

SURA YA NNE

UWASILISHAJI NA MJADALAWAMATOKEO YA UTAFITI

4.1 Utangulizi

Sura hii inajadili matokeo ya utafiti uliolenga kuchunguza falsafa ya Kiafrika katika

semi: mifano kutoka vitendawili vya Kiswahili. Sura imewasilisha data za uwandani

na maktabani pamoja na kufanya mjadala wa matokeo ya utafiti. Uwasilishaji wa

matokeo hayo umegawanywa katika sehemu tatu kulingana na malengo ya utafiti.

Sehemu ya kwanza, inabainisha vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa

kitamaduni. Sehemu ya pili, inajadili namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika

vitendawili vya Kiswahili na sehemu ya tatu ni tathmini ya athari ya falsafa ya

Kiafrika kwa jamii kama inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili.

4.2 Vijenzi vya Falsafa ya Kiafrika katika Muktadha wa Kitamaduni

Sehemu hii inaonesha mjadala kuhusu vijenzi vinavyoijenga falsafa ya Kiafrika

katika muktadha wa kitamaduni. Kupitia mahojiano na watafitiwa, mijadala ya

vikundi lengwa na udurusu wa nyaraka, matokeo ya utafiti yamebainisha kuwa,

falsafa ya Kiafrika hujengwa katika misingi ya kitamaduni. Utafiti ulibainisha kwa

kina baadhi ya mambo wanayoyafanya katika maisha yao ya kila siku ambayo

yanabeba au kuwakilisha utamaduni wao. Mambo hayo ndiyo huijenga falsafa ya

Kiafrika. Nayo ni:

4.2.1 Suala la Umoja na Ushirikiano

Umoja ni dhana inayorejelea hali ya kuunganika na kuwa wamoja katika jamii

(Mlelwa, 2017). Utafiti umebaini kuwa, Waafrika wanaishi kwa umoja na

ushirikiano katika taabu na raha. Faustine (2017) anaeleza kuwa suala la umoja na

ushikamano ni jambo linalotazamwa kwa namna ya pekee na Waafrika. Hii ni kwa

kuwa kwao, umoja ndio msingi wa kuimarisha na kudumisha mahusiano ya jamii

kuanzia katika familia, ukoo hadi jamii nzima. Anamnukuu Wiredu (1980)

anayeeleza kuwa, kwa jamii ya Waafrika, suala la umoja linaanzia katika ngazi za

familia, ukoo na hatimaye jamii nzima. Hivyo, wanaamini kuwa, hakuna jambo

linaweza kufanyika vizuri pasipo kushirikiana na wengine ndio maana wanafanya

kazi zao kwa umoja.

Page 47: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

34

Kupitia mahojiano uwandani, utafiti umebaini kuwa, Waafrika wanaishi kwa

kushirikiana katika kufanya kazi pamoja, kula pamoja na kushirikiana katika kutatua

shida mbalimbali zinazowakumba wanajamii. Kwa mfano, Wanajamii wa wilaya ya

Bukoba ambao ni kiwakilishi cha jamii za Kiafrika huishi kwa kushirikiana katika

shughuli mbalimbali za kijamii. Watafitiwa walieleza baadhi ya mambo ambayo

huibua suala la umoja na ushirikiano kama vile sherehe mbalimbali zinazotokea

katika jamii na shughuli za kitanzia. Hili lilibainishwa na Bw. Rwiza1 anaposema:

Waswahili wana kawaida ya kushirikiana kwa hali na mali. Ikitokeatatizo lolote, jamii huchukulia tatizo hilo kama ni letu sote. Watuhupenda kufanya kazi kwa umoja na hivyo kunaonesha kuwa jamiiinatambua suala la umoja na ushirikiano kuwa ni nguzo ya kuletamaendeleo katika jamii. Kwa mfano watu wanashirikiana katikashughuli za kilimo, ufugaji, uvuvi na hata kusomesha watoto. Hii nikutokana na sababu kuwa ushirikiano unaanza katika ngazi ya familiahadi katika ukoo.

Maelezo katika nukuu hii yanaonesha kuwa wanajamii hufanya kazi kwa umoja,

jambo ambalo linaijenga falsafa ya Kiafrika ya umoja na ushirikiano. Hivyo jamii

inatambua kwamba, bila kuwa na umoja haiwezi kufikia kiwango kikubwa cha

maendeleo yanayotakiwa au kutimiza malengo waliyojiwekea kwa urahisi.

Aidha, mtafitiwa mwingine aliongeza kuwa, suala la kushirikiana katika shida na

raha kuwa si la hiari. Hii inaonesha dhahiri kuwa, kwa Waafrika mtu akipatwa na

msiba watu wote kama sehemu ya jamii hiyo ni lazima kuhudhuria msibani. Mawazo

haya yamefafanuliwa na Johansen2 anayesema:

Kama mwanakijiji ni lazima uende kwenye msiba haijalishi ni nduguau jirani. Watu wote, wake kwa waume, hutakiwa kuwa katika eneo lamsiba na kusaidiana kufanya kazi mbalimbali, kula na kulala hapokwa siku tatu. Mtu wa jamii yao akifiwa ndugu, jamaa, marafiki, nahata majirani huacha shughuli zao na kukusanyika sehemu ya tukiokwa lengo la kuwafariji wafiwa.

1 Bw. Boniface Rwiza ni Mstaafu katika Utumishi wa Umma, Mwalimu wa dini na mtumishi wakiroho wa Parokia ya Bikira Maria Mama Mwenye Heri Jimbo Kuu Katoliki la Bukoba. Mahojiano namtafiti yaliyofanyika tarehe 4.3.2020 kijiji cha Nyamkazi kata ya Kashai.2 Elvis Johansen ni mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari ya Kashai iliyopomanispaa ya Bukoba kata ya Kashai. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 25.2.2020 shuleni hapo.

Page 48: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

35

Nukuu hiyo inathibitisha kuwa, katika misiba ndipo jamii ya Waswahili huonyesha

ushirikiano wa hali ya juu. Dhana hii imejengeka kutokana na kaida za maisha yao

ya kila siku zilizozoeleka katika kutatua matatizo yanayowakumba katika jamii yao.

Kupitia maelezo hayo, utafiti ulibaini kuwa, kwa kufanya hivyo, wanajenga na

kuhamasisha umoja na mshikamano katika jamii. Maelezo haya yanatupa picha halisi

ya namna Waafrika wanavyoishi kwa kushirikiana na kila jambo linalompata mtu

linachukuliwa kama ni jambo lao wote hivyo wanashirikiana katika kulitatua.

Hoja hii inatiwa nguvu na nadharia ya Kisosholojia kupitia msingi wake unaosema

kazi ya fasihi kama taswira ya kijiografia, kimazingira na kiutamaduni ambamo kazi

hiyo imechimbuka kutoka katika jamii husika. Kwa kuwa nadharia ya Kisosholojia

inasisitiza kuhusu kuchunguza matendo ya jamii na kila tendo linalofanyika katika

jamii za Waafrika linakuwa na maana halisi. Kwa hiyo, mambo mbalimbali

yanayotokea katika jamii yanachagiza suala la umoja na ushirikiano na hivyo kuibua

falsafa ya umoja na ushirikiano.

4.2.2 Suala la Maadili katika Jamii

Maadili ni mwenendo mwema, onyo au mafundisho yatolewayo kwa njia ya hadithi

au shairi na yenye nia ya kufundisha mafundisho mazuri (TUKI, 2004). Ni ukweli

usiopingika kuwa jamii yoyote isiyo kuwa na maadili mema ni mfu. Hii inatokana na

ukweli kwamba binadamu ni kiumbe ambaye huhitaji uhuru sana. Hivyo, iwapo

ataachwa afanye mambo kulingana na anavyotaka basi kuna uwezekano mkubwa wa

jamii kutoishi kwa amani. Ili kuwe na namna bora ya kuishi ndani ya jamii, sheria

mbalimbali hutungwa ambazo jamii husika hulazimika kuzifuata. Sheria hizo ndizo

zinaifanya jamii kuishi katika misingi ya maadili. Kaponda (2018) anaeleza kuwa ili

mwanadamu atambulike kuwa na utu sharti atende mambo yanayolingana na misingi

ya kimaadili ya jamii inayomhusu. Iwapo mwanajamii atatenda tofauti na misingi ya

jamii yake, moja kwa moja jamii itamtenga na kumbagua kwa kuwa hafanani na utu.

Matendo hayo ni kama vile; kutokushirikiana na wanajamii wengine katika masuala

muhimu ya kijamii, wizi, chuki, ukatili na mengine yanayofanana na haya.

Naye Chuachua (2016) anathibitisha kuwa, maadili na itikeli ni sehemu ya falsafa ya

Kibantu. Anaeleza kuwa wabantu wana uelewa wa kutosha kuhusu maadili na itikeli.

Maarifa yao kuhusu maadili na itikeli yanajiegemeza zaidi kwenye ontolojia yao.

Page 49: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

36

Mtazamo wao ni kuwa hata kama maadili na itikeli vinasababishwa na kuongozwa

na kani uhai, unadhihirisha kuwa Mbantu anaona kuwa, maisha yake si mali yake

peke yake. Hii ni kutokana na kuwa, kuwapo kwake kunawezekana kwa kuwa

wengine wapo. Kwa hiyo, maisha yake yapo chini ya mamlaka ya Mungu, ambaye ni

chanzo cha kani-uhai. Na uhusianao wake na Mungu unadumishwa na wahenga na

wazee.

Aidha, kupitia mahojiano na watafitiwa, utafiti umebaini kwamba, suala la maadili

linaenda sambamba na utii, adabu na uvumilivu. Mtu asipokuwa na utii hawezi kuwa

na maadili mema. Watoto hufundishwa kutii wakubwa na hivyo kuwafanya wakue

katika maadili yanayofaa. Haya yamebainika pale Bi. Theresa3 anaposema:

Kila jamii inaishi kwa kuzingatia maadili ya jamii. Watoto hufunzwakutii na kuwaheshimu wakubwa wao. Suala la utii linawajengeawatoto kuwa na adabu mbele za wakubwa wao na hivyo inawajengeaunyenyekevu na kutokuwa na kiburi. Kwa namna hiyo, watoto haohukua katika misingi ya maadili mema yanayofaa katika jamii.

Maelezo ya mtafitiwa katika nukuu hapo juu yanathibitisha kuwa, wanajamii

hufanya mambo mbalimbali yanayohusu maadili ambayo kupitia hayo falsafa ya

maadili huibuliwa katika jamii. Mambo hayo ndiyo yanayoijenga falsafa ya maadili

katika jamii. Baadhi ya mambo hayo ni kama vile kuheshimu wakubwa, kutokuwa

na kiburi, kuvumilia katika mambo mbalimbali na kuwa na adabu mbele za wakubwa.

Aidha, watafitiwa walieleza kuwa, chanzo kikubwa cha mmomonyoko wa maadili

katika jamii ni kupata malezi duni, kuiga tabia na desturi zisizofaa, elimu duni na

mikumbo ya marafiki wabaya wasio na tabia nzuri.

Pia, hoja hii inatiwa nguvu na nadharia ya Kisosholojia inayojihusisha na uchunguzi

wa jamii mahsusi na kukieleza kile kinachopatikana katika jamii husika. Hii ni

kutokana na msingi kuwa, fasihi ni taswira ya kimazingira na kiutamaduni

inayochipuzwa kutoka katika jamii husika. Hivyo, Utafiti huu umebaini kuwa,

mambo mbalimbali yanayofanywa katika jamii kama vile kuheshimu wakubwa,

kuwa na adabu na utii na kuwa na uvumilivu ni baadhi ya vitu vinavyojenga suala la

3 Bi. Theresa ni mwanajamii, mzazi na mlezi wa watoto anayeishi wilaya ya Bukoba kata ya Bakoba,mtaa wa Buyekera. Mahojiano yalifanyika tarehe 5.3.2020

Page 50: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

37

maadili katika jamii. Kutokuwa na vitu hivyo basi maaadili hayatakuwepo. Kwa

kufanya hivyo kunaibua falsafa ya umuhimu wa maadili kwa jamii za Kiafrika.

4.2.3 Suala la Uhai na Kifo

Kifo ni kipimo cha fursa ya kuwapo au kutokuwapo duniani (Chuachua, 2016).

Maneno haya yanamaanisha kuwa, kifo huondoa urazini na kumfanya mtu

kutokuonekana katika uso wa dunia baada ya kukata kwa pumzi ambayo huashiria

uhai wa mtu. Masuala yanayohusu uhai na kifo yameweza kubainika kupitia

matokeo ya utafiti huu. Mtafiti amebaini kwamba, maisha ya mwanadamu yapo

katika mambo mawili yaani uhai na kifo na suala la kifo linaogopwa na kila mtu

katika jamii. Suala hili linaibua imani kuwa mwanadamu huzaliwa, huishi na kisha

hufariki.

Kimsingi hakuna kiumbe hai ambacho huishi milele bila kufa. Temples (1959)

anaeleza kuwa, fikra za Waafrika zimetawaliwa na vitu viwili ambavyo ni uhai na

kifo. Kwa mawazo yake, Waafrika wanaamini kuwa mtu akiumwa nguvu za uhai

zinapungua hivyo anaamini atakufa. Naye Faustine (2017) anabainisha kuwa, suala

la uhai na kifo ni mambo yanayowashughulisha sana Waafrika. Wafrika wanaamini

kuwa kifo kipo na ni matokeo ya laana inayotokana na kupungua kwa nguvu-hai.

Wakati mwingine kifo kinahusishwa na imani za kichawi. Kupitia mjadala wa

vikundi lengwa na mahojiano, mtafiti amebaini kwamba, baadhi ya mambo

yanayojenga falsafa ya Kiafrika kuhusu kifo yanajitokeza katika mambo mbalimbali.

Mambo hayo ni kama vile kuwa na hofu juu ya kuumwa au kufa. Hili limebainika

katika mahojiano na Bw. Kigoye4 anapoeleza kuwa:

Kama ingekuwa inawezekana kwamba mtu anakiona kifo kablahakijamfika na kukimbia basi watu wangekuwa wanakimbia kifokisiwafikie. Hii ni kwa sababu kila mtu anapenda aendelee kuishi. Piamtu akiwa anaumwa anakuwa na huzuni na kukosa furaha kwasababu anaogopa asije akafa. Watu wanaokufa hatujui huwawanaenda wapi. Kwa hiyo, mtu akiumwa anaogopa itakuwaje kamaakifa, familia yake ataiacha vipi na hata mali alizozichuma ataziachapia.

4 Bw. Mwesigwa Kigoye ni mwanajamii na mtaalamu wa masuala ya mila za wahaya wilayaniBukoba. Mahojiano na mtafiti yaliyofanyika tarehe 4.3.2020 mtaa wa Hamgembe Nyangoye.

Page 51: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

38

Mtafitiwa alipoulizwa na mtafiti kuwa, yawezekana watu wanaogopaa kufa kwa

kuhofia wanaowaacha au mali zao, mtafitiwa alionekana kutokuwa na uhakika sana

na jambo hilo. Maelezo yake yalithibitisha kuwa hofu yao juu ya kifo ni kwa sababu

wanapenda kuishi maisha marefu wakiwa na wapendwa wao. Hivyo, suala hili

linaijenga falsafa ya Kiafrika kuwa kuna kufa na kifo hakiepukiki kwa kila mtu.

Ni dhahiri kwamba, masuala yanayohusu kifo yanawashughulisha wanajamii wote.

Hata hivyo, kifo kinapotokea katika jamii taratibu fulani hufuatwa ikiwa ni pamoja

na suala la kuzika. Suala la mazishi ikiwa ni shughuli za kitanzia pia linaijenga

falsafa ya Waafrika ya uduara. Hii inatokana na sababu kuwa, watu wanapokuwa

katika msiba taratibu za mazishi hufanywa katika sura ya duara. Haya yalibainika

kupitia majadiliano pale Marwa5 alipoeleza kuwa:

Jamii ya watu wa Bukoba wanapofikwa na msiba hufanya taratibu zakuaga mwili wa marehemu kabla ya kuzika. Shughuli hiyo hufanywawakati jeneza la mwili wa marehemu likiwa limewekwa katikati nawatu wote hujipanga katika mzunguko unaotengeneza duarakulizunguka jeneza hilo na wengine kuendelea kupita kuaga mwilihuo.

Maelezo katika nukuu hiyo yanaonesha namna usimamaji wa kulizunguka jeneza

wakati wa kuzika unajenga falsafa ya uduara kama mojawapo ya falsafa ya Kiafrika.

Utafiti ulibaini kuwa, taratibu za kuaga zikikamilika suala la kuzika hufuatia ambalo

pia hufanyika katika sura ya duara kwa kulizunguka kaburi wakati shughuli za

kuzika zikiendelea. Kwa jumla, ushahidi uliopatikana katika mahojiano na

majadiliano ya vikundi umedhihirisha kwamba, suala la kifo linaogopwa sana na

wanajamii kwa kuamini kuwa kifo hakiepukiki kwa kila mtu. Hivyo, suala la uhai na

kifo linaibua imani kuhusu kifo na falsafa ya uduara.

4.2.4 Dhana ya Uduara

Uduara ni hali ya kitu au mambo kuwa au kufanyika katika sura ya duara au

mviringo (Duwe, 2016). Utafiti umebaini kuwa, dhana ya uduara kwa Waafrika ni

mojawapo ya msingi wa kuyaendesha maisha yao na kuutafakari ulimwengu. Maisha

ya Waafrika yametawaliwa na dhana ya uduara. Duwe (2016) anafafanua kuwa,

uduara ni moja ya mambo yanayodhihirisha kuwapo kwa falsafa ya Kiafrika kwa

5 Alexander Marwa ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Kashai iliyopomanispaa ya Bukoba kata ya Kashai. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 25.2.2020 shuleni hapo.

Page 52: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

39

sababu katika maisha yao huthamini na kupenda vitu vilivyo katika sura ya duara.

Uduara ulianza sambamba na fasihi simulizi ya jamii ya Waafrika kwa sababu

katika maisha yao walishirikiana katika masuala mbalimbali kwa suara ya duara.

Aidha, Faustine (2017) anabainisha miktadha miwili ambayo kwayo dhana ya uduara

inajitokeza. Muktadha wa kwanza ni ule unaoiangalia dhana ya uduara kama namna

ya kutafsiri maarifa yanayopatikana ndani ya jamii na kuujengea maana ulimwengu

wao. Muktadha wa pili ni ule unaoitazama dhana ya uduara kama dhana ya kiujumi.

Akimnukuu Mbiti (2010) anaeleza kuwa:

Dhana ya uduara imekuwa ikitumika kama alama ya kuwakokusikokuwa na mwisho ambako kunaashiria mwendelezo wa jambo,kitu au maisha. Kwa Waafrika, mtazamo kuhusu dhana ya uduaraumekuwa ukijidhihirisha katika mambo mbalimbali kama vile namnawanavyoutazama wakati, ufanyaji wa matambiko, kazi zao za kisanaana utengenezaji wa vitu vya nyumbani.

Maelezo katika nukuu hiyo yanabainisha kuwa, kwa Waafrika dhana ya uduara

inajitokeza katika mambo mbalimbali. Hivyo, inathibitisha kuwa Waafrika

wanafanya vitu mbalimbali kwa uduara na kwa kufanya hivyo kunaibua falsafa ya

uduara. Aidha, katika muktadha wa kiujumi, uduara unatazamwa kama kigezo cha

kupima uzuri au ubaya wa kitu. Kuhusu hili, Faustine (k.h.j) anafafanua kuwa,

Waafrika wanaamini kuwa uzuri wa kitu umo katika hali ya uduara. Ndiyo maana,

kwa kiasi kikubwa, mazingira yao yametawaliwa na vitu vyenye asili ya uduara.

Kwa hiyo, katika duara ndimo unamopatikana uzuri.

Vilevile, kupitia mahojiano uwandani, watafitiwa walifafanua kuhusu vijenzi vya

falsafa ya Kiafrika ya uduara katika jamii kwa jumla. Imebainika kupitia mahojiano

hayo kuwa, watu wa wilaya ya Bukoba ambao ni kiwakilishi cha jamii za Kiafrika,

hufanya mambo mbalimbali kwa uduara. Mambo hayo ndiyo yanayoijenga falsafa ya

uduara. Mambo hayo ni pamoja na vitu wanavyovitengeneza kwa ajili ya matumizi

ya nyumbani kama vile vigoda, nyungo, mapambo yao ya ndani na samani. Aidha,

uduara unajitokeza katika mkao wa kula kwani wanapokula, huwa wamekaa kwa

Page 53: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

40

kutengeneza mduara kuzunguka chakula ambacho huwa kimewekwa katikati yao.

Madai haya yanaelezwa na Bi. Kokwenda6 anayesema kuwa:

Mkao wa kula wa watu wa jamii ya Wahaya ni ule unaotengenezaumbo la duara. Iwe ni nyumbani au katika misiba watu wa jamii yaWahaya hupenda kula huku wakiwa wamekizunguka chakulaambacho hupakuliwa kwenye sinia au sahani kubwa kulingana nawatu watakaoshiriki katika kundi hilo. Chakula kikishapakuliwamboga huwekwa juu ya chakula katikati na hapo watu hukaakuzunguka chakula na kila mtu humega upande wake. Suala hililina maana kubwa kwa sababu lilianza zamani mpaka sasa badolinaendelezwa. Wazee wetu walilianzisha ili kuwafunza watotokuwa na umoja na kuacha tabia ya ubinafsi.”

Aidha, mtafitiwa mwingine ameshadadia hoja hii kwa kusema kwamba, mambo

mengi wanayoyafanya yanafanyika katika umbo la duara. Haya yamethibitika katika

majadiliano na watafitiwa pale Emilian7 anaposema:

Suala la uduara kwetu sisi ni la msingi sana. Katika jamii yetu hatatunapocheza ngoma zetu mara zote wachezaji hutengeneza duarakuwazunguka wale wanaopiga ngoma ambao wanakuwa katikati.Hapo ndipo ngoma hukolea na huchezwa huku wakizunguka. Pia,hata wakati wa mazishi, watu hulizunguka kaburi ili kuwa naushirikiano katika kuzika.

