Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa...

32
Biblia INA UJUMBE GANI?

Transcript of Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa...

Page 1: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Biblia

I N A U J U M B E G A N I ?

Page 2: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Printed by WatchTower Bibleand Tract Society of South Africa NPC1 Robert Broom Drive East, Rangeview,Krugersdorp, 1739, R.S.A.Made in the Republic of South AfricaLimechapishwa Katika Jamhuri yaAfrika Kusini

1 Muumba Ampa MwanadamuParadiso [ukurasa wa 4]

2 Paradiso Yapotea[ukurasa wa 5]

3 Wanadamu WaokokaGharika [ukurasa wa 6]

4 Mungu Afanya Agano naAbrahamu [ukurasa wa 7]

5 Mungu Ambariki Abrahamuna Familia Yake [ukurasa wa 8]

6 Ayubu Adumisha Utimilifu[ukurasa wa 9]

7 Mungu Awakomboa Wanawa Israeli [ukurasa wa 10]

8 Waisraeli Waingia Kanaani[ukurasa wa 11]

9 Waisraeli Wataka Mfalme[ukurasa wa 12]

10 Sulemani Atawala kwaHekima [ukurasa wa 13]

11 Nyimbo Zilizoongozwana Roho Ambazo Zinafarijina Kufundisha [ukurasa wa 14]

12 Hekima Kutoka kwa MunguInayotuongoza Maishani[ukurasa wa 15]

13 Wafalme Wazurina Wafalme Wabaya[ukurasa wa 16]

14 Mungu Asema KupitiaManabii Wake [ukurasa wa 17]

15 Nabii Aliye UhamishoniApata Maono ya Wakati Ujao[ukurasa wa 18]

16 Masihi Afika [ukurasa wa 19]

17 Yesu Afundisha KuhusuUfalme wa Mungu[ukurasa wa 20]

18 Yesu Afanya Miujiza[ukurasa wa 21]

19 Yesu Atabiri Matukio yaWakati Ujao YatakayoikumbaDunia Nzima [ukurasa wa 22]

20 Yesu Kristo Auawa[ukurasa wa 23]

21 Yesu Yuko Hai! [ukurasa wa 24]

22 Mitume Wahubiri kwaUjasiri [ukurasa wa 25]

23 Habari Njema Yaenea[ukurasa wa 26]

24 Paulo AyaandikiaMakutaniko [ukurasa wa 27]

25 Mashauri Kuhusu Imani,Mwenendo, na Upendo[ukurasa wa 29]

26 Paradiso Yarudishwa![ukurasa wa 30]

BibliaI N A U J U M B E G A N I ?

Y A L I Y O M OSehemu Sehemu

Broshua hii haiuzwi. Ni sehemu ya kaziya elimu ya Biblia ulimwenguni poteinayotegemezwa kwa michango ya hiari.Ikiwa ungependa kutoa mchangotafadhali tembelea tovuti yawww.jw.org/swIsipokuwa iwe imeonyeshwa vingine,manukuu ya Maandiko yametokakatika Biblia Takatifu—Tafsiriya Ulimwengu Mpya.

The Bible—What Is Its Message?Chapa ya Aprili 2017

Swahili (bm-SW)

˘ 2009WATCH TOWER BIBLE AND TRACTSOCIETY OF PENNSYLVANIA

Wachapishaji

Page 3: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

KABLA ya kuchukua Biblia na kuanza kuisoma,ingefaa kujua mpangilio wake. Biblia, ambayo

pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo.

Biblia ilitungwa na nani? Hilo ni swali ambalo lime-wasumbua watu wengi. Ukweli ni kwamba Maandikohayo yaliandikwa na wanaume wapatao 40 katika ki-pindi cha miaka 1,600 hivi. Hata hivyo, wanaume haohawakudai kamwe kuwa watungaji wa Biblia. Mmojawao aliandika: “Andiko lote limeongozwa na roho yaMungu.” (2 Timotheo 3:16) Mwandikaji mwinginealisema: “Roho ya Yehova ndiyo iliyosema kupitiamimi, na neno lake lilikuwa kwenye ulimi wangu.”(2 Samweli 23:2) Kulingana na waandikaji hao, Yeho-va Mungu ndiye Mtungaji wa Biblia naye anatakakuwa na uhusiano wa karibu na wanadamu.

Kuna jambo lingine muhimu linalohitajika ili kuie-lewa Biblia. Biblia ina ujumbe mmoja wa msingi: ku-tetewa kwa haki ya Mungu ya kuwatawala wanadamukupitia Ufalme wa mbinguni. Katika broshua hii,utaona jinsi ujumbe huo unavyojitokeza kuanzia kita-bu cha Mwanzo mpaka Ufunuo.

Ukiwa na hayo akilini, sasa chunguza ujumbe uliokatika kitabu maarufu zaidi ulimwenguni, Biblia.

Kwa Nini Uichunguze Biblia?Je, wewe unaifahamu Biblia? Hakuna kitabu kingine chochotekatika historia ambacho kimesambazwa sana kama Biblia.Ujumbe wake umewafariji na kuwapa tumaini watu wa tamadunizote, nao wamefaidika na mashauri yake maishani. Hata hivyo,watu wengi leo hawaijui Biblia vizuri. Iwe wewe ni mfuasi wa dinifulani au sivyo, huenda kuna mambo fulani ambayo ungependakujua kuhusu Biblia. Broshua hii imekusudiwa kukusaidiakupata picha ya ujumla kuhusu Biblia.

˛ Ilichukua miaka 1,610 kuandikwa,tangu mwaka wa 1513 K.W.K. mpakamwaka wa 98W.K.�

˛ Vitabu 39 vya kwanza—vilivyoandi-kwa hasa katika Kiebrania, na sehe-mu kadhaa katika Kiaramu—vinaitwaMaandiko ya Kiebrania, au “Agano laKale.”

˛ Vitabu 27 vya mwisho—vilivyoandi-kwa katika Kigiriki—vinaitwa Maandi-ko ya Kigiriki ya Kikristo, au “AganoJipya.”

˛ Biblia imegawanywa katika sura namistari. Kwa mfano, Mathayo 6:9, 10inarejelea sura ya 6 ya kitabu chaMathayo, mstari wa 9 na wa 10.

� Kuna njia mbalimbali za kutaja tarehe. Katikabroshua hii, herufiW.K. zinamaanisha “Wakati waKawaida” na K.W.K. zinamaanisha “Kabla ya Wa-kati wa Kawaida.” Herufi hizo zinatumiwa katikachati iliyo sehemu ya chini ya kurasa.

HABARI MUHIMU KUHUSU BIBLIA

3

Page 4: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

4

“HAPO mwanzo Mungu aliumba mbi-ngu na dunia.” (Mwanzo 1:1) Mane-

no hayo yamesemwa kuwa maneno maa-rufu zaidi ya ufunguzi ambayo yamepatakuandikwa. Katika maneno hayo rahisi la-kini yenye kujaa maana, Biblia inamta-mbulisha mhusika mkuu wa MaandikoMatakatifu—Mungu mweza-yote, Yehova.Mstari huo wa kwanza wa Biblia unafunuakwamba Mungu ndiye Muumba wa uli-mwengu wote kutia ndani dunia yetu. Mi-stari inayofuata inaeleza kwamba katika vi-pindi virefu vya wakati, vinavyoitwa siku,Mungu alitayarisha makao yetu hapa du-niani, akitokeza vitu vyote vya ajabu vilivyokatika ulimwengu.

Mwanadamu ndiye kiumbe kikuu zaididuniani alichoumba Mungu. Aliumbwa ka-tika mfano wa Mungu—akiwa na uwezowa kuonyesha sifa za Yehova mwenyewe,kama vile upendo na hekima. Mungu ali-muumba mwanadamu kutoka katika ma-vumbi ya dunia, na kumwita Adamu. Ki-sha, akamweka katika paradiso—bustani yaEdeni. Mungu mwenyewe ndiye aliyetaya-risha bustani hiyo na kuweka miti yenyekupendeza ya matunda.

Mungu aliona kwamba mwanamumehuyo anahitaji mwenzi. Akitumia ubavuwa Adamu, Mungu alimfanyiza mwana-mke na kumleta kwa mwanamume huyoili awe mke wake. Mwanamke huyo alii-twa Hawa. Akiwa na shangwe kubwa, Ada-mu akasema kishairi: “Mwishowe huyu nimfupa wa mifupa yangu na nyama ya nya-ma yangu.” Mungu akaeleza: “Ndiyo saba-bu mwanamume atamwacha baba yake namama yake naye atashikamana na mkewake nao watakuwa mwili mmoja.”—Mwa-nzo 2:22-24; 3:20.

Mungu aliwapa Adamu na Hawa amrimbili. Kwanza, aliwaagiza walime na kutu-

nza makao yao ya kidunia na hatimayekuijaza dunia. Pili, aliwaambia wasile tu-nda la mti mmoja tu katika bustani yotehiyo, “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.”(Mwanzo 2:17) Ikiwa wangekosa kutii, wa-ngekufa. Kupitia amri hizo, Mungu ali-mpa mwanamume na mwanamke huyonjia ya kuonyesha kwamba wanamkubalikuwa Mtawala wao. Pia, kutii kwao kungeo-nyesha upendo na shukrani zao. Hawaku-wa na sababu yoyote ya kuukataa utawalawake wenye fadhili. Wanadamu hao waka-milifu hawakuwa na kasoro yoyote. Bibliainatuambia: “Mungu akaona kila kitu ali-chokuwa amefanya na, tazama! kilikuwachema sana.”—Mwanzo 1:31.—Mwanzo sura ya 1 na 2.��������������

˛ Biblia inasimulia jinsi gani kuumbwa kwa wana-damu na makao yao?˛ Mungu aliwatayarishia wanadamu maisha yaaina gani?˛ Mungu aliwapa wanadamu wa kwanza amrigani?

1 Muumba Ampa Mwanadamu ParadisoMungu aumba ulimwengu na viumbe; aumba mwanamumena mwanamke wakamilifu, awaweka katika bustani nzuri, nakuwapa amri wanazopaswa kutii

˘ MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo2 TimotheoTitoFilemoniWaebraniaYakobo1Petro2Petro1Yohana2Yohana3YohanaYudaUfunuo

Maandiko Matakatifu humwita Mu-ngu majina mbalimbali ya heshima,kama vile Muumba na Mungu Mweza-Yote. Majina fulani ya heshima hukaziasifa za Mungu, kama vile utakatifu, ngu-vu, haki, hekima, na upendo. Hatahivyo, Mungu alijipatia mwenyewe jinala pekee—Yehova. Jina hilo lilitumiwamara 7,000 hivi katika lugha za awali,mara ya kwanza ikiwa katika andiko laMwanzo 2:4. Jina Yehova linamaanisha“Yeye Husababisha Kuwa.” Hilo ni wazolenye kufariji, kwa kuwa linamaanishakwamba Mungu anaweza kutimiza lolo-te analokusudia naye anaweza kutimizaahadi yoyote anayotoa.

JINA LA MUNGU

“Hapo mwanzo . . . ” Kuumbwa kwa Adamu 4026 K.W.K.

Page 5: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Kifo cha Adamu 3096 2500 K.W.K.

5

MUDA mrefu kabla ya kuwaumbawanadamu, Mungu aliumba viu-

mbe wengi wa kiroho wasiooneka-na—malaika. Katika bustani ya Edeni,malaika mwasi, ambaye baadaye ali-kuja kuitwa Shetani Ibilisi, alimshawi-shi kwa hila Hawa ale tunda la ule mtiambao Mungu alikuwa amewakataza.

Akimtumia nyoka kuzungumza, She-tani alidai kwamba Mungu alikuwa aki-mnyima mwanamke huyo na mumewake kitu fulani chenye kutamanika.Malaika huyo alimwambia Hawa kwa-mba yeye na mume wake wakila tu-nda hilo hawatakufa. Hivyo, Shetanialidai kwamba Mungu aliwadanganyawatoto wake wa kibinadamu. Mdanga-nyi huyo alifanya ionekane kana kwa-mba kumwasi Mungu ni jambo lenyekupendeza ambalo lingewapa ujuzi nauhuru mwingi zaidi. Huo ulikuwa uwo-ngo, uwongo wa kwanza duniani. Sualakuu lilikuwa enzi au utawala wa Mungu—iwapo Mungu ana haki ya kutawala naikiwa anaitumia ifaavyo.

Hawa alimwamini Shetani. Akaanzakutamani tunda hilo, kisha akala

sehemu yake. Baadaye akampa mumewake, naye pia akala. Hivyo wakawawatenda-dhambi. Tendo hilo lililoone-kana kuwa dogo lilikuwa uasi. Kwa ku-kataa kimakusudi kutii amri ya Mungu,Adamu na Hawa waliukataa utawala waMuumba aliyekuwa amewapa kila kitu,kutia ndani uhai mkamilifu.

Mungu aliwahukumu waasi hao. Ali-tabiri Uzao au Mkombozi aliyeahidiwaambaye angemharibu Shetani, anaye-wakilishwa na nyoka. Kwa kutotekele-za hukumu ya kifo papo hapo, Mungualiwaonyesha rehema wa-zao wa Adamu na Hawaambao hawakuwa wame-zaliwa. Watoto hao wa-ngekuwa na tumaini kwakuwa Yule ambaye Mu-ngu angemtuma, angeo-ndolea mbali madhara ya uasi huo ka-tika Edeni. Hatua kwa hatua, kadiriBiblia ilivyoendelea kuandikwa, ilijuli-kana wazi Mwokozi huyo ni nani, na ji-nsi atakavyotimiza kusudi la Mungu.

Mungu alimfukuza Adamu na Hawakutoka katika Paradiso. Walilazimika ku-toa jasho na kuchoka ili kujiruzuku njeya bustani ya Edeni. Kisha Hawa akawamja-mzito na kumzaa Kaini, mtoto wakwanza wa Adamu na Hawa. Wazazi haowa kwanza walipata wana na mabintiwengine, kutia ndani Abeli na Sethi,babu ya Noa.—Mwanzo sura ya 3 mpaka 5; Ufunuo 12:9.��������������

˛ Uwongo wa kwanza uliosemwa ni gani, na ninani aliyeusema?˛ Adamu na Hawa waliipoteza Paradiso jinsi gani?˛ Mungu alipowahukumu waasi, aliwaandalia wa-zao wao tumaini jinsi gani?

2 Paradiso YapoteaMalaika mwasi amchochea mwanamume na mwanamkewa kwanza, Adamu na Hawa, waukatae utawala waMungu. Dhambi na kifo zaingia ulimwenguni

“Atakuponda kichwanawe utamtia jerahakwenye kisigino.”—Mwanzo 3:15

Mwanzo ˘

KutokaMamboyaWalawi

HesabuKumbukumbu la Torati

YoshuaWaamuzi

Ruthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieliHosea

MalakiMathayo

MarkoLuka

YohanaMatendoWaroma

1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefesoWafilipi

Wakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike

1 Timotheo2 Timotheo

TitoFilemoni

WaebraniaYakobo1 Petro2 Petro

1 Yohana2 Yohana3 Yohana

YudaUfunuo

Adamu na Hawa waliumbwa na Munguwakiwa wakamilifu, wakiwa na tumaini lakuishi milele katika Paradiso. Walitendadhambi kwa kumwasi Mungu. Hivyo,Adamu na Hawa wakapoteza ukamilifu nakukata uhusiano wao na Chanzo cha uhai,Yehova. Tangu wakati huo na kuendelea,wao na wazao wao wote wasio wakamilifuhawangeweza kuepuka dhambi na hati-maye kifo.—Waroma 5:12.

KUTOKAMILIKA NA KIFO

Page 6: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

2500 K.W.K. Gharika yaanza 2370

WANADAMU walipozidi kuongezeka,dhambi na uovu zilizidi duniani.

Enoko, nabii aliyekuwa peke yake, alionyakwamba siku moja Mungu atawaharibuwaovu. Hata hivyo, uovu ulizidi. Malaikafulani walimwasi Yehova kwa kuacha ma-kaoyao mbinguni, wakajivika miili ya kibi-nadamu, wakaja duniani na kujitwalia wa-nawake kuwa wake zao. Mahusiano hayoyasiyo ya kawaida yalitokeza Wanefili, ma-jitu yenye kukandamiza yaliyozidisha jeurina umwagaji damu duniani. Mungu alihu-zunika sana kuona uumbaji wake ukihari-biwa.

Baada ya kifo cha Enoko, kuna mtummoja aliyekuwa tofauti kabisa na uli-mwengu mwovu uliomzunguka. AliitwaNoa. Yeye na familia yake walijitahidi ku-fanya yaliyo sawa machoni pa Mungu.Mungu aliamua kuwaharibu waovu. Hatahivyo, hakutaka kumwangamiza Noa nawanyama pamoja nao. Kwa hiyo Munguakamwambia ajenge safina—chombo kiku-bwa chenye umbo la sanduku. Humo, Noana familia yake wangehifadhiwa wakiwahai, pamoja na wanyama wa aina mbali-mbali, na kuokoka gharikaya dunia nzima.Noa alimtii Mungu. Kwa makumi ya mia-ka ambayo Noa alijenga safina hiyo, aliku-wa pia “mhubiri wa uadilifu.” (2 Petro 2:5)Aliwaonya watu kuhusu Gharika iliyoku-wa ikikaribia, lakini wakampuuza. Wakati

ulipofika, Noa na familia yake wakaingiakatika safina pamoja na wanyama. Munguakaufunga mlango wa safina. Mvua ika-nyesha.

Mvua ikamwagika bila kukoma kwasiku 40, mchana na usiku, mpaka duniayote ikafunikwa. Waovu wote wakaanga-mia. Miezi kadhaa baadaye, maji yalipopu-ngua, safina ikatua juu ya mlima. Kufikiawakati ambapo Noa na familia yake pa-moja na wanyama wangeweza kutoka njeya safina, mwaka mzima ulikuwa umepi-ta. Noa alionyesha shukrani zake kwa ku-mtolea Yehova toleo. Mungu alikubali to-leo hilo na kumhakikishia Noa na familiayake kwamba hataleta tena gharika ili kuo-ndolea mbali kila kitu chenye uhai kutokakatika uso wa dunia. Yehova aliandaa upi-nde wa mvua uwe ishara ya kuwakumbu-sha ahadi hiyo yenye kufariji.

Baada ya Gharika, Mungu aliwapa wana-damu amri kadhaa mpya. Aliwaruhusukula nyama za wanyama. Hata hivyo ali-wakataza wasile damu. Pia aliwaamuru wa-zao wa Noa waijaze dunia, lakini baadhiyao wakaasi. Watu walijiunga na Nimrodikatika uasi nao wakaanza kujenga mnaramkubwa katika jiji la Babeli, ambalo baa-daye lilikuja kuitwa Babiloni. Lengo lao li-likuwa kukaidi amri ya Mungu ya kuijazadunia. Hata hivyo, Mungu alivunja mipa-ngo ya waasi hao kwa kuvuruga lugha yaomoja na kuwafanya wazungumze lughambalimbali. Kwa kuwa hawakuweza kuwa-siliana, waliuacha mradi huo na kutawa-nyika.—Mwanzo sura ya 6 hadi 11; Yuda 14, 15.��������������

˛ Uovu ulienea jinsi gani duniani?˛ Noa alionyesha uaminifu wake kwa njia gani?˛ Baada ya Gharika, Mungu aliwakataza wanadamunini?

3 Wanadamu Waokoka GharikaMungu auharibu ulimwengu mwovu; amwokoaNoa na familia yake

˘ MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo

Wengi wa wazao wa Adamu na Hawa waliukataa utawalawa Yehova. Hata hivyo, baadhi yao walikuwa tofauti, kamavile mwana wao mwaminifu Abeli. Baadaye, inasemekanakwamba Enoko na Noa walitembea pamoja na Mungu,yaani, waliishi maisha yanayompendeza Yehova. (Mwanzo5:22; 6:9) Sehemu kubwa ya Biblia inazungumzia wanaumena wanawake waliomchagua Mungu kuwa Mtawala wao.

KUTEMBEA PAMOJA NA MUNGU

Page 7: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Abrahamu azaliwa 2018 1943 Agano la Kiabrahamu 1800 K.W.K.

7

MIAKA 350 baada ya Gharika ya sikuza Noa, Abrahamu alikuwa akiishi

katika jiji lenye ufanisi la Uru, eneo amba-lo leo linaitwa Iraki. Abrahamu alikuwamtu mwenye imani ya pekee. Hata hivyoimani yake ilijaribiwa.

Yehova alimwambia Abrahamu aondokekatika nchi alimozaliwa na kwenda nchiasiyoijua, nchi ya Kanaani. Abrahamu alitiibila kusita. Alikusanya watu wa nyumbayake, kutia ndani mke wake, Sara, na mpwawake Loti, akafunga safari ndefu na kwe-nda kuishi katika mahema huko Kanaani.Katika agano alilofanya pamoja na Abraha-mu, Yehova alimwahidi kwamba atamfa-nya kuwa taifa kubwa, na kwamba familiazote za dunia zitajibariki kupitia kwake,nao uzao wake utaimiliki nchi ya Kanaani.

Abrahamu na Loti walipata ufanisi, wa-kajikusanyia kondoo na ng’ombe wengi.Abrahamu alimtanguliza Loti kwa kumpanafasi achague eneo analotaka. Loti alicha-gua mkoa wenye rutuba wa Mto Yordani nakwenda kukaa karibu na jiji la Sodoma.Lakini, watu wa Sodoma walikuwa wapo-tovu kiadili—watenda-dhambi nzito mbeleza Yehova.

Yehova Mungu alimhakikishia Abraha-mu baadaye kwamba uzao wake ungeo-ngezeka na kuwa kama nyota za mbingu-ni. Abrahamu aliamini ahadi hiyo. Hatahivyo, Sara, mke wake mpendwa haku-wa na mtoto. Kisha, Abrahamu alipokuwana umri wa miaka 99, naye Sara akikaribiaumri wa miaka 90, Mungu alimwambiaAbrahamu kwamba Sara atapata mtoto.Maneno ya Mungu yalitimia. Sara akamzaaIsaka. Abrahamu alikuwa na watoto wengi-ne, hata hivyo, yule Mkombozi aliyeahidi-wa katika Edeni angetokana na ukoo waIsaka.

Wakati huohuo, Loti na familia yake wa-likuwa wakiishi Sodoma, lakini Loti haku-wa kama wakaaji wa jiji hilo waliokuwana maadili mapotovu. Yehova alipoamuakutekeleza hukumu juu ya Sodoma, ali-watuma malaika wawili wakamwonye Lotikuhusu uharibifu uliokuwa ukikaribia. Ma-laika hao walimhimiza Loti na familia yakewakimbie kutoka Sodoma na wasitazamenyuma. Kisha Mungu akanyesha mvua yamoto na kiberiti juu ya Sodoma na jiji jira-ni la Gomora lililojaa uovu. Wakaaji wotewa majiji hayo wakaangamia. Loti na bintizake wawili waliokoka. Mke wa Loti alitaza-ma nyuma, huenda akitamani vitu alivyo-kuwa ameviacha. Kutotii huko kulimfanyaapoteze uhai wake.—Mwanzo 11:10–19:38.��������������

˛ Kwa nini Abrahamu alihamia Kanaani?˛ Yehova alifanya agano gani pamoja na Abra-hamu?˛ Kwa nini Yehova aliangamiza Sodoma na Go-mora?

4 Mungu Afanya Agano na AbrahamuAbrahamu aonyesha imani kwa kumtii Mungu; Yehova aahidikumbariki na kuzidisha uzao wake

Mwanzo ˘

KutokaMamboyaWalawi

HesabuKumbukumbu la Torati

YoshuaWaamuzi

Ruthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieliHoseaYoeli

AmosiObadia

YonaMika

NahumuHabakukiSefaniaHagai

ZekariaMalaki

MathayoMarkoLuka

YohanaMatendoWaroma

1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefesoWafilipi

Wakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike

1 Timotheo2 Timotheo

TitoFilemoni

WaebraniaYakobo1Petro2Petro

1Yohana2Yohana3Yohana

YudaUfunuo

Katika nyakati za Biblia, agano lili-kuwa mkataba au mapatano rasmi.Kupitia maagano mbalimbali, auahadi takatifu, Yehova alifunua ha-tua kwa hatua jinsi ambavyo kusudilake kuhusu Mkombozi aliyeahidiwakatika Edeni lingetimizwa. Aganolililofanywa pamoja na Abrahamu li-lionyesha kwamba Yule aliyeahidiwaangekuja kupitia ukoo wa Abraha-mu. Maagano yaliyofanywa baadayeyalisaidia kumtambulisha.

MUNGU WA MAAGANO

Page 8: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

1800 K.W.K. Yosefu auzwa utumwani 1750

8

YEHOVA alijua kwamba kuna wakatiambapo mwana wake mpendwa ata-

teseka na kufa. Unabii uliorekodiwa katikaMwanzo 3:15 ulidokeza hilo. Je, Munguangeweza kuwasaidia wanadamu waelewejinsi kifo cha mwana wake kingemhuzuni-sha? Biblia ina mfano halisi uliotokea. Mu-ngu alimwagiza Abrahamu amtoe dhabi-hu Isaka mwana wake mpendwa.

Abrahamu alikuwa na imani kubwa. Ku-mbuka kwamba Mungu alikuwa ameahidikwamba Mkombozi, au Uzao ulioahidiwa,angetokea katika ukoo wa Isaka. Akiwa naimani kwamba Mungu atamfufua Isakaikihitajika, Abrahamu alikuwa tayari kutiina kumtoa mwana wake mwenyewe awedhabihu. Lakini malaika wa Mungu aka-mzuia Abrahamu dakika ya mwisho. Aki-msifu Abrahamu kwa nia yake ya kumto-lea Mungu kitu kilichokuwa na thamanizaidi kwake, Mungu alirudia ahadi Yakealiyokuwa amemtolea.

Baadaye, Isaka alipata wana wawili, Esauna Yakobo. Tofauti na Esau, Yakobo alitha-mini mambo ya kiroho naye akathawabi-shwa. Mungu alibadili jina la Yakobo lika-wa Israeli, na wana 12 wa Israeli wakawavichwa vya makabila ya Israeli. Lakini fa-milia hiyo ilipataje kuwa taifa kubwa?

Mambo yalianza wakati ambapo wengikati ya wana hao walianza kumwonea ki-jicho Yosefu, ndugu yao mdogo. Wali-muuza utumwani, naye akapelekwa Misri.Hata hivyo Mungu alimbariki kijana huyomwenye ujasiri. Ijapokuwa alikabili halingumu, Yosefu aliteuliwa na Farao, mta-wala wa Misri, na kupewa mamlaka ku-bwa. Hilo lilitokea wakati barabara, kwakuwa njaa kali ilimfanya Yakobo awatumebaadhi ya wana wake waende Misri kunu-nua vyakula—naye Yosefu ndiye aliyekuwa

akisimamia ugawanyaji wa chakula! Baadaya kuungana tena na ndugu zake wenyetoba, Yosefu aliwasamehe na kupanga fa-milia nzima ihamie Misri. Walipewa eneozuri sana, ambapo wangeweza kukaa nakupata ufanisi. Yosefu alielewa kwambaMungu alikuwa ameelekeza mambo hivyoili atimize ahadi Zake.

Yakobo alimalizia maisha yake hukoMisri, akiwa na familia yake iliyoku-wa ikizidi kuongezeka. Alipokuwa akika-ribia kufa, alitabiri kwamba Mkombozi,au Uzao ulioahidiwa, angekuwa Mtawalamwenye nguvu ambaye angezaliwa katikaukoo wa mwana wake Yuda. Kabla haja-fa miaka kadhaa baadaye, Yosefu alitabirikwamba siku moja, Mungu angeitoa fami-lia ya Yakobo nchini Misri.—Mwanzo sura ya 20 hadi 50; Waebrania 11:17-22.��������������

˛ Mungu alimwagiza Abrahamu afanye nini, nahilo lingewasaidia wanadamu kuelewa nini?˛ Yosefu alifikaje Misri, na matokeo yalikuwa nini?˛ Yakobo alitabiri nini kabla ya kufa?

5 Mungu AmbarikiAbrahamu na Familia YakeWazao wa Abrahamu wapata ufanisi. Munguamlinda Yosefu nchini Misri

˘ MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo2 TimotheoTitoFilemoniWaebraniaYakobo1 Petro2 Petro1 Yohana2 Yohana3 YohanaYudaUfunuo

Page 9: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Ayubu ajaribiwa kabla ya 1613 1600 K.W.K.

9

JE, MWANADAMU yeyote angeweza kue-ndelea kuwa mwaminifu kwa Mungu

ikiwa angejaribiwa vya kutosha na iwa-po ingeonekana kana kwamba kuendeleakwake kumtii Mungu hakuna faida yoyote?Swali hilo lilitokezwa—na kujibiwa—katikakisa cha mtu anayeitwa Ayubu.

Waisraeli walipokuwa wangali Misri, Ayu-bu, mtu wa jamaa ya Abrahamu, alikuwaakiishi katika eneo ambalo leo ni Uarabuni.Wakati huohuo, malaika mbinguni waliku-sanyika mbele za Mungu, na yule mwasi,Shetani, alikuwa katikati yao. Katika mkuta-no huo huko mbinguni, Yehova alimsifumtumishi wake mwaminifu Ayubu. Alise-ma kwamba hakuna mwanadamu mwi-ngine yeyote aliye na utimilifu kama waAyubu. Lakini Shetani alisisitiza kwambaAyubu anamtumikia Mungu kwa sababuMungu anambariki na kumlinda. Shetanialidai kwamba ikiwa Ayubu angenyang’a-nywa kila kitu alichokuwa nacho, ange-mlaani Mungu.

Kwanza, Mungu alimruhusu Shetaniamnyang’anye Ayubu mali yake na watotowake, kisha aingilie afya yake. Kwa kuwaAyubu hakujua Shetani anahusika, hakuele-wa ni kwa nini Mungu anaruhusu apatwena mambo yote hayo. Hata hivyo, Ayubuhakumkana Mungu kamwe.

Marafiki watatu bandia walimjia Ayu-bu. Walisema mengi wakijaribu kumsadiki-sha eti Mungu anamhukumu kwa sababuya dhambi alizofanya kisiri. Hata walidaikwamba Mungu hapendezwi na watumishiwake wala hana imani nao. Ayubu alikataamaoni yao yenye kosa. Akiwa na uhakika,Ayubu alitangaza kwamba atadumisha uti-milifu wake mpaka kifo!

Hata hivyo, Ayubu alikosea kwa kutakasana kuonyesha kwamba hana kosa lolo-

te. Kijana anayeitwa Elihu, ambaye alikuwaakisikiliza mjadala wote huo, akaanza kuzu-ngumza. Elihu alimkaripia Ayubu kwa kuto-tambua kwamba kutetewa kwa enzi kuu yaYehova Mungu ni muhimu kuliko kutetewakwa mwanadamu yeyote. Pia aliwakaripiavikali rafiki watatu bandia wa Ayubu.

Kisha Yehova Mungu akazungumza naAyubu, akirekebisha maoni yake. Akitajauumbaji mbalimbali wa ajabu, Yehova ali-msaidia Ayubu kuona jinsi mwanadamu ali-vyo duni kwa kulinganishwa na ukuu waMungu. Ayubu alikubali nidhamu hiyo ku-toka kwa Mungu. Kwa kuwa Yehova ni“mwenye upendo mwororo sana na mwe-nye rehema,” alimponya Ayubu, akampamaradufu mali aliyokuwa nayo, na kumba-riki kwa wana wengine kumi. (Yakobo 5:11)Kwa kudumisha utimilifu wake kwa Yehovachini ya jaribu kali, Ayubu alitoa jibu toshakwa dai la Shetani kwamba wanadamu ha-wawezi kuwa waaminifu kwa Mungu waki-jaribiwa.—Kitabu cha Ayubu.��������������

˛ Shetani alidai nini kuhusu Ayubu?˛ Utimilifu wa Ayubu kwa Yehova ulitimiza nini?

6 Ayubu Adumisha UtimilifuShetani atilia shaka utimilifu wa Ayubu mbele za Mungu,lakini Ayubu abaki mwaminifu kwa Yehova

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubu ˘

ZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieliHoseaYoeli

AmosiObadia

YonaMika

NahumuHabakukiSefaniaHagai

ZekariaMalaki

MathayoMarkoLuka

YohanaMatendoWaroma

1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefesoWafilipi

Wakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike

1 Timotheo2 Timotheo

TitoFilemoni

WaebraniaYakobo1Petro2Petro

1Yohana2Yohana3Yohana

YudaUfunuo

Shetani alidai kwamba Ayubu, mtu asi-ye na lawama na mwenye kumwogopaMungu kuliko watu wote waliokuwa dunia-ni wakati huo, anamtumikia Yehova Mungukwa sababu za kibinafsi. Dai hilo la Shetanililidokeza pia kwamba viumbe wenginewote wenye akili wanamtumikia Yehovakwa sababu za kibinafsi. Suala hilo ni sehe-mu ya suala kuu zaidi ambalo Shetanializusha katika shamba la Edeni, yaani, hakina kustahili kwa enzi kuu ya Yehova. Kita-bu cha Ayubu kinaonyesha kwamba viumbewa Mungu wanaweza kuchangia kutetewakwa enzi kuu ya Yehova kwa kudumishautimilifu wao Kwake.

MASUALA MUHIMU

Page 10: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

1600 K.W.K. Kutoka Misri 1513

WANA wa Israeli waliishi Misri kwa mia-ka mingi, wakizidi kuongezeka na

kupata ufanisi. Hata hivyo, Farao mpya ali-tokea. Mtawala huyo hakumjua Yosefu. Mta-wala huyo mkatili aliyehofu idadi inayozidikuongezeka ya Waisraeli, aliwafanya kuwawatumwa na kuagiza wazaliwa wote wa kwa-nza wa kiume wauawe kwa kutupwa kati-ka Mto Nile. Lakini mama mmoja mwenyeujasiri alimhifadhi mwana wake mchanga,akamweka katika kikapu na kumficha kati-kati ya matete. Binti ya Farao alimpata mto-to huyo, akamwita Musa, na kumlea katikanyumba ya kifalme ya Misri.

Musa alipokuwa na umri wa miaka 40, ali-jikuta taabani alipompiga Mmisri aliyeku-wa akimpiga mtumwa Mwisraeli. Musa aliki-mbilia nchi ya mbali, alikoishi uhamishoni.Musa alipokuwa na umri wa miaka 80, Yeho-va alimtuma arudi Misri, asimame mbele yaFarao na kudai watu wa Mungu waachiliwe.

Farao alikataa katakata. Kwa hiyo Munguakaleta mapigo kumi juu ya Misri. Kila maraMusa aliposimama mbele ya Farao na ku-mpa nafasi ya kuepuka pigo linalofuata, Fa-rao alikuwa mkaidi, na kumwonyesha Musana Mungu wake, Yehova, dharau. Mwisho-we, pigo la kumi lilitokeza kifo cha wa-zaliwa wote wa kwanza nchini—isipokuwawale wa familia zilizomtii Yehova kwa ku-tia alama miimo ya milango yao kwa damuya mwana-kondoo aliyetolewa dhabihu. Ma-laika wa Mungu aliyetumwa kuwaangamizawazaliwa wote wa kwanza alipita nyumba

zilizokuwa na alama. Baadaye Waisraeli wali-fanya maadhimisho ya kila mwaka yanayoi-twa Pasaka ili kukumbuka ukombozi huo wapekee.

Baada ya kumpoteza mwana wake mwe-nyewe mzaliwa wa kwanza, Farao aliagizaMusa na Waisraeli wengine wote waondokeMisri. Mara moja wakapanga safari ya kuo-ndoka Misri. Lakini Farao akabadili nia. Aka-wafuata akiwa na askari wengi na magari yavita. Ilionekana kana kwamba Waisraeli ha-wana pa kwenda kwa kuwa walikuwa kati-ka ufuo wa Bahari Nyekundu. Yehova alite-nganisha maji ya Bahari Nyekundu, na hivyoWaisraeli wakapita katika sakafu kavu ya ba-hari, katikati ya kuta za maji! Wamisri wa-lipoingia wakiwafuata, Mungu aliyaachiliayale maji, yakarudi kwa kishindo na kumfu-nika Farao pamoja na jeshi lake.

Baadaye, Waisraeli walipopiga kambi kati-ka Mlima Sinai, Yehova alifanya agano pa-moja nao. Akimtumia Musa kuwa mpata-nishi, Mungu aliwapa Waisraeli sheria zakuwaongoza na kuwalinda katika nya-nja zote maishani. Maadamu Waisraeli wa-ngeukubali kabisa utawala wa Mungu, Yeho-va angekuwa pamoja nao na kulifanya taifahilo kuwa baraka kwa wengine.

Hata hivyo, inasikitisha kwamba Wais-raeli wengi hawakumwamini Mungu. Kwahiyo, Yehova akafanya kizazi hicho kitange-tange nyikani kwa miaka 40. Kisha, Musaakamteua Yoshua, aliyekuwa mtu mnyoo-fu, achukue mahali pake. Hatimaye, taifa laIsraeli likakaribia kuingia nchi ambayo Mu-ngu alimwahidi Abrahamu.—Kutoka; Mambo ya Walawi; Hesabu; Kumbuku-mbu la Torati; Zaburi 136:10-15; Matendo 7:17-36.��������������

˛ Musa alikujaje kutumiwa na Mungu kuwako-mboa Waisraeli?˛ Maadhimisho ya Pasaka yalianzaje?˛ Yehova aliwakomboa jinsi gani Waisraeli kutokakatika utumwa nchini Misri?

7 Mungu Awakomboa Wana wa IsraeliYehova aleta mapigo juu ya Misri, na Musa awaongoza wana waIsraeli kutoka katika nchi hiyo. Mungu awapa Waisraeli Sheriakupitia Musa

Mwanzo˘ Kutoka˘ MamboyaWalawi˘ Hesabu˘ Kumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo

Kati ya sheria 600 hivi zilizotolewa kupitia Musa,Amri Kumi, zilizorekodiwa katika Kutoka 20:1-17, ndizozinazojulikana sana. Hata hivyo, Yesu Kristo alipoulizwani sheria gani kati ya sheria za Mungu iliyo kuu zaidi,alichagua hii: “Lazima umpende Yehova Mungu wakokwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwaakili yako yote na kwa nguvu zako zote.”—Marko12:28-30; Kumbukumbu la Torati 6:5.

SHERIA KUU ZAIDI

Page 11: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

1473 Taifa la Israeli laingia Kanaani likiongozwa na Yoshua

1467 Ushindi dhidi ya Kanaani wakamilika 1200 K.W.K.

11

KARNE nyingi kabla ya Waisraeli kui-ngia Kanaani, Yehova alikuwa amea-

hidi kwamba wazao wa Abrahamu wa-ngeimiliki nchi hiyo. Wakiongozwa naYoshua, sasa Waisraeli wako tayari kuimi-liki Nchi ya Ahadi.

Mungu aliamua Wakanaani wanastahilikuangamizwa. Walikuwa wameijaza nchimazoea machafu ya ngono na umwagajiwa damu kimakusudi. Hivyo, majiji ya Ka-naani yaliyokuwa yametwaliwa na Wais-raeli yalipaswa kuharibiwa kabisa.

Hata hivyo, kabla ya kuingia nchi hiyo,Yoshua aliwatuma wapelelezi wawili. Wa-pelelezi haowalikaa katika nyumbaya Ra-habu jijini Yeriko. Rahabu aliwapokea nakuwalinda, ingawa alijua ni Waisraeli. Ra-habu alimwamini Mungu wa Waisraelikwa sababu alikuwa amesikia jinsi Yehovaalivyokuwa ametenda ili kuwakomboawatu wake. Aliwaambia wapelelezi haowamwapie kwamba yeye na watu wa nyu-mba yake hawataangamizwa.

Baadaye, Waisraeli walipoingia Kanaa-ni na kulizunguka Yeriko, Yehova alia-ngusha kuta za Yeriko kimuujiza. Vikosivya Yoshua vikaingia ndani na kuliharibujiji hilo, hata hivyo, Rahabu na familiayake hawakuangamizwa. Kisha, kwa mia-ka sita tu, Yoshua akatwaa sehemu ku-bwa ya Nchi ya Ahadi. Baadaye, makabilaya Israeli yakagawiwa nchi hiyo.

Akikaribia mwisho wa utumishi wakewa muda mrefu kwa Mungu, Yoshuaaliwakusanya watu pamoja. Akawaambiajinsi Yehova alivyoshughulika na babuzao, kisha akawatia moyo wamtumikieYehova. Hata hivyo, baada ya Yoshuana wanaume wazee kufa, Waisraeli wa-limwacha Yehova, wakaanza kutumikia

miungu ya uwongo. Kwa miaka 300 hivi,taifa hilo halikushikamana kabisa na she-ria za Yehova. Wakati huo, Yehova aliru-husu Waisraeli wakandamizwe na aduizao, kama vile Wafilisti. Lakini Waisraeliwalipomwomba Yehova msaada, aliwe-ka rasmi jumla ya waamuzi 12 wawako-mboe.

Kipindi cha Waamuzi wanaotajwa kati-ka kitabu cha Waamuzi kilianza sikuza Othnieli mpaka siku za Samsoni,mwanadamu mwenye nguvu zaidialiyepata kuishi. Ukweli wa msi-ngi unaothibitishwa tena na tenakatika masimulizi yenye kusisi-mua ya kitabu cha Biblia chaWaamuzi ni: Kumtii Yehovahuleta baraka, kutotii huletamsiba.—Yoshua; Waamuzi; Mambo yaWalawi 18:24, 25.��������������

˛ Kwa nini Yehova alimwokoaRahabu na familia yake?˛ Waisraeli walifanya nini baa-da ya Yoshua kufa?˛ Ni ukweli gani wa msingiunaothibitishwa katika ki-tabu cha Biblia cha Waa-muzi?

8 Waisraeli Waingia KanaaniWaisraeli waitwaa nchi ya Kanaani wakiongozwa na Yoshua.Yehova atumia waamuzi kuwakomboa watu wake kutokamikononi mwa adui zao

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua ˘

Waamuzi ˘

Ruthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

K

A

N

AA

NI

FO

IN

IK

E

UFILISTI

Yeriko

Yerusalemu

Kuingia KanaaniMajiji ambayo Waisraeli walimiliki kwanza

Page 12: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

1200 K.W.K. Sauli atiwa mafuta awe mfalme 1117

12

BAADA ya siku za Samsoni, Samwe-li alikuwa nabii na mwamuzi katika

taifa la Israeli. Waisraeli walikuwa waki-mwambia kwamba wanataka kuwa kamamataifa mengine, na kuwa na mfalme wakibinadamu. Ijapokuwa ombi hilo hali-kumpendeza Yehova, alimwagiza Samwe-li alitekeleze. Mungu alimchagua mwana-mume mnyenyekevu anayeitwa Sauli awemfalme. Hata hivyo, baada ya muda,Mfalme Sauli alibadilika na kuwa mwe-

nye kiburi na mkaidi. Yeho-va alimkataa na kumwambiaSamweli amteue mwingine—kijana anayeitwa Daudi.Hatahivyo, miaka kadhaa ili-pita kabla ya Daudi kuanzakutawala.

Yamkini akiwa katika mia-ka ya utineja, Daudi aliwatembelea nduguzake waliokuwa katika jeshi la Sauli. Je-shi zima lilikuwa limebabaishwa na askarimmoja adui, jitu linaloitwa Goliathi, lililo-kuwa likimdhihaki Mungu wao. Akiwa naghadhabu, Daudi alijitolea kupigana na jituhilo. Akiwa na kombeo na mawe matano,kijana huyo alikwenda kukutana na mpi-nzani wake, aliyekuwa na urefu wa karibumita tatu. Goliathi alipomdhihaki, Daudialijibu kwamba amejihami kuliko jitu hilokwa kuwa anapigana kwa jina la YehovaMungu! Daudi alilipiga na kuliangusha jituhilo kwa jiwe moja tu kisha akauchukuaupanga wa jitu hilo na kulikata kichwa. Je-shi la Wafilisti likakimbia kwa hofu.

Mwanzoni, Sauli alipendezwa sana naujasiri wa Daudi na kumweka aongoze je-shi lake. Hata hivyo, mafanikio ya Daudiyalimfanya Sauli awe nawivu mbaya. Dau-di alilazimika kukimbia aokoe uhai wake.Aliishi akiwa mkimbizi kwa miaka mingi.

Hata hivyo, Daudi alibaki mshikamani-fu kwa Sauli aliyekuwa akijaribu kumuua,akijua kwamba Mfalme Sauli aliwekwa naYehovaMungu. Hatimaye, Sauli akafavita-ni. Muda mfupi baadaye, Daudi akatawa-zwa, kama vile Yehova alivyokuwa amea-hidi.

Akiwa mfalme, Daudi alitamani sanakumjengea Yehova hekalu. Lakini Yeho-va akamwambia Daudi kwamba mmojawa wazao wake ndiye atakayefanya hivyo.Mzao aliyepata pendeleo hilo ni Sulemani,mwana wa Daudi. Hata hivyo, Mungu ali-mthawabisha Daudi kwa kufanya pamojanaye agano lenye kusisimua: Familia yakeingetokeza ukoo wa kifalme usio na kifa-ni. Hatimaye, Mkombozi, au Uzao ulioahi-diwa katika shamba la Edeni ungetokeakupitia ukoo huo. Mkombozi huyo ange-kuwa Masihi, yaani, “Mtiwa Mafuta,” ali-yewekwa rasmi na Mungu. Yehova aliahidikwamba Masihi huyo angekuwa Mtawalawa Ufalme au serikali ambayo ingedumumilele.

Akiwa na shukrani nyingi, Daudi aliku-sanya vifaa vingi sana vya ujenzi na madi-ni ya thamani kwa ajili ya mradi wa ujenziwa hekalu. Pia, aliongozwa na roho kua-ndika zaburi nyingi. Alipokuwa akikaribiakufa, Daudi alikiri hivi: “Roho ya Yehovandiyo iliyosema kupitia mimi, na nenolake lilikuwa kwenye ulimi wangu.”—2 Sa-mweli 23:2.—1 Samweli; 2 Samweli; 1 Nyakati; Isaya 9:7; Ma-thayo 21:9; Luka 1:32; Yohana 7:42.��������������

˛ Kwa nini Yehova alimchagua Daudi achukue ma-hali pa Mfalme Sauli?˛ Daudi alionyesha sifa gani hata kabla ya kuwamfalme?˛ Mkombozi, au Uzao ulioahidiwa ambao ungeto-kea kupitia ukoo wa Daudi ni nani?

9 Waisraeli Wataka MfalmeSauli, mfalme wa kwanza wa Israeli, akosa kutii. Daudi,ambaye Mungu afanya pamoja naye agano la ufalmewa kudumu, atawala baada yake

“Nitakifanya imarakiti cha ufalmewake mpaka wakatiusio na kipimo.”—2 Samweli 7:13

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu

˘ 1 Samweli˘ 2 Samweli1Wafalme2Wafalme

˘ 1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremia

HagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo2 TimotheoTitoFilemoniWaebraniaYakobo1 Petro2 Petro1 Yohana2 Yohana3 YohanaYudaUfunuo

Page 13: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

1070Mungu amwahidi Daudi Ufalme

Sulemani awa mfalme 1037 1027 Hekalu laYerusalemu lakamilika

mnamo 1020Wimbo wa Sulemani wakamilika

1000 K.W.K.

MAISHA yangekuwaje ikiwa taifa zimana mtawala wake wangemtambua

Yehova kuwa Mwenye Enzi Kuu na kutiisheria Zake? Ndivyo ilivyokuwa wakati wautawala wa miaka 40 ya Mfalme Sulemani.

Kabla ya Daudi kufa, alimteua Sulemaniatawale baada yake. Katika ndoto, Mungualimwambia Sulemani aombe anachota-ka. Sulemani aliomba hekima na ujuziwa kuwahukumu watu kwa haki na busa-ra. Yehova alipendezwa na jibu lake nayeakampa Sulemani moyo wenye hekimana uelewaji. Pia, Yehova alimwahidi utaji-ri, utukufu, na maisha marefu maadamuangeendelea kuwa mtiifu.

Sulemani alipata umaarufu kwa sababuya hekima yake katika kuhukumu. Katikakisa kimoja, wanawake wawili walikuwawakibishania mtoto mvulana, kila mmojaakidai kuwa mama yake. Sulemani alia-giza mtoto huyo akatwe vipande viwilina kila mwanamke apewe nusu ya mtotohuyo. Mwanamke wa kwanza akakubali,lakini mara moja mama halisi ya mtotohuyo akaanza kusihi mtoto huyo akabidhi-we mwanamke yule mwingine. Sulemaniakaona wazi kwamba mwanamke mwenyehuruma ndiye mama ya mtoto huyo, aka-mkabidhi. Muda si muda taifa zima laIsraeli likasikia kuhusu uamuzi huo wa ki-hukumu, na watu wakatambua kwambaSulemani ana hekima kutoka kwa Mungu.

Mojawapo ya mafanikio makuu ya Sule-mani ni ujenzi wa hekalu la Yehova—jengolenye fahari jijini Yerusalemu ambalo li-ngekuwa kituo cha ibada katika taifa laIsraeli. Wakati wa kuzinduliwa kwa hekaluhilo, Sulemani alisali hivi: “Tazama! Mbi-ngu, ndiyo, mbingu za mbingu, haziwezikukutosha; jinsi gani basi, nyumba hiiambayo nimeijenga!”—1 Wafalme 8:27.

Sifa za Sulemani zilifika katika nchi zambali, hata kufikia Sheba, Uarabuni. Mal-kia wa Sheba alisafiri kwenda kuuona utu-kufu na utajiri wa Sulemani, na kupimahekima yake. Malkia huyo alivutiwa sanana hekima ya Sulemani na ufanisi wa tai-fa la Israeli hivi kwamba akamsifu Yehovakwa kumtawaza mfalme mwenye hekimahivyo. Kwa kweli, Yehova aliubariki utawa-la wa Sulemani, nao ukawa utawala wenyeufanisi na amani zaidi katika historia yoteya taifa la kale la Israeli.

Kwa kusikitisha, Sulemani hakuendeleakutenda kulingana na hekima ya Yehova.Alipuuza amri ya Mungu, akaoa mamiaya wanawake, kutia ndani wengi walioku-wa wakiabudu miungu ya kigeni. Polekwa pole wake zake wakaugeuza moyowake kutoka kwa Yehova, akaanza kuabu-du sanamu. Yehova akamwambia Sule-mani kwamba atanyang’anywa sehemuya ufalme. Sehemu ndo-go tu ndiyo ingebaki kati-ka familia yake, kwa sa-babu ya ahadi ambayoMungu alimtolea Daudi,baba ya Sulemani. Lichaya kutotii kwa Sulemani,Yehova aliendelea kuwamshikamanifu kwa aganola Ufalme alilofanya naDaudi.—1 Wafalme, sura ya 1 hadi 11;2 Nyakati, sura ya 1 hadi 9; Ku-mbukumbu la Torati 17:17.��������������

˛ Mungu alijibu jinsi gani ombila Sulemani?˛ Sulemani alionyesha hekimayake kwa njia gani?˛ Sulemani alikengeuka namnagani na kuziacha njia za Yehova,na matokeo yakawa nini?

10 Sulemani Atawala kwa HekimaYehova ampa Mfalme Sulemani moyo wa hekima;wakati wa utawala wa Sulemani, Waisraeli waishikwa amani na ufanisi usio na kifani

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

1 Samweli2 Samweli1Wafalme ˘

2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati ˘

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieliHoseaYoeli

AmosiObadia

YonaMika

NahumuHabakukiSefaniaHagai

Zekaria

Page 14: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

1000 K.W.K. 997 Taifa la Israeli lagawanyika na kuwa falme mbili

14

KITABU kikubwa zaidi katika Biblia nimkusanyo wa nyimbo takatifu. Kita-

bu hicho kilichukua miaka 1,000 hivi kua-ndikwa. Kitabu cha Zaburi kina manenoyenye kupendeza nayenye kuchochea sanaya imani kuliko kitabu kingine chochote.Nyimbo hizo za sifa zinafunua hisia mbali-mbali za wanadamu, kama vile, shangwe,shukrani, huzuni, sikitiko, na toba. Ni wazikwamba mtunga-zaburi alikuwa na uhu-siano wa karibu pamoja na Mungu nayealimtumaini. Fikiria baadhi ya mambo ya-liyo katika nyimbo hizo.

Yehova ana haki ya kutawala, kua-budiwa na kusifiwa. Katika Zaburi 83:18tunasoma: “Wewe peke yako ndiye UliyeJuu Zaidi, juu ya dunia yote.” Zaburi nyingizinamsifu Yehova kwa kazi zake za uumba-ji, kama vile mbingu zenye nyota, viumbevya ajabu duniani, na jinsi mwanadamualivyoumbwa kwa njia ya ajabu. (Zaburi8, 19, 139, 148) Zaburi nyingine humtu-kuza Yehova kuwa Mungu ambaye hu-wawaokoa na kuwalinda washikamanifuwake. (Zaburi 18, 97, 138) Na katika zaburi

nyingine anatajwa kuwa Mungu mwenyehaki, anayewafariji walioonewa na kuwaa-dhibu waovu.—Zaburi 11, 68, 146.

Yehova huwasaidia na kuwafarijiwanaompenda. Huenda zaburi inayoju-likana sana ni ya 23. Katika zaburi hiyo,Daudi anamtaja Yehova kuwa Mchungajimwenye upendo anayewaongoza, kuwali-nda, na kuwajali kondoo wake. Zaburi 65:2inawakumbushawaabudu wa Mungu kwa-mba Yehova ni “msikiaji wa sala.” Wengiambao wametenda dhambi nzito wamefa-rijiwa sana na Zaburi ya 39 na ya 51. Katikazaburi hizo, Daudi anatubu kwa unyoo-fu dhambi nzito alizofanya nayo manenoyake yanaonyesha wazi anaamini kwambaYehova husamehe. Zaburi 55:22 inatuhi-miza tumtegemee Yehova na kumtupia mi-zigo yetu yote.

Yehova ataubadili ulimwengu ku-pitia Ufalme wa Masihi. Sehemu mbali-mbali za kitabu cha Zaburi zinamhusumoja kwa moja Masihi, Mfalme aliyeahidi-wa. Zaburi ya 2 inatabiri kwamba Mtawalahuyo ataharibu mataifa maovu yanayo-mpinga. Zaburi ya 72 inaonyesha kwa-mba Mfalme huyo ataondoa njaa, ukosefuwa haki, na uonevu. Kulingana na Zaburi46:9, Mungu atakomesha vita na kuharibusilaha zote za vita kupitia Ufalme wa Kima-sihi. Katika Zaburi ya 37, tunasoma kwa-mba waovu wataharibiwa, lakini waadilifuwataishi milele duniani, wakifurahia ama-ni na upatano.—Kitabu cha Zaburi.��������������

˛ Zaburi zinaunga mkono jinsi gani haki ya Yehovaya kutawala?˛ Ni zaburi gani zinazoonyesha jinsi Mungu ana-vyowasaidia na kuwafariji wanaompenda?˛ Kulingana na kitabu cha Zaburi, Yehova atauba-dili ulimwengu jinsi gani?

11 Nyimbo Zilizoongozwa na RohoAmbazo Zinafariji na KufundishaDaudi na wengine watunga nyimbo kwa ajili ya ibada.Kitabu cha Zaburi kina nyimbo 150

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubu

˘ ZaburiMethaliMhubiri

˘ Wimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo2 TimotheoTitoFilemoniWaebraniaYakobo1 Petro2 Petro1 Yohana2 Yohana3 YohanaYudaUfunuo

Katika Wimbo wa Sulemani, mfalme ana-funua kwamba hata mtu awe na mali nyingikiasi gani haimaanishi kwamba anawezakupata chochote anachotaka hasa kuhusumasuala ya mahaba. Anaandika jinsi alivyo-jaribu kumshawishi bikira mrembo ambayetayari alikuwa anampenda mvulana mchu-ngaji. Wimbo huo ulioongozwa na rohounaonyesha kwamba hata watu wanapovu-tiwa na wengine kimahaba wanapaswakujizuia wasijiendeshe kwa njia isiyofaa.Mchungaji huyo na mwenzake ni mfanomzuri wa sifa ya kujizuia, kudumisha usafiwa kiadili, na kuwa washikamanifu.

WIMBO ULIO BORA

Page 15: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Kuandikwa kwa Methali kwakamilikamnamo 717 700 K.W.K.

JE, Yehova ni Mtawala mwenye hekima?Njia moja yenye kuridhisha ya kujibu

swali hilo ni kuchunguza mashauri anayo-toa. Je, yanafanya kazi? Je, kuyatumia kuna-fanya maisha yawe mazuri zaidi na yenyekusudi? Mfalme Sulemani mwenye hekimaaliandika mamia ya methali. Methali hizozinazungumzia nyanja zote za maisha. Fiki-ria mifano kadhaa.

Kumtegemea Mungu. Ili kuwa na uhu-siano mzuri pamoja na Yehova, lazima tu-mtegemee. Sulemani aliandika: “MtegemeeYehova kwa moyo wako wote wala usitege-mee uelewaji wako mwenyewe. Mtambueyeye katika njia zako zote, naye atanyooshamapito yako.” (Methali 3:5, 6) KumtegemeaMungu kwa kufuata mwongozo wake na ku-mtii hufanya maisha yawe na kusudi. Mtuanayefanya hivyo huufurahisha moyo waMungu na kumpa Yehova jibu la masualayaliyozushwa na mpinzani Wake, Shetani.—Methali 27:11.

Kushughulika na watu wenginekwa hekima. Leo, kuliko wakati mwingi-ne wowote, tunafaidika na shauri la Mungukwa waume, wake, na watoto. “Ushangiliepamoja na mke wa ujana wako,” Munguawashauri waume, akiwaagiza wawe waami-nifu kwa wake zao. (Methali 5:18-20) Wana-wake walioolewa wanaweza kufaidika naufafanuzi wenye kupendeza ulio katika kita-bu cha Methali kuhusu mke mwenye uwezoanayejipatia sifa kutoka kwa mumewe nawatoto wake. (Methali, sura ya 31) Naowatoto wanaagizwa wawatii wazazi wao.(Methali 6:20) Kitabu hicho kinaonyeshakwamba urafiki ni muhimu, kwa kuwa kuji-tenga hutokeza ubinafsi. (Methali 18:1) Ma-rafiki wanaweza kuwa na uvutano mzuri aumbaya, kwa hiyo tunapaswa kuwachaguakwa uangalifu.—Methali 13:20; 17:17.

Kujitunza kwa hekima. Kitabu chaMethali kina mashauri mazuri kuhusu kue-

puka matumizi yasiyofaa ya vileo, kusitawi-sha hisia zinazofaa na kuondolea mbali zisi-zofaa, na kuwa mfanyakazi mwenye bidii.(Methali 6:6; 14:30; 20:1) Kitabu hicho ki-naonya kwamba kutegemea akili ya mwana-damu na kupuuza shauri la Mungu huto-keza msiba. (Methali 14:12) Kinatuhimizatumlinde yule mtu wa ndani, moyo wetu,dhidi ya uvutano mbalimbali usiofaa, nakutukumbusha kwamba katika moyo “ndi-ko zinakotoka chemchemi za uzima.”—Me-thali 4:23.

Mamilioni ya watu ulimwenguni wame-jionea kwamba kuishi kupatana na mashau-ri hayo hufanya maisha yawe mazuri zaidi.Kwa sababu hiyo, wana sababu nzuri ya ku-mkubali Yehova kuwa Mtawala wao.—Kitabu cha Methali.��������������

˛ Tunaweza kujifunza nini kwa kuchunguza kitabucha Methali?˛ Ni mwongozo gani ambao kitabu cha Methali ki-natoa kuhusu kumtegemea Mungu na kushughuli-ka kwa hekima na watu wengine, na pia tunapoji-tunza?

12 Hekima Kutoka kwa MunguInayotuongoza MaishaniKitabu cha Methali ni hazina ya mashauri kutoka kwa Mungu yanayotupamwongozo maishani. Nyingi za methali hizo ziliandikwa na Sulemani

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethali ˘

Mhubiri ˘

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieliHoseaYoeli

AmosiObadia

YonaMika

NahumuHabakukiSefaniaHagai

ZekariaMalaki

MathayoMarko

Mtu anaweza kupata maisha yenye kusudi na yenyekuridhisha jinsi gani? Kati ya watu wote, Sulemani hasaangeweza kupata jibu la swali hilo. Kwa kuwa alikuwana utajiri mwingi, hekima, na mamlaka, angeweza ku-fanya uchunguzi na kuona ikiwa vitu hivyo vinaletafuraha ya kweli maishani. Aliishi maisha ya anasa,akaoa wanawake wengi warembo, na kufurahia buru-dani bora zaidi. Alianzisha miradi mikubwa ya ujenzi.Alichunguza maandishi ya wasomi. Alipata jibu gani?“Kila kitu ni ubatili.” Hata hivyo, alikata kauli hii: “Huundio mwisho wa mambo, kila jambo limekwisha sikiwa:Mwogope Mungu wa kweli na kushika amri zake. Kwamaana huo ndio wajibu wote wa mwanadamu.”—Mhubiri 12:8, 13.

MHUBIRI

Page 16: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

700 K.W.K. Jiji la Yerusalemu laharibiwa; uhamisho wa Babiloni waanza 607

KAMA Yehova alivyotabiri, kwa sababu Su-lemani aliiacha ibada safi, taifa la Israeli

liligawanyika. Mwana wake aliyetawala baadayake, Rehoboamu, alikuwa mkali. Kwa hiyo,makabila kumi ya Israeli yakaasi na kufanyizaufalme wa kaskazini wa Israeli. Makabila ma-wili yakaendelea kuwa chini ya mtawala ali-yeketi katika kiti cha ufalme cha Daudi jijiniYerusalemu, yakifanyiza ufalme wa kusini waYuda.

Falme zote mbili zilikuwa na misukosuko,hasa kwa sababu ya wafalme wake ambao ha-wakuwa watiifu. Hali ya Israeli ilikuwa mbayakuliko ya Yuda, kwa kuwa wafalme wake wa-liunga mkono ibada ya uwongo tangu mwa-nzo. Licha ya kazi zenye nguvu za manabiikama vile Eliya na Elisha—ambao hata waliwa-fufua wafu—taifa la Israeli lilirudia njia mbayatena na tena. Mwishowe, Mungu akawaruhu-su Waashuru wauharibu ufalme wa kaskazini.

Ufalme wa Yuda ulidumu miaka mia mojahivi baada ya ufalme wa Israeli kuangamizwa,

lakini huo pia ulihukumiwa na Mungu. Niwafalme wachache wa Yuda waliotii maonyoya manabii wa Mungu na kujaribu kuliongo-za taifa limrudie Yehova. Kwa mfano, Mfal-me Yosia alianza kusafisha Yuda, akiondoleambali ibadaya uwongo na kurekebisha heka-lu la Yehova. Nakala ya awali ya Sheria yaMungu iliyotolewa kupitia Musa ilipopati-kana, Yosia alichochewa sana naye akazidi-sha kampeni yake ya kufanya mabadiliko.

Hata hivyo, inasikitisha kwamba wafal-me waliotawala baada ya Yosia hawakufua-ta mfano wake mzuri. Kwa hiyo, Yehovaakaruhusu taifa la Babiloni lishinde Yuda,na kuharibu Yerusalemu pamoja na hekalulake. Waliookoka walipelekwa uhamishoniBabiloni. Mungu alitabiri kwamba wangekaauhamishoni kwa miaka 70. Wakati wote huoYuda palikuwa magofu—hadi, kama ilivyota-biriwa, taifa hilo liliporuhusiwa kurudi kati-ka nchi yao.

Hata hivyo, hakuna wafalme wowote waukoo wa Daudi wangetawala hadi utawala wayule Mkombozi aliyeahidiwa, Masihi aliyeta-biriwa. Utawala wa wengi kati ya wafalmewalioketi katika kiti cha ufalme cha Dau-di jijini Yerusalemu ulionyesha wazi kwa-mba wanadamu wasio wakamilifu hawasta-hili kutawala. Masihi tu ndiye angestahilikikweli. Hivyo, Yehova akamwambia mfal-me wa mwisho katika ukoo huo wa Daudi:‘Livue taji. Hakika hili halitakuwa la mtu ye-yote mpaka atakapokuja yule aliye na hakiya kisheria, nami nitampa yeye.’—Ezekieli21:26, 27.—1 Wafalme; 2 Wafalme; 2 Nyakati, sura ya 10 hadi36; Yeremia 25:8-11.��������������

˛ Ufalme wa Israeli uligawanyika kwa nini, na fa-lme mbili zilizotokea ziliendelea jinsi gani?˛ Ni nini kilichoipata nasaba ya wafalme wa fami-lia ya Daudi, na kwa nini?˛ Hadithi ya Yona inatufundisha nini kumhusu Ye-hova? (Ona sanduku.)

13 Wafalme Wazuri na Wafalme WabayaTaifa la Israeli limegawanyika. Wafalme wengi watawala taifahilo, na wengi wao si waaminifu. Yerusalemu laharibiwa naWababiloni

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli

˘ 1Wafalme˘ 2Wafalme1MamboyaNyakati

˘ 2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadia

˘ YonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalaki

Ufalme ulipokuwa umegawanyika, Mungu alimtumaYona aende kutangaza ujumbe wa kuonya kwa watuwa Ninawi, jiji la mbali lililojaa jeuri. Yona alipanda melina kwenda upande mwingine. Hali hiyo ilitokeza muuji-za—Mungu alimfanya samaki mkubwa ammeze Yona.Akiwa ndani ya samaki huyo, Yona alimwomba Yehova,ambaye alimfanya samaki huyo amtapike kwenye nchikavu. Kisha Yona akatimiza mgawo wake.Baada ya Mungu kumfundisha Yona kuhusu utii, ta-

tizo la pili likatokea: Yona aliwahubiria Waninawi, lakinialichukizwa sana Mungu alipowaonyesha rehema kwakuwahurumia na kutotekeleza hukumu yake kwa sababuwalitubu. Soma kitabu hicho chenye kusisimua uone ji-nsi Mungu alivyotumia mfano wa pili kumfundisha Yonakuwa mwenye huruma.

YONA

Page 17: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

539 Koreshi aangusha Babiloni

537Wayahudi warudi Yerusalemu 455 K.W.K.Kuta za Yerusalemu zajengwa upya;majuma 69 ya miaka yaanza

17

WAKATI wa wafalme wa Israeli naYuda, kulikuwa na kikundi fulani

cha wanaume wa pekee—manabii. Wali-kuwa na imani ya pekee na ujasiri wa ku-tangaza ujumbe mbalimbali wa Mungu.Fikiria mambo manne makuu yaliyozu-ngumziwa na manabii hao wa Mungu.

1. Kuharibiwa kwa Yerusalemu.Mapema sana, manabii wa Mungu—Isayana Yeremia hasa—walianza kuonya kwa-mba Yerusalemu lingeharibiwa na kua-chwa ukiwa. Walitangaza waziwazi nikwa nini jiji hilo lilistahili hasira ya Mu-ngu. Mazoea yake ya dini za uongo, ufi-sadi, na jeuri yalithibitisha dai lake lakumwakilisha Yehova kuwa la uwongo.—2 Wafalme 21:10-15; Isaya 3:1-8, 16-26;Yeremia 2:1–3:13.

2. Kurudishwa kwa ibada ya kweli.Baada ya miaka 70 ya uhamisho, watu waMungu waliachiliwa kutoka Babiloni. Wa-lirudi katika makao yao yaliyokuwa uki-wa na kujenga upya hekalu la Yehova ji-jini Yerusalemu. (Yeremia 46:27; Amosi9:13-15) Miaka 200 hivi mapema, Isayaalitabiri jina la mshindi—Koreshi—amba-ye angeshinda Babiloni na kuwaruhusuwatu wa Mungu warudishe tena ibada

safi. Isaya hata alieleza waziwazi jinsiambavyo Koreshi angefanya hivyo.—Isa-ya 44:24–45:3.

3. Kufika kwa Masihi na mamboyaliyompata. Masihi angezaliwa katikamji wa Bethlehemu. (Mika 5:2) Angeku-wa mnyenyekevu, angeingia Yerusalemuakiwa amepanda punda. (Zekaria 9:9)Ijapokuwa alikuwa mpole na mwenyefadhili, hangependwa na wengi, badalayake wengi wangemkataa. (Isaya 42:1-3;53:1, 3) Angeuawa kikatili. Je, huo ndioungekuwa mwisho wake? Hapana, kwakuwa dhabihu yake ingewezesha msama-ha wa dhambi za watu wengi. (Isaya 53:4,5, 9-12) Ufufuo wake tu ndio ungeweze-sha hilo.

4. Utawala wa Masihi juu ya dunia.Wanadamu wasio wakamilifu hawawezikujitawala wenyewe kwa amani, lakiniMfalme wa Kimasihi angeitwa Mkuu waAmani. (Isaya 9:6, 7; Yeremia 10:23) Chi-ni ya utawala wake, kungekuwa na amanikati ya wanadamu wote na pia wanyama.(Isaya 11:3-7) Magonjwa hayatakuwako.(Isaya 33:24) Hata kifo kitamezwa milele.(Isaya 25:8) Wakati wa utawala wa Masi-hi, wafu watafufuliwa waishi duniani.

—Danieli 12:13.—Isaya, Yeremia, Danieli, Amosi,Mika, na Zekaria.��������������

˛ Manabii wa Mungu walitangazaujumbe gani?˛ Manabii walitabiri kuharibiwana kujengwa upya kwa Yerusale-mu jinsi gani?˛ Manabii wa Yehova walisemanini kuhusu Masihi na mamboambayo yangempata?˛ Manabii walifafanua jinsi ganiutawala wa Masihi juu ya dunia?

14 Mungu Asema Kupitia Manabii WakeManabii wawekwa na Yehova watangaze ujumbe kuhusuhukumu, ibada safi, na tumaini la Kimasihi

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya ˘

Yeremia ˘

Maombolezo ˘

Ezekieli ˘

Danieli ˘

Hosea ˘

Yoeli ˘

Amosi ˘

Obadia ˘

Yona ˘

Mika ˘

Nahumu ˘

Habakuki ˘

Sefania ˘

Hagai ˘

Zekaria ˘

Malaki ˘

MathayoMarkoLuka

YohanaMatendoWaroma

1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefesoWafilipi

Wakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike

1 Timotheo2 Timotheo

TitoFilemoni

WaebraniaYakobo1Petro2Petro

1Yohana2Yohana3Yohana

YudaUfunuo

Page 18: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

455 K.W.K.

Baada ya 443 K.W.K.Malaki akamilisha kitabu chake cha kinabii

Majuma 69 ya miaka yaanza

18

DANIELI, kijana mwenye utimilifu wapekee, alipelekwa uhamishoni Babi-

loni kabla ya Yerusalemu kuharibiwa.Yeye na Wayahudi wengine—waliohami-shwa kutoka katika ufalme ulioshindwa waYuda—walipewa kiasi fulani cha uhuru nawale waliowateka. Kwa muda mrefu alioku-wa Babiloni, Danieli alibarikiwa sana naMungu, hata akaponyoka kifo katika shimola simba na kupokea maono yaliyomweze-sha kuona wakati ujao ulio mbali. Unabiimuhimu zaidi wa Danieli ulikazia Masihina utawala Wake.

Danieli apata kujua Masihi atafikawakati gani. Danieli aliambiwa wakatiambapo watu wa Mungu wangeweza kuta-zamia “Masihi Kiongozi” afike—Majuma 69ya miaka baada ya amri ya kujengwa upyakuta za Yerusalemu kutolewa. Juma la ka-waida lina siku saba; juma la miaka ni mia-ka saba. Amri hiyo ilitolewa muda mrefubaada ya wakati wa Danieli, yaani, mwakawa 455 K.W.K. “Majuma” hayo 69 yalia-nza wakati huo na kuendelea kwa mudawa miaka 483, hadi mwaka wa 29 W.K.Katika sehemu inayofuata ya broshua hii,tutaona kilichotokea mwaka huo. Danielialiona kimbele kwamba Masihi “angekatili-wa mbali,” au kuuawa, ili kufanya upatani-sho wa dhambi.—Danieli 9:24-26.

Masihi angekuwa Mfalme mbingu-ni. Katika maono yasiyo ya kawaida yambingu zenyewe, Danieli alimwona Ma-sihi, akirejelewa kuwa “mtu fulani kamamwana wa binadamu,” akikaribia kiticha ufalme cha Yehova mwenyewe. Yehovaalimkabidhi “utawala na heshima na ufal-me.” Ufalme huo ungedumu milele. Danie-li alipata kujua jambo lingine lenye kusisi-mua kuhusu Ufalme wa Kimasihi—Mfalmehuyo angetawala pamoja na wengine, ki-

kundi kinachoitwa “watakatifu wa AliyeMkuu Zaidi.”—Danieli 7:13, 14, 27.

Ufalme utaharibu serikali za uli-mwengu huu. Mungu alimpa Danieliuwezo wa kufasiri ndoto ambayo ilimka-nganya Nebukadneza, mfalme wa Babilo-ni. Mfalme huyo aliona sanamu kubwa ye-nye kichwa cha dhahabu, kifua na mikonoya fedha, tumbo na mapaja ya shaba, mi-guu ya chuma, na nyayo za mchanganyikowa chuma na udongo. Jiwe lililokatwa ku-toka katika mlima lilipiga nyayo dhaifuza sanamu hiyo na kuivunjavunja. Da-nieli alieleza kwamba sehemu mbalimba-li za sanamu hiyo ziliwakilisha mfuata-no wa serikali mbalimbali za ulimwengu,kuanzia Babiloni iliyowakilishwa na kilekichwa cha dhahabu. Danieli aliona ki-mbele kwamba wakati wa utawala wa seri-kali ya mwisho ya ulimwengu huu mwo-vu, Ufalme wa Mungu ungechukua hatua.Ungezivunja-vunja serikali zote za ulimwe-ngu huu. Kisha utawale milele.—Danieli,sura ya 2.

Akiwa mzee sana, Danieli alijionea kua-nguka kwa Babiloni. Mfalme Koreshialilipindua jiji hilo kama manabii wali-vyotabiri. Punde baadaye, Wayahudi wa-kaachiliwa huru kutoka uhamishoni—wa-kati barabara ulioahidiwa, baada ya ilemiaka 70 ya ukiwa wa nchi yao. Wa-kiongozwa na magavana, makuhani, namanabii waaminifu, Wayahudi walijengaupya Yerusalemu na kulirekebisha hekalula Yehova. Hata hivyo, ni nini ambacho ki-ngetokea baada ya ile miaka 483 kumali-zika?—Kitabu cha Danieli.��������������

˛ Danieli alipata kujua nini kuhusu Masihi na Ufal-me wa Mungu?˛ Ufalme wa Mungu ungezifanyia nini serikali zaulimwengu huu?

15 Nabii Aliye Uhamishoni ApataMaono ya Wakati UjaoDanieli atabiri kuhusu Ufalme wa Mungu na Masihiatakayekuja. Ufalme wa Babiloni waanguka

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

˘ Ezra˘ NehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieli

˘ DanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo2 TimotheoTitoFilemoniWaebraniaYakobo1 Petro2 Petro1 Yohana2 Yohana3 YohanaYudaUfunuo

Page 19: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Kuzaliwa kwa Yesumnamo2 K.W.K.

1 K.W.K. 1W.K.taarifa:

Hakuna mwaka wa sufuri

29W.K.Yesu abatizwa

JE, Yehova angewasaidia watu wake ku-mtambua Masihi? Ndiyo. Fikiria aliyo-

fanya. Karne nne baada ya Maandiko yaKiebrania kumalizika, katika jiji linaloi-twa Nazareti, eneo la kaskazini la Gali-laya, mwanamke kijana anayeitwa Mariaalitembelewa na mgeni asiye wa kawai-da. Malaika anayeitwa Gabrieli alimto-kea na kumwambia kwamba ijapokuwayeye ni bikira, Mungu angetumia ngu-vu zake za utendaji, roho takatifu, ku-mfanya azae mwana. Mwana huyo ndiyeMfalme aliyeahidiwa zamani, yule amba-ye angetawala milele! Mtoto huyo angeku-wa Mwana wa Mungu mwenyewe. Munguangeuhamisha uhai wake kutoka mbingu-ni na kuutia katika tumbo la uzazi la Ma-ria.

Maria alikubali kwa unyenyekevu mga-wo huo wa pekee. Mchumba wake, se-remala anayeitwa Yosefu, alimwoa baadaya Mungu kumtuma malaika amhakiki-shie chanzo cha uja-uzito wa Maria. Hatahivyo, unabii uliosema kwamba Masihiangezaliwa Bethlehemu ungetimizwa jinsigani? (Mika 5:2) Jiji hilo dogo lilikuwaumbali wa kilomita 140 hivi kutoka Naza-reti!

Mtawala Mroma aliagiza watu wahesa-biwe. Watu walipaswa kujiandikisha kati-ka miji ya nyumbani kwao. Inaonekanakwamba Bethlehemu kulikuwa nyumbanikwa Yosefu na Maria, kwa hiyo Yosefu namke wake wakasafiri hadi huko. (Luka 2:3)Maria alizalia zizini, na kumlaza mtotowake katika hori. Kisha Mungu akatumamalaika wengi wakawaambie wachungajiwaliokuwa mlimani kwamba mtoto amba-ye amezaliwa ndiye Masihi, au Kristo, ali-yeahidiwa.

Baadaye, wengine pia walishuhudia kwa-

mba Yesu ndiye Masihi aliyeahidiwa. NabiiIsaya alitabiri kwamba mtu fulani angeto-kea na kutayarisha njia kwa ajili ya kazimuhimu ya Masihi. (Isaya 40:3) Mtu huyoni Yohana Mbatizaji. Alipomwona Yesu, ali-paaza sauti: “Ona, Mwana-Kondoo wa Mu-ngu ambaye huondolea mbali dhambi yaulimwengu!” Baadhi ya wanafunzi wa Yo-hana wakamfuata Yesu mara moja. Mmojawao akasema: “Tumempata Masihi.”—Yo-hana 1:29, 36, 41.

Kulikuwa na ushuhuda zaidi. Yohana ali-pombatiza Yesu, Yehova mwenyewe alise-ma kutoka mbinguni. Akitumia roho taka-tifu, alimweka rasmi Yesu kuwa Masihi nakusema: “Huyu ni Mwanangu, mpendwa,ambaye nimemkubali.” (Mathayo 3:16, 17)Masihi aliyeahidiwa akawa amefika!

Hilo lililotokea wakati gani? Mwaka wa29 W.K., wakati ambapo ile miaka 483 ili-yotabiriwa na Danieli ilipokamilika. Ndiyo,utimizo huo ni mojawapo ya ushuhuda we-nye kuthibitisha kwamba Yesu ndiye Masi-hi, au Kristo. Hata hivyo, alitangaza uju-mbe gani alipokuwa duniani?—Mathayo, sura ya 1 hadi 3; Marko, sura ya 1; Luka,sura ya 2; Yohana, sura ya 1.��������������

˛ Ni kwa njia gani Yehova aliwatumia malaika ku-mtambulisha Yesu kuwa ndiye Masihi?˛ Mungu alimtumia Yohana Mbatizaji jinsi ganikumtambulisha Yesu kuwa ndiye Masihi?˛ Yehova mwenyewe alimtambulisha jinsi ganiMwana wake kuwa ndiye Masihi?

16 Masihi AfikaYehova amtambulisha Yesu wa Nazaretikuwa Masihi aliyeahidiwa

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieliHoseaYoeli

AmosiObadia

YonaMika

NahumuHabakukiSefaniaHagai

ZekariaMalaki

Mathayo ˘

Marko ˘

Luka ˘

Yohana ˘

MatendoWaroma

1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefesoWafilipi

Wakolosai1Wathesalonike

Yehova ndiye Baba ya Yesu—lakini si kwa njia ileileambayo wanaume wa kibinadamu walivyo baba. Uhai waYesu haukuanzia katika tumbo la uzazi la mwanamke, balialiumbwa na Mungu. Yeye ndiye mtu wa kwanza aliyeu-mbwa na Yehova. (Wakolosai 1:15-17) Kwa kuwa Yehovaalimpa Yesu uhai alipomuumba, anaweza kuitwa Baba yaYesu. Baada ya kumuumba Mwana wake wa kiroho, Yeho-va alimtumia akiwa “stadi wa kazi” kutokeza vitu vinginevyote, kutia ndani ulimwengu tunaojua.—Methali 8:30.

YESU NI MWANA WA MUNGU JINSI GANI?

Page 20: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

29W.K. Yesu aanza kuhubirikuhusu Ufalme wa Mungu

Yesu achagua mitume 12; Mahubiri ya Mlimani 31

20

KWA nini Yesu alikuja duniani? Yeyemwenyewe alisema: “Lazima nita-

ngaze habari njema ya ufalme wa Mungu. . . kwa sababu nilitumwa kufanya hi-vyo.” (Luka 4:43) Fikiria mambo manneambayo Yesu alifundisha kuhusu Ufalme,jambo kuu katika mahubiri yake.

1. Yesu aliteuliwa kuwaMfalme. Yesu alisema wa-ziwazi kwamba yeye ndiyeMasihi aliyeahidiwa. (Yoha-na 4:25, 26) Pia, alionye-sha kwamba ndiye Mfalmeambaye nabii Danieli alionakatika maono. Yesu aliwaa-mbia mitume wake kwamba

siku moja ataketi juu ya ‘kiti cha ufalmechenye utukufu’ na kwamba wao pia wa-taketi juu ya viti vya ufalme. (Mathayo19:28) Alikiita kikundi hicho cha watawa-la “kundi dogo,” naye alisema kwambaana “kondoo wengine,” ambao si sehe-mu ya kikundi hicho.—Luka 12:32; Yoha-na 10:16.

2. Ufalme wa Mungu utaleta hakiya kweli. Yesu alionyesha kwamba Ufal-me utaondolea mbali ukosefu mkubwazaidi wa haki kwa kulitakasa, au kulifanyakuwa takatifu, jina la Yehova Mungu nakuliondolea masuto yote ambayo Shetaniamelimbikiza juu ya jina hilo tangu uasiwa Edeni. (Mathayo 6:9,10) Pia, Yesu alio-nyesha kila siku kwamba hana ubaguzi,kwa kuwahubiria wanaume kwa wanawa-ke, matajiri kwa maskini. Ijapokuwa alipa-swa kuwafundisha Waisraeli hasa, aliku-wa tayari kuwasaidia Wasamaria na Watuwa Mataifa au wasio Wayahudi. Tofauti naviongozi wa dini wa siku zake, hakuonye-sha upendeleo hata kidogo.

3. Ufalme wa Mungu si sehemu yaulimwengu huu. Yesu aliishi wakatiambapo kulikuwa na misukosuko mingi.Nchi ya kwao ilikuwa ikitawaliwa na seri-kali ya nchi nyingine. Hata hivyo, watuwalipojaribu kumhusisha katika masualaya kisiasa ya siku zake, alijiondoa. (Yohana6:14, 15) Alimwambia mwanasiasa mmoja:“Ufalme wangu si sehemu ya ulimwenguhuu.” (Yohana 18:36) Nao wafuasi wake,aliwaambia: “Ninyi si sehemu ya ulimwe-ngu.” (Yohana 15:19) Hakuwaruhusu kutu-mia silahazavita, hatakwa kusudi la kumli-nda yeye mwenyewe.—Mathayo 26:51, 52.

4. Kristo atatawala kwa upendo.Yesu aliahidi kwamba atawaburudishawatu, na kuwapumzisha mizigo yao. (Ma-thayo 11:28-30) Ndivyo alivyofanya. Alitoamashauri yenye upendo na yenye kutu-mika kuhusu kukabiliana na mahangaikoya maisha, kuboresha mahusiano, kuepukakufuatiavitu vya kimwili, na kupata furaha.(Mathayo, sura ya 5-7) Kwa sababu alionye-sha upendo watu wa tabaka zote walipe-nda kuwa pamoja naye. Hata watu wa haliya chini walimiminika kwake, wakiwa nahakika kwamba atawatendea kwa fadhili naheshima. Kwa kweli Yesu atakuwa Mtawalaasiye na kifani!

Kuna njia nyingine yenye matokeo sanaambayo Yesu alitumia kuwafundisha watukuhusu Ufalme wa Mungu. Alifanya miuji-za mingi. Kwa nini? Tutaona.—Kitabu cha Mathayo, Marko, Luka, na Yohana.��������������

˛ Yesu alifundisha jinsi gani kwamba yeye ndiye Mfalmewa Kimasihi?˛ Yesu alionyesha jinsi gani kwamba atatawala kwa haki?˛ Ni kwa njia gani Yesu alionyesha waziwazi kwambaUfalme wake si sehemu ya ulimwengu huu?˛ NikwanjiaganiYesualionyeshakwambaatatawalakwaupendo?

17 Yesu Afundisha KuhusuUfalme wa MunguYesu awafundisha wanafunzi wake mambo mengi, hatahivyo akazia jambo moja kuu—Ufalme wa Mungu

“Akaanza kusafiri . . .kutoka kijiji mpakakijiji, akihubiri nakutangaza habarinjema ya ufalme waMungu.”—Luka 8:1

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburi

MikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalaki

˘ Mathayo˘ Marko˘ Luka˘ YohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo2 TimotheoTitoFilemoniWaebraniaYakobo1 Petro2 Petro1 Yohana2 Yohana3 YohanaYudaUfunuo

Page 21: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

32 Yesu amfufua Lazaro Nisani 1, 33W.K.

21

MUNGU alimwezesha Yesu kufanyamambo ambayo wanadamu we-

ngine hawangeweza kufanya. Yesu alifa-nya miujiza mingi—mara nyingi mbeleya watazamaji wengi. Miujiza hiyo ilio-nyesha kwamba Yesu ana nguvu kulikoadui zake na pia kuliko vizuizi vingineambavyo wanadamu wasio wakamilifuhawangeweza kamwe kushinda kwa ma-fanikio. Fikiria mifano kadhaa.

Njaa. Muujiza wa kwanza wa Yesu uli-kuwa kubadili maji yawe divai. Katikapindi nyingine mbili, alilisha maelfu yawatu kwa mikate na samaki wachache.Pindi zote hizo kulikuwa na chakulacha kumtosha kila mtu na hata kubaki.

Ugonjwa. Yesu aliwaponya watu “kilanamna ya ugonjwa na kila namna yaudhaifu.” (Mathayo 4:23) Aliwaponyavipofu, viziwi, wenye ukoma, wenye ki-fafa, vilema, viwete, na wasiojiweza. Ha-kuna ugonjwa uliomshinda.

Dhoruba kali. Yesu na wanafunziwake walipokuwa wakisafiri katika Ba-hari ya Galilaya, dhoruba kali ilizuka.Wanafunzi waliogopa sana. Yesu aliita-zama dhoruba hiyo na kusema: “Nya-maza, utulie!” Nayo dhoruba hiyo ika-tulia. (Marko 4:37-39) Pindi nyingine,alitembea juu ya maji kulipokuwa nadhoruba yenye kuogopesha.—Mathayo14:24-33.

Roho waovu. Roho waovu wana ngu-vu kuliko wanadamu. Watu wengi wa-meshindwa kujitoa katika mtego waadui hao hatari wa Mungu. Hata hivyo,tena na tena, Yesu alipowaamuru wato-ke watu, roho hao hawangeweza tenakuendelea kuwasumbua. Hakuwaogo-

pa. Badala yake, walita-mbua mamlaka yake naowalimwogopa.

Kifo. Kifo ni aduiambaye hakuna mwana-damu anaweza kumshi-nda. Ndiyo sababu kinai-twa “adui wa mwisho.”(1 Wakorintho 15:26)Hata hivyo, Yesu aliwafu-fua wafu. Alimfufua kija-na wa mjane na binti yawazazi waliokuwa na hu-zuni. Katika kisa cha pe-kee, Yesu alimfufua rafikiyake mpendwa, Lazaro, mbele ya uma-ti wa waombolezaji, ijapokuwa alikuwamfu kwa karibu siku nne! Hata adui zaYesu walikiri kwamba alifanya muuji-za huo.—Yohana 11:38-48; 12:9-11.

Kwa kuwa wote waliosaidiwa na Yesuhatimaye walikufa, kwa nini alifanyamiujiza yote hiyo? Miujiza ya Yesuilitimiza mambo mazuri yenye kudu-mu. Ilithibitisha kwamba unabii wotewenye kupendeza kuhusu utawala waMfalme wa Kimasihi una msingi. Haku-na haja ya kuwa na shaka kwambaMfalme aliyewekwa na Mungu hawezikuondolea mbali njaa, magonjwa, halihatari ya hewa, roho waovu, au kifochenyewe. Tayari amethibitisha kwa-mba Mungu amemkabidhi nguvu zakufanya hivyo.—Kitabu cha Mathayo, Marko, Luka na Yohana.��������������

˛ Yesu alionyesha jinsi gani kwamba ana nguvuza kukabiliana na njaa? magonjwa? dhoruba kali?roho waovu? kifo?˛ Miujiza ya Yesu inaonyesha nini kuhusu utawalawake wa wakati ujao juu ya dunia?

18 Yesu Afanya MiujizaYesu, kupitia miujiza aliyofanya, alionyesha jinsiatakavyotumia nguvu zake akiwa Mfalme

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu

YonaMika

NahumuHabakukiSefaniaHagai

ZekariaMalaki

Mathayo ˘

Marko ˘

Luka ˘

Yohana ˘

MatendoWaroma

1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefesoWafilipi

Wakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike

1 Timotheo2 Timotheo

TitoFilemoni

WaebraniaYakobo1Petro2Petro

1Yohana2Yohana3Yohana

YudaUfunuo

Page 22: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Nisani 1, 33W.K. (Sehemu ya mwezi wa 3 na sehemu ya mweziwa 4 katika kalenda ya leo)

Yesu atundikwa Nisani 14 Nisani 16Yesu afufuliwa

22

KATIKA Mlimawa Mizeituni, ambapo jijila Yerusalemu na hekalu lake lilikuwa

likionekana vizuri, mitume wanne wa Yesuwalimuuliza faraghani kuhusu mambo fu-lani aliyokuwa amezungumzia. Yesu aliku-wa ametoka kusema kwamba hekalu lililoYerusalemu litaharibiwa. Na mapema, ali-kuwa amewaambia kuhusu “umalizio wamfumo wa mambo.” (Mathayo 13:40, 49)Sasa mitume wakamuuliza: “Ni nini itaka-yokuwa ishara ya kuwapo kwako na yaumalizio wa mfumo wa mambo?”—Matha-yo 24:3.

Akiwajibu, Yesu aliwaambia mamboambayo yangetokea kabla ya Yerusalemukuharibiwa. Lakini maneno yake yaliku-wa na utimizo zaidi. Unabii wake unge-timizwa kwa kiwango kikubwa zaidi uli-mwenguni pote. Yesu alitabiri matukio nahali za ulimwengu ambazo zingekuwa isha-ra. Ishara hiyo ingewaonyesha walio dunia-ni kwamba kuwapo kwa Yesu akiwa Mfal-me mbinguni kumeanza. Yaani, ishara hiyoingeonyesha kwamba Yehova Mungu ame-mfanya Yesu kuwa Mfalme wa Ufalme wa

Kimasihi ulioahidiwa zamani za kale. Isharahiyo ingemaanisha kwamba karibuni Ufal-me huo utaondolea mbali uovu na kuwale-teawanadamu amani. Mambo ambayo Yesualitabiri yangetia alama siku za mwisho zamfumo huu wa kale wa mambo—mifumoya dini, siasa, na kijamii iliyopo leo—na kua-shiria mwanzo wa mfumo mpya.

Akieleza mambo ambayo yangetokea du-niani wakati wa kuwapo kwake akiwa Mfal-me mbinguni, Yesu alisema kwamba kunge-kuwa na vita kati ya mataifa, upungufu wachakula, matetemeko makuu ya ardhi, namagonjwayenye kuenea.Uvunjaji wa sheriaungeongezeka. Wanafunzi wa kweli wa Yesuwangehubiri habari njema za Ufalme waMungu katika dunia yote. Yote hayo yangei-shia katika “dhiki kuu” ambayo haijapatakutokea tena.—Mathayo 24:21.

Wafuasi wa Yesu wangejua jinsi gani kwa-mba dhiki hiyo iko karibu? Yesu aliwaa-mbia: “Jifunzeni jambo hili kutokana namtini.” (Mathayo 24:32) Majani ya mtini ya-napotokea kwenye matawi ni ishara ya kwa-mba msimu wa kiangazi unakaribia. Vivyohivyo, kutokea kwa ishara zote hizo alizota-biri Yesu katika kipindi kimoja cha wakatikungekuwa ishara ya kwamba mwisho ukokaribu. Hakuna yeyote ila Baba aliyejua sikuna saa barabara ambayo dhiki kuu ingeanza.Kwa hiyo, Yesu aliwahimiza hivi wanafunziwake: “Endeleeni kukesha, kwa maana ha-mjui wakati uliowekwa ni gani.”—Marko13:33.—Mathayo, sura ya 24 na 25; Marko, sura ya 13;Luka, sura ya 21.��������������

˛ Mitume wa Yesu walitaka kupata habari zaidi ku-husu nini?˛ Ishara aliyotoa Yesu ilimaanisha nini, na ilitiandani mambo gani?˛ Yesu aliwashauri nini wanafunzi wake?

19 Yesu Atabiri Matukio ya Wakati UjaoYatakayoikumba Dunia NzimaYesu ataja mambo yatakayotia alama kuwapo kwake katikamamlaka ya kifalme na ya umalizio wa mfumo wa mambo

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalaki

˘ Mathayo˘ Marko˘ LukaYohana

Yesu alitabiri kwamba kungekuwa na ishara ya kuonyeshakwamba wakati wa Mungu kuuharibu mfumo mbovu wamambo uliopo uko karibu. Tangu wakati wa Vita vya Kwa-nza vya Ulimwengu, wanadamu wamejionea mamboambayo Yesu alitabiri. Matukio mbalimbali katika dini, sia-sa, na jamii ulimwenguni pote yanaelekeza moja kwa mojakatika mwisho usioepukika wa mfumo wa mambo. Yesualiwafundisha wafuasi wake kwamba ili kuokoka, lazima mtu‘akeshe’ na kuchukua hatua ya kuwa upande wa Mungu ka-tika lile suala la enzi kuu.�—Luka 21:36; Mathayo 24:3-14.

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu unabii wa Yesu katikaukurasa wa 86-95 wa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kili-chochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

ISHARA YA KUWAPO KWA KRISTO

Page 23: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Nisani 30,33W.K.

BAADA ya Yesu kuhubiri na kufundishakwa miaka mitatu na nusu, alijua

kwamba anakaribia mwisho wa maishayake duniani. Viongozi wa dini Wayahudiwalikuwa wakipanga njama ya kumuua,lakini wakawaogopa watu walioaminikwamba yeye ni nabii. Wakati huohuo,Shetani alimshawishi mmoja wa mitu-me 12 wa Yesu—Yuda Iskariote—akawamsaliti. Viongozi wa dini walimpa Yudavipande 30 vya fedha ili amsaliti Yesu.

Usiku wake wa mwisho, Yesu aliwakusa-nya mitume wake kuadhimisha Pasaka.Baada ya Yuda kuondoka, Yesu alianzishamaadhimisho mapya, Mlo wa Jioni waBwana. Akachukua mkate, akashukuru,akawapa wale mitume 11 waliobaki. Aka-sema: “Huu unamaanisha mwili wanguambao utatolewa kwa ajili yenu. Endelee-ni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”Alifanya vivyo hivyo kuhusiana na kiko-mbe na kusema: “Kikombe hiki kinamaa-nisha agano jipya kwa msingi wa damu ya-ngu.”—Luka 22:19, 20.

Yesu alikuwa na mengi ya kuwaambiamitume wake usiku huo. Aliwapa amrimpya—kwamba wapendane bila ubinafsi.Aliwaambia: “Kwa jambo hili wote wata-jua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu,mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.”(Yohana 13:34, 35) Aliwahimiza wasiru-husu mioyo yao itaabike kwa sababu yamambo yenye kuhuzunisha yaliyokuwakaribu kutokea. Yesu alisali sana kwa ajiliyao. Wakaimba nyimbo za sifa na kuo-ndoka.

Wakiwa katika bustani ya Gethsemane,Yesu akapiga magoti na kumimina moyowake katika sala. Punde si punde askari-jeshi wenye silaha, makuhani, nawatu we-ngine wakaja kumkamata. Yuda akakari-

bia na kumtambulisha Yesu kwao kwakumbusu. Askari-jeshi hao walipomkama-ta Yesu, mitume wakatoroka.

Yesu akiwa mbele ya mahakama kuu yaWayahudi, alijitambulisha kuwa Mwanawa Mungu. Mahakama hiyo ilimhukumukuwa na hatia ya kukufuru na anastahilikifo. Baada ya hapo Yesu akapelekwa kwaGavana Mroma, Pontio Pilato. Ingawa ha-kumpata Yesu kuwa na hatia, alimkabidhiYesu kwa umati uliotaka auawe.

Kisha Yesu akapelekwa Golgotha,ambapo askari-jeshi Waroma walimtundi-ka mtini. Kimuujiza, giza likaingia katika-ti ya mchana. Baadaye, alasiri hiyohiyo,Yesu akafa na kukawa na tetemeko ku-bwa la nchi. Mwili wake ukalazwa kati-ka kaburi lililokuwa limechongwa katikamwamba. Siku iliyofuata, makuhani wa-kalifunika kaburi na kuweka mlinzi kati-ka mwingilio wake. Je, Yesu angeendeleakuwa kaburini? Hapana. Muujiza mku-bwa kuliko yote ulikuwa karibu kutokea.—Mathayo, sura ya 26 na 27; Marko sura, ya 14na 15; Luka, sura ya 22 na 23; Yohana, sura ya 12hadi 19.��������������

˛ Yesu alianzisha maadhimisho gani mapya?˛ Ni mambo gani yaliyotokea kabla ya kifo chaYesu?

20 Yesu Kristo AuawaYesu aanzisha maadhimisho mapya;asalitiwa na kutundikwa mtini

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieliHoseaYoeli

AmosiObadia

YonaMika

NahumuHabakukiSefaniaHagai

ZekariaMalaki

Mathayo ˘

Marko ˘

Luka ˘

Yohana ˘

MatendoWaroma

1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefeso

Kifo cha Yesu kilikuwa muhimu katika kutimizwa kwa kusudila Yehova. Kwa sababu mama ya Yesu alichukua mimba kupitiaroho takatifu ya Mungu, Yesu alizaliwa akiwa mkamilifu na kwahiyo angeweza kuishi milele pasipo kufa. Hata hivyo, aliutoauhai wake ili wanadamu wapate nafasi ya kuishi milele na kufu-rahia uhai ambao ulipotezwa na Adamu mwasi.�—Mathayo20:28; Luka 1:34, 35; Yohana 3:16, 36; 2 Petro 3:13.

� Unaweza kupata habari zaidi kuhusu thamani ya kifo chaYesu katika ukurasa wa 47-56 katika kitabu Biblia Inafundisha NiniHasa?

DARAKA MUHIMU LA YESU

Page 24: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Nisani 30,33W.K.

Sivani 6, 33 Pentekoste; roho takatifuyamiminwa (Sehemu ya mwezi wa 5 nasehemu ya mwezi wa 6 katika kalenda ya leo)

36 Kornelioawa Mkristo

SIKU ya tatu baada ya kifo cha Yesu, wa-nawake fulani waliokuwa wanafunzi

wake waligundua kwamba jiwe lililokuwakwenye mwingilio wa kaburi limeondole-wa. Isitoshe, kaburi lilikuwa tupu!

Malaika wawili wakatokea. Mmoja waoakasema: “Mnamtafuta Yesu Mnazareti.. . . Alifufuliwa.” (Marko 16:6) Bila kuka-wia, wanawake hao wakakimbia kwendakuwaambia mitume. Wakiwa njiani, waka-kutana na Yesu. Akawaambia: “Msiogope!Nendeni, mkawajulishe ndugu zangu, iliwapate kwenda zao Galilaya; na huko wa-taniona.”—Mathayo 28:10.

Baadaye siku hiyo, wanafunzi wawili wa-likuwa wakitembea kutoka Yerusalemukuelekea kijiji cha Emau. Mtu wasiyemjuaalijiunga nao na kuwauliza wanazungu-mzia nini. Mtu huyo alikuwa Yesu aliyefu-fuliwa, aliyewatokea katika umbo amba-lo hawakutambua mwanzoni. Wakiwana nyuso zenye huzuni wakamjibu kwa-mba wanaongea kuhusu Yesu. Kisha mtuhuyo akaanza kuwaeleza mambo kuhusuMasihi katika Maandiko yote. Kwa kweli,Yesu alikuwa ametimiza mambo yote ya-liyotabiriwa kuhusu Masihi.� Wanafunzihao walipotambua kwamba ni Yesualiyefufuliwa akiwa na mwili wa roho, aka-toweka.

� Unabii mbalimbali wa Kimasihi ambao Yesualitimiza unazungumziwa katika broshua hii uku-rasa wa 17-19 na pia katika kitabu Biblia Inafundi-sha Nini Hasa? ukurasa wa 199-201.

Wanafunzi hao wawili wakarudi Yerusa-lemu mara moja. Wakawakuta mitumewamekusanyika katika chumba kilicho-kuwa kimefungwa. Walipokuwa wakisi-mulia mambo waliyokuwa wamejionea,Yesu akatokea. Wafuasi wake walioduwaahawakuamini macho yao! Yesu akawauli-za: “Kwa nini shaka zinatokea mioyonimwenu?” Kisha akawaambia: “Imeandi-kwa kwamba Kristo angeteseka na kufufu-liwa kutoka kati ya wafu siku ya tatu.”—Luka 24:38, 46.

Kwa siku 40 baada ya kufufuliwa, Yesualiwatokea wanafunzi wake katika pinditofauti-tofauti. Katika pindi moja, aliwato-kea wanafunzi zaidi ya 500! Pengine katikapindi hiyo ndiyo alipowapa mgawo huumzito: “Nendeni mkafanye wanafunzi ku-toka kwa watu wa mataifa yote, . . . na ku-wafundisha kushika mambo yote ambayonimewaamuru ninyi. Na, tazama! miminipo pamoja nanyi siku zote mpaka uma-lizio wa mfumo wa mambo.”—Mathayo28:19, 20.

Alipokutana kwa mara ya mwisho pa-moja na mitume wake 11 waliokuwa waa-minifu, Yesu aliwaahidi: “Mtapokea nguvuwakati roho takatifu itakapofika juu yenu,nanyi mtakuwa mashahidi wangu . . .mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”(Matendo 1:8) Kisha Yesu akapanda juu namawingu yakamfunika.—Mathayo, sura ya 28; Marko, sura ya 16; Luka, suraya 24; Yohana, sura ya 20 na 21; 1 Wakorintho15:5, 6.��������������

˛ Wanafunzi wa Yesu walijua jinsi gani kwambaMungu amemfufua?˛ Yesu aliwaambia nini wanafunzi wawili walioku-wa wakielekea Emau?˛ Yesu aliwapa wanafunzi wake maagizo gani kablaya kupanda mbinguni?

21 Yesu Yuko Hai!Yesu awatokea wafuasi wake ili kuwapamaagizo na kuwatia moyo

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalaki

˘ Mathayo˘ Marko˘ Luka˘ YohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo

Roho takatifu ya Mungu ndiyo kani yenye nguvu zaidiiliyopo. Yehova Mungu alitumia roho yake, au nguvu zautendaji, kuumba mbingu na dunia na kuongoza uandi-kaji wa Biblia. Roho hiyo ilitumiwa kufanya miujiza yoteambayo tumezungumzia kufikia sasa, kutia ndani muujizamkuu zaidi, yaani, kufufuliwa kwa Yesu Kristo akiwa kiu-mbe wa roho mwenye nguvu.—Mwanzo 1:2; 2 Samweli23:2; Matendo 10:38; 1 Petro 3:18.

ROHO TAKATIFU

Page 25: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

mnamo 47-48Safari ya kwanza yaPaulo ya kuhubiri

mnamo 49-52Safari ya pili ya Pauloya kuhubiri

mnamo 52-56Safari ya tatu ya Pauloya kuhubiri

60W.K.

25

SIKU kumi baada ya Yesu kurudi mbi-nguni, wanafunzi wake 120 hivi wa-

likusanyika katika nyumba fulani jijiniYerusalemu wakati wa Sikukuu ya Kiya-hudi ya Pentekoste, mwaka wa 33 W.K.Ghafula, katika nyumba hiyo kukawa nakelele kama ile ya upepo wenye nguvuunaovuma. Wanafunzi wakaanza kuzu-ngumza lugha ambazo hawakuwa wanazi-jua. Iliwezekanaje? Mungu alikuwa ame-wapa wanafunzi roho takatifu.

Nje, kulikuwa na umati kwa sababuwatu walikuwa wametoka sehemu mbali-mbali ili kusherehekea sikukuu hiyo. Wa-lishangaa kuwasikia wanafunzi wa Yesuwakizungumza kwa ufasaha lugha zaowenyewe. Akieleza yaliyotokea, Petro ali-rejelea unabii wa Yoeli kwamba Mungu‘angemimina’ roho yake, ambayo ingewa-wezesha wenye kuipokea kufanya miujiza.(Yoeli 2:28, 29) Uthibitisho huo wenyenguvu wa roho takatifu ulionyesha wazikwamba badiliko kubwa limetokea: Mu-ngu ameacha kushughulika na taifa laIsraeli na kuanza kushughulika na kutani-ko jipya la Kikristo lililokuwa limeanzi-shwa. Sasa, wote waliotaka kumtumikiaMungu walipaswa kuwa wafuasi wa Kristo.

Wakati huohuo upinzani uliongezeka,nao adui wakawatupa wanafunzi gerezani.Hata hivyo, wakati wa usiku, malaika waYehova alifungua milango ya gereza nakuwaambia wanafunzi waendelee kuhu-biri. Ilipofika asubuhi wakaendelea kuhu-biri. Wakaingia hekaluni na kuanza ku-fundisha habari njema kumhusu Yesu.Wapinzani wao wa kidini walikuwa na ha-sira nao wakawaagiza waache kuhubiri.Mitume wakajibu kwa ujasiri: “Lazima tu-mtii Mungu kuwa mtawala kuliko wana-damu.”—Matendo 5:28, 29.

Mateso yakaongezeka. Wayahudi fulaniwalimshtaki mwanafunzi Stefano wakidaikwamba amekufuru, nao wakamuua kwakumpiga kwa mawe. Kijana, anayeitwa Sauliwa Tarso, alikuwa akitazama na kukubalianana mauaji hayo. Kisha akaenda Damaskokumkamata mfuasi yeyote wa Kristo. Sauliakiwa njiani, nuru kutoka mbinguni ilimu-lika kumzunguka na akasikia sauti: “Sauli,Sauli, kwa nini unanitesa?”Akiwa amepofu-shwa na nuru hiyo, Sauli akauliza: “Wewe ninani?” Sauti hiyo ikasema: “Mimi ni Yesu.”—Matendo 9:3-5.

Siku tatu baadaye, Yesu alimtuma mwa-nafunzi anayeitwa Anania ili kumponyaSauli. Sauli akabatizwa na kuanza kuhubirikwa ujasiri kumhusu Yesu. Baadaye, Sauliakaitwa mtume Paulo naye akawa Mkristomwenye bidii wa kutaniko la Kikristo.

Wanafunzi wa Yesu walikuwa wakiwata-ngazia habari njema za Ufalme wa Mu-ngu Wayahudi na Wasamaria pekee. Sasamalaika amtokea Kornelio, ofisa-jeshi Mro-ma, anayemwogopa Mungu na kumwa-mbia awatume watu wakamwite mtumePetro. Akiwa pamoja na wengine, Petro aka-mhubiria Kornelio na watu wa nyumba-ni mwake. Petro alipokuwa akizungumza,rohotakatifu ikaja juu ya waamini hