Dar es Saalam - 2014
Transcript of Dar es Saalam - 2014
![Page 1: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/1.jpg)
![Page 2: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/2.jpg)
![Page 3: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/3.jpg)
Dar es Saalam - 2014
![Page 4: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/4.jpg)
As-Salaam Islamic Center Plot 354 Mbezi Beach, Makonde, Dar Es Salaam - TanzaniaCell: +255 254 734 362, Email: [email protected]
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kutolesha sehemu yoyote ya toleo hili, kuitunza katika mfumo utakaowezesha kunakiliwa au kukisambaza katika aina au namna yoyote ile, iwe elektroniki, kuchapa, kunakilisha, kurekodi au vinginevyo bila kupata ruhusa kutoka kwa mwenye haki miliki.
ISBN: 978-9944-83-670-8Mwandishi: Othman Nuri TopbashMsimamizi Mkuu: Abdi Mohamed AdamMfasiri: Ibrahimu H. Kabuga Mhariri: Saad AbdullahKupangiliwa vizuri na: Sarkhan Isgandarov Nijat Garibov
![Page 5: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/5.jpg)
Othman Nuri TOPBASH
101
![Page 6: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/6.jpg)
![Page 7: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/7.jpg)
5
Maneno Maridhawa kutoka ndani ya Qur’an Tukufu yanasema:
“…Nawe fanya wema (kwa watu) kama
Mwenyezi Mungu alivyo kufanyia
wema wewe…”
(Al-Qasas, 28:77)
“Tena bila ya shaka mtaulizwa siku hiyo juu ya
neema [uhai, mali, vipawa na suhula
nyingine zote].”
(At-Takaathur, 102:8)
![Page 8: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/8.jpg)
6
1Malezi ya mtoto huanzia tumboni mwa
mama. Hivyo, mlezi na mwalimu wa
kwanza wa mwanadamu ni mama yake.
![Page 9: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/9.jpg)
7
2Watoto ni baraka kutoka kwa Mwenyezi
Mungu ambazo wazazi na walimu
wamekabidhiwa kama amana ili
wawaandae kwa mwenendo mwema
na maadili yaliyotukuka.
![Page 10: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/10.jpg)
8
3Maadili mema, tabia na shakhsia
imara ndiyo urithi wenye thamani ya
juu kabisa ambao wazazi wanaweza
kuwaachia watoto wao. Njia ya kulifikia
hili hupitia katika malezi ya kiwango
bora na cha juu.
![Page 11: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/11.jpg)
9
4Katika viumbe wote, mwanadamu
anahitajia zaidi malezi maalumu na
maarifa. Kazi na sanaa bora kabisa
katika maisha ya mwanadamu ni kulea
na kutengeneza wanadamu wema na
wazuri. Mwenyezi Mungu Mtukufu
aliwatuma mitume Wake kama walimu,
waelimishaji na walezi wakubwa kabisa wa
mwanadamu. Kwa maneno mengine, kazi
ya ulezi na ufundaji ni kazi ya mitume.
![Page 12: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/12.jpg)
10
5Mwalimu sio tu yule anayempa
mwanafunzi taarifa juu ya mada
fulani, bali ni yule pia anayepandikiza
mbegu ya usafi, kufungua anga mpya,
kujitambua, na kumfundisha tabia
njema na maadili sahihi. Kwa maneno
mengine, mwalimu ni yule anayejenga
dhamiri salama na imara ndani ya
mwanafunzi wake.
![Page 13: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/13.jpg)
11
6Katika kumlea mtoto, haitoshi tu kumpa
mahali pa kulala na chakula kinachompa
virutubisho. Hitajio kubwa zaidi kuliko
yote ni kuupamba ulimwengu wake
wa kiakili na kiroho kwa maarifa na
mafunzo.
![Page 14: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/14.jpg)
12
7Mwalimu anatakiwa kumfundisha
mwanafunzi wake kwa hali ya kiroho.
Anatakiwa sio tu kumfanya mwanafunzi
azipende taalumu za kidunia, bali pia
mafunzo ya kidini, hali ya kiroho na
hikma.