Kutokana na maelezo katika nukuu hizo ni ithibati kuwa, masuala haya yanayohusu

mkao wa kula, uchezaji ngoma na hata mazishi, hufanyika katika sura ya duara na

kuijenga falsafa ya uduara. Aidha, mawazo yanayofanana na haya yameelezwa na

Temples (1957) anayesema kuwa, maisha ya Waafrika yametawaliwa na dhana ya

uzuri unaopatikana katika sura ya duara. Falsafa ya uduara pia, inadhihirika kupitia

vitu mbalimbali wanavyovitumia katika shughuli zao za kila siku. Vitu kama vile

vigoda, viti, meza, ungo na sinia vina maumbo ya duara. Kwa hiyo, kitendo cha

kukaa pamoja na kushirikiana kula katika sahani moja kwa kukizunguka chakula

kilichowekwa katikati kunaijenga falsafa ya uduara

6 Bi. Olivia Kokwenda ni mwanajamii na mwalimu wa dini anayefundisha watoto katika Kigango chaBuyekera Jimbo kuu Katoliki la Bukoba. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe 3.3.2020 mtaa waBuyekera kata ya Bakoba.7 Frank Emilian ni mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Kashai iliyopo manispaaya Bukoba kata ya Kashai. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 25.2.2020 shuleni hapo.

Page 54: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

41

4.2.5 Suala la Imani katika Mungu na Mizimu

Tafsiri ya Ki-biblia ya imani inapatikana katika Waebrania11.1. Mtume Paulo

anasema , “imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo

yasiyoonekana.” Kwa hiyo, imani ni jambo ambalo haliwezi kuthibitika kisayansi.

Matokeo ya utafiti huu yamebainisha kuwa, Waafrika wanaamini katika nguvu

zinazotokana na Mungu na mizimu. Mbiti (1969) anabainisha kuwa, Waafrika

walikuwa na wanayo dini ambayo wameirithi kutoka katika vizazi vilivyotangulia.

Chuachua (2016) anafafanua mawazo ya Idowu (1966) ambaye anamtaja Lang

akibainisha dhana ya umosi katika imani ya Waafrika kwa kusema, “African

Traditional Religion is a monotheistic religion in which God is believed to be

Eternal” (uk 92). Hapa ana maana kwamba, dini ya kiasili ya Mwafrika inaamini

katika umosi ambapo Mungu anaaminika kuwa ni wa milele. Mawazo haya

yanaonesha kuwa, Waafrika wanaamini kuna nguvu yenye uwezo mkubwa kuliko

nguvu zote; na kwamba nguvu hiyo ni moja na ambayo husababisha kuwapo kwa

kila kitu. Chuachua (2016) anafafanua kuwa nguvu hiyo ni Mungu ambaye ni

ukamilisho wa ubinadamu; na kuwapo kwa mtu kunawezeshwa na Mungu ambaye ni

muumba wa roho na ulimwengu. Mungu ndiye anayetawala huombwa na

kukumbukwa na wanadamu katika shida na raha. Pia, Temples (1959) anatueleza

kuwa:

The Bantu speak of God himself as “the stong one,” he who possessesforce in himself. He is also the source of the source of every creature.(uk. 22)

Wabantu wanamwongelea Mungu kama “mwenye nguvu,” yeyeanayemiliki kani ndani yake. Pia Mungu ni chanzo cha kani kwa kilakiumbe (Tafsiri ya mtafiti).

Maelezo ya mtaalamu huyu yanathibitisha kuwa, Mungu ndiye mwenye nguvu

kuliko kitu kingine na ni chanzo cha kani kwa viumbe wengine. Maelezo haya

yanatupatia dhana kuwa Mungu ndiye mkuu kuliko viumbe wengine.

Kupitia mahojiano uwandani, utafiti umebaini kuwa, watu wengi wa jamii ya

Waafrika ni waabudu au wacha Mungu. Hii ni kutokana na sababu kuwa wanaamini

yupo Mungu au Allah mmoja tu mwenye nguvu na awezaye kutatua matatizo

mbalimbali yanayowakumba wanadamu. Haya yalithibitika kutokana na uwepo wa

Page 55: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

42

madhehebu mbalimbali katika jamii ya watu waishio wilaya ya Bukoba. Watafitiwa

walieleza kuwa, katika jamii hiyo siku za ibada watu hukusanyika katika makanisa

yao na misikitini kwa lengo la kuabudu Mungu. Kwa hiyo, imani ya Waafrika

imejengwa katika misingi miwili ambayo ni Mungu au Allah na mizimu. Katika

kuthibitisha hili, Bi. Abdallah8 anaeleza kuwa:

Jamii ya watu waishio Bukoba ina mchanganyiko wa dini namadhehebu mbalimbali. Wote wanamwamini na kumwabudu Mungummoja lakini tofauti ni za kimatazamo. Kuna wanaosali Jumamosi(wasabato) na makanisa mengi ya Jumapili. Mifano kuna makanisa yaKKKT, Roman Catholic, Anglican, Pentekoste (PAG), TanzaniaAssembles of God (TAG), Kanisa la Wokovu, na makanisa yamaombezi. Kwa upande wa Waislamu pia si haba kutokana na wingiwa misikiti katika kila kata na vijiji. Kama ilivyo kwa waamini wakidini wapatapo matatizo huenda mbele za Mungu au Allah nakumuomba ili aweze kuwatatulia matatizo yao hivyo hivyo pia kwaupande wa waamini wa miungu nao wapatapo matatizo huenda kwawaganga wa kienyeji kuomba mizimu ya mababu na mabibi zao.

Maelezo katika nukuu hapo juu yanathibitisha kuwa, Waafrika wanaamini Mungu na

mizimu. Wapo wanaoamini kuwa, tatizo likitokea katika jamii na likashindikana

kupatiwa majibu basi hupelekwa kwa wataalamu ambako huko hutatuliwa kwa

nguvu za mizimu ya mababu na mabibi zao. Kwa hiyo, kitendo cha kwenda kuabudu

katika makanisa na misikitini pamoja na kwenda kwa waganga wa kienyeji katika

vilingeni kunaijenga falsafa ya Kiafrika ya imani katika Mungu na mizimu. Hii ni

kwa kuamini kuwa, watu hao ndio wenye uwezo wa kutatua matatizo mbalimbali

yanayotokea katika jamii.

Kwa kuhitimisha hoja hii, tunaweza kusema kuwa, ni dhahiri kuwa watu wa jamii za

Waafrika imani yao imekitwa katika masuala ya Mungu na mizimu. Hii inajenga

falsafa ya imani katika Mungu au mizimu na kuwa Mungu ndiye mwenye uweza

wote. Mambo haya kwa jumla yanaijenga falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa

kiutamaduni. Hii inatokanna na nadharia ya Kisosholojia inayoona kuwa, kazi ya

fasihi kama taswira ya kijiografia, kiutamaduni na kimazingira ambayo imechimbuka

8 Bi Farida Abdallah ni mwanajamii na mwalimu mstaafu wa Shule ya Qudus Nursery and PrimarySchool iliyopo manispaa ya Bukoba. Mahojiano na mtafiti yaliyofanyika tarehe 4.3.2020 mtaa waNational housing- Kashai.

Page 56: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

43

kutoka katika jami husika. Kwa hiyo, inaweka mkazo wa fasihi kuendana na

miktadha ya jamii husika kijiografia na kiutamaduni.

4.2.6 Suala la Uchawi na Ushirikina

Chuachua (2016: 248) anaufasili uchawi kuwa, ni dhana ya kimetafizikia9 na wakati

mwingine kiontolojia10 kwa kuwa inafungamana na kuwapo kwa mtu. Nguvu za

kichawi ni kani zinazoweza kuleta athari kutoka kwa mchawi hadi kwa

aliyekusudiwa akiwa umbali wowote ule. Masuala yanayohusu uchawi yamekuwa

yakijitokeza katika kila jamii kwa Waafrika. Mtazamo kuhusu kuwapo kwa uchawi

katika jamii za Kiafrika umekuwa ukijidhihirisha katika maisha yao ya kila siku

kupitia tanzu mbalimbali za fasihi. Faustine (2017) anaeleza kuwa, Waafrika

wanaamini mchawi huweza kusabaisha kifo cha mtu katika hali ya kimiujiza pasipo

yeye kugundulika ni kwa namna gani amefanya jambo hilo. Jambo baya linapotokea

kama vile kifo, kushuka kwa mtu kiuchumi, na hali mbaya ya kimaisha mara nyingi

ni vigumu kwa wanajamii kuamini kuwa limetokana na sababu mbalimbali kama vile

za kimazingira, bali hulihusisha na imani za kichawi. Akimnukuu Mbiti (2010)

anasema:

It is believed too, that a witch can cause harm by looking ata a personor speaking to him words intended to inflict harm on him. All theseare the ways in which evil magic and witchcraft are believed tofunction. In some cases it is even held that powerful magic can make aperson change into ana animal or bird which then goes to attack thevictim (uk 167).

Inasadikika pia kwamba mchawi ana uwezo wa kumdhuru mtu kwakumwangalia au kumnenea maneno yatakayomdhuru. Hizi ndizo njiaambazo uchawi unaaminika kufanya kazi. Katika mazingira mengine,inasadikiwa pia kwamba, nguvu za kimiujiza zinaweza kumbadilishamtu akawa mnyama au ndege ambaye huenda kumdhuru mtumwingine (tafsiri ya mtafiti).

Maelezo yaliyo katika nukuu hapo juu yanathibitisha uwepo wa uchawi katika jamii

za Kiafrika na athari za uchawi kama vile kusababisha vifo na kuwadhuru watu

9Metafizikia ni tawi la falsafa linalotumika kutafakari kuhusu mambo na matukio ya kiulimwengu ilikuyabainisha na kuyatofautisha yale halisi na yasiyokuwa halisi (Chuachua, 2016)10 Ontolojia ni taaluma ya falsafa inayoshughulikia asili ya kuwapo au kuishi. Pia hushughulikiakategoria za kuwapo pamoja na mahusiano yake (Chuachua, 2016)

Page 57: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

44

wengine. Aidha, mawazo yanayofanana na haya yanaelezwa na Manala (2004)

anayesema:

In the African’s world of thought, when ill-health, misfortune,accident or death occuers, traditional Africans will immeadiatelyprobe witch crafts as the likely cause (uk. 1501).

Katika mtazamo wa Waafrika, ikitokea vitu kama magonjwa, bahatimbaya, ajali au kifo, Waafrika kwa haraka watamwona mchawi kuwandiye aliyesababisha (Tafsiri ya mtafiti).

Aidha, kupitia mahojiano na watafitiwa, utafiti huu umebaini kuwa, jamii ya watu wa

Bukoba inaamini kuwa uchawi upo na wachawi wapo ingawa ni kwa kiasi kidogo.

Hii ni kutokana na sababu kuwa baada ya kuingia kwa dini mbalimbali watu wengi

waliacha shughuli za kichawi na kuanza kumwabudu Mungu. Pia, ilielezwa kuwa

wachawi kwa sasa hawaogopwi na hawana nguvu ya kudhuru watu kama ilivyokuwa

zamani. Akieleza kuhusu suala hili Bw. Jonas11 anasema:

Katika masuala ya dini watu wameitikia sana ndio maana imetusaidiakatika kufanya njama za kuwahujumu wachawi. Uchawi katika jamiiyetu upo lakini umefifishwa sana na dini kutokana na sababu kuwawatu wengi wanasali sana wachawi wamekuwa hawana nguvu zakudhuru watu kama ilivyokuwa zamani.

Kupitia nukuu hiyo, tunapata ushahidi kuwa, suala la uchawi katika jamii za

Waafrika bado lipo japo kwa sasa wachawi wamepungua kwa kiasi kikubwa. Hata

hivyo, suala la uchawi linashabihiana na suala la uganga ambapo baadhi ya

wanajamii wanaamini kuwa mchawi ni mtu anayeloga na mtu aliyelogwa anatibiwa

na mganga (Samwel, 2015). Naye Chuachua (2016) anafafanua zaidi kuwa, mganga

ndiye anayeweza kutibu uchawi. Uganga na uchawi ni mambo yanayokwenda

pamoja. Mchawi kazi yake ni kuharibu na akiharibu hawezi kutengeneza. Mganga ni

mjuzi zaidi ya mchawi. Mganga anaweza kuutoa uchawi. Aidha, data za uwandani

kupitia mahojiano zinathibitisha jambo hili pale Bi. Kayanga12 anaposema:

11 Bw. Philbert Jonas ni mwanajamii na mtumishi wa kiroho katika Taasisi ya Adolph KolpingSocieties of Tanzania Jimbo Kuu la Katoliki Bukoba. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe2.3.2020 mtaa wa Kamizilente- Rwamishenye.12 Bi. Salma Kayanga ni mama wa familia na Afisa Afya ofisi ya Kata Kibeta. Mahojiano na mtafitiyalifanyika tarehe 5.3.2020 ofisini kwake.

Page 58: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

45

Kila familia inapitia changamoto mbalimbali ambazo zinawezakushindwa kupatiwa majibu. Kwa mfano mtu akiumwa muda mrefuna ikashindikana kupona kwa tiba za kitabibu watu hufikiria kuwahuenda mtu huyo amelogwa na hivyo hutafutwa mganga wa kienyeji(mtaalamu) ili aweze kumtibia. (Tafsiri ya msisitizo kwenye mabanoni ya mtafiti).

Maelezo yaliyo katika nukuu hiyo yanathibitisha namna ambavyo Waafrika

wanaamini katika masuala yanayohusu uchawi. Pia mtu aliyelogwa na mchawi

anaweza kupona kwa kupatiwa tiba na mganga wa kienyeji.

Aidha, tunaishadadia hoja hii kwa kutumia nadharia ya Kisosholojia kupitia msingi

wake unaosema kazi ya fasihi kama taswira ya kijiografia, kimazingira na

kiutamaduni ambamo kazi hiyo imechimbuka kutoka katika jamii husika. Msingi huu

unahusiana moja kwa moja na lengo letu kwani kipengele hiki kimejikita katika

kubainisha vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa utamaduni wa jamii

za Kiafrika ambavyo vimetokana na fasihi ya Waafrika. Katika kuhitimisha

kipengele hiki kwa jumla tunaweza kusema kuwa, mambo yanayohusu uchawi kama

vile kubadilisha maumbo ya mtu kuwa mnyama au ndege na kuloga ndiyo

yanaijenga falsafa ya Kiafrika ya “uchawi na ushirikina”.

4.2.7 Dhana ya Ndoa na Uzazi

Dhana ya uzazi kwa Mwafrika kama inavyoelezwa na Faustine (2017) imekitwa

katika mambo makuu manne. Jambo la kwanza Waafrika wanautazama uzazi kama

njia ya kuwapo kwa mtu. Pili, uzazi unatazamwa kama njia pekee ya kuviunganisha

vizazi vilivyopo na visivyokuwapo. Tatu, uzazi hutazamwa kama kigezo muhimu

kinachoashiria uimara wa ndoa. Nne, uzazi unatazamwa kama nyenzo ya ujenzi wa

ukoo wenye nguvu, heshima na thamani. Kitendo cha mke au mume kuwa na watoto

kinatazamwa kama njia pekee ya kuukuza na kuuendeleza ukoo. Mlelwa (2017)

anabainisha mawazo kuwa, ndoa ni jambo la msingi sana na ni jambo la heshima

kwa Waafrika. Hii ni kutokana na sababu kuwa wanaamini kuwa kupitia ndoa

familia inaweza kujengwa na hivyo kupanua ukoo. Jambo hili linabainika pale

anaposema:

Ufahari wa Waafrika unatokana na kuoa au kuolewa. Mtu anapokuwahajaoa au kuolewa anaonekana kuwa ana upungufu fulani katika

Page 59: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

46

maumbile yake. Lakini ufahari huo huongezeka pale mtu anapozaawatoto.

Maelezo yanayotolewa na mtaalamu huyu yanabainisha wazi kuwa, kwa Waafrika

suala la ndoa na uzazi linapewa heshima na ni jambo la ufahari. Pia, suala la ndoa

linaenda sambamba na kuzaa kwa mwanamke ambapo mwanamke anayeolewa na

asizae haonekani kuwa na thamani sawa na yule anayezaa. Mawazo haya

yanashabihiana na yale ya Faustine (2017) anayeeleza kuwa, furaha ya ndoa

inakamilishwa na uwezo wa wanandoa hao kupata watoto. Wanandoa wasiobahatika

kupata watoto hawathaminiwi katika jamii na mara nyingi ndoa zao hazidumu.

Mimba ni kiashiria cha uimara wa ndoa. Akimnukuu mbiti (2011) anasema kuwa:

In some African societies, marriage is not fully recognized until thewife has given birth. First pregnant becomes, therefore, the final sealof marriage, the sign of complete intergration of the woman into herhusband’s family and kinship circle (uk 110).

Katika baadhi ya jamii za Waafrika, ndoa haitambuliki kikamilifumpaka pale mke anapopata mtoto. Ujauzito wa kwanza, kwa hiyo,ndiyo kihalalisho cha mwisho cha ndoa, ishara ya kuingizwakikamilifu kwa mwanamke katika familia ya mumewe na jamii yaukoo wake (Tafsiri ya mtafiti).

Maelezo ya mtaalamu huyo yanadhihirisha kuhusu umuhimu wa watoto katika

familia za Waafrika. Aidha, kupitia data za uwandani, utafiti ulibaini kuwa, ndoa ni

kipengele muhimu katika kujenga familia na hivyo hujenga falsafa ya umuhimu wa

uzazi na ulezi ambayo inajidhihirisha kupitia suala la ndoa na mahusiano. Jambo hilo

lilithibitika pale Bi. Mnyambo13 anaposema kuwa:

Kwa upande wa binti anapoolewa hutolewa posa na kulipiwa mahari.Kisha hufanyiwa sherehe ya kuagwa mjubulo14 (kapu la mama) nahatimaye sherehe ya harusi. Sherehe za mjubulo huandaliwa nawanawake na huhusisha wanawake katika kumfunda binti anayeolewanamna ya kwenda kuishi na mume na kukabiliana na changamoto zandoa. Pindi mwanamke huyo anapoenda ukweni anatarajiwa kumzalia

13 Bi. Schola Mnyambo ni mwanajamii, mama wa familia na mjasiriamali mdogo wa wilaya yaBukoba. Mahojiano kati yake na mtafiti yalifanyika tarehe 6.3.2020 mtaa wa Kamagera- Kibeta.

14 Mjubulo ni sherehe za kumuaga binti anapoolewa. Maelezo yaliyotolewa katika mahojiano namtafitiwa 6.3.2020.

Page 60: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

47

mwanamme watoto. Mwanamke anayezaa hupendwa sana na wakwezake ukilinganisha na yule asiyezaa. Katika jamii mwanamkealiyeolewa na asizae hudharauliwa na hata kusemwa na ndugu wamwanaume kuwa hajailetea faida familia yao kwa sababu hajazaa(Tafsiri katika mabano ni ya mtafiti).

Maelezo katika nukuu hiyo hapo juu yanathibitisha namna ilivyo muhimu kwa

Waafrika kuhusun kuzaa watoto kama kiashiria cha ukamilifu wa ndoa za Waafrika.

Kwa kuzingatia msingi ya nadharia ya Kisosholojia unaosisitiza kuwa fasihi ni kama

taswira ya kijiografia, kiutamaduni na kimazingira ambayo imechimbuka kutoka

katika jamii husika ina maana kuwa fasihi ina akisi kile kinachotendeka katika jamii

katika nyanja mbalimbali. Hivyo, matokeo ua utafiti huu yamebainisha kuwa,

masuala yahusuyo ndoa na mahusiano yamekuwa yakipewa kipaumbele na umuhimu

mkubwa kwa jamii za Kiafrika na ndio maana tukio lenyewe la harusi na mijubulo

hufanywa kwa shamra shamra nyingi. Kwa Waafrika ni suala la heshima kwa mtoto

kuoa au kuolewa kwa hivyo masuala hayo hupewa uzito kwa kiasi fulani.

Kwa hiyo, masuala yahusuyo ndoa kama kijenzi cha falsafa ya Kiafrika ya uzazi na

ulezi huonekana kuwa na umuhimu kwa Waafrika. Jambo hili linatokana na sababu

kuwa, kwa Waafrika ndoa ni suala la muhimu na sehemu ya kumtoa mtu katika utoto

kuingia utu uzima. Hii inathibitika katika jamii ambapo mtu asiyeolewa au kuoa

haheshimiwi katika sawa na mtu aliyeoa au kuolewa. Na pia mtu asiye na uwezo wa

kupata watoto haheshimiwi kama yule anayezaa. Hivyo kupitia maelezo hayo

tunaweza kusema kuwa, ndoa na familia kwa Waafrika ni mojawapo ya jambo

linaloijenga falsafa ya Waafrika kuhusu umuhimu wa uzazi na ulezi.

4.3 Falsafa ya Kiafrika katika Vitendawili vya Kiswahili

Ni dhahiri kuwa falsafa ya Kiafrika imekuwa ikisawiriwa katika tanzu mbalimbali za

fasihi simulizi ya Kiafrika. Kama nadharia ya Kisosholojia inavyosisitiza kuwa,

fasihi haiwezi kujitenga na jamii ambayo kwayo imechipuzwa. Hivyo, mambo

mbalimbali yanayojitokeza katika jamii husawiriwa ndani yake. Hii ina maana kuwa,

fasihi inasawiri matendo ya jamii na kuonesha uhalisia wake kwa jamii. Utafiti huu

umebaini falsafa mbalimbali zinazojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili.

Sehemu hii inajadili kwa kina namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika

vitendawili vya Kiswahili. Miongoni mwa falsafa zinazosawiriwa katika vitendawili

vya Kiswahili ni kama zifuatazo:

Page 61: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

48

4.3.1 Falsafa ya Umoja na Ushirikiano

Suala la umoja na ushirikiano ni miongoni mwa mambo yanayozingatiwa katika

jamii za Waafrika. Utafiti huu umebaini kuwa, Waafrika wanaamini kuwa umoja na

ushirikiano ni nguzo katika kufanikisha shughuli mbalimbali. Wanaamini kuwa

hakuna jambo linaweza kufanyika vizuri pasipo kushirikiana na wengine. Mitazamo

yao imekitwa katika imani kuwa, ushirikiano unajenga undugu na katika umoja

hakuna ubinafsi. Kwa hiyo, ushirikiano ndiyo nguzo ya kuimarisha mahusiano

kuanzia katika ngazi ya kifamilia hadi kwa jamii nzima kwa jumla. Kwa mfano suala

la umoja na mshikamano linadhihirika pia kupitia vitendawili mbalimbali vya

Kiswahili. Katika mjadala wa vikundi lengwa, Godifrey15 alitega kitendawili

ambacho kinasawiri suala la umoja na mshikamano. Nacho kinasema:

a) Kitendawili: Huyu kambeba huyu na huyu kambeba huyu, huyu kambeba

huyu na huyu kambeba huyu.

Jibu: Ardhi imebeba maji, maji yamebeba meli na meli imebeba watu.

(Chanzo: Uwandani katika mjadala wa vikundi).

Katika kitendawili hiki tumebaini uwepo wa falsafa ya Kiafrika ya umoja na

mshikamano. Falsafa hii inasisitiza suala la umoja na kutegemeana. Kupitia

kitendawili hiki jamii inapata funzo la namna umoja na mshikamano unavyoweza

kufanikisha mambo mbalimbali. Ushirikiano huo utarahisisha kazi hivyo kufikia

mafanikio yaliyokusudiwa kwa muda mfupi. Katika falsafa iliyotumika katika

kitendawili hiki tunaona mnyororo wa utendaji kazi kwa kushirikiana toka upande

mmoja kwenda upande mwingine. Mawazo haya yanabainishwa na baadhi ya

watafitiwa waliotoa mitazamo yao kuhusu umuhimu wa umoja na mshikamano kama

inavyojitokeza katika kitendawili hapo juu. Kwa mfano Bw. Kazaula16 akifafanua

kuhusu kitendawili hiki anasema:

Kutokana na hali ya umaskini tulionao, umoja unaonekana kamanguzo ya kutatua matatizo mbalimbali yanayowakumba wanajamii.Watu wanalazimika kushirikiana katika matatizo mbalimbali ili

15 Belina Godfrey ni mwanafunzi wa shule ya msingi Katerero iliyopo halmashauri ya wilaya yaBukoba kata ya Kyeitema. Majadiliano kati ya mtafiti na watafitiwa yalifanyika tarehe 26.2.2020shuleni hapo.16 Bw. Abel Kazaula ni Afisa Utamaduni wa Halmashauri ya wilaya ya Bukoba. Mahojiano na mtafitiyalifanyika tarehe 2.3.2020 katika ofisi za Halmashauri zilizopo Bukoba vijijini kata ya Kemondo.

Page 62: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

49

kufanya wepesi wa kutatua matatizo hayo. Wenyeji wa wilaya yaBukoba ni wakulima, wavuvi na wafugaji. Hivyo katika kufanyashughuli hizo za maendeleo hufanya kwa pamoja na kwa umoja.Ndiyo maana kitendawili hicho kimebeba dhana ya kubebana kwamaana ya kusaidiana. Kwa kufanya hivyo inarahisisha kumaliza kazikubwa kwa muda mfupi.

Maelezo katika nukuu hapo juu yanathibitisha kuwa, suala la umoja na ushirikiano

kama linavyojitokeza katika kitendawili hicho, ni nyenzo katika kutatua matatizo

mbalimbali. Aidha, inasaidia katika kufanikisha jambo ambalo yawezekana

lisingewezekana pasipo ushirikiano. Hii inadhihirisha kuwa mtazamo wa Waafrika

kuhusu ushirikiano umejikita katika imani kuwa jamii inaposhirikiana huondoa

madhaifu ya upande mwingine hivyo kufikia mafanikio kwa haraka. Kitendawili

kingine kinachosawiri falsafa ya umoja na ushirikiano kinasema:

b) Kitendawili: Hufanya kazi daima wakiwa watatu.

Jibu: Mafiga.

(Chanzo: Salla, 2014).

Kitendawili hapo juu kinadhihirisha falsafa ya Kiafrika juu ya umoja na ushirikiano

ndani ya jamii. Akifafanua kuhusu kitendawili hiki, Bw. Rwiza17 (k.h.j) katika

mahojiano alieleza kuwa, “Waafrika wanaamini kuwa mtu hawezi kukamilika akiwa

peke yake bali ukamilifu wake unategemea uwepo wa watu wengine ndio maana

kitendawili hiki kinasema hufanya kazi wakiwa watatu”. Ufafanuzi wa mtaalamu

huyu unatubainishia kuwa, mitazamo ya Waafrika kuhusu falsafa hii imekitwa katika

imani kuwa, ushirikiano ndiyo chachu ya kuyafikia maendeleo yanayotakiwa katika

jamii kwa haraka. Pia, mtafitiwa mwingine akisisitiza kuhusu umuhimu wa

ushirikiano kama unavyojitokeza katika kitendawili hapo juu, Bw. Katabazi18 katika

mahojiano anasema:

Kazi yoyote ndani ya jamii kama kilimo, sherehe na zinginezikifanywa kwa ushirikiano mafanikio yake ni makubwa. Hivyo,falsafa ya umoja na ushirikiano ndani ya jamii hufuatwa kwa kiasikikubwa ili kurahisisha utendaji kazi. Hii ndiyo sababu mfano wakitendawili hicho kinaonesha watu hao hufanya kazi wakiwa watatu.

17 Amekwishatajwa hapo awali.18 Bw. Jualikali Katabazi ni mwanajamii wa wilaya ya Bukoba anayeishi mtaa wa Buyekera kata yaBakoba. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe 3.3.2020 nyumbani kwake.

Page 63: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

50

Ufafanuzi wa hoja hii katika nukuu hapo juu unaonesha kuwa, jamii za Kiafrika

huishi kwa kushirikiana katika mambo mbalimbali na katika shughuli za uzalishaji

mali. Falsafa ya umoja na ushirikiano inaendelea kujitokeza katika kitendawili

kifuatacho:

c) Kitendawili: Kaa huku tukae kule tulenge mawe pangoni.

Jibu: Kula matonge ya ugali.

(Chanzo: Badru, 2015).

Utafiti huu umebaini kuwa, kitendawili hiki kinasawiri suala la umoja katika kufanya

jambo. Dhana ya umoja inayobebwa katika kitendawili hiki inaonesha uwepo wa

watu wawili au zaidi wanaotoa ushirikiano katika kufanya jambo fulani na hivyo,

kuibua falsafa ya umoja na ushirikiano. Bi. Kokwenda19 anashadadia jambo hili

kama linavyojitokeza katika kitendawili hiki kwa kusema kuwa, “mkao wa kula wa

watu waishio Bukoba ni ule unaotengeneza duara. Hii ni kwa sababu watu

wanapokula huwa wamekaa katika uduara kuzunguka chakula kinachowekwa

katikati”. Katika uduara huo ndipo wanaweza kufahamishana na kujadiliana kuhusu

mambo mbalimbali yanayotokea na kuyapatia ufumbuzi. Mtazamo huu unatokana na

imani za Waafrika katika ushirikiano kuwa ndiyo msingi wa mafanikio katika jamii.

Hivyo, wanashirikiana katika kufanya mambo mbalimbali kwa pamoja na kula kwa

pamoja. Aidha, falsafa ya umoja na ushirikiano inajidhihirisha kupitia kitendawili

kingine kinachosema:

d) Kitendawili: Adui tumemzingira lakini hatumuwezi.

Jibu: Kuota moto.

(Chanzo: Salla, 2014).

Licha ya kitendawili hiki kuonesha kuwa hawamuwezi adui huyo bado kinasawiri

suala la umoja ambao unaonekana kuwa ni nguzo katika kukabiliana na adui.

Ilibainika kuwa, maana ya kitendawili hiki inaonesha ushirikiano wa watu hao katika

kumzingira adui huyo kwani Waafrika husaidiana katika shida na raha. Hii ni kwa

sababu watu wanapoota moto huwa wameuzunguka moto katikati na kutengeneza

duara. Uduara ndio kitovu cha umoja wao. Kwa Waafrika, suala la kushirikiana

linatazamwa kama nguzo ya kuwawezesha kukabiliana na matatizo mbalimbali

wanayokumbana nayo. Mtu mmoja pekee hawezi kutatua matatizo yake, bali

19 Amekwishatajwa hapo awali.

Page 64: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

51

anategemea uwepo wa watu wengine. Ndiyo maana kitendawili hiki kinasawiri

namna watu hao walivyomzingira adui yao. Kwa namna hii tunaona mtazamo wa

Waafrika kuhusu falsafa hii umejikita katika imani kuwa, mtu mmoja hawezi

kukamilika katika kupambana na tatizo linalompata bali kwa kushirikiana na

wengine ndipo wanaweza kufanikiwa. Pia, falsafa ya umoja imedhihirika katika

kitendawili kinachosema:

e) Kitendawili: Nina bibi watatu, akiondoka mmoja wawili hawafanyi kazi.

Jibu: Mafiga.

(Chanzo: Salla, 2014).

Vilevile, utafiti umebaini kwamba, kitendawili hapo juu kinaibua suala la umoja na

ushirikiano. Maana ya kitendawili hiki imebeba dhana ya ushirikiano. Hii inatokana

na sababu kuwa katika jamii ambazo hutumia mafiga kupika, ni dhahiri kuwa,

huwezi kufanikisha zoezi la kupika kama figa moja litaondolewa. Hii inaonesha

kuwa, bibi hawa watatu wanafanya kazi kwa pamoja na umoja na kila mmoja ana

nafasi kwa mwingine. Mmoja akitoka wawili wanaobaki hawawezi kufanya kazi

mpaka mwingine huyu wa tatu arudi. Akifafanua kuhusu falsafa hii kama

inavyojitokeza katika kitendawili hapo juu, Rhenus20 katika mjadala anadhihirisha

mawazo haya anaposema:

Katika maisha ya kila siku ya Waafrika wana kawaida ya kushirikianakatika masuala mbalimbali. Waafrika wanaamini kuwa kila mtu ananafasi yake kwa mwingine, hivyo, huishi kwa kutegemeana katikamambo mbalimbali. Jambo hili linadhihirika katika tanzu mbalimbaliambazo zinasawiri mawazo na utendaji wa Waafrika. Ni katika tanzuhizo kama vile vitendawili ambapo Waafrika huonya, hukosoa nahuifunza jamii yao.

Maelezo katika nukuu hapo juu yanathibitisha suala la kutegemeana kwa Waafrika

katika kufanya kazi mbalimbali. Hivyo, kufanya kazi kwa umoja kunasaidia kuleta

mafanikio kwa sababu umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.

20Amina Rhenus ni mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari Kashai iliyopo manispaaya Bukoba kata ya Kashai. Majadiliano kati ya mtafiti na watafitiwa yalifanyika tarehe 25.2. 2020shuleni hapo.

Page 65: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

52

Kwa hiyo, kitendawili hiki kinasawiri falsafa inayosisitiza umuhimu wa ushirikiano

miongoni mwa wanajamii kwa kufanya mambo kwa kutegemeana. Jambo hili

linadhihirika katika maisha ya kila siku ya Waafrika kwani wanaamini kuwa kila mtu

ana nafasi yake kwa mwingine, hivyo, huishi kwa kutegemeana katika mambo

mbalimbali.

Hoja hii inashadidiwa na Faustine (2019) anayesema kuwa suala la umoja na

ushirikiano kwa Waafrika ndio msingi wa kuimarisha na kudumisha mahusiano ya

jamii kuanzia katika familia, ukoo hadi jamii nzima. Anasema:

Mahusiano mazuri katika jamii za Waafrika yamesababisha kuwapokwa umoja unaotazamwa kama kitambulisho kwa mgeni yeyote ajayeAfrika. Umoja na ushirikiano hufungamanishwa na sababu za kuwapokwa mtu katika ukamilifu wa utu wake. Utu ambao umekitwa katikaimani ya kuwapo kwa nguvu hai inayopatikana kutokana na namnamtu anavyoishi kwa kutii na kuzingatia mitazamo na maadili ya jamiiyake. Hivyo, kwa Waafrika, ukamilifu wa mtu unatokana na auhutegemea uwepo wa watu wengine.

Kupitia mawazo yaliyo katika nukuu hiyo, tunaweza kusema kuwa, kwa Waafrika

mtu tajiri ni yule mwenye watu wengi kwa sababu kupitia watu hao kunamfanya

yeye kuwa mtu aliyekamilika. Mawazo hayo yanadhihirisha kuwa, Waafrika

wanaishi kwa umoja na ushirikiano kwa kiasi kikubwa.

Kwa namna hii tunaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa, suala la umoja na

mshikamano ni vyema likazingatiwa katika jamii kwani jamii inayoungana katika

kufanya jambo lolote katika misingi ya usawa hupiga hatua za kimaendeleo haraka

kuliko jamii isiyoungana. Umoja na mshikamano unaweza kufanywa kwenye

shughuli za kilimo, sherehe, viwandani, kwenye biashara na hata kwenye siasa.

Hivyo, itasaidia kufanikisha mambo mbalimbali kwa haraka.

4.3.2 Falsafa ya Umuhimu wa Maadili Katika Jamii

Maadili ni mwenendo unaokubalika ambao jamii imejiwekea kama msingi wa

kuongoza jamii katika utaratibu unaofaa. Kila mtu, jamii au taifa kwa jumla huishi

kulingana na maadili ya jamii hiyo. Nadharia ya Kisosholojia inasisitiza fasihi

kumulika matendo ya jamii na kuyaweka bayana. Matokeo ya utafiti huu yamebaini

kuwa, Waafrika ni miongoni mwa watu wanaoheshimu mila na desturi zao na huishi

Page 66: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

53

kwa kufuata miiko ya jamii yao. Watafitiwa walieleza kuwa, miiko hiyo ikikiukwa

huweza kuleta athari au maafa kwa jamii. Baadhi ya mila hizo ni kama vile

kuheshimu wakubwa, kutoshiriki mahusiano ya kimapenzi na ndugu wa damu na

wizi. Waafrika wanaamini kuwa, suala la maadili ni msingi katika kuyaendesha

maisha yao; hivyo maadili hayo yanajengwa kuanzia katika ngazi ya kifamilia, ukoo

na hata jamii nzima. Aidha, mfumo wa maadili ya Waafrika unajengwa kidarajia

kuanzia kwa mkubwa mpaka mdogo (Faustine, 2017). Wanaamini kuwa, maadili

mema ni msingi wa kujenga amani, utu na adabu katika jamii. Falsafa ya Kiafrika

kuhusu umuhimu wa maadili inathibitika kupitia mifano ya vitendawili vya

Kiswahili. Vitendawili hivyo ni kama vifuatavyo:

a) Kitendawili: Miti yote nitakwea, mtarawanda utanishinda.

Jibu: Ndugu wa damu kutoweza kuoana.

(Chanzo: Badru, 2015).

Kitendawili kinaonesha mtu mwenye uwezo wa kupanda miti yote isipokuwa mti wa

mtarawanda. Swali linaloibuka akilini ni kwanini ashindwe kupanda mti huo wakati

mingine yote anaweza kupanda? Je huo ni mti wa namna gani? Hivyo jibu

lililotolewa kwa kitendawili hiki ni ndugu wa damu ambao hawawezi kuoana. Maana

ya kitendawili hiki ni kuwa, mtu huyo anaweza kuoa au kuolewa na watu wengine

lakini si ndugu wa damu. Mtafiti alipouliza sababu ya kuwakataza ndugu wa damu

wasioane kama inavyobainika katika kitendawili hicho, mtafitiwa (hakutaka jina lake

lijulikane)21 alieleza kuwa:

Kukiuka miiko ya jamii kunasababisha matatizo mbalimbali. Jamiiinatambua kuwa, kama ndugu wa damu wataoana basi huendawakapata laana ambayo hupatilizwa na mizimu ya ukoo husika nawahenga. Laana hizo zinaambatana na kuzaa viumbe visivyoeleweka.Zamani ilikuwa watu wakifanya hivyo wanazaa vilema au viumbe waajabu. Wakati mwingine maovu yakizidi mizimu inaweza kukasirikana kusababisha mvua isinyeshe kwa muda mrefu hadi wazeewatakapoenda kuomba msamaha kwa mizimu au kutubu kwa Mungu.Kwa kufanya hivyo, jamii inaziishi mila na desturi zao na kulindamaadili ya jamii. Na ndiyo maana kitendawili hicho kinasisitiza kuwampandaji (kaka) hawezi kukwea mti huo (dada) kwa sababu yakutunza maadili ya jamii.

21 Ni mwanajamii anayeishi wilaya ya Bukoba kata ya Bakoba. Mahojiano na mtafiti yalifanyikatarehe 2.3.2020 nyumbani kwake.

Page 67: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

54

Maelezo yaliyo katika nukuu hapo juu yanathibitisha kuwa, suala la kulinda maadili

ya jamii ni msingi wa kuyaendesha maisha ya Mwafrika. Iwapo maadili yakakiukwa

basi huenda madhara makubwa yakatokea. Kwa hiyo, suala hili linaiendeleza falsafa

hii ya maadili. Falsafa ya maadili inaendelea kujitokeza katika kitendawili

kinachosema:

b) Kitendawili: Nyumbani kwetu kuna papai lililoiva, lakini siwezi kulichuma.

Jibu: Mwali.

(Chanzo: Badru, 2015).

Kitendawili hiki kinaonesha taswira ya papai ambalo tayari limeiva lakini

anayezungumza anasema kuwa hawezi kulichuma. Akieleza kuhusu kitendawili hiki,

Dismas22 katika mjadala anafafanua kuwa:

Taswira ya papai linalotajwa hapa inamaanisha binti au mwaliambaye tayari amefikia umri wa kuolewa lakini msemaji (kaka)anasema hawezi kulichuma (kumuoa au kuwa na uhusiano naye wakimapenzi). Kwa hiyo, kitendawili hiki kinaibua suala la umuhimu wakuzingatia maadili ya jamii za Waafrika yanayowakataza ndugu wadamu kuoana.

Nukuu hiyo inaonesha kuwa, falsafa hii ya maadili inayojitokeza katika kitendawili

hapo juu ndiyo inayomzuia kaka kumuoa dada yake na hivyo kutenda kinyume na

katazo hilo ni kuvunja taratibu za jamii yenyewe. Hii ni kutokana na sababu kuwa,

Waafrika wanaamini kwamba kama ndugu wa damu wataachwa waoane basi kuna

madhara yanayoweza kutokea katika familia, ukoo au jamii kwa jumla. Pia, kupitia

mjadala, Josbert23 alitega kitendawili kingine chenye maudhui sawa na haya. Nacho

kinasema:

c) Kitendawili: Nina kitu kizuri sana nyumbani kwetu lakini siwezi

kukichukua.

Jibu: Dada.

(Chanzo: Uwandani katika mjadala wa vikundi lengwa).

22 Azas Dismas ni mwanafunzi wa wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari Kashai iliyopomanispaa ya Bukoba kata ya Kashai. Majadiliano kati ya mtafiti na watafitiwa yalifanyika tarehe 25.2.2020 shuleni hapo.23 Jasintha Josbert ni mwanafunzi wa shule ya msingi Katerero iliyopo Halmashauri ya Wilaya yaBukoba kata ya Kyeitema. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 26.2.2020 shuleni hapo.

Page 68: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

55

Kitendawili hiki pia kinaibua maswali ya kujiuliza kuwa, kwanini mzungumzaji

anasema ana kitu kizuri nyumbani kwao na asikichukue? Ni kitu gani kinamzuia

asikichukue? Katika kujiuliza maswali hayo tunapata jawabu kuwa kitu kizuri hicho

ni dada yake ambaye ni mzuri sana lakini kwa kuwa yeye ni ndugu hawezi

kumchukua au kumuoa. Mawazo haya yanabainishwa na Bw. Rwekaza24 katika

mahojiano anayefafanua kuhusu kitendawili hiki kwa kusema:

Kwa kufanya hivyo siku zote watoto wa Kiafrika wamekuwa wakiishikwa kuheshimu maadili hayo kuwa, dada au kaka hata awe mzurikiasi gani haupaswi kumfikiria katika masuala ya kimapenzi ni katazokatika jamii. Hii ni kwa sababu za kimaadili ya Kiafrika zinazokatazandugu wa damu kuoana. Kwa kuwa, jamii inatambua kuwa inatakiwakuishi katika maadili yanayofaa ndiyo maana kitendawili hikikinadhihirisha mawazo kuwa ndugu wa damu hawawezi kushirikikatika mahusiano ya kimapenzi.

Maelezo katika nukuu hapo juu yanaonesha wazi kuhusu maadili ya Waafrika.

Umuhimu wa maadili mema yanayosisitizwa na falsafa hii ni pamoja na kuifanya

jamii kuwa sehemu ya amani hivyo kusaidia utendaji wa kazi katika hali nzuri.

Hivyo, kupitia mifano ya vitendawili hivyo kama vilivyofafanuliwa na watafitiwa

hao tumebaini kuwa, jamii wa Waafrika ina maadili yake na mfumo wake wa kutolea

na kujifunza mambo mbalimbali. Waafrika hujifunza maadili kutokana na maisha

yao ya kila siku, hivyo mtu huishi akijifunza.

4.3.3 Falsafa ya Uhai na Kifo

Waafrika wanaamini kuwa kifo kipo kwa kila mwanadamu. Utafiti umebaini kuwa,

Waafrika wanaamini kuwa, wakati mwingine kifo kikitokea basi kuna mtu

anayesababisha kifo ambaye ni mchawi. Temples (1959) anaeleza kuwa, fikra za

Mwafrika zimetawaliwa na vitu viwili ambavyo ni uhai na kifo. Waafrika huamini

kuwa mtu akiumwa nguvu uhai zinapungua hivyo anaamini atakufa. Imani katika

uhai na kifo ni vitu vinavyowashughulisha sana Waafrika. Data za uwandani

zinathibitisha hoja hii kwani watafitiwa walieleza kuwa, kila mwanadamu atakufa

ingawa sio kila kifo kinachotokea ni mpango wa Mungu. Hii ina maana kuwa, vifo

24Hasimu Rwekaza ni mwanajamii katika wilaya ya Bukoba kata ya Hamugembe mtaa wa Nyangoye.Mahojiano kati yake na mtafiti yalifanyika tarehe 4.3.2020 nyumbani kwake.

Page 69: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

56

vingine vinasababishwa na wachawi. Mawazo haya yanathibitishwa na Bi.

Abdallah25 anayesema:

Hatukatai kuwa ni kweli binadamu lazima afe lakini sio kila kifo nimpango wa Mungu. Mungu hakumuumba mwanadamu iliamwangamize lakini kuna watu wachache wasiopenda maendeleo yawatu wengine ndio hutumia nafasi za nguvu zao kuwaangamizawenzao kwa faida yao binafsi au kufanya visasi.

Maelezo katika nukuu hapo juu ni ithibati tosha kuwa, Waafrika wana imani

mbalimbali katika masuala ya kifo. Aidha, falsafa ya kifo imebainika kupitia

vitendawili vya Kiswahili vinavyotumika katika jamii za Kiafrika. Utafiti huu

umebaini kuwa, Waafrika wanaamini mtu akiumwa basi atakufa. Tunapoongelea

kuhusu mitazamo ya Waafrika kuhusu uhai na kifo, tunapata ushahidi kutoka katika

vitendawili vifuatavyo:

a) Kitendawili: Ini la ng’ombe huliwa hata na walioko mbali.

Jibu: Kifo.

(Chanzo: Badru, 2015).

Watafitiwa walifafanua kuwa, Waafrika wanayo falsafa yao inayohusu masuala ya

uhai na kifo. Akifafanua kuhusu suala la kifo kama linavyojitokeza katika

kitendawili hiki Bi. Katunzi26 katika mahojiano alieleza kuwa, “kifo humtokea mtu

yeyote katika dunia na hakuna ambaye anaweza kukikimbia kifo ili aishi miaka yote

hapa duniani. Walioko mbali hukumbwa na kifo na hata walioko karibu nao

hukumbwa na kifo”. Maelezo hayo yanaonesha dhahiri kuwa kifo kwa mwanadamu

hakiepukiki. Kwa upande mwingine mfano wa kitendawili chetu unaibua dhana ya

ushirikiano wa Waafrika katika suala la kifo kwamba linawashughulisha hata

walioko mbali. Hii ni kwa sababu wanaamini kuwa, hili ni suala zito la kijamii hivyo,

linatakiwa kupewa uzito fulani kwa kuzingatia kuwa, kila mtu ataweza kukumbana

nalo wakati wowote. Aidha, Badru (2015) anaunga mkono mawazo haya

anapofafanua kuwa, taarifa kuhusu msiba huwashughulisha sana Waafrika bila kujali

25 Bi Farida Abdallah ni mwanajamii na mwalimu mstaafu wa Shule ya msingi ya Qudus iliyopomanispaa ya Bukoba. Mahojiano na mtafiti yaliyofanyika tarehe 4.3.2020 mtaa wa National housing-Kashai.26 Bi. Marina Katunzi ni mwanajamii wa wilaya ya Bukoba na mtumishi katika taasisi ya WolrdVision tawi la Bukoba. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe 3.3.2020 ofisini kwake.

Page 70: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

57

umbali ambao kifo hicho kimetokea. Taarifa za kifo hata kama kimetokea mbali

zinaweza kusambaa na kuwafikia hata walioko mbali. Falsafa hii inatukumbusha

kuwa, hakuna mtu atakayekwepa kifo haijalishi umbali atakaokuwa, kifo kitamfuata

popote alipo. Falsafa ya Waafrika ya uhai na kifo inaendelea kujidhihirisha katika

kitendawili kifuatacho:

b) Kitendawili: Akitokea watu wote hunung’unika na kuwa na huzuni.

Jibu: Ugonjwa au kifo.

(Chanzo: Salla, 2014).

Kitendawili hiki kinaonesha namna ambavyo taarifa za ugonjwa au msiba huwa ni za

masikitiko na huzuni pale vinapotokea katika jamii. Kwa hiyo, kifo kinapotokea

watu huomboleza na kuwa na majonzi. Bw. Kigoye27 (k.h.j) katika mahojiano

alifafanua kuwa, “kitendawili hiki kinaibua suala la hofu kuhusu kifo kwa Waafrika.

Kwa kuwa, wanaogopa kufa, wanakuwa na huzuni pindi mtu akiumwa kwa sababu

wanaamini atakufa”. Hata hivyo, utafiti umebaini kuwa, wanajamii katika jamii ya

Waafrika, huamini mtu akifa hawezi kurudi tena na kuishi kama mtu mwenye nafsi

hai ndiyo maana watu wanaogopa kufa au kuumwa. Kitendawili kinachoshadadia

mawazo haya kilitegwa na Gidius28 katika mjadala. Nacho kinasema:

c) Kitendawili: Kitanda changu cha dhahabu nikilalia siamki tena.

Jibu: Jeneza.

(Chanzo: Uwandani kupitia mjadala wa vikundi lengwa).

Anaendelea kufafanua kuwa, dhana ya kitanda hapa imechukuliwa kama jeneza

ambalo msemaji anakiri kuwa akilalia hataamka tena. Utafiti umebaini kuwa, maana

inayotolewa katika kitendawili hiki inahusisha suala la kifo ambapo mtu aliyefariki

akishalazwa kwenye jeneza hataweza kuamka tena. Suala hili linaibua falsafa ya

Waafrika katika kifo na uhai kwani ni ukweli kwamba mtu akifa hawezi kurudi kuwa

nafsi hai. Katika uhalisia hakuna mwanadamu ambaye atakufa na kurudi tena duniani

27 Amekwishatajwa.28 Nicera Gidius ni mwanfunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Kashai iliyopo manispaaya Bukoba kata ya Kashai. Majadiliano kati ya mtafiti na watafitiwa yalifanyika tarehe 25.2.2020shuleni hapo.

Page 71: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

58

na kuishi kama mwanadamu wa kawaida. Aidha, kitendawili chenye maudhui sawa

na haya ni kile kinachosema:

d) Kitendawili: Nikipanda gari la baba sirudi kamwe.

Jibu: Jeneza.

(Chanzo: Salla, 2014).

Kitendawili hiki kinafanana na kilichotegwa awali hapo juu. Gari inayoelezwa hapa

ni jeneza na dhana ya kutorudi inahusishwa na dhana ya kifo, ambapo mtu akifa

hawezi kurudi tena. Vitendawili hivi vinafafanua kuwa, mtu akifa hawezi kurudi tena

na kuweza kuishi kama binadamu wa kawaida mwenye nafsi hai. Kupitia vitendawili

hivi ambavyo ni fasihi ya Waafrika, vinaonesha kuhusu falsafa ya Waafrika katika

suala la uhai na kifo.

Vilevile, imani na mitazamo ya Waafrika kuhusu kifo imebainishwa na Kaponda

(2018) anayesema kuwa, kwa Waafrika, kifo husababishwa na mchawi, roho za wafu,

laana na kifo cha asili. Kimsingi mtu hufa taratibu mpaka watu wanaomkumbuka

waishe. Waafrika wana hofu na kifo. Katika msiba watu huweza kulia na hata

kuzimia pale wanapoondokewa na mtu ambaye walikuwa wanampenda na alikuwa

na umuhimu kwao. Hii ni kutokana na imani kuwa mtu huyo hawataweza kumwona

tena. Hivyo, tunaweza kuhitimisha hoja hii kwa kusema kuwa, vitendawili hivyo

pamoja na maelezo mbalimbali tuliyoeleza hapo juu yanathibitisha kwamba, masuala

yahusuyo uhai na kifo ni mojawapo ya falsafa ya Kiafrika na kuwa Waafrika wana

hofu na kifo.

4.3.4 Falsafa ya Uduara

Uduara ni mojawapo ya falsafa inayojitokeza katika jamii za Waafrika. Kwa

Waafrika, mtazamo kuhusu uduara ni namna ya kuufasli ulimwengu wao. Matokeo

ya utafiti huu yamebainisha kuwa, Waafrika wanaamini kuwa vitu vizuri ni vile

vilivyo katika umbo la duara. Falsafa ya uduara inajitokeza katika jamii nyingi za

Waafrika kutokana na vitu wanavyotumia au mambo wanayoyafanya kuwa na umbo

la duara. Aidha, kupitia data za uwandani, utafiti umebaini kwamba, jamii za

Kiafrika hufanya mambo mbalimbali kama michezo ya watoto, mikao ya kula,

shughuli za kijamii kama misibani na katika sherehe hufanywa kwa uduara.

Page 72: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

59

Katika utafiti huu, falsafa ya uduara imeweza kuthibitika kupitia vitendawili vya

Kiswahili vinavyotumika katika jamii za Kiafrika. Ipo mifano mingi ya vitendawili

inayodhihirisha falsafa ya uduara kwa Waafrika. Vitendawili hivi vipo katika namna

mbili. Mosi, vinaonesha dhana ya uduara katika vitu na pili, vinaibua uduara katika

utendekaji wa jambo. Kwa kuanza na mifano ya vitendawili vinavyoonyesha

utendekaji wa jambo katika uduara ni kama vifuatavyo:

a) Kitendawili: Amekaa kimya na watoto wamemzunguka pande zote.

Jibu: Mgomba katikati na machipukizi yake pembeni yake.

(Chanzo: Salla, 2014).

Katika kukichunguza kitendawili tajwa hapo juu tumebaini uwepo wa falsafa ya

uduara. Maana inayopatikana katika kitendawili hiki inaibua falsafa ya uduara kwa

kuwa, Waafrika wanaamini kuwa, kukaa kwa uduara kunasaidia kujenga

mshikamano kuanzia katika familia, ukoo mpaka katika jamii nzima. Akifafanua

kuhusu kitendawili hiki, mtafitiwa (hakutaka jina litajwe)29 katika mahojiano

anasema:

Uduara unajitokeza katika mambo mengi. Karibia kila jambolinalofanyika hufanywa kwa uduara. Kwa mfano kwenye shughuli zakitanzia, sherehe mbalimbali za kijamii zote matukio yake hufanyikakwa uduara. Hii inasaidia hata kufahamiana kwa watu kwa kuwamnakuwa mnaonana. Hapa inakuwa ni rahisi kutambua naniameshiriki na ambaye hajashiriki katika shughuli hiyo ya kijamii. Kwhiyo utakuta wanapokula, wanapocheza au hata wanapozika huwawanakuwa katika mzunguko unaotengeneza duara. Hiindio maanakitendawili kinaonesha kuna kitu kilichopo katikati na wenginewamekizunguka pande zote kutengeneza duara.

Maelezo yaliyo katika nukuu hapo juu ni ithibati kuwa, kitendawili hicho kimesawiri

vema falsafa ya uduara kwani mambo mengi yanayofanywa katika jamii za Waafrika

hufanywa kwa suara ya duara. Hivyo, inadhihirisha imani kuwa uzuri wa kitu au

mambo katika jamii unatokana na umviringo au uduara. Pia, kupitia mjadala wa

vikundi lengwa, Clophas30 alitega kitendawili kinachosawiri falsafa ya uduara.

Kitendawili hicho kinasema:

29 Ni mwanajamii anayeishi katika wilaya ya Bukoba kata ya Kibeta. Mahojiano na mtafiti yalifanyikatarehe 5.2.2020 nyumbani kwake.30 Eneliko Clophas ni mwanafunzi wa shule ya msingi Katerero iliyopo Halmashauri ya Wilaya yaBukoba kata ya Kyeitema. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 26.2.2020 shuleni hapo.

Page 73: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

60

b) Kitendawili: Askari wamekaa pembeni na mfalme yupo katikati.

Jibu: Watu wakiota moto huku wakiwa wameuzunguka.

(Chanzo: Uwandani katika mjadala wa vikundi lengwa).

Falsafa ya Kiafrika katika kitendawili hiki imejikita katika masuala ya uduara.

Akiendelea kufafanua kuhusu kitendawili hiki mtafitiwa huyo alisema, “Waafrika

huamini katika uduara ndiyo maana, kwao mambo mazuri ni yale yaliyoko kwenye

umbo la duara”. Wanaamini kuwa vitu vizuri ni vile vilivyoko kwenye umbo la

duara. Kwa hiyo, kupitia falsafa hii hujikuta wakifanya mambo yao wakiwa kwa

uduara. Kwa kufanya hivyo kunawawezesha watu hao kujadiliana kuhusu mambo

mbalimbali ya kimaendeleo jambo ambalo litasababisha kufanikiwa katika

maendeleo yanayofanywa na jamii. Akishadadia kuhusu falsafa ya uduara kama

inavyojitokeza katika kitendawili hicho, Muganyizi31 katika mahojiano uwandani

anasema:

Falsafa ya uduara inasisitizwa ndani ya jamii huku wakifundishwakupitia njia mbalimbali umuhimu wa kuthamini vitu vilivyokokwenye umbo la duara. Kwa mfano masuala ya tambiko hufanywakwa uduara na hata baadhi ya nyumba za kuishi hujengwa kwa umbola uduara. Kwa hiyo, kitendawili hiki kinaibua falsafa ya uduaraambao unajitokeza kutokana na kitendo cha kuuzunguka moto uliopokatikati.

Kupitia maelezo katika nukuu hiyo, mtafiti amebaini kuwa, uduara ni mhimili

mkubwa wa ushirikiano wa Waafrika. Ipo mifano mingi ya vitu au mambo

yanayofanywa kwa uduara katika jamii Waafrika. Wao huamini katikati

panapozungukwa na kitu huwa ndiyo chanzo cha nguvu zao, ndiyo maana katika

kitendawili hapo juu tunaona moto upo katikati. Aidha, Mussa32 katika mjadala

alitega kitendawili kinachoonesha falsafa ya uduara katika kitu. Nacho kinasema:

c) Kitendawili: Nina nyumba yangu ya mviringo.

Jibu: Yai.

(Chanzo: Uwandani katika mjadala wa vikundi lengwa).

31 Binamungu Muganyizi ni mwanajamii wa wilaya ya Bukoba anayeishi kata ya Kibeta mtaa waKankwila. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe 2.3.2020 nyumbani kwake.32 Akramu Mussa ni mwanafunzi wa shule ya msingi Katerero iliyopo Halmashauri ya Wilaya yaBukoba kata ya Kyeitema. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 26.2.2020 shuleni hapo.

Page 74: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

61

Utafiti umebaini kuwa, kitendawili hiki kinachomoza falsafa ya uduara ambapo

msemaji anaeleza kuwa, “nyumba yake ni ya mviringo”. Akiendelea kufafanua

kuhusu kitendawili hiki, mtafitiwa huyo anasema, “suala la nyumba kuwa ya

mviringo linaibua dhana ya uzuri wa nyumba hiyo katika uduara. Kwa hiyo, uzuri

katika kitu umedhihirika kupitia kitendawili hiki na hivyo, kuibua falsafa ya

Waafrika kupenda vitu vilivyo katika umbo la duara kwani wanaamini vitu hivyo ni

vizuri kuliko vile ambavyo siyo vya duara.” Maelezo hayo yandhihirisha kuwa, ni

jambo la kawaida kusikia watu katika jamii ya Kiafrika wakisifia vitu vya duara.

Vitu kama vile nyumba zao za misonge huwa ni za duara, mitungi, vyombo vyao vya

kupikia na hata vifaa vya kukamulia maziwa. Pia kitendawili kingine kinasema:

d) Kitendawili: Fupi fupi la mviringo limeleta utamu.

Jibu: Ngoma.

(Chanzo: Salla, 2014).

Dhana ya uzuri katika kitu imejibainisha katika kitendawili hiki ambapo kichocheo

chake cha msingi ni “fupi fupi la mviringo kuleta utamu”. Kupitia mfano huu

tumeweza kutambua kuwa, kumbe utamu unatokana na umviringo wa kitu hicho na

hapo dhana ya uzuri katika duara inaibuliwa. Aidha, hapa inaonesha ni kwa namna

gani Waafrika huona vitu vya duara kuwa na thamani kubwa, ndiyo maana katika

jamii inasisitizwa kuthamini vitu vyenye umbo la duara. Kwa mfano visima vyao na

hata mabwawa ambayo huyachimba kwa lengo la kunyweshea mifugo huwa ya

duara. Mawazo yaliyo katika kitendawili hicho yanafanana na Mlelwa, (2017)

anayesema:

Utamaduni wa Waafrika unaonesha wazi kuwa wanaamini kituchochote kikifanyika katika hali ya duara kinakuwa kizuri. Hii ni kwasababu kunakuwa na umoja katika kutenda. Pia kitu kikiwa katikaumbo la duara kinakuwa ni kizuri. Kwa hiyo, umbo la duara ni kigezocha uzuri kwa Waafrika.

Maelezo katika nukuu hiyo hapo juu ni ithibati kuwa, mtazamo wa Waafrika kuhusu

uzuri au kitu kizuri ni kile kilicho katika umbo la duara. Kwa maana hiyo baadhi ya

vitu wanavyovitumia Waafrika ni vya umbo la duara. Pia, utendekaji wa mambo

katika uduara kunahamasisha umoja na mshikamano katika jamii.

Page 75: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

62

Hoja hii inatiwa nguvu na nadharia ya Kisosholojia kupitia msingi wake unaosema

fasihi haiwezi kujitenga na jamii ambayo kwayo imechipuzwa. Hii ina maana kuwa

fasihi inaakisi kile kinachotendeka na kukitoa kwa jamii. Vitendawili hivi vinaakisi

maisha halisi ya jamii na hivyo kutupatia picha halisi ya Waafrika wanavyoishi

katika mazingira yao. Hata hivyo, utafiti huu umebaini kuwa, falsafa ya uduara

inaenda sambamba na masuala ya umoja na ushirikiano kwa maana kuwa mambo

mengi yanayofanywa na Waafrika, hufanywa kwa kushirikiana na hivyo kujenga

falsafa ya uduara. Kwa hiyo, uduara wa Waafrika una maana kubwa katika jamii

kwani husaidia kuleta umoja na mshikamano katika jamii na hivyo, kurahisisha

kufikiwa kwa mafanikio makubwa katika mambo mbalimbali.

4.3.5 Falsafa ya Imani katika Mungu na Mizimu

Hii ni mojawapo ya falsafa ya Kiafrika inayosawiriwa katika fasihi simulizi

mathalani katika vitendawili vya Kiswahili. Utafiti huu umebaini kuwa, Waafrika

wanaamini katika nguvu na uweza wa Mwenyezi Mungu kwa kuwa, Mungu ndiye

muweza wa yote na ndiye suluhisho la matatizo ya mwanadamu. Katika utafiti huu,

falsafa ya imani katika Mungu na mizimu imeweza kudhihirika kupitia mifano ya

baadhi ya vitendawili wanavyovitumia katika jamii zao kusawiri suala hili. Mifano

ya vitendawili hivyo ni kama:

a) Kitendawili: Ana nguvu na uwezo kutushinda sote.

Jibu: Mungu.

(Chanzo: Salla, 2014).

Falsafa ya imani katika Mungu inajidhihirisha katika kitendawili hapo juu kwani

jamii huamini kuwa, ipo nguvu isiyoonekana ambayo ndiyo hutumika kuongoza

maisha ya mwanadamu. Akifafanua kuhusu kitendawili hiki, Bw. Kigoye (k.h.j)

katika mahojiano anasema:

Kwa asili Muhaya anajua kuwa, Mungu yupo ndio maana Munguamepewa majina mengi kudhihirisha uwezo na nguvu zake. Baadhiya majina hayo ni kama Ruanga33, Katonda34 na Nyarubamba35.Majina hayo yana maana tofautitofauti kudhihirisha uwezo na

33 Ruanga ni jina la Mungu wa Kihaya linalomaanisha kuwa na uwezo wa kutoa maamuzi sahihi naanachokitolea maamuzi kinakuwa mwafaka.34 Katonda ni jina la Mungu lenye maana kuwa yeye ni asili ya kila kitu kilichopo duniani (muumbaji).35Nyarubamba ni Mungu ana uwezo wa kila kitu hasa kwa upande wa kutoa riziki kwa watu.

Page 76: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

63

nguvu alizo nazo Mungu. Hata kabla ya kuja kwa wamisionari,watu wa jamii ya Wahaya tulikuwa tunatambua kuwa Mungundiye muweza wa yote katika kufanya mambo mbalimbali. Hatahivyo suala la kuamini wahenga na mababu lipo sambamba.Kwenye familia hapawezi kukosa changamoto ambazo zitashindwakupatiwa majibu. Kwa hiyo, tunaamini kuwa mababu au wazazi niwatu wa hekima hata wakifa hawatuzuii sisi kuendeleakuwaheshimu na kuwaomba katika shida mbalimbali. Kama mtuhuyo aliyefariki alikuwa maarufu kama vile Mfalme au Mtemi,ataendelea kupelekewa maombi kwa kufuata taratibu fulani zakimila. Taratibu hizo ni kama vile, kumgawia kahawa na pombekwa muda wa siku tatu na hapo maombi yakishakamilika siku yatatu pombe hurudishwa nyumbani na kunywewa.

Maelezo ya mtafitiwa huyo yanadhihirisha kuwa, kwa Waafrika Mungu ndiye

mtawala, asili ya kila kitu duniani na mwenye uwezo wa kutoa riziki kwa watu.

Licha ya imani kuwa Mungu ndiye muweza bado Waafrika wanaamini katika wafu

yaani wahenga na mizimu ambayo huendelea kuwasikia wakiomba katika shida

mbalimbali. Edisson36 katika mjadala anashadadia kitendawili hiki kwa kusema

kuwa:

Mungu hashindwi na jambo lolote; akiamua jambo lolote limtokeemwanadamu huwa linatokea. Jamii ya Waafrika wanaamini kuwa,kuna viumbe vyenye nguvu na uwezo mkubwa wa kutenda mamboambayo binadamu wa kawaida hawezi kufanya. Viumbe hao ni kamavile Mungu, mizimu, wahenga na mababu. Ndio maana jibu lakitendawili chetu linaonesha ni Mungu tu ndiye mwenye uwezo huo.

Maelezo haya yanathibitisha kuwa, Waafrika wanaamini katika nguvu na uwezo wa

Mungu katika kutenda mambo yasiyowezekana kufanyika kwa hali ya kawaida.

Aidha, kitendawili kingine kinasema:

b) Kitendawili: Anatuona lakini sisi hatumuoni.

Jibu: Mungu.

(Chanzo: Badru, 2015).

Katika kuichunguza falsafa ya imani katika Mungu, utafiti huu umebaini kuwa,

Waafrika wanaamini kuhusu uwepo wa nguvu zisizoonekana ambazo ndizo

huongoza maisha yao hivyo, zinapaswa kuheshimiwa na kuaminiwa. Katika

36 Happiness Edisson ni mwanafunzi wa shule ya msingi Katerero iliyopo Halmashauri ya Wilaya yaBukoba. Majadiliano na watafitiwa yalifanyika tarehe 26.2.2020 shuleni hapo

Page 77: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

64

kitendawili hiki “anatuona lakini sisi hatumuoni” jibu lake ni “Mungu”, kinasawiri

falsafa ya imani katika Mungu. Katika mjadala, Projestus37 alieleza kuwa, “Waafrika

katika imani wanafahamu kuwa Mungu ana uwezo mkubwa kuliko kiumbe chochote,

ana uwezo wa kutuona wakati wowote na mahali popote tulipo”. Hivyo, kwa

kuamini kuwa Mungu anaona matendo ya kila mwanadamu; inawafanya Waafrika

kuishi kwa kufuata misingi ya utu bora siku zote na kuogopa kutenda mabaya.

Kitendawili kingine chenye maudhui yanayofanana na haya ni kile kilichotegwa na

Selestine38 ambacho pia kinasawiri falsafa ya imani katika Mungu. Kitendawili

kinasema:

c) Kitendawili: Popote niendapo yupo lakini haonekani.

Jibu: Mungu.

(Chanzo: Uwandani katika mjadala wa vikundi lengwa).

Kitendawili hiki kinaonesha masuala ya imani ya Waafrika katika Mungu.

Akifafanua kuhusu kitendawili hiki, Kaigara39 katika mahojiano uwandani anasema:

Waafrika wanaamini kuwa, wapo viumbe wenye nguvu na uwezowanaoaminika kuwepo lakini binadamu wa kawaida hawawezikuwaona isipokuwa kupitia imani tu kuwa yupo. Uwezo wakeunatokana na nguvu za kiuajabu alizonazo ambazo zinamfanya yeyekuwepo popote na asionekane. Waafrika huamini Mungu ana uwezowa kutembea mahai popote na asiweze kuonekana kwa macho yakawaida. Kwa hiyo kitendawili hiki kimesawiri vema falsafa ya imanikatika Mungu na mizimu.

Maelezo katika nukuu hapo juu yanaonesha namna ambavyo Waafrika huamini

katika Mungu na kuwa yeye ndiye muweza wa yote. Falsafa ya imani inawapelekea

Waafrika kuishi katika misingi ya maadili mema yanayompendeza Mungu na

kuyakataa maovu yaliyo kinyume na maagizo ya Mungu. Hii inasababishwa na

imani kuwa Mungu anamuona kila mtu na kila tendo jema au ovu alifanyalo

mwanadamu. Kupitia Mungu au miungu Waafrika hujenga familia na jamii yenye

37 Proscovia Projestus ni mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari iliyopo manispaaya Bukoba. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 25.2.2020 shuleni hapo.38 Faustine Selestine ni mwanafunzi wa kitato cha nne katika shule ya Sekondari Kashsi iliyopomanispaa ya Bukoba. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 25.2.2020 shuleni hapo.39 Elizabeth Kaigara ni mama na mlezi wa watoto katika kigango cha Mt. Inyasi parokia ya YohanePaulo wa pili kata ya Kibeta- Tanesco. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe 4.3.2020 ofisini kwake.

Page 78: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

65

misingi bora na imani thabiti katika masuala ya dini. Hivyo, yeyote anayefanya

maovu huadhibiwa na Mungu.

Aidha, hoja hii imetiliwa nguvu na Temples (1959) anayesema kuwa, Mwafrika

anaamini kuna nguvu kubwa kuliko zote ambayo ni Mungu. Hivyo, ameamua

kugawa nguvu hizo katika darajia za nguvu ambazo ni: Mungu- mizimu- wahenga-

wazee- binadamu wa kawaida- wanyama- miti. Kwa hiyo, kupitia maelezo ya

mtaalamu huyu na nukuu hapo juu ni dhahiri kuwa Waafrika wanaamini katika

nguvu za Mungu na mizimu katika kuwawezesha kufanikisha mambo mbalimbali.

Hussein (1976) anakubaliana na hoja hii kwa mtazamo kuwa, Waafrika wanaamini

watu waliokufa wapo karibu na Mungu na wale walio hai humwomba Mungu kupitia

wale waliokufa. Hili linadhihirika kupitia matambiko au kuomba mizimu ya mababu

inayofanywa na Waafrika wengi katika maisha yao ya kila siku. Hivyo, Waafrika

wengi wanaamini kuwa, wahenga wanaweza kuwa na nguvu katika kila kitu

kinachowatokea katika maisha yao. Mambo kama vile kuumwa, vifo, ajali, talaka,

mimba kuharibika, ulemavu na mikosi inaaminiwa kutokea kwa sababu ya wachawi

au hasira za mababu na wahenga. Kwa jumla mawazo haya yanatudhihirishia

mtazamo wao kuhusu imani katika nguvu za Mungu na mizimu.

4.3.6 Falsafa ya Uchawi na Ushirikina

Makame, (2016) anafafanua kuwa ushirikina ni tabia ya mshirikina kufanya matendo

au maneno juu ya uwezo mkubwa wa kiumbe kingine kuleta madhara badala ya ule

wa Mwenyezi Mungu kwa kutumia majini, mizimu, talasimu za kisihiri na hirizi

katika kufanikisha jambo fulani. Ushirikina hujitokeza katika nyanja mbalimbali

ambazo ni; Mosi, kufanya matendo yasiyo ya kawaida ya kuogofya na kushangaza.

Pili, mtendaji wa ushirikina hushiriki na kufuata maelekezo ya viumbe wa ajabu na

kuwasiliana nao katika ufanikishaji wake. Tatu, mshirikina hutawaliwa na lugha za

majini na mashetani pamoja na kuzungumza nao katika sehemu maalumu kama vile

mapango au kilingeni. Utafiti huu umebaini kuwa, jamii nyingi za Kiafrika huamini

katika nguvu za miujiza katika kutenda mambo yasiyo ya kawaida. Nguvu hizo

hujulikana kuwa ni za kichawi au kishirikina. Mtafiti amebaini uwepo wa vitendawili

vya Kiswahili vyenye falsafa ya “uchawi na ushirikina”. Falsafa hii inadhihirika

katika vitendawili vifuatavyo:

Page 79: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

66

a) Kitendawili: Mchawi wa manga hulala mchana na kufanya kazi usiku.

Jibu: Mwezi.

(Chanzo: Salla, 2014).

Kupitia kitendawili hiki, utafiti huu umebaini uwepo wa falsafa ya Kiafrika

inayozungumzia masuala ya “uchawi na ushirikina”. Kitendawili kinaonesha namna

ambavyo wachawi hufanya kazi usiku na hii inasawiri suala la imani za Waafrika

kuhusu uchawi na wachawi ambao huaminika kufanya shughuli zao nyakati za usiku.

Akisisitiza kuhusu falsafa hii kama inavyojitokeza katika kitendawili hicho, Bw.

Bwemero40 alieleza kuwa, “mambo hayo hufanyika kupitia nguvu za giza, yaani

“uchawi na ushirikina” na shughuli hizo hufanyika usiku kwa kuwa ni jambo ovu

ambalo halikubaliki katika jamii”. Maelezo hayo yanathibitisha mtazamo wa

Waafrika kuhusu uwepo wa uchawi katika jamii. Aidha, kupitia mahojiano na

watafitiwa ilielezwa kuwa, uchawi na wachawi wapo katika jamii za Kiafrika na

hutumia nguvu zao kuwadhuru watu wengine. Na kwa kutambua hilo ndio maana

watu wengi wameokoka na wanamwabudu Mungu ili kupata ulinzi wa Mungu dhidi

ya wachawi. Mawazo haya yanayothibitisha kuhusu uwepo wa uchawi katika jamii

yanabainishwa katika mahojiano pale Bw. Rwegasira41 anaposema:

Tunaamini kuwa uchawi upo na unafanya kazi katika mazingirahalisi. Jambo hili linathibitika katika jamii zetu kutokana na sababukuwa, hata wakristo wanaomjua Mungu hufanya baadhi ya vituvinavyoashiria kuwa wanaamini katika uwepo wa uchawi. Mambohayo ni kama vile kuomba kabla ya kulala na baada ya kuamka.Kwa mfano katika salamu zao huomba ulinzi wa Mwenyezi Munguna kukemea nguvu za kichawi dhidi yao. Hii inadhihirisha kuwa,wanaamini kuwa wachawi wapo na wanaweza kuja kuwadhuruwakati wakiwa wamelala kama kitendawili hicho kinavyooneshakuwa wachawi wanafanya kazi usiku.

Maelezo katika nukuu hii ni ushahidi kuwa, Waafrika wanaamini kuwa wachawi

wapo na wanaweza kutumia nguvu zao kuwadhuru watu wengine. Mambo hayo ni

kama vile kusababisha vifo, kujibadili au kumbadili mtu mwingine katika maumbo

40 Bw. Deogratius Bwemero ni mwanajamii katika wilaya ya Bukoba anayeishi kata ya Rwamishenyemtaa wa Kamizilente. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe 2.3.2020 nyumbani kwake.41 Bw. Audax Rwegasira ni mwanajamii wa wilaya ya Bukoba, mstaafu katika utumishi wa umma naaliwahi kuwa afisa katika Ofisi ya Utamaduni Halmashauri ya Bukoba. Mahojiano na mtafitiyalifanyika mnamo tarehe 6.3.2020 mtaa wa Buyekera kata ya Bakoba.

Page 80: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

67

mbalimbali. Pia, falsafa ya “uchawi na ushirikina” imedhihirika katika kitendawili

kisemacho:

b) Kitendawili: Kaa huku nikae kule tumfinye mchawi.

Jibu: Kula ugali kwa mikono.

(Chanzo: Badru, 2015).

Kitendawili hiki kinasawiri mapokeo ya jamii kuhusiana na uchawi. Akifafanua

kuhusu kitendawili hiki, Theobard42 katika mjadala anasema:

Katika jamii za Kiafrika japo uchawi upo, lakini bado haukubalikimiongoni mwa wanajamii na unapingwa vikali. Pindi wanapojuakuwa mtu wa jamii yao ni mchawi huweza kumkemea na kumdhihakiili aachane na uchawi. Hivyo, maana ya kitendawili hiki inaibuadhana ya ushirikiano katika (kumfinya) kumuadhibu mchawi”.

Hivyo, maelezo haya yanayofafanua kitendawili hapo juu yanaonesha kuwa,

Waafrika wanaamini katika masuala yanayohusu “uchawi na ushirikina” na pia

wanawachukia wachawi na shughuli zao za kichawi. Katika kuunga mkono mtazamo

wa hoja hii, Manala (2004) anasema:

Witches are not only feared, but also hated because they make lifeunbearably difficult for individuals, families, communities andsocieties. In the African’s world of thought, when ill-health,misfortune, accident or death occuers, traditional Africans willimmeadiately probe witch crafts as the likely cause (uk. 1501).

Wachawi sio tu kwamba wanaogopwa lakini pia wanachukiwa kwasababu wanayafanya maisha bila shaka kuwa magumu kwa mtubinafsi, familia na hata jamii kwa ujumla. Kwa mtazamo wa Waafrika,ikitokea magonjwa, bahati mbaya, ajali au hata vifo basiwatamtazama moja kwa moja mchawi kwamba ndiye aliyesababisha(Tafsiri ya mtafiti).

Nukuu hiyo inathibitisha kuwa, wachawi hawapendwi katika jamii na hivyo,

wanapingwa kwa sababu uchawi unahusisha matendo maovu. Pia, Faustine (2017)

anaeleza kuwa, Waafrika wanaamini mchawi anaweza kutumia viumbe wengine

katika kutenda matendo mbalimbali kinyume na uhalisi wao au kumbadilisha mtu na

kumfanya aishi katika ulimwengu wa wachawi bila watu wengine kumwona. Huko

42 Adelaida Theobard ni mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari Kashai iliyopomanispaa ya Bukoba. Majadiliano na watafitiwa hao yalifanyika tarehe 25.2.2020 shuleni hapo.

Page 81: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

68

hutumikishwa na mchawi huyo kwa kufanyishwa kazi mbalimbali kama ilivyo katika

ulimwengu wa kawaida. Hivyo, tunaweza kuhitimisha hoja hii kwa kusema kuwa,

mtazamo wa Waafrika kuhusu falsafa hii ya uchawi unajipambanua kwa kiasi

kikubwa katika jamii za Kiafrika. Mawazo haya yanafungamanishwa na nadharia ya

Kisosholojia inayosisitiza kuwa fasihi haiwezi kujitenga na jamii ambayo kwayo

imechipuzwa. Hii ni kutokana na sababu kuwa kazi nyingi za fasihi ya Waafrika

zimesawiri kwa wingi falsafa hii kama tulivyoona katika vitendawili tulivyovitumia

katika hoja yetu vimedhihirisha kuwepo kwa falsafa ya “uchawi na ushirikina” katika

jamii ya Waafrika.

4.3.7 Falsafa ya Uzazi na Malezi

Suala la uzazi linaonekana kuwa ni la muhimu sana kwa Waafrika. Matokeo ya

utafiti huu yamebaini kuwa, Waafrika wanaamini kuwa, ukamilifu wa ndoa za

Waafrika unategemea uwezo wa mwanamke kuzaa watoto. Waafrika wanaamini

katika familia pana ambapo kuzaa watoto wengi ni ufahari na kunaifanya familia au

ukoo kupanuka. Aidha, Faustine (2017) anaeleza kuwa, mtu mwenye uzazi

hutazamwa kama mtu mwenye baraka nyingi zinazotokana na kuwapo kwa nguvu-

hai. Waafrika wanautazama uzazi kama njia ya kuwapo kwa mtu na njia pekee ya

kuukuza na kuuendeleza ukoo. Hivyo, mtu mwenye uzazi hupewa heshima kuliko

yule asiye na uwezo wa kuzaa. Hata hivyo, kupitia utafiti huu imebainika kwamba,

Waafrika wanaamini kuwa suala la malezi ya watoto hao ni jukumu la wanawake

kwa kiasi kikubwa. Hoja hii inaungwa mkono na mtafitiwa aliyeeleza kuwa, suala la

uzazi na malezi ya watoto kwa Waafrika linamshughulisha mwanamke wa Kiafrika

kuliko mwanaume. Haya yamethibitika pale Bi. Kayanga43 (k.h.j) anaposema:

Suala la ndoa kwa jamii zetu linaenda sambamba na kuzaa kwamwanamke. Mwanamke anapoolewa na kwenda ukweni anatarajiwakumzalia mwanaume watoto. Mwanamke anayezaa hupendwa sana nawakwe zake ukilinganisha na yule asiyezaa. Siku zote mwanamkealiyeolewa na asizae hudharauliwa na hata kusemwa na ndugu wamwanamme kwa kuwa hajailetea faida familia au ukoo wao.

Maelezo katika nukuu hiyo hapo juu ni ithibati tosha kuwa wanawake wa Kiafrika

ndio wanaobebeshwa mzigo wa malezi ya watoto na pindi mwanamke huyo asipozaa

43 Bi. Salma Kayanga ni mwanajamii, mama wa familia na Afisa afya ofisi ya kata Kibeta.Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe 5.3.2020 ofisini kwake.

Page 82: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

69

basi yeye ndiye hupewa lawama za kutokuzaa. Pia, utafiti umebaini kuwa, falsafa ya

uzazi na ulezi imejitokeza katika vitendawili mbalimbali vya Kiswahili. Theobard44

alitega kitendawili kinachosawiri falsafa ya uzazi. Kitendawili kinasema:

a) Kitendawili: Dada yangu hazai mtoto mmoja mmoja, bali mapacha wengi

wakubwa kwa wadogo.

Jibu: Mapapai.

(Chanzo: Uwandani katika mjadala wa vikundi lengwa).

Katika Kitendawili hiki tunaona uwepo wa falsafa ya Kiafrika ambayo imejikita

kwenye uzazi. Akiendelea kufafanua kuhusu kitendawili hiki, Theobard45 (k.h.j)

katika mjadala anasema:

Hapa tunaiona falsafa ya uzazi ambayo inasisitiza umuhimu wa kuzaawatoto wengi. Kama mti wa mpapai unavyozaa matunda mengindivyo unavyofananishwa na uzazi wa watoto kwa Mwafrika. Hii nikwa sababu, Waafrika wanaamini katika uzazi wa watoto wengi kamaufahari na kwa kufanya hivyo, wanapanua ukoo na kuwa na familiapana.

Maelezo katika nukuu hiyo yanahibitisha kuwa, katika jamii za Kiafrika ni jambo la

kawaida kuzikuta familia zenye watoto zaidi ya kumi. Hata hivyo, suala la malezi

husisitizwa na kuzingatiwa kwa jamii ili kuwaandaa watoto hao kuja kushika

majukumu ya jamii husika.. Familia yenye watoto wengi huwa imara na thabiti

katika nyanja mbalimbali. Pia, Clemens46 anatoa mfano mwingine wa kitendawili

chenye falsafa ya malezi. Kitendawili kinasema:

b) Kitendawili: Mama yangu kila aendako na mtoto wake mgongoni.

Jibu: Konokono.

(Chanzo: Uwandani katika mjadala wa vikundi lengwa).

Utafiti umebaini kuwa, kitendawili hiki kinasawiri suala la uzazi na malezi.

Kitendawili hiki kinamtaja mama na mtoto wake mgongoni. Kinaeleza kuwa, mama

44 Teodata Teobard ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Katerero iliyopaHalmashauri ya Wilaya ya Bukoba. Majadiliano na mtafiti yalifanyika tarehe 26.2.2020 shuleni hapo.45 Amekwishatajwa46 Filipo Clemens ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Katerero iliyopoHalmashauri ya Wilaya ya Bukoba. Majadiliano kati ya mtafiti na watafitiwa yalifanyikatarehe26.2.2020 shuleni hapo.

Page 83: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

70

huyu kila anapokwenda anakuwa na mtoto wake na katu hamwachi. Akisisitiza

kuhusu maudhui ya kitendawili hiki, Mwemezi47 katika mjadala alifafanua kuwa,

“kitendawili hiki kinaibua suala la mahusiano ya mama na mtoto katika mazingira

halisi ya maisha ya jamii. Mahusiano hayo yanadhihirika katika jamii zetu kwani

mama wa Kiafrika ndiye anayeonekana akijali sana kuhusu watoto wake kila wakati

kuliko baba”. Maelezo haya yanathibitisha kuwa, falsafa tunayoipata kwenye

kitendawili hiki ni ya malezi ya watoto katika jamii kwani ni jukumu la mama zaidi

ya baba. Falsafa ya uzazi na ulezi inaendelea kudhihirika katika kitendawili kingine

kinachosema:

c) Kitendawili: Bibi hutembea na mzigo wake, daima hautui chini.

Jibu: Kobe au konokono.

(Chanzo: Badru, 2015).

Japo kitendawili kinamtaja bibi, lakini ni suala la umri kwamba huyu bibi naye

alikuwa mama ambaye amefikia umri mkubwa wa kuitwa bibi. Utafiti umebaini

kuwa, kitendawili hiki kinasawiri suala la malezi ambapo bibi anawakilisha nafasi ya

mama katika malezi. Mara nyingi mama ndiye anayeonekana kulemewa na mzigo

wa malezi ya mtoto wake tangu anapozaliwa anamlea mpaka anapokuwa mtu mzima.

Kwa namna yeyote wazazi wa kike huwa tayari kufa na watoto wao katika mazingira

ya aina yeyote. Kitendawili hiki kinadhihirisha uwepo wa falsafa ya Kiafrika ya

uzazi na malezi. Aidha, kitendawili kingine ni kile kinachosema:

d) Kitendawili: Wakikua mama yao huwatupa nje kwa kishindo.

Jibu: Mbaazi au mnyonyo.

(Chanzo: Badru, 2015).

Katika kukichunguza kitendawili hiki, tumebaini uwepo wa falsafa ya Kiafrika juu

ya uzazi na malezi. Falsafa hii inasisitiza juu ya kuwa na watoto ambao wanapaswa

kupewa malezi bora. Medadi48 katika mjadala anafafanua maudhui ya kitendawili

hiki kwa kusema kuwa:

47 Venezuela Mwemezi ni mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari Kashai iliyopomanispaa ya Bukoba. Majadiliano na watafitiwa hao yalifanyika tarehe 25.2.2020 shuleni hapo.48 Dicksoni Medadi ni mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Katerero iliyopoHalmashauri ya wilaya ya Bukoba. Majadiliano na watafitiwa yalifanyika tarehe 26.2.2020 shulenihapo.

Page 84: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

71

Tukikitazama kitendawili hiki, tunabaini wazi uwepo wa falsafa yauzazi na ulezi. Hapa tunaona namna wazazi (mama)wanavyohakikisha malezi ya watoto kuwa yako sawa ndipo huwaachaili wakajitegemee. Hii ina maana kuwa wakiwa wadogo wanakuwakatika uangalizi wa mama mpaka pale watakapokuwa wakubwa nakuweza kujitegemea.

Maelezo katika nukuu hiyo yanaonesha namna kitendawili hiki kinavyosawiri falsafa

ya ulezi wa watoto na kwamba, watoto hao tangu wakiwa wadogo, wanakuwa katika

mikono ya malezi ya mama zao.

Kwa kuhitimisha hoja hii, utafiti umebaini baadhi ya vitendawili vya Kiswahili

vinavyosawiri falsafa ya uzazi na malezi. Falsafa hii inasisitiza umuhimu wa jamii

kuwa na watoto na pia, watoto hao kupewa malezi bora. Aidha, kupitia nadharia ya

Kisosholojia katika msingi wake unaosisitiza kuwa, fasihi haiwezi kujitenga na jamii

ambayo kwayo imechipuzwa; tumeweza kuthibitisha kuwa, falsafa ya Kiafrika

haitoki katika ombwe, bali hutoka katika jamii husika. Hii ni kwa sababu vitendawili

tulivyovitumia katika hoja yetu vimedhihirisha suala la malezi ya watoto katika jamii

za Kiafrika kuwa ni jukumu la mama zaidi kuliko baba. Kwa hiyo, vitendawili hivi

ni mali ya jamii kwani yanayozungumzwa ndani yake yanahusu jamii husika. Hivyo,

tunaweza kuhitimisha hoja zetu kwa kusema kuwa, falsafa mbalimbali zilizojadiliwa

katika sehemu hii zimedhihirika vema katika vitendawili vya Kiswahili.

4.4 Athari za Falsafa ya Kiafrika kwa Jamii Kama Inavyosawiriwa katika

Vitendawili vya Kiswahili

Athari za falsafa ya Kiafrika zimeweza kuthibitika kupitia matendo mbalimbali ya

jamii. Kila jambo linalofanywa na jamii kwa kuzingatia mila na desturi za Waafrika

linaakisi falsafa yao. Kupitia mahojiano, pamoja na vitendawili vilivyochambuliwa

na kusawiri falsafa ya Kiafrika, mtafiti ameweza kutathmini athari zitokanazo na

falsafa ya Kiafrika kwa jamii kama zinavyosawiriwa katika vitendawili vya

Kiswahili. Athari hizo zipo katika namna mbili yaani uzuri na ubaya wake. Mtafiti

ameziita athari chanya kwa upande wa yale mazuri na athari hasi kwa upande wa

ubaya. Ufafanuzi kuhusu athari hizo ni kama ifuatavyo:

Page 85: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

72

4.4.1. Athari Chanya za Falsafa ya Kiafrika kwa Jamii

Fasihi ni zao la jamii hivyo, chochote kinachosawiriwa katika kazi za fasihi ni kwa

ajili ya jamii. Inaweza kuwa ni katika kuonya, kuelimisha au kukosoa jamii katika

mambo mbalimbali. Kupitia vitendawili vya Kiswahili, utafiti huu umebaini kuwa,

falsafa ya Kiafrika ina athari kubwa kwa jamii. Miongoni mwa athari hizo ni kama

vile kuhifadhi na kurithisha amali za kitamaduni za jamii husika, kudumisha umoja

na mshikamano miongoni mwa wanajamii, kulinda maadili ya jamii. Maelezo

yaliyoko hapa chini ni ufafanuzi wa athari chanya za falsafa ya Kiafrika kama

inavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili.

4.4.1.1 Inasaidia Kudumisha Umoja na Mshikamano

Utafiti huu umebaini kuwa, falsafa ya Kiafrika inayopatikana katika vitendawili vya

Kiswahili inasaidia kudumisha umoja na mshikamano miongoni mwa wanajamii. Hii

inatokana na sababu kwamba, matukio mbalimbali ya kijamii yanayotokea kama

misiba au sherehe huifanya jamii nzima kuweza kushiriki katika shughuli hizo. Kwa

mfano kifo kama kipengele kimojawapo cha falsafa ya Kiafrika huwakumbusha watu

kukumbuka uhalisia wa jambo lenyewe na hivyo kuwahamasisha kushiriki kwa dhati.

Kwa kuwa wao ni binadamu ni binadamu na wanaamini ipo siku nao watafikwa na

umauti au wapendwa wao watapoteza maisha na hivyo, watahitaji msaada wa watu

wengine. Jambo hili lilithibitishwa na Bw. Jonas49 anaposema:

Masuala haya ni endelevu kwa sababu tangu mababu zetuwamekuwa wakiishi kwa misingi hii. Mta akipata tatizo wanajamiitunasaidiana kulitatua. Akiwepo mtu asiyeshirikiana na wenzakebasi jamii humtenga kwa maana kwamba mtu huyo atakapopatwana tatizo lolote hatapata ushirikiano mzuri kutoka kwa wenzake.Kutokana na adhabu hii humfanya mtu huyo kubadilika na kuishikulingana na taratibu ambazo jamii imejiwekea.

Maelezo katika nukuu hiyo yanathibitisha kuwa, jamii hushinikiza watu kushirikiana

katika kutatua matatizo mbalimbali ya kijamii. Kwa kufanya hivyo, wanadumisha

umoja na mshikamano na kuwafanya wanajamii kushiriki kikamilifu katika shughuli

mbalimbali za kijamii zinazotokea katika jamii yao. Kwa hiyo, suala la umoja na

ushirikiano kwa jamii za Kiafrika huendelea kudumishwa kwa njia hiyo. Hii

49 Bw. Philbert Jonas ni mwanajamii na mtumishi wa kiroho katika Taasisi ya Adolph KolpingSocieties of Tanzania Jimbo Kuu la Katoliki Bukoba. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe2.3.2020 mtaa wa Kamizilente- Rwamishenye.

Page 86: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

73

inatokana na kaida walizojiwekea ambazo kila mwanajamii huishi kwa misingi ya

taratibu hizo.

Aidha, suala la kudumisha umoja na mshikamano kama linavyodhihirika katika

kitendawili kilichojadiliwa kipengele 4.3.1 uk 49 kinaonesha kuwa suala la umoja na

ushirikiano katika jamii ni nguzo katika kufanikisha kukamilika kwa jambo fulani

kwa muda mfupi. Jambo hili lilibainishwa pale Bi. Tiimanywa50 alipoeleza kuwa,

“Faida ya kufanya kazi kwa kushirikiana ni pamoja na kufikia mafanikio kwa muda

mfupi. Kazi inayofanywa na kundi la watu lililoungana haiwezi kulingana na mtu

mmoja. Hivyo basi, hapa tunasisitizwa kufanya kazi kwa kushirikiana ambapo kwa

kufanya hivyo tunadumisha na kuuendeleza umoja wetu. Kitendawili kingine chenye

falsafa ya Kiafrika kinasema:

50 Atugonza Tiimanywa ni mwanajamii na mfanyabiashara katika wilaya ya Bukoba. Anaishi katikamtaa wa National Housing kata ya Kashai. Mahojiano kati yake na mtafiti yalifanyika tarehe 2.3.2020ofisini kwake.

Page 87: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

74

a) Kitendawili: Nina wanangu watatu, mmoja akiondoka wawili

hawafanyi kazi.

Jibu: Mafiga.

(Chanzo: Salla, 2014).

Suala la umoja na ushirikiano linalojitokeza katika kitendawili hiki inasababisha

athari katika kudumisha umoja huo ili kuleta maendeleo ya jamii. Kitendawili

kinaonesha kuwa, watoto hawa watatu wanaishi kwa kutegemeana na kila mmoja

ana nafasi katika maisha ya mwingine. Vivyo hivyo, katika jamii ya Waafrika, Bw.

Byabato51 alifafanua kuwa, “kila mtu ana nafasi yake katika maisha ya mtu

mwingine kiasi kwamba akiondoka wanaobaki hawawezi kufanya kazi hiyo kwa

ufanisi”. Hapa tunaona kuwa tunapoungana tunakuwa na uwanja mkubwa wa kufikia

mafanikio ukilinganisha na kutoungana.

Katika kuhitimisha hoja hii tunaweza kusema kuwa, mojawapo ya athari ya falsafa

ya Kiafrika katika jamii ni pamoja na kusisitiza umoja na mshikamano. Jamii

inapaswa kufanya kazi kwa kushirikiana ili kufikia mafanikio haraka na kwa ufanisi

zaidi. Kwa hiyo, ni vizuri kuendeleza falsafa hii kutoka kizazi kimoja kwenda

kingine ili kuifanya jamii ya Waafrika kunufaika nayo. Hivyo basi, katika utafiti

wetu tumeona kuwa falsafa ya Kiafrika inayo athari kubwa katika jamii hasa katika

kudumisha umoja na mshikamano.

4.4.1.2 Inasaidia Kulinda Maadili ya Jamii

Utafiti umebaini athari nyingine za falsafa ya Kiafrika kwa jamii ambayo ni kulinda

na kuikuza jamii katika maadili yanayofaa. Imebainishwa katika utafiti huu kuwa,

kila mtu, jamii au taifa kwa ujumla hutakiwa kuwa na maadili mema na huishi kwa

misingi ya maadili ya jamii. Utafiti umegundua kuwa, vipengele mbalimbali vya

falsafa ya Kiafrika vinavyojitokeza katika vitendawili vya Kiswahili husaidia katika

kulinda maadili ya jamii kwa kuikumbusha jamii kuzingatia kanuni na taratibu

zilizowekwa. Kukumbusha huku ndiko huifanya jamii kuwa na maadili mema pindi

wanapozifuata taratibu hizo. Kwa mfano katika kitendawili kilichojadiliwa kipengele

4.3.2 uk 53 kimejikita katika imani kuwa ndugu wa damu kwa Waafrika hawaoani

51 Amos Byabato ni mwanajamii wa wilaya ya bukoba anayeishi kata ya Hamugembe mtaa waomukishenye. Mahojiano kati yake na mtafiti yalifanyika tarehe 5.3.2020 nyumbani kwake.

Page 88: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

75

wala kuwa na uhusiano wa kimapenzi. Hivyo, suala la miiko ambayo inatokana na

uzingatizi wa maadili ya jamii katika suala la ndoa na mahusiano kama

inavyojitokeza katika kitendawili hicho linaifanya jamii kuwa na hofu juu ya

masuala ya mahusiano na ndugu. Kama ilivyofafanuliwa na Bw. Rwekaza52 (k.h.j)

kuwa, “kwa kufanya hivyo siku zote watoto wa Kiafrika wamekuwa wakiishi kwa

kuheshimu maadili hayo kuwa, dada au kaka hata awe mzuri kiasi gani haupaswi

kumfikiria katika masuala ya kimapenzi ni katazo katika jamii ya Kiafrika”. Kwa

hiyo, jamii inaishi kwa kufuata misingi ya maadili hayo na hivyo, kuikuza jamii

katika maadili yanayofaa. Mfano mwingine wa kitendawili ni kile kinachosema:

a) Kitendawili: Nimeuona mti mmoja mzuri lakini kuukata nashindwa.

Jibu : Dada yako.

(Chanzo: Salla, 2014).

Kitendawili hiki kinaeleza kuhusu mti mzuri ambao msemaji ameuona, lakini anakiri

kushindwa kuukata mti huo. Maswali yanayozuka katika hili ni kuwa kwa nini

ashindwe kuukata? Je huo ni mti wa aina gani? Jibu linalotolewa linajibu maswali

tuliyojiuliza kwa sababu huenda kutokana na kuzingatia maadili ya Kiafrika ndio

maana msemaji anasema hawezi kuukata mti huo akimaanisha kuwa hawezi kuwa na

mahusiano ya kimapenzi na ndugu yake huyo. Kwa kuendelea kufuata miiko hii,

ndiyo kunaifanya jamii kulinda maadili yao.

Aidha, kupitia mahojiano na watafitiwa walieleza kuwa, masuala ya kimaadili

huenda sambamba na kushika imani ya dini. Kwa hiyo, watu wakishika dini

hawawezi kufanya matendo maovu. Bw. Rwegasira53 (k.h.j) anathibitisha jambo hili

kwa kusema kuwa,

Katika jamii za Kiafrika watu wengi wameshika imani ya diniijapokuwa wanaonekana kutokuacha mizizi ya dini zao za jadi.Watu wengi wanashiriki ibada za kumwabudu mwenyezi Mungu.Mambo haya ni miongoni mwa nguzo zinazoshikilia falsafa yaKiafrika. Kushiriki katika masuala ya ibada husaidiakuwaunganisha na Mungu wao na kwa kuwa, wanaamini kuwaMungu ndiye mwenye nguvu na mamlaka iliyo kuu, basi

52Hasimu Rwekaza ni mwanajamii katika wilaya ya Bukoba kata ya Hamugembe mtaa wa Nyangoye.Mahojiano kati yake na mtafiti yalifanyika tarehe 4.3.2020 nyumbani kwake.53 Keshatajwa hapo awali. Mahojiano na mtafiti yalifanyika tarehe 6.3.2020.

Page 89: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

76

wanadamu wanapaswa kutenda kulingana na matakwa ya Mungu.Wakifanya kinyume wataadhibiwa na Mungu. Hii inasaidia katikakutenda mambo mema ya kimaadili na kuepuka kutenda maovu.

Maelezo katika nukuu hii yanathibitisha kuwa, watu wanaoshika dini kikamilifu

wapo mstari wa mbele katika kutenda matendo mema na maisha yao hujengeka

katika misingi ya kimaadili. Kwa kufanya hivyo, wanalinda maadili ya jamii na

kuikuza jamii katika maadili yanayofaa.

Kwa kuhitimisha hoja hii, tunaweza kusema, falsafa ya Kiafrika ina athari chanya

katika maisha ya jamii. Kulingana na athari hiyo, ndiyo maana falsafa hii imeendelea

kurithishwa kizazi kimoja kwenda kingine. Falsafa ya Kiafrika inasaidia katika

kulinda na kuendeleza maadili mema ndani ya jamii ili kuleta amani. Jamii yeyote

iliyo na amani hutokana na uimara wa maadili yaliyopo ambayo yanaifanya jamii

hiyo kuepukana na vitendo viovu kama wizi, ukabaji, umalaya, na mambo mengine

yanayofanana na hayo. Hivyo basi, tunaweza kusema kuwa ufafanuzi wa hoja hii

hapo juu ni ithibati kuwa, falsafa ya Kiafrika ina athari chanya kwa jamii ya Kiafrika.

4.4.1.3 Inasaidia Kutambulisha Jamii ya Waafrika Ndani na Nje ya Afrika

Maelezo na ufafanuzi kuhusu falsafa ya Waafrika kwa ujumla yameweza

kuwapambanua waafrika katika mawanda mapana ya kiutamaduni. Waafrika

(Wabantu) wamejibainisha kupitia falsafa waliyonayo inayopambanua imani na

mitazamo yao katika vipengele mbalimbali vya falsafa. Utafiti umebaini kuwa,

falsafa ya Kiafrika kama ilivyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili inasaidia

watu kupata elimu kama mojawapo ya njia ya kufundisha jamii nyingine kuhusu

mawazo na mitazamo ya Waafrika juu ya mambo mbalimbali. Kwa mfano masuala

ya uduara, maadili, “uchawi na ushirikina”, uzazi na ulezi, kifo na maisha baada ya

kifo ni mambo yanayowashughulisha sana Waafrika. Mathalani, kitendawili

kinachosawiri suala la maadili lilichojadiliwa katika kipengele 4.3.2 (uk 54)

kinatambulisha suala la maadili ya Waafrika yanayowakataza kuwa na mahusiano ya

kimapenzi na ndugu wa damu. Aidha, mawazo haya yanashadidiwa na Bw. Katto54

anapoeleza kuwa:

54 Bw. Vedasto Katto ni mwanajamii wa wilaya ya Bukoba anayeishi kata ya Hamugembe mtaa waomukishenye. Mahojiano kati yake na mtafiti yalifanyika tarehe 2.3.2020 nyumbani kwake.

Page 90: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

77

Jamii inatambua kuwa ndugu wa damu hawawezi kuoana. Ikifikiasuala la kuoa, kijana anatakiwa kumtafuta mtu wa koo tofauti kabisana akishampata anatakiwa kuwataarifu wazee ili apate ruhusa yaokama anaweza kumwoa huyo mtu au la. Hii inasaidia kulinda maadiliili vijana wasije wakaoa ndugu zao mwisho wa siku ikawa aibu nalaana kwa familia.

Maelezo katika nukuu hiyo yanadhihirisha miiko ya Waafrika katika masuala ya

ndoa na mahusiano na hivyo, yanatambulisha falsafa ya maadili ya Kiafrika kwa

Waafrika wenyewe na kwa jamii nyingine zisizo za Kiafrika. Kwa hiyo falsafa ya

Kiafrika ina athari katika kutambulisha jamii za Kiafrika ndani na nje ya Afrika kwa

ujumla.

4.4.1.4 Inasaidia Kuhifadhi na Kurithisha Amali za Kitamaduni za jamii

Utafiti huu umebaini kuwa, falsafa ya Kiafrika inasaidia katika kutunza na kurithisha

amali za jamii kama vile mila na desturi. Mlacha (1996) anaeleza kuwa, usambazaji

na utunzaji wa mila na desturi unaweza kufanyika kwa njia nyingi na kwa viwango

tofauti. Njia hizo zaweza kuwa kwa mapokezi ya mdomo au kwa maandishi.

Utunzaji na usambazaji huo unaweza kuwa kwenye kiwango cha familia moja, kwa

jamii moja au hata baina ya jamii moja na nyingine. Matokeo ya utafiti huu

yamebaini kuwa, athari hii ya falsafa ya kuhifadhi na kurithisha amali za

kiutamaduni imeweza kuthibitika kutokana na mifano ya vitendawili mbalimbali

iliyojadiliwa katika kipengele 4.3. Aidha, kupitia mahojiano na watafitiwa, suala hili

limethibitika pale Bw. Rwezaula55 anapoeleza kuwa, watoto wa jamii za Kiafrika

wanalelewa katika misingi ya dini ambao humo hufunzwa kutii na kuheshimu wazazi.

Anasema:

Suala la utii linaenda sambamba na heshima kwani kuwezi kutiikama hujamheshimu mtu huyo. Kupitia dini watoto wanafunzwakutii na kuheshimu wazazi wao na watu wanaowazidi umri. Hiiinawajengea unyenyekevu na kutokuwa na kiburi. Vilevile utii kwaupande wa wakubwa unajitokeza katika shughuli mbalimbali zakijamii zinazojitokeza. Imejengeka kasumba kuwa mtu apatapotatizo tunasaidiana kulitatua tatizo hilo na kwa namna hiyo tunatiikulingana na utaratibu tuliojiwekea.

55 Bw. Kamugisha Rwezaula ni mwanajamii wa wilaya ya Bukoba. Aliwahi kuwa mtumishi wa ummakatika Ofisi ya Kata ya Kibeta mtaa wa Magoti; pia ni mzee wa kimila. Mahojiano na mtafitiyalifanyika tarehe 2.3.2020 mtaa wa Kamagera – Kibeta.

Page 91: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

78

Maelezo katika nukuu hiyo ni ithibati tosha kuwa, falsafa ya maadili inayo athari

yake inayoonekana kwa jamii za Kiafrika zinazoishi kwa kufuata mila na desturi zao.

Jamii za Kiafrika zinatambua kwamba, vijana hawawezi kutimiza wajibu wao

endapo hawataandaliwa vema. Hivyo basi, katika jamii suala la kurithisha amali za

jamii limekuwa endelevu. Kizazi kilichopo kimerithishwa falsafa ya jamii hiyo na

hutegemewa kuendelea kurithisha amali hizo za kifalsafa kwa vizazi vinavyofuata

kupitia vitendawili vya Kiswahili.

4.4.1.5 Inasaidia wanajamii kushika imani ya dini

Mbali na maadili, suala la imani katika Mungu na mizimu kama kipengele

kimojawapo cha falsafa ya Waafrika kimeelezwa kuwa na athari chanya kwa jamii.

Utafiti huu umebaini kuwa, wanajamii wa wilaya ya Bukoba ambao ni kiwakilishi

cha jamii za Waafrika wameshika imani ya dini ya Kikristo na Kiislamu. Pia, wapo

wanaoamini katika mizimu. Mbali na kushiriki katika ibada kwenye makanisa na

misikiti yao, wamekuwa pia wakiomba mizimu. Hivyo, kupitia imani kuwa yupo

Mungu, na kwa kuwa wanatambua kuwa Mungu ndiye mwenye nguvu na mamlaka

iliyo kuu, basi wanadamu hutenda kulingana na matakwa ya Mungu. Kwa mfano

kitendawili kinachobainisha falsafa ya imani katika Mungu katika kipengele 4.3.4

(uk 62) kinaonesha namna Waafrika wanavyoishi kwa kutambua kuwa Mungu ndiye

mwenye mamlaka iliyo kuu, hivyo inamlazimu mwanadamu kutii na kufuata

mapenzi ya Mungu ambayo yanajengwa katika misingi ya mambo mema

yanayokubalika. Pia, wanatambua kuwa Mungu na wahenga wanaona kila jambo

baya au zuri analofanya mwanadamu kwa hiyo yule anayetenda mabaya ataadhibiwa

na wahenga hao. Hii inasazidia wanajamii wengi kuishi kwa kufuata misingi sahihi

ya jamii na kuogopa kukiuka taratibu za jamii yao kwa hofu ya kupewa adhabu kali

na wahenga. Kupitia imani hizo, inawafanya wanajamii hao washike kikamilifu

imani ya dini na hivyo kutenda mamtendo mema yanayokubalika katika jamii.

4.4.2. Athari Hasi za Falsafa ya Kiafrika kwa Jamii

Matokeo ya utafiti huu yamebainisha kuwa, falsafa ya Kiafrika kwa upande

mwingine huweza kusababisha athari hasi kwa jamii. Miongoni mwa athari hasi hizo

ni kuchochea vitendo vya uvunjifu wa amani, kukwamisha maendeleo ya jamii na

kuendeleza ukoloni. Ufuatao ni ufafanuzi wa athari hizo kama zinavyojitokeza katika

vitendawili vya Kiswahili.

Page 92: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

79

4.4.2.1. Kuchochea Vitendo vya Uvunjifu wa Amani katika Jamii

Utafiti umebaini kwamba, imani kuhusu masuala yahusuyo “uchawi” na “ushirikina”

huweza kusababisha uvunjifu wa amani kwa baadhi ya jamii za Kiafrika. Kupitia

mahojiano na watafititwa pamoja na vitendawili mbalimbali, utafiti umebaini kuwa,

jambo hili linatokana na sababu kwamba, watu wenye hasira kali wamekuwa

wakijichukulia sheria mkononi kwa kuwaua watu wanaohisiwa kuwa wachawi kama

vikongwe. Pia, mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yanatokana na sababu za

“kishirikina” zinazohusisha watu wanaofanya ramli chonganishi. Kuwepo kwa imani

ya “uchawi” kunachochea maovu kutendeka ndani ya jamii juu ya wahusika wa

“uchawi” na “ushirikina”. Masuala ya uchawi kama yalivyodhihirika katika

kitendawili kilichojadiliwa katika kipengele 4.3.6 (uk 67) yanaonesha kuwa uchawi

na wachawi hawakubaliki na wanapingwa katika jamii. Pindi wanajamii

wanapobaini kuwa mtu fulani ni mchawi huweza kumshambulia na kumdhuru.

Matokeo ya jambo hili huweza kusababisha umwagaji wa damu wa watu wasio na

hatia kwani uchawi hauonekani na hauwezi kuthibitika kisayansi. Iwapo kila mmoja

atajichukulia sheria ya kumdhuru mwanadamu mwenziwe anayemhisi kuwa ni

mchawi huweza kusababisha kupotea kwa amani. Aidha, matokeo ya utafiti huu

kupitia mahojiano yalibainisha kuwa, suala la uchawi halikubaliki na linachangia

katika kuchochea vitendo vya uvunjifu wa amani katika jamii. Haya yanathibitika

pale Bi. Mnyambo56 anaposema:

Imedhihirika katika jamii ya Tanzania baadhi ya mikoa yakitokeamauaji ya wazee na vikongwe waliodhaniwa kuwa wachawi kwasababu mbalimbali. Vilevile, imani kuhusu masuala yanayohusuushirikina yamesababisha kutokea kwa matukio mbalimbaliyanayohusu mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino)kutokana na sababu za kishirikiana na ramli chonganishi zawaganga wa jadi wasiokuwa na maadili. Pia wapo walewanaotafuta utajiri kupitia njia za kishirikina. Kutokana na kutakautajiri wa haraka wengi wao wamejikuta wakiwauwa ndugu zao ilikupata mali. Matokeo ya hili ni kupoteza nguvu kazi ya jamiikutokana na mauaji hayo. Masuala haya yalihusishwa na imani zakishirikina za watu wachache katika kupata utajiri. Pindi inapokujakujulikana kuwa kuna mtu kama huyo anayeua ndugu zake kwaajili ya mali huweza kupewa adhabu na hata kumuua.

56 Bi..Schola Mnyambo ni mwanajamii, mama wa familia na mjasiriamali mdogo wa wilaya yaBukoba. Mahojiano kati yake na mtafiti yalifanyika tarehe 6.3.2020 mtaa wa Kamagera- Kibeta.

Page 93: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

80

Maelezo katika nukuu hiyo yanaonesha kuwa, masuala ya uchawi katika jamii

hayakubaliki na hivyo uwepo wa wachawi unasababisha au kuchochea vitendo vya

uvunjifu wa amani na kupelekea mauaji. Kwa namna hiyo, tunaona falsafa hii ya

“uchawi na ushirikina” inasababisha uvunjifu wa amani ndani ya jamii.

4.4.2.2 Kukwamisha Maendeleo ya Jamii

Athari mojawapo inayosababishwa na falsafa ya ““uchawi na ushirikina”” katika

jamii ni kukwamisha maendeleo ya jamii. Utafiti umebaini kwamba, jambo hili

linatokana na hofu ya baadhi ya wanajamii kuhusu masuala yahusuyo uchawi.

Wachawi wengi hawapendi maendeleo ya watu wengine ndio maana suala la

“uchawi” halikubaliki katika jamii. Kwa mfano, kama kitendawili kilivyofafanuliwa

katika kipengele 4.3.6 (uk 68) kinaonesha kuwa uchawi haukubaliki katika jamii za

Kiafrika na hivyo unapingwa vikali. Baadhi ya watu waishio kwenye vijiji ambavyo

watu wake wanashikilia masuala ya “uchawi” huogopa hata kujenga nyumba nzuri

huko vijijini kwa kuhofia kulogwa. Kwa asilimia kubwa, “uchawi” unapotumiwa

vibaya huleta madhara makubwa ndani ya jamii. Madhara hayo ni pamoja na

upotevu wa mali, mauaji, magonjwa, kukosekana kwa amani na mambo mengine

yanayofana na hayo. Pia, hofu kuhusu kifo inaweza kukwamisha maendeleo ya jamii

kwani mtu anaweza kuhofia kufanya vitu vya maendeleo kwa imani kuwa atakufa na

kuziacha mali zote alizozichuma. Falsafa hii siyo nzuri kwa msakabali wa maendeleo

ya jamii kwani, kuufuata mtazamo huu wa kifalsafa kunaweza kurudisha nyuma

maendeleo ya jamii.

Hapa tunajifunza kuwa, falsafa ya Kiafrika kuhusu masuala ya “uchawi na

ushirikina” bado yanafanya kazi katika jamii na hivyo kusababisha athari kwa namna

moja au nyingine. Kutokana na maelezo haya tunaona ni jinsi gani falsafa ya

Kiafrika (““uchawi na ushirikina””) inasababisha madhara kwa jamii na kurudisha

nyuma maendeleo ya jamii. Athari hii pia, inaweza kutokea kutokana na falsafa ya

imani kuhusu kifo kama ilivyofafanuliwa hapo juu.

4.4.2.3 Inasababisha Hofu na Mashaka kwa Wanajamii

Utafiti huu umebaini kuwa, falsafa inayohusu “uchawi na ushirikina” kama

ilivyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili inaweza kusababisha hofu na

mashaka kwa jamii hasa kwa kuhofia kuwa wachawi wanaweza kutumia nguvu zao

Page 94: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

81

na kuja kuwaroga pindi wafanyapo mambo makubwa kuwashinda wao kwa kuwa

wachawi hawapendi maendeleo ya watu wengine. Kwa mfano katika kitendawili

kilichofafanuliwa katika kipengele 4.3.6 uk 67 imedhihrika kuwa wachawi hufanya

shughuli zao za kichawi nyakati za usiku kwa kuwa ni jambo ovu ambalo

halikubaliki ndani ya jamii. Kwa hiyo, wanajamii huwa na hofu kutembea nyakati

hizo au hata wakilala huomba ulinzi wa Mwenyezi Mungu dhidi yao wakiamini

kuwa wachawi wanaweza kuja kuwadhuru wakati wakiwa wamelala. Pia, imani za

kishirikina zinazohusisha mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino)

zinasabaisha watu hao kuishi kwa hofu na mashaka katika jamii. Akitolea mfano

katika mahojiano Bi. Mnyambo57 (k.h.j) katika suala hili anasema kuwa, “baadhi ya

wanafamilia wenye mtoto mwenye ulemavu wa ngozi wamekuwa wakiishi kwa

mashaka wakijua kuwa mtoto wao anaweza kukamatwa na watu wanaotumwa

kupeleka viungo vya albino kwa waganga wa kienyeji kwa ajili ya kupata utajiri.”

Hali hii inasababisha watu wengine kukimbia makazi yao na kwenda kuishi mbali

kwa kujificha ili wasionekane. Kwahiyo, kupitia imani hizi za kishirikina huwafanya

wanajamaii kuishi kwa hofu na mashaka kama athari hasi ya falsafa ya Kiafrika.

Kwa jumla mawazo haya yanashadidiwa na nadharia ya Kisosholojia kupitia msingi

wake unaoona kuwa, fasihi haiwezi kujitenga na jamii kwani dhima yake ni

kuyamulika matendo ya jamii na kuyaweka bayana. Hivyo, kupitia vitendawili vya

Kiswahili tumeweza kubaini mawazo, imani na mitazamo mbalimbali ya Waafrika

juu ya mambo mbalimbali. Aidha, mitazamo hiyo ina athari kwa jamii kama utafiti

huu ulivyotathmini hapo juu. Athari za falsafa ya Kiafrika kupitia vitendawili

huzikumba jamii moja kwa moja kwa kuwa falsafa hizo ni amali ya jamii.

4.5 Muhtasari wa Sura ya Nne

Sura hii imejadili kwa kina matokeo ya data zilizokusanywa uwandani na maktabani

kutokana na malengo matatu mahsusi ya utafiti huu. Lengo kuu la utafiti huu

lilikuwa ni kuchunguza usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka

vitendawili vya Kiswahili. Mjadala wa matokeo ya utafiti huu umejikita katika

malengo matatu mahsusi. Nayo ni; Mosi, kubainisha vijenzi vya falsafa ya Kiafrika

katika muktadha wa kitamaduni. Hapa utafiti umebainisha mambo mbalimbali

57 Bi..Schola Mnyambo ni mwanajamii, mama wa familia na mjasiriamali mdogo wa wilaya yaBukoba. Mahojiano kati yake na mtafiti yalifanyika tarehe 6.3.2020 mtaa wa Kamagera- Kibeta.

Page 95: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

82

yanayofanywa na Waafrika ambayo yanaitambulisha falsafa ya Kiafrika katika

muktadha wa kitamaduni. Vijenzi hivyo vimejitokeza katika masuala ya umoja na

ushirikiano, maadili, uhai na kifo, ndoa na uzazi, dhana ya uduara, imani katika

Mungu na mizimu; na “uchawi na ushirikina”. Mambo hayo kwa ujumla yanaijenga

falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni.

Pili, tumejadili falsafa ya Kiafrika kama inavyojitokeza katika vitendawili vya

Kiswahili. Hapa, utafiti umejikita katika ufafanuzi wa falsafa yenyewe kwa kuonesha

imani na mitazamo ya Waafrika kuhusiana na falsafa husika huku tukithibitisha kwa

mifano mbalimbali ya vitendawili vya Kiswahili. Miongoni mwa falsafa

zilizojadiliwa ni falsafa kuhusu umoja na ushirikiano, ““uchawi na ushirikina””,

uzazi na ulezi, falsafa ya uduara, falsafa ya kifo na uhai, falsafa kuhusu maadili

katika jamii na falsafa kuhusu imani katika nguvu za Mungu na mizimu.

Aidha, lengo la tatu lilikuwa ni kutathmini athari za falsafa ya Kiafrika kwa jamii

kama zinavyosawiriwa katika vitendawili vya Kiswahili. Athari hizo zimetathminiwa

katika pande mbili yaani athari hasi na athari chanya. Athari chanya ni zile

zinazohusiana na kutunza na kuhifadhi amali za kiutamaduni, kulinda maadili ya

jamii na kudumisha umoja na mshikamano katika jamii, kutambulisha jamii ya

Kiafrika ndani na nje ya Afrika na kushika imani za kidini. Aidha, kwa upande wa

athari hasi ni pamoja na kuchochea vitendo vya uvunjifu wa amani, kukwamisha

maendeleo ya jamii na kusababisha hofu na mashaka kwa jamii. Sura inayofuata

inatoa muhtasari wa tasnifu nzima, mahitimisho pamoja na kutoa mapendekezo ya

nini kifanyike katika tafiti zijazo..

Page 96: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

83

SURA YA TANO

MUHTASARI, HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

5.1 Utangulizi

Sura hii imejadili muhtasari wa tasnifu nzima ambapo mtafiti ameigawa katika

sehemu tatu. Sehemu ya kwanza ya sura hii inaeleza muhtasari wa tasnifu nzima,

sehemu ya pili inaonesha hitimisho na mchango wa utafiti huu katika jamii na

sehemu ya tatu inatoa maoni na mapendekezo kwa tafiti zijazo.

5.2 Muhtasari wa Tasnifu

Tasnifu hii imejadili kuhusu Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: Mifano

kutoka vitendawili vya Kiswahili. Utafiti huu umehusisha vitendawili vya Kiswahili

vinavyosawiri falsafa ya Kiafrika. Ripoti ya utafiti huu imewasilishwa katika sura

tano. Nazo ni utangulizi, mapitio ya maandiko na kiunzi cha nadharia, methodolojia,

uwasilishaji wa data na hitimisho. Utafiti huu umeonesha umuhimu wa vitendawili

kama amali za kifalsafa na hutumika katika kutunza, kuhifadhi na kurithisha amali za

kitamaduni za jamii.

Sura ya kwanza ni ya utangulizi wa tasnifu. Sura hii ya utangulizi imetoa ufafanuzi

wa vipengele muhimu katika utafiti wetu. Vipengele vilivyofafanuliwa katika sura

hii ni pamoja ufafanuzi wa istilahi muhimu zilizotumika katika utafiti, usuli wa tatizo

la utafiti na tamko la utafiti. Vipengele vingine vilivyojadiliwa ni malengo ya utafiti,

maswali ya utafiti, manufaa ya utafiti na mawanda ya utafiti.

Sura ya pili imejadili kuhusu kiunzi cha nadharia na mapitio ya maandiko

mbalimbali yaliyopitiwa na mtafiti ili kubaini pengo la utafiti huu kuhusu falsafa ya

Kiafrika katika vitendawili. Mapitio ya maandiko yamegawanywa katika makundi

matatu. Kundi la kwanza, linahusu falsafa ya Kiafrika kwa jumla, kundi la pili ni

falsafa ya Kiafrika katika fasihi na kundi la tatu ni maandiko kuhusu vitendawili vya

Kiswahili. Pia, mapengo ya utafiti yamebainishwa katika sura hiyo.

Sura ya tatu imefafanua methodolojia iliyotumika katika utafiti huu. Hii ni pamoja na

mbinu na zana mbalimbali zilizotumika. Sura imeeleza kuhusu usanifu wa utafiti,

mkabala wa utafiti, eneo la utafiti, walengwa wa utafiti, mbinu za ukusanyaji wa data,

uchanganuzi wa data, itikeli za utafiti na uhalali na uthabiti wa matokeo ya utafiti.

Page 97: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

84

Aidha, changamoto mbalimbali zilizojitokeza wakati wa ukusanyaji data pamoja na

namna zilivyotatuliwa zimefafanuliwa katika sura hiyo.

Sura ya nne ndiyo imebeba kiini cha utafiti huu. Sura hii inajibu maswali matatu ya

utafiti huu yaliyotokana na malengo mahsusi. Sura hii imeanza kwa kufafanua

kuhusu vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni. Utafiti

umebaini kuwa, Waafrika wanaishi kulingana na mila na desturi za jamii. Baadhi ya

mambo wanayoyafanya katika maisha ya kila siku yanajenga au kubeba falsafa yao

katika muktadha wa utamaduni. Mambo hayo yanajitokeza katika masuala ya umoja

na ushirikiano, suala la maadili katika jamii, dhana ya uhai na kifo, dhana ya uduara,

suala la uchawi, imani katika Mungu na mizimu na suala la ndoa na uzazi. Mambo

hayo ndiyo yanaijenga falsafa ya Kiafrika.

Lengo la pili limefafanua vipengele vya falsafa ya Kiafrika vinavyojitokeza katika

vitendawili vya Kiswahili. Baadhi ya vipengele vilivyojadiliwa ni falsafa kuhusu

umoja na ushirikiano wa Waafrika. Utafiti ulibaini kuwa, Waafrika hufanya mambo

mbalimbali kwa kushirikiana miongoni mwa wanajamii. Mtu akipata tatizo,

wanajamii huchukulia tatizo hilo kama ni la jamii nzima hivyo hushirikiana kulitatua.

Vipengele vingine ni kama vile, falsafa kuhusu umuhimu wa maadili katika jamii,

falsafa ya “uchawi na ushirikina” na falsafa ya uzazi na ulezi. Kikubwa zaidi ni

katika ushirikiano wa Waafrika ambao kwa namna nyingine unasababisha kuwa na

sura ya uduara kwa vitu na mambo mbalimbali ya kijamii wanayoyafanya. Uduara

wa Waafrika umejidhihirisha kupitia vitendawili vya Kiswahili wanavyovitumia

katika mazingira yao. Baadhi ya vitu vinavyotajwa katika vitendawili kama vile

nyumba na ngoma ni vya umbo la duara.

Aidha, lengo la tatu limejadili kuhusu athari za falsafa ya Kiafrika kwa jamii. Falsafa

ya Kiafrika ina athari nyingi kwa jamii kama zilivyofafanuliwa katika utafiti huu.

Mtafiti amefafanua athari za falsafa ya Kiafrika kwa jamii kama vile kutunza na

kuhifadhi amali za kitamaduni za jamii, kulinda maadili yanayofaa, kudumisha

umoja na mshikamano katika jamii, kuitambulisha jamii ya Waafrika na kushika

imani ya dini. Kwa upande mwingine, athari hasi za falsafa ya Kiafrika ni kama

kuchochea vitendo vya uvunjifu wa amani, kukwamisha maendeleo ya kijamii na

kusababisha hofu na mashaka kwa jamii.

Page 98: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

85

Sura ya tano ya tasnifu hii imejadili kuhusu muhtasari wa kazi nzima kwa ufupi

ambapo muhtasari huo umefafanua mwelekeo wa sura moja baada ya nyingine

zinazounda tasnifu hii. Aidha, hitimisho lililotolewa limejikita katika kueleza

mchango wa utafiti huu kwa jamii. Mwisho, ni mapendekezo yaliyotolewa juu ya

nini kifanyike katika jamii na kwa wanazuoni kwa jumla katika kutoa mchango wa

kuikuza na kuiendeleza sanaa ya vitendawili.

5.3 Hitimisho

Kutokana na matokeo ya utafiti huu, ni wazi kuwa dhana hasi ya baadhi ya

wataalamu kuhusu umuhimu wa vitendawili imepanuka. Hivyo, jamii itaweza

kuondokana na dhana hii na kutilia maanani umuhimu mkubwa wa vitendawili

katika jamii na uga wa fasihi.

5.3.1 Mchango Mpya wa Utafiti

Utafiti huu umejikita katika kuchunguza falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya

Kiswahili. Tafiti nyingi zilizofanyika katika uga wa fasihi na falsafa kwa ujumla

hazikuhusisha au kutambulisha vitendawili kama amali za kifalsafa za jamii. Utafiti

huu utawafanya wanazuoni kuondokana na ile dhana ya kuwa vitendawili havina

umuhimu mkubwa kwa jamii kama ilivyo misemo na methali hivyo kuchukulia

vitendawili kama sanaa yenye lengo la kuwaburudisha watoto tu. Matokeo ya utafiti

huu yameonesha kuwa vitendawili ni nyenzo muhimu katika jamii kwani hutumika

katika kutunza na kuhifadhi amali za kifalsafa za jamii.

Pia, utafiti huu ni mojawapo ya kazi nyingi zilizowashughulisha sana wanataaluma

katika kutetea falsafa ya Kiafrika na fasihi ya Kiafrika. Maandiko mbalimbali

pamoja na utafiti huu vinathibitisha uwepo wa falsafa ya Kiafrika unaodhihirika

kupitia kazi mbalimbali za fasihi simulizi na fasihi andishi kwa jumla. Hivyo, utafiti

huu utaweza kuondoa ile dhana ya wachache wanaowabeza na kudharau Waafrika

kuwa ni watu wasio na utamaduni wao na hivyo, hawana falsafa yao. Data

zilizochambuliwa na kuwasilishwa katika utafiti huu zimeweza kubainisha vipengele

vya falsafa ya Kiafrika katika vitendawili vya Kiswahili ambavyo ni zao la uzoefu

wa maisha yao katika mazingira yao.

Page 99: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

86

5.3.2 Utoshelevu wa Nadharia

Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya Kisosholojia. Nadharia hii imetumika katika

uchambuzi wa data hadi kupata matokeo ya utafiti kwa kutumia misingi ya nadharia

hii. Msingi mkubwa wa nadharia hii ni ule unaosisitiza kuhusu uhusiano wa fasihi na

jamii na kuona kuwa, fasihi haiwezi kujitenga na jamii bali ina mfungamano

mkubwa na maisha ya jamii. Kwahiyo, jambo linalosawiriwa katika fasihi limebeba

maisha halisi ya jamii kwa jumla. Kwa maana hiyo, falsafa ya jamii ya Kiafrika

imeweza kusawiriwa vema katika vitendawili vya Kiswahili vinavyotumika katika

jamii za Kiafrika. Pia, kuhusu kazi ya fasihi kama taswira ya kimazingira na

kitamaduni ambamo kazi hiyo imechipuka utafiti umeweza kutusaidia katika kupata

vijenzi vya falsafa ya Kiafrika katika muktadha wa kitamaduni.

5.4 Maoni na Mapendekezo kwa Tafiti Zijazo

Utafiti huu ulihusisha dhana kuu mbili ambazo ni falsafa ya Kiafrika na Vitendawili

vya Kiswahili. Kwa maana hiyo, utafiti huu umekuwa ni sehemu ndogo sana katika

fasihi simulizi ambayo ina tanzu nyingi na vipera vingi ambavyo yamkini ni muhimu

zaidi na vinahitaji utafiti wa kina. Hivyo, utafiti huu, unapendekeza kuwa, wataalamu

waone umuhimu wa vitendawili vya Kiswahili na vile vya lugha za kibantu na hivyo

kutilia maanani katika kutafiti zaidi eneo hili la vitendawili. Utafiti unaweza

kufanywa kwa kuchunguza Ontolojia ya Waafrika katika vitendawili Kiswahili na

vile vya lugha za kibantu. Pia, utafiti unapendekeza kuwa, bado kuna haja ya tafiti

nyingi zaidi kufanyika katika uga wa fasihi simulizi, ili kubaini ni kwa namna gani

tanzu za fasihi simulizi zinaweza kutumika kama darasa la kufunza na kuhifadhi

maarifa ya kifalsafa ya jamii za Waafrika.

Aidha, kwa upande wa falsafa ya Kiafrika, watafiti wa baadae wanaweza

kuchunguza zaidi katika tanzu nyingine za fasihi simulizi kama vile hadithi za

Kiswahili, maigizo, na ushairi wa Kiswahili na hivyo kuisheheneza zaidi fasihi

simulizi ya Kiswahili. Pia, vipengele vya falsafa ya Kiafrika vina mawanda mapana

sana. Ni dhahiri kuwa tafiti nyingine zinaweza kufanywa kwa kuchunguza kipengele

kimojawapo cha falsafa ya Kiafrika namna kinavyojitokeza katika utanzu mwingine

wa fasihi. Kwa mfano, utafiti unaweza kufanywa kwa kuchunguza kipengele cha

uchawi na uganga ambayo ni falsafa ya Waafrika namna kinavyojitokeza katika

ushairi wa Kiswahili.

Page 100: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

87

5.5 Muhtasari wa Sura ya Tano

Sura hii inahusu muhtasari, hitimisho na mapendekezo. Vipendele vilivyojadiliwa

katika sura hii ni utangulizi, muhtasari wa tasnifu nzima na hitimisho. Aidha,

mchango mpya wa utafiti umetolewa pamoja na utoshelevu wa nadharia. Mwisho,

sura hii imetoa mapendekezo kwa tafiti zijazo na muhtasari wa sura. Sehemu

inayofuata ni marejeleo ya kazi mbalimbali zilizopitiwa na mtafiti wakati wa

kuandika kazi hii.

Page 101: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

88

MAREJELEO

Amana, B. (2013). Vitendawili katika http://educationkenyan.Blogspot.com/2013/11/

vitendawili.html (imepakuliwa tarehe 17/1/2020).

Anaclet, A. O na Wenzake (1979). Utamaduni chombo cha maendeleo. Dar es

Salaam: Wizara ya Utamaduni.

Babbie, E. (1999). The Basics of Social Research. Belmont: Wadisworth Publishing

Company.

Badru, Z. A. (2015). “Taswira na Ubainishaji wa Mabadiliko ya Kiujumi katika

Vitendawili: Mfano wa Vitendawili vya Kiswahili”. Tasnifu ya Shahada ya

Uzamivu ya Sayansi ya Jamii katika Fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa).

Chuo Kikuu cha Dodoma.

Balisidya, M. L. Y. (1973). “Fasihi ya Kiswahili”. Katika Mulika. TUKI: Chuo

Kikuu cha Dar es salaam. Na. 2 uk 12-17.

Burke, K. (1941). The Philosophy of Literary Form: Studies in Symbolic Action.

Baton Rouge, Louisiana: Louisiana State University Press.

Chuachua, R. (2010). “Suala la Itikadi katika Riwaya za Shaaban Robert”. Tasnifu

ya Shahada ya Umahiri katika Fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa). Chuo

Kikuu cha Dodoma.

Chuachua, R. (2016). “Falsafa ya Riwaya za Shaaban Robert na Euphrase Kezilahabi

katika Muktadha wa Epistemolojia ya Kibantu”. Tasnifu ya Shahada ya

Uzamivu (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dodoma.

Damka, A. B. (2015). “Kuchunguza Dhima ya Vitendawili vya Jamii ya Wanyisanzu

wa Iramba, Singida, Tanzania”. Tasnifu ya Shahada ya Uzamili katika Kitivo

cha Fani na Sayansi Jamii (Haijachapishwa). Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Duwe, M. (2016). “Mdhihiriko wa Falsafa ya Uduara katika Sanaa za Maonyesho za

Jamii ya Wangoni”. Tasnifu ya Uzamili katika Fasihi ya Kiswahili

(Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dodoma.

Page 102: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

89

Enon, J. C. (1998). Educational Reseach; Statistics and Measurement. Kampala:

Makerere University.

Faustine, S. (2012). “Matumizi ya Mtindo wa Uhalisiamazingaombwe katika Riwaya

Teule za E. Kezilahabi: Dhima na Athari Zake kwa Hadhira”. Tasnifu ya

Shahada ya Uzamili ya Sayansi ya Jamii katika Fasihi ya Kiswahili

(Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dodoma.

Faustine, S. (2017). “Falsafa ya Waafrika na Mtindo wa Uhalisiajabu katika Riwaya

ya Kiswahili”. Tasnifu ya Shahada ya Uzamivu katika Fasihi ya Kiswahili

(Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dodoma.

Fautine, S. (2019). “Falsafa ya Waafrika kama Kijenzi cha Mtindo wa Uhalisiajabu

katika Riwaya za Kiswahili.” Katika Ponera, A. S & Badru, Z. A (Wah),

Koja la Taaluma za Insia: Kwa heshima ya Prof. Madumulla. Dar es salaam:

Karljamer Publishers Ltd.

Gay, L. R. (1987). Educational Research: Competence for Analysis and Application.

Ohio: Merril Publishing House.

Gyekye, K. (1987). An Essay on African Philosophical Thoughts. Philadephia:

Combridge University Press.

Hoppenau A. na Wenzake. (2009). “Kubadilisha Tamaduni za Kijerumani na za

Kitanzania”: Katika DTP & TYC (Wah), Mwongozo wa Utamaduni. German:

vol.1. Iliyosomwa tarehe 8/9/2020 katika http://www.beyondintractability.

org/action/essay.jsp?id=26234&nid=1186.

Hountondji, P.J. (2004). “Knowledge as a Development Issue”, katika A Companion

to AfricanPhilosophy. Blackwell Publishing. Ilisomwa Tarehe 12/7/2019

katika http:// philosophy.org/archive/manamba.

Hussein, E. (1976). Kinjekitile. Nairobi: Oxford University Press.

Jengo, E. na Wenzake. (1982). Falsafa ya Sanaa Tanzania. Dar es Salaam: Baraza la

Sanaa la Taifa Tanzania.

Page 103: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

90

Kaponda, G. J. (2018). “Ontolojia ya Kiafrika katika Mbolezi za Wanyasa.” Tasnifu

ya Shahada ya Umahiri katika fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa). Chuo

Kikuu cha Dodoma.

Katamba, L. (2011). “Utamaduni wa Kupeana Majina katika Jamii ya Wanyakyusa.”

Tasnifu ya Shahada ya Uzamili katika Fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa).

Chuo Kikuu cha Dodoma.

Khumalo, J. S. M. (1974). “Zulu Riddles”. Katika African Studies, vol. 33, Na. 4,

Uk 193-226.

Kombo, D. K na Tromp, D, L. (2006). Proposal and Thesis Writing and Introduction.

Nairobi: Pauliness Publications.

Kothari, C. R. (2009). Research Methodology, Methods and Techniques. New Delhi:

New Age Internation Publishing Ltd.

Kothari, C. R. (2004). Research Methodology. Methods and Techniques 2 Edition.

New Delh Wiley.

Mbiti, J. S. (1969). African Religion and Philosophy. London: Morrison and Gibb

Ltd.

________ (1975). Introduction to African Religion. Heinemann: University of

Michigan

Makame, S. F. (2016). “Matumizi ya Falsafa ya Usihiri katika Riwaya Teule za

Euphrase Kezilahabi.” Tasnifu ya Shahada ya Uzamili katika Fasihi ya

Kiswahili (Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Dodoma.

Page 104: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

91

Manala, J. M. (2004). “Witchcrafts and its Impact on Black African Christians”: A

Lacuna in the Ministry of Hervormde Kerk in Suidelike Africa. University of

South Africa. Katika http://www.researchgate.net/publication/45681425.

Ilisomwa tarehe 28.9.2020.

Menkiti, I. (1984). “Person and Community in African Traditional Thought”. Katika

R. Wright (mhariri). African Philosophy, An Introduction of Lanham. MD:

University Press of America.

Mgunda, J. M (2014). “Dhima ya Visasili katika Kuhifadhi na Kurithisha Amali za

Kitamaduni: Mifano kutoka kwa Wasukuma.” Tasnifu ya Shahada ya

Uzamili katika Fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa) Chuo Kikuu Cha

Dodoma

Mlacha, S. A. K (1996). “Utamaduni wa Mwafrika katika Riwaya ya Bwana

Myombekere na Bibi Bugonoka.” Katika Kiango, J.G na Masabo, Z. N (Wah)

Mulika 23. TUKI: Dar es salaam.

Mlelwa, A. A (2017). “Falsafa ya Kiafrika katika Vitabu Teule vya Fasihi ya

Kiswahili: Dunia Uwanja wa Fujo na Ngoma ya Ng’wanamalundi”. Tasnifu

ya Shahada ya Umahiri katika Fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa). Chuo

Kikuu cha Dodoma.

Mng’aruti, T. K. (2008). Fasihi Simulizi na Utamaduni: Kitabu cha Walimu na

Wanafunzi (Shule na Vyuo). Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation.

Mshana, S. K (2015). “Kuchunguza Usawiri Chanya wa Mwanamke katika

Vitendawili vya Jamii ya Wanyiha”. Tasnifu ya Shahada ya Umahiri katika

Fasihi ya Kiswahili. (Haijachapishwa) Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Mulokozi, M. M (2017). Utangulizi wa Fasihi ya Kiswahili. Dar es salaam:

KAUTTU

Mungah, C. I. (1999). “Dhana ya Maisha katika Novela mbili za Kezilahabi: Nagona

na Mzingile”. Tasnifu ya Shahada ya Umahiri katika Fasihi.

(Haijachapishwa). Chuo Kikuu cha Nairobi.

Page 105: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

92

Narizvi, S. (1982). The Sociology of Literature of Politics. Nairobi: Standard

Textbooks Graphics and Publishing Company.

Ponera, A. S. (2016). “Suala la Matumizi ya Nadharia kama Kiunzi cha Tafiti za

Kitaamuli: Mfano wa Matumizi ya Nadharia ya Ukanivali”. Katika Jounal of

Humanities, vol.3, The University of Dodoma.

Ponera, A. S. (2019). Misingi ya Utafiti wa Kitaamuli na Uandishi wa Tasnifu.

Dodoma: Central Tanganyika Press.

Salla, H. D. (2014). Vitendawili vya Kikwetu. Dar es salaam: African Proper

Education Network

Samwel, M. (2015). Umahiri katika Fasihi ya Kiswahili: Mwongozo kwa

Mwanafunzi na Mwalimu wa Fasihi Simulizi na Andishi. Dar es Salaam:

Meveli Publishers (MVT)

Senkoro, F. E. M. K. (1996). Nadharia ya Fasihi na Fasihi ya Kiswahili ya

Majaribio. Katika Kioo cha Lugha. Na. 2 TUKI. Dar es salaam.

Simchimba, E.A. (2012). “Falsafa ya Kiafrika katika Methali za Kiswahili”. Tasnifu

ya Shahada ya Uzamili katika Fasihi ya Kiswahili (Haijachapishwa). Chuo

Kikuu cha Dodoma.

Stanley, A. (2018). Katika http://tamadunizetu547216239.wordpress.com.

Imesomwa tarehe24/12/2019.

Stefanova, A. (2003). “Riddles as a Community Psychological Phenomenon: Myths,

Fairy Tales, Personal Literature Art”. In folkrole, vol 35.

Stumph, S. E. & Fierser, J. (2009). Socrates to Sartre and Beyond a History of

Philosophy. New York: Mac Graw- Hill Company.

Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. (2004). Kiswahili. Chuo Kikuu cha Dar-es-

salaam Tanzania: TUKI.

Taine, H. (1873). The Philosophy of Art. New York: Holt & Williams.

Page 106: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

93

Temples, P. (1959). Bantu Philosophy. Paris: Presence Africaine.

TUKI. (2004). Kamusi la Kiswahili Sanifu. Nairobi: Oxford University Press.

Wafula, R. M. na Njogu, K. (2007). Nadharia za Uhakiki wa Fasihi. Nairobi: Jomo

Kenyata Foundation

Wamitila, K.W. (2010). Kanzi ya Fasihi: Misingi ya Uchanganuzi wa Fasihi.

Nairobi: Vide Muwa Publishers.

Wamitila, K. W. (2003). Kichocheo cha Fasihi Simulizi na Andishi. Nairobi: Focus

Books Publication Limited.

Wizara ya Elimu na Utamaduni. (1992). Historia ya Falsafa ya Elimu. Dar es salaam:

National Printing Company.

Page 107: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

94

VIAMBATANISHO

Kiambatanisho 1: Miongozo ya Mijadala ya Vikundi na Mahojiano

A. Mwongozo wa Mjadala wa vikundi kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi

1. Tafadhali tutajie jina lako na umri wako.

2. Je, unasoma darasa la ngapi?

3. Je, unafahamu vitendawili ni nini?

4. Taja vitendawili kumi unavyovifahamu

5. Eleza kwa kifupi majawabu ya vitendawili hivyo

6. Je, unadhani vitendawili vina tija kwa jamii? Kama jibu ni ndio eleza kwa

ufupi kwa nini unaona vitendawili vina tija

B. Mwongozo wa Mjadala wa Vikundi kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari

1. Tafadhali ututajie jina lako na kidato unachosoma.

2. Eleza namna unavyoifahamu dhana ya vitendawili katika fasihi ya Kiswahili.

3. Taja vitendawili vya Kiswahili unavyovifahamu na ueleze majibu ya

vitendawili hivyo. Vitendawili vijikite katika mambo yafuatayo

a) Umoja na ushirikiano

b) Maadili ya jamii

c) Kifo

d) Masuala ya uzazi na ulezi

e) Dhana ya uduara

f) “uchawi na ushirikina”

4. Je, kwa mtazamo wako unadhani vitendawili vina umuhimu wowote kwa

jamii? kama jibu ni ndio eleza kwa nini?

5. Vitendawili vinatumika katika kuhifadhi amali za kitamaduni, taja

vitendawili vinavyohusiana na masuala ya kitamaduni unavyovifahamu.

C. Mwongozo wa Mahojiano kwa Wanajamii Kuanzia Miaka Hamsini na Tano

na Kuendelea

Taarifa za Mtafiti

Mtafiti ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma wa ngazi ya umahiri katika

fasihi ya Kiswahili (MA KISWAHILI LITERATURE). Utafiti huu unahusu usawiri

wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka vitendawili vya Kiswahili.

Page 108: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

95

Unaombwa kutoa mchango wako kadri uwezavyo na unahakikishiwa kuwa maelezo

utakayoyatoa yatatumiwa kuleta ufanisi kwa malengo yaliyokusudiwa katika utafiti

huu tu.

SEHEMU A

TAARIFA ZA MTAFITIWA

Jina la mtafitiwa………………….

Jinsia………………………………

Umri………………………………….

Mahali unapoishi………………………

Cheo/ kazi unayofanya…………………

SEHEMU B

Maswali kwa Watafitiwa

1. Vitendawili ni nyenzo muhimu katika kutunza na kurithisha amali za

jamii, kwa maoni yako eleza namna unavyouelewa utanzu huu wa

vitendawili.

2. Kila jamii inaishi kwa kufuata mila na desturi za jamii yao. Je katika

jamii yenu ni mila na desturi zipi zinazozingatiwa sana na wanajamii?

3. Unafahamu nini kuhusu falsafa ya jamii yenu ambayo kwa jumla inaunda

falsafa ya Waafrika?

4. Eleza mambo yanayofanywa na jamii ambayo kupitia mambo hayo

masuala ya mila, desturi, tamaduni na uzoefu wa jamii hujipambanua.

5. Taja na ueleze kwa ufupi vijenzivya falsafa ya Kiafrika katika muktadha

wa utamaduni unavyovifahamu.

6. Je, unadhani falsafa ya Kiafrika inaweza kusawiriwa kupitia vitendawili

vya Kiswahili?

7. Eleza namna falsafa ya Kiafrika inavyojitokeza katika vitendawili vya

Kiswahili

8. Je, unahisi kwamba falsafa ya Kiafrika kama inavyosawiriwa katika

vitendawili vya Kiswahili inaweza kuwa na athari yoyote kwa jamii?

9. Taja athari hizo na ueleze kwa ufupi.

Page 109: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

96

D. Mwongozo wa Udurusu wa Matini

Udurusu wa maandiko ulishughulika na usomaji wa maandiko mbalimbali

yanayohusiana na mada ya utafiti. Maandiko yaliyodurusiwa ni yale ya maktabani na

kwenye vyanzo vya kielektroniki. Udurusu wa vyanzo vya kielektroniki ulizingatia

vyanzo vinavyohusisha Taasisi zinazojulikana na kuaminika. Mwongozo wa udurusu

wa maandiko umefafanuliwa katika jedwali lifuatalo:

Vyanzo vya

Maarifa

Vipengele Vinavyodurusiwa Lengo

Vitabu, tasnifu,

makala, tahakiki,

majarida na

vyanzo vya

kieletroniki

Vitabu vya fasihi simulizi, nakala

zinazohusiana na falsafa ya

Kiafrika, tasinifu zinazohusiana na

falsafa ya Kiafrika na tasinifu za

vitendawili vya Kiswhili.

Kupata mawazo/

taarifa mbalimbali

kutoka kwa wataalamu

mbalimbali kuhusiana

na mada ya utafiti

Page 110: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

97

Kiambatanisho 2: Orodha ya Watafitiwa

2A Mahojiano

Na Jina Jinsia Umri Mtaa

1 Boniface Rwiza Me 68 Nyamkazi

2 Mwesigwa Kigoye Me 64 Hamgembe

3 Farida Abdallah Ke 60 National Housing

4 Olivia Kokwenda Ke 58 Buyekera

5 Salma Kayanga Ke 56 Kibeta

6 Kamugisha Rwezaula Me 70 Kamagera

7 Philbert Jonas Me 57 Kamizilente

8 Bi. Theresa Ke 67 Buyekera

9 Vedasto Katto Me 56 Omukishenye

10 Scholastica Mnyambo Ke 58 Kamagera

11 Aabel Kazaula Me 58 Uswahilini

12 Audax Rwegasira Me 62 Buyekera

13 Hashim Rwekaza Me 61 Nyangoye

14 Amos Byabato Me 58 Omukishenye

15 Atugonza Tiimanywa Ke 60 National Housing

16 Jualikali Katabazi Me 58 Buyekera

17 Deogratius Bwemero Me 72 Kamizilente

18 Elizabeth Kaigara Ke 64 Kibeta Tanesco

19 Binamungu Muganyizi Me 55 Kankwila

20 Marina Katunzi Ke 63 Nyamkazi

21 Debora Mushegezi Ke 59 Uswahilini

22 Renatus Rugema Me 57 Kamagera

Page 111: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

98

2B Majadiliano

Na. Jina Umri Jinsia Shule

1 Alexander Marwa 17 Me Kashai

2 Adelaida Theobard 16 Ke Kashai

3 Frank Emilian 17 Me Kashai

4 Dion Dickson 17 Me Kashai

5 Faustine Selestine 17 Me Kashai

6 Proscovia Projestus 17 Ke Kashai

7 Richard Egidius 16 Me Kashai

8 Dismas Azas 17 Me Kashai

9 Nicera Gosbert 17 Ke Kashai

10 Elvis Johansen 17 Me Kashai

11 Venezuela Mwemezi 17 Ke Kashai

12 Innocensia Abel 13 Me Katerero

13 Akramu Musa 13 Me Katerero

14 Nusura Zuberi 12 Ke Katerero

15 Belina Godfrey 13 Ke Katerero

16 Jasintha Josbert 13 Ke Katerero

17 Abdul Samilati 13 Me Katerero

18 Jacklina Johansen 12 Ke Katerero

19 Lidya Godwin 12 Ke Katerero

20 Happiness Edisson 13 Ke Katerero

21 Gisela Gidison 13 Ke Katerero

22 Aodatha Aodax 13 Ke Katerero

23 Timoni Eneliko 12 Me Katerero

24 Dickson Medadi 13 Me Katerero

25 Levina Gosbert 12 Ke Katerero

Page 112: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

99

26 Filipo Clemens 13 Me Katerero

27 Amina Rhenus 13 Ke Katerero

28 Datius Chilizostom 13 Me Katerero

29 Eneliko Clophas 13 Me Katerero

30 Teodata Theodory 13 Ke Katerero

Page 113: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

100

Kiambatanisho 3: Barua za Utambulisho wa Kufanya Utafiti

3A: Barua Kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma

Page 114: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

101

3B: Barua Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

Page 115: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

102

3C: Barua Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bukoba

Page 116: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

103

Kiambatanisho 4: Picha Mbalimbali za Utafiti

Picha 1: Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Katerero iliyopo Hlamashauri ya

Wilaya ya Bukoba wakiwa wamenyoosha mikono ili kutoa jibu la

kitendawili kilichotegwa katika mjadala wa vikundi katika uwanja uliopo

nyuma ya madarasa shuleni hapo. (Utafiti, 2020)

Page 117: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

104

Picha 2: Mtafiti akiwa na wanafunzi wa shule ya msingi Katerero iliyopo

Halmashauri ya wilaya ya Bukoba baada ya mjadala. (Utafiti, 2020)

Page 118: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

105

Picha 3: Mtafiti akiwa na wanafunzi wa shule ya sekondari Kashai iliyopo Bukoba

mjini katika mjadala wa vikundi katika mojawapo ya darasa shuleni hapo.

(Utafiti, 2020)

Page 119: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

106

Picha 4: Mtafiti akiwa kwenye mahojiano na Bw. Mwesigwa Kigoye katika kata ya

Hamgembe mtaa wa Nyangoye wilayani Bukoba. (Utafiti, 2020)

Page 120: Usawiri wa falsafa ya Kiafrika katika semi: mifano kutoka ...

107

Picha5: Mtafiti akiandika maelezo yaliyoelezwa na Bw. Boniface Rwiza katika

mahojiano nyumbani kwa mtafitiwa katika kata ya Kashai wilayani Bukoba.

(Utafiti, 2020)