![Page 15: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/15.jpg)
13
8Elimu na mafunzo yanayotolewa
kuegemea upande mmoja bila kuangalia
upande wa kiroho ni yenye upungufu
na kasoro. Kuna ulazima wa kuweka
uwiano na mizania baina ya ulimwengu
wa kimaada (wa kimwili) na ule wa
kimaanawi (wa kiroho). Vinginevyo,
kama ndege anayejaribu kuruka kwa
kutumia ubawa mmoja, mwanafunzi
naye atakuwa mawindo ya paka
mwenye njaa.
![Page 16: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/16.jpg)
14
9Kila kiumbe anayeshindwa kwenda
pamoja na mkondo wa maisha, lazima
ataangamia na kupotea kabisa. Ndiyo
maana Ali (r.a) alitupatia wosia ufuatao:
“Usiwalee watoto wako kuendana na
mazingira ya zama zako, bali kuendana na
zama watakazoishi.”
![Page 17: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/17.jpg)
15
10Taifa linapokuwa na watu wachache
waliofundwa vizuri na wenye kujitoa
kwa moyo wote, taifa hilo litayapita
mataifa mengine; la sivyo, litaendelea
kubaki nyuma.
![Page 18: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/18.jpg)
16
11Haihitaji muujiza ili uweze kuuona mustakbali
wa taifa. Inatosha tu kuwaangalia watoto
na vijana wa taifa hilo. Kama wanatumia
nishati na nguvu zao katika njia ya mambo
mazuri, hali ya kiroho na wema, basi taifa
hilo litakuwa na mustakbali wenye kung’aa.
Kinyume chake, iwapo wanatumia nishati
na nguvu yao kubwa katika kuyashibisha na
kuyatosheleza matamanio yao ya kihayawani,
basi mustakbali wa taifa hilo utakuwa wenye
kusikitisha na wenye kuhuzunisha.
![Page 19: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/19.jpg)
17
12Wale wenye mtaji huwekeza katika eneo
bora na lenye ufanisi. Hata hivyo, elimu
ndilo eneo muhimu zaidi tunalotakiwa
kuwekeza. Maandalizi sahihi kwa ajili
ya mustakbali ni kuwatengeneza na
kuwalea watu bora na wenye sifa
adhimu.
![Page 20: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/20.jpg)
18
13Kitu cha kwanza ambacho mwalimu
anatakiwa kuwa nacho ni shakhsia bora
ambayo wanafunzi wataistaajabia na
kuitamani; na anapaswa kueneza na
kusambaza nuru, hali ya kiroho, maarifa
na nishati chanya kutoka moyoni
mwake, na awe na huruma na upendo
wa hali ya juu kwa wanafunzi wake.
![Page 21: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/21.jpg)
19
14Mwalimu hawezi kuwa na taathira
chanya kwa wanafunzi wake kama
matendo yake yanapingana na maneno
yake. Kama malenga maarufu wa
Kituruki Ziya Pasha asemavyo:
“Kazi ya mtu ni kama kioo kinachoionesha
tabia yake; hivyo usidanganywe na
maneno tu.”
![Page 22: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/22.jpg)
20
15Mwelimishaji anapaswa kujipamba
kwa mema anayowashauri wengine na
ajitahidi kuwa mfano hai.
![Page 23: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/23.jpg)
21
16Lazima mlezi na mwalimu watengeneze
nguvu chanya mahali walipo. Maisha
ya baadhi ya wanyama ni mfano mzuri:
kuku huwalinda na kuwahifadhi vifaranga
wake chini ya mbawa zake wakati wa
kuwalea. Nyoka huwatunza wanaye kwa
macho yake. Nge huwabeba watoto
wake mgongoni. Kama wanyama
wanawaangalia watoto wao kwa
umuhimu mkubwa kiasi hicho, vipi kuhusu
wanadamu?
![Page 24: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/24.jpg)
22
17Hapawezi kuwa na elimu bora iwapo
hakuna uaminifu baina ya mwalimu
na mwanafunzi. Aidha, mwalimu
anapaswa kuonesha shakhsia imara
kwa watu wanaomzunguka kwa
sababu watu huwapenda watu wa
mfano na waliojipamba kwa shakhsia
yenye kuvutia. Huwaadhimisha na
kufuata nyayo zao.
![Page 25: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/25.jpg)
23
18Raia hutengenezwa kulingana na watu
wanaowaongoza. Zama za Furaha (Asr
Sa’adah) watu walitengenezwa kwa ruwaza
za kiroho za Mtukufu Mtume (s.a.w).
Maswahaba wa Suffa ni mfano bora wa
jambo hili. Abdullah ibn Mas’ud, ambaye ni
mmoja wa Maswahaba wa Suffa, alisema
akionesha kiwango cha ukamilifu wa
kimaanawi alichokifikia chini ya mafunzo ya
Mtukufu Mtume (s.a.w):
“Tuliweza kusikia dhikr ya chakula
wakati kikipita kooni.”
![Page 26: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/26.jpg)
24
19Mikusanyiko ya kiroho kwa lengo la kutoa
nasaha za kidini (suhba) ndiyo iliyokuwa
njia kubwa ya Mtukufu Mtume (s.a.w)
katika kuelimisha, kwa maana kulikuwa na
mawasiliano ya kiroho katika mikusanyiko hiyo.
Mikusanyiko hiyo ilikuwa ikitoa virutubisho vya
kiroho vinavyohitajika kwa wale waliohudhuria.
Hivyo, kutoa nasaha hizo ilikuwa sawa na
kuwaandikia suluhu ya mahitaji yao.
![Page 27: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/27.jpg)
25
20Mwalimu anatakiwa kuuzingatia
uwezekano wa kwamba mwanafunzi
aliyekabidhiwa kama amana anaweza
kuwa mtu mkubwa hapo baadaye; na
asisahau kuwa huwenda anawafundisha
watu mahiri wanaoweza kuleta
mabadiliko ulimwengu.
![Page 28: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/28.jpg)
26
21Ili kutoa huduma yenye kiwango
cha juu, mwalimu anatakiwa kuwa
makini kuhusu kujiendeleza. Juhudi za
kujiendeleza zinatakiwa tabia yake ya
kawaida na endelevu. Vinginevyo, tunu
na vipawa vingi vinaweza kudhoofika na
kufifia kwa sababu ya uzembe wake.
![Page 29: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/29.jpg)
27
22Kizazi bora ni matunda ya walimu bora
wanaoweza kutoa maarifa na maadili
bora. Wale wanaofundishwa na walimu
dhaifu na wasiokuwa na viwango
watageuka kuwa watu dhaifu na
wasiokuwa na sifa.
![Page 30: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/30.jpg)
28
23Tukitaka kutengeneza na kulea
wanafunzi bora, tunatakiwa walimu
bora.
![Page 31: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/31.jpg)
29
24Fundi hutambulika kwa kile
alichokitengeneza. Vivyo hivyo, ubora
wa mwalimu hutathminiwa kwa ubora
wa mwanafunzi aliyemfunda.
![Page 32: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/32.jpg)
30
25Dhima kubwa kabisa ya mwalimu ni
kujifunda vyema yeye mwenyewe, kwa
maana mwalimu dhaifu hupoteza muda
wa wanafunzi aliokabidhiwa.
![Page 33: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/33.jpg)
31
26Mchunga kondoo ana dhima kwa
kondoo anaowachunga. Anatakiwa
kumbeba kondoo aliyevunjika mguu.
Vivyo hivyo, wanafunzi ni amana kwa
walimu wao.
![Page 34: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/34.jpg)
32
27Kila mtu huamini kuwa maneno yake ni
muhimu, yana thamani na yanatakiwa
kusikilizwa na kuzingatiwa. Ndiyo
maana mwalimu anatakiwa kuwa makini
kumsikiliza mwanafunzi anayekuja
kutaka msaada juu ya tatizo fulani.
![Page 35: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/35.jpg)
33
28Mwalimu anatakiwa kumchukulia
mwanafunzi wake kwa uzito,
amheshimu, na ajitahidi kwamba
mwanafunzi wake alione hilo kupitia
matendo yake.
![Page 36: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/36.jpg)
34
29Mwalimu anayemgeuza mwanafunzi
wake kuwa kijiti kisichoweza kuwa
mti mkubwa bila shaka atawajibika na
atasailiwa mbele ya Mwenyezi Mungu
Mtukufu.
![Page 37: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/37.jpg)
35
30Mwalimu anapaswa kuzijua vyema tabia
za wanafunzi wake kiasi cha kuweza
kuutambua mshipa utakaompeleka
kwenye nyoyo zao.
![Page 38: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/38.jpg)
36
31Kwa kuwa tabia na shakhsia
zinatofautiana, mbinu au ushauri
unaweza kumfaa mwanafunzi mmoja,
lakini mbinu na ushauri huo huo
unaweza kumdhuru mwengine. Ndiyo
maana mwalimu anapaswa kuijua hali
ya kiroho ya wanafunzi wake.
![Page 39: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/39.jpg)
37
32Mwalimu anapaswa kuvijua vipaji,
vipawa na tunu za wanafunzi wake
kama anavyovijua vipande vya tasbihi
yake, ili aweze kuwaongoza kwenye
uelekeo na njia ya vipawa vyao.
![Page 40: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/40.jpg)
38
33Leo tunaishi katika zama ambazo watu
wanaelea kama vipande vya miti katika
maji ya mafuriko bila kujua. La kusikitisha
zaidi, mto unaoweza kuzipa uhai
ardhi unazozipitia unatiririka kwenye
mfereji wa maji machafu kwa sababu
hayajaelekezwa kwenye uelekeo sahihi.
![Page 41: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/41.jpg)
39
34Mwalimu anapaswa kuwa mkarimu,
mwadilifu na mwenye huruma kwa
wanafunzi wake. Hatakiwi kuwapa
mzigo mkubwa wa kazi wasioweza
kuubeba. Anatakiwa kumuongoza kila
mmoja kulingana na uwezo wake.
![Page 42: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/42.jpg)
40
35Mwalimu mwadilifu ni mwalimu wa
darasa zima. Darasa haliwezi kuwa na
amani bila uadilifu; darasa lisilokuwa
na amani, hakuna somo linaloweza
kufundishwa; mahali ambapo hakuna
masomo yanayofundishwa, hapawezi
kuwa na elimu.
![Page 43: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/43.jpg)
41
36Mwalimu anapaswa kujua vyema
kwamba uadilifu sio kufanya usawa kwa
kila mtu bali ni kumpa kile anachostahiki.
Vilevile, mwalimu anatakiwa kujiepusha
na tabia inayoweza kuvuruga na
kuharibu hisia ya uadilifu.
![Page 44: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/44.jpg)
42
37Mwalimu anapaswa kuwa muadilifu,
sio tu katika kutoa uamuzi, bali katika
kutathmini mitihani. Kwa mukhtasari,
anatakiwa kuwa muadilifu muda wote
na katika mambo yote.
![Page 45: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/45.jpg)
43
38Mwalimu anatakiwa kuweka mipango
kulingana na muundo wa darasa lake
na nyenzo za masomo ili kwamba aweze
kufundisha kwa ukamilifu.
![Page 46: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/46.jpg)
44
39Mwalimu mwenye mipango na nidhamu
huweza kuona mahali alipoishia, kipi
alichofundisha na ufundishaji wake
umeleta matokeo ya aina gani.
![Page 47: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/47.jpg)
45
40Wakati wa kutengeneza mipango
na programu mbalimbali, mwalimu
anatakiwa kufikiria lini, wapi na
namna atakavyoitekeleza mbinu zake
ufundishaji.
![Page 48: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/48.jpg)
46
41Mwalimu anapaswa kujua kwamba dhima
yake sio tu kuhamisha maarifa. Wakati
wa kupangilia masomo yake, anapaswa
kuandaa vipengele vitakavyowavutia
wanafunzi. Kuwasilisha somo kwa kutoa
mifano halisi na kutumia mbinu ya maswali
na majibu itawafanya wanafunzi wawe
wachangamfu na wasikivu.
![Page 49: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/49.jpg)
47
42Subira, ustahmilivu na kujitoa kwa moyo
ni funguo muhimu kabisa za mafanikio
katika elimu na malezi.
![Page 50: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/50.jpg)
48
43Mwalimu hapaswi kukata tamaa
anapokabiliwa na tabu na ugumu;
badala yake subira yake inatakiwa kuwa
imara na madhubuti anapokutana na
mazingira magumu.
![Page 51: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/51.jpg)
49
44Mwalimu hatakiwi kupoteza matumaini
au kuonesha uzembe na unyonge
Kwa sababu ya udhaifu na ukosefu wa
nyenzo.
![Page 52: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/52.jpg)
50
45Ni lazima tusisahau kuwa siku zote maji
ya uhai yanapatikana katika nyakati
ngumu na maeneo ya shida na tabu;
kwa maana kinachoyafanya maisha
kuwa yenye thamani na ustawi ni juhudi
na kujitolea katika njia ya kulifikia lengo
tukufu.
![Page 53: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/53.jpg)
51
46Malezi sio upendo wa muda mfupi
na wa kupita. Ni kazi tukufu kabisa
inayotakiwa kutekelezwa kwa upendo
na bidii mpaka pumzi ya mwisho. Katika
kufanikisha hilo, subira inatakiwa kuwa
ndio kirutubisho cha mlezi na Mwenyezi
Mungu awe msaada wake.
![Page 54: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/54.jpg)
52
47Mwalimu ni mtu anayeweza kuilinda
imani yake katika jamii yoyote ile
anayoishi; anayeweza kuuepusha moyo
wake usishughulishwe na mali na
manufaa; anayeweza kuzisikia sauti za
ukimya wa wale wanaopiga kelele ya
kuhitajia elimu na malezi.
![Page 55: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/55.jpg)
53
48Kama ambavyo ni kosa kuwapuuza
watoto, wazazi na kazi inayokupatia
riziki kwa kisingizio cha kuwahudumia
watu, vilevile ni kosa kutumia mambo
hayo kama kisingizio cha kutowasaidia
watu.
![Page 56: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/56.jpg)
54
49Mwalimu hatakiwi kuhuzunika kwa
kukosa fursa za kimaada, wala kufurahia
na kuharibiwa na wingi wa mali za
kidunia.
![Page 57: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/57.jpg)
55
50Mwalimu anatakiwa kutenga muda kwa
ajili ya wanafunzi wake nje ya muda
wa masomo ya darasani. Asiwe kama
mfanyakazi anayeingia na kutoka huku
akisubiri zamu yake imalizike.
![Page 58: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/58.jpg)
56
51Mwalimu asiwe mtengenezaji wa
matatizo bali awe mtatuzi wa matatizo.
Badala ya kutafuta makosa na kasoro za
kukosoa, anatakiwa kuyakabili mambo
kwa moyo na mtazamo chanya.
![Page 59: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/59.jpg)
57
52Mwalimu asiwe mtu wa kuwalaumu
wengine kwa makosa mbalimbali wakati
wa kutoa elimu; anatakiwa kujiona kama
chanzo cha makosa hayo.
![Page 60: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/60.jpg)
58
53Mwalimu kutafuta visingizio kwa kusema
“nifanye nini? Sina uwezo wala vipawa.
Ninapoteza muda. Hakuna anayekuja
darasani kwangu,” Mwenyezi Mungu
huvijibu visingizio hivyo kwa kuumba
mitini katika miamba na kutoa matunda
kutokana na mitini hiyo.
![Page 61: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/61.jpg)
59
54Malezi ni sanaa ya kusahau visingizo
mbele ya aina zote za shida. Malezi
hayawezi kufanikiwa mahali ambapo
ukosefu wa uvumilivu na visingizio
hutawala.
![Page 62: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/62.jpg)
60
55Mwalimu mzuri hatakiwi kusubiri fursa
suhula zimjie. Siku zote anatakiwa
atafute nje za kuwahudumia watu.
![Page 63: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/63.jpg)
61
56Malezi na maadilisho sio kazi ya kukaa
na kusubiri. Inahitaji kiwango cha juu
cha nishati. Hivyo mwalimu anatakiwa
kuujaza moyo wake kwa nishati chanya.
![Page 64: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/64.jpg)
62
57Mbegu za maarifa zinazopandwa kwa
upendo na bidii hapo baadaye zitakuwa
miti mikubwa ya mkuyu.
![Page 65: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/65.jpg)
63
58Mwalimu anatakiwa azijue vyema
adabu na maadili yanayokubalika na
kuheshimiwa na jamii na asizipuuze.
![Page 66: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/66.jpg)
64
59Mwalimu maridadi, mwenye adabu
na moyo safi anatakiwa kuwahudumia
watu kwa msisimko; asiziumize hisia za
wengine na pia asiruhusu hisia zake
ziumizwe kwa urahisi. Tukumbuke kuwa
nyoyo ni mahali panapotazamwa na
Mwenyezi Mungu Mtukufu.
![Page 67: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/67.jpg)
65
60Mwalimu anatakiwa kuwa makini sana
kwa kila tendo na mwanendo wake.
Anatakiwa kuwa mtaratibu na mwenye
adabu hata wakati wa kufanya mzaha.
![Page 68: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/68.jpg)
66
61Mwalimu mzuri anatakiwa kuijua mipaka
myembamba iliyopo kati ya nidhamu na
purukushani, staha na udhalili, heshima
na ufakhari. Asivichangaye.
![Page 69: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/69.jpg)
67
62Katika kila hatua ya maisha, mwalimu
anatakiwa afanye mambo kwa
namna inayoendana na mwenendo
wa Kiislamu. Asisahau kuwa kila
anachofanya na kila analosema ni kama
tofali linalowekwa katika shakhsia ya
wanafunzi wake.
![Page 70: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/70.jpg)
68
63Mwalimu anatakiwa kujua kuwa
elimu sio tu kuhamisha maarifa, bali
pia kuhamisha tabia. Afikirie kuhusu
makosa anayoweza kuambukiza wakati
wa mchakato huu wa uhamishaji wa
maarifa na muda wote ahisi kuwa
atakuwa na dhima iwapo atahamisha
na kuwaambukiza wanafunzi tabia na
mwenendo mbaya.
![Page 71: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/71.jpg)
69
64Mwalimu anatakiwa kuwa mtu wa
nyoyo anayefanya juhudi ya kutaka
msamaha wa Mwenyezi Mungu kwa
kuwasamehe wengine.
![Page 72: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/72.jpg)
70
65Kila mtu anahitaji upendo na huruma.
Kuwahurumia na kuwapenda watu
hupunguza uadui na kuongeza upendo
na urafiki.
![Page 73: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/73.jpg)
71
66Malezi muafaka hayawezi kupatikana
kwa mbinu za kifidhuli, zenye kuvunja
moyo na ukali.
![Page 74: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/74.jpg)
72
67Ni jambo lisilokubalika kwa mwalimu
kuwatesa wale walio chini yake kwa ajili
ya kuwaadabisha.
![Page 75: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/75.jpg)
73
68Ukali uliopitiliza hutengeneza mfundo na
kinyongo. Subira iliyopitiliza hudhoofisha
mamlaka. Mafanikio hupatikana kwa
kuweka uwiano mzuri baina ya mambo
hayo mawili.
![Page 76: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/76.jpg)
74
69Mwalimu anapaswa kuzungumza kwa
upole na uzuri, na daima azungumzie
mambo mazuri. Kwa maana hakuna
apendaye maneno makali na ya
kifedhuli. Unyenyekevu, upole na
maneno matamu ndiyo njia bora kabisa
ya kuingia katika nyoyo za watu.
![Page 77: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/77.jpg)
75
70Kama ambavyo rubani asiyejisikia
vizuri kisaikolojia hawezi kuruhusiwa
kurusha ndege, mwalimu mwenye
hasira au ambaye morali wake upo chini
asiruhusiwe kuingia darasani.
![Page 78: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/78.jpg)
76
71Mwalimu anatakiwa kutoa maonyo na
nasaha zake kwa amani na asisahau
kuwa matendo na tabia zinazoumiza
hisia za wengine ni ishara ya udhaifu
mkubwa kabisa wa shakhsia yake.
![Page 79: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/79.jpg)
77
72Siku zote watu huathiriwa na hisia zao.
Hufikiria na kufanya uamuzi kutokana
na taathira hiyo. Hivyo, mwalimu
mzuri anatakiwa afanye uamuzi baada
ya kushauriana na wenzake. Hii
inamuwezesha kutoa huduma sahihi..
![Page 80: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/80.jpg)
78
73Taathira ya mwalimu mwenye moyo
uliojaa upendo na hali ya kiroho ni
mfano wa taathira ya upepo mwanana
unaovuma juu ya mabustani yaliyojaa
maua yenye kunukia na kuyachukua
manukato hayo mazuri mpaka sehemu
za mbali.
![Page 81: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/81.jpg)
79
74Vitu vitatu huigeuza dunia kuwa Pepo:
Huruma ya mikono yako, ulimi na
moyo…
![Page 82: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/82.jpg)
80
75Katika kuufikia wokovu, waumini wenye
ukomavu huwatafuta watu katika jamii
na kuwapa elimu, kuwahudumia na
kuwahurumia ili wapate kuokolewa.
![Page 83: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/83.jpg)
81
76Ushindi wa kweli ni ushindi wa nyoyo.
Hili linaweza tu kufikiwa na wale
wanaozigeuza nyoyo zao kuwa makazi
ya upendo.
![Page 84: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/84.jpg)
82
77Mwalimu wa mfano ni mtaalamu wa
nyoyo. Ni daktari anayezichanja nyoyo
kwa chanjo ya uhai wa milele.
![Page 85: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/85.jpg)
83
78Moyo wa mwalimu unatakiwa kugeuka
kuwa kitovu cha kiroho cha urekebishaji
kwa kupata uwezo wa kuwatazama
viumbe kupitia jicho la Muumba.
![Page 86: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/86.jpg)
84
79Upendo na juhudi hutatua matatizo
yote. Tunawavuta watu ambao
tumetatua matatizo yao. Tunapata
thawabu kwa kila tunaemvuta
na kubeba dhima kubwa ya yule
tunayeshindwa kumvuta.
![Page 87: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/87.jpg)
85
80Kujitoa mhanga ni kipimo cha upendo.
Kuzungumza tu hakufai chochote.
Mawlana Jalaluddin Rumi anasema:
“Usiwe mpumbavu wa maneno.”
Madai ya kumpenda mtu yanatakiwa
kuthibitishwa kwa kujitoa.
![Page 88: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/88.jpg)
86
81Mwalimu anatakiwa kuhisi maumivu
ya wanafunzi wake na kufurahi pale
wanapokuwa na furaha. Awachukulie
kama marafiki na ndugu. Pia anatakiwa
kuijua lugha ya urafiki na udugu.
![Page 89: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/89.jpg)
87
82Mwalimu hatakiwi kuwa mtu
anayetafuta makosa na kasoro za
wanafunzi wake; bali awe mtu
anayefanya juhudi za kuyarekebisha
makosa yao kwa kutoyaweka hadharani.
![Page 90: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/90.jpg)
88
83Upendo ni kama mkondo
unaoziunganisha nyoyo mbili. Utimamu
wa elimu na malezo hutegemea nguvu
za mkondo huu.
![Page 91: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/91.jpg)
89
84Mwalimu anatakiwa kuifungua sana
milango ya moyo wake kwa ajili ya
wanafunzi kiasi kwamba milango hiyo
inaweza kutengeneza mkondo imara wa
ushawishi na taathira kwao.
![Page 92: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/92.jpg)
90
85Upendo wa kuipenda elimu huongeza
hamu katika kile anachokifundisha.
Kuamiliana na wanafunzi kwa upendo
na huruma humuwezesha mwalimu
kufikisha ujumbe wake, sio kwa njia ya
akili, bali kupitia njia za moyo.
![Page 93: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/93.jpg)
91
86Mwalimu anatakiwa kwenda
darasani katika hali ya heshima kama
anavyokwenda kwenye nyumba ya
ibada. Atambue kuwa zana yake kuu ni
upendo na udugu.
![Page 94: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/94.jpg)
92
87Elimu isiyofika moyoni haiwezi kugeuka
kuwa maarifa na hekma.
![Page 95: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/95.jpg)
93
88Walimu hujenga mtazamo wa dunia
katika viungo vya watoto vyenye
thamani kubwa kabisa, navyo ni akili na
moyo. Hivyo, ni sahihi kuwaita walimu
kuwa “wajenzi wa mustakbali.”
![Page 96: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/96.jpg)
94
89Maarifa na hekma vinaweza kuwa na
taathira pindi unapoishi kwa moyo
msafi na upendo. Unapofikia hali hii,
huwaona wanafunzi wako kupitia
miwani ya upendo na huruma. Mbegu
zilizopandikizwa kwa upendo na
huruma hudumu milele.
![Page 97: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/97.jpg)
95
90Ili uwe mwalimu mzuri, unapaswa
kuwa na hisia madhubuti za upendo na
huruma.
![Page 98: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/98.jpg)
96
91Wanafunzi wanatakiwa kutazamwa
kama ndege waliovunjika mbawa na
kuhudumiwa kwa upole na huruma.
Kwa maana upole na huruma ni tiba
mujarabu na madhubuti kabisa katika
kulea akili na nyoyo salama na imara.
![Page 99: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/99.jpg)
97
92Huruma ni kama moto usiozimika ndani
ya moyo wa mwalimu.
![Page 100: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/100.jpg)
98
93Ni dhulma kubwa kumteua kuwa
mwalimu mtu mwenye ubinafsi na
asiyekuwa na upole na huruma.
![Page 101: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/101.jpg)
99
94Kama ambavyo mandhari ya
mawaridi na maua huzifanya nyuso
za watu wakali kutabasamu, watu
wanaowaongoza wenzao wanatakiwa
kuwa na sifa za mawaridi na maua
mazuri. Wawe na uwezo wa kuzilainisha
nyoyo ngumu kabisa na kuzifanya nyuso
zilizokunjamana zitabasamu.
![Page 102: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/102.jpg)
100
95Jambo muhimu kabisa ambalo mwalimu
anatakiwa kulizingatia ni kujua kwamba
makosa yanatokana na yeye mwenyewe
na mafanikio hutoka kwa Mwenyezi
Mungu.
![Page 103: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/103.jpg)
101
96Mwalimu anapaswa kuitazama kazi yake
kama baraka na tunu kubwa kwake.
Ili kuonesha shukran kwa kupewa
baraka hii, anatakiwa kuwa na hisia
ya kuwajibika kujiandaa kwa zana za
kimaada na kiroho.
![Page 104: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/104.jpg)
102
97“Umimi” na “kujidai” vinatakiwa
kuondoka na mahala pake mwalimu
akawa na “upendo” na “upole”.
![Page 105: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/105.jpg)
103
98Maisha ya mwalimu yanatakiwa
kujengeka kwenye msingi wa udhati,
juhudi na kutoa huduma bila majivuno.
![Page 106: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/106.jpg)
104
99Kila siku ni ukurasa mpya na msafi
kutoka katika kalenda ya maisha. Mikono
yako ndiyo inayoujaza ukurasa huu kwa
namna bora kabisa.
![Page 107: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/107.jpg)
105
100Mwalimu anatakiwa kuichukulia kila
dakika anayokaa na wanafunzi wake
kama pumzi yake ya mwisho katika
ulimwengu huu na hivyo anatakiwa
kuutumia muda huo namna iliyo nzuri.
Awe na hisia ya kushukuru na aoneshe
shukrani zake kwa vitendo.
![Page 108: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/108.jpg)
106
101Watoto wanahitaji malezi ya wazazi na
walio wao katika ulimwengu huu, nao
walimu na wazazi wanahitajia dua na
sadaka zenye kuendelea (sadaqatul –
jaariyah) za watoto hao huko Akhera.
![Page 109: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/109.jpg)
107
Kutoka katika muongozo bora wa elimu na malezi
QUR’AN TUKUFU NA HADITH NA MJUMBE
WA MWENYEZI MUNGU
Maneno bora ni Kitabu cha Mwenyezi Mungu.
Njia bora ni njia ya Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Uchamungu ndiyo ngao imara.
Mazungumzo bora ni kumdhukuru Mwenyezi Mungu.
Visa maridhawa ni visa vya Qur’an Tukufu.
Njea zenye nuru ni njia za Mitume.
Elimu bora na yenye manufaa ni ile inayogeuka kuwa maarifa na hekma.
Mali kidogo inayokufanya umshukuru Mwenyezi Mungu ni bora kuliko mali nyingi itakayokufanya umkufuru.
![Page 110: Dar es Saalam - 2014](https://reader034.fdocuments.in/reader034/viewer/2022042421/625f9db891600b58e06ba325/html5/thumbnails/110.jpg)
108
Kisingizo kibaya kabisa ni kile kinachotolewa wakati wa kufa.
Majuto mabaya kabisa ni yale ambayo mtu atakayokuwa nayo Siku ya Hukumu.
Uongo ni dhambi kubwa kabisa.
Utajiri bora ni utajiri wa moyo na kutajirika kwa kuridhika na kutosheka.
Imani bora ni ile iliyokita mizizi moyoni.
Mali bila kutoka sadaka na zaka itageuka kuwa fedheha siku ya Kiyama.
Kamari na riba ndiyo aina mbaya kabisa ya mapato.
Upofu mweusi kabisa ni kuipoteza njia baada ya kuingia kwenye njia ya haki.
Upofu mbaya kabisa ni upofu wa moyo.
Kumuongoza mtu kwenye njia iliyonyooka (Uislamu) ni bora kuliko chochote kinachochomozewa na jua. Haya ni matunda ya kuulea moyo.
Japokuwa aina zote za israfu zinazidiana kwa ubaya; aina mbaya kabisa ni “kumfayia israfu mwanadamu.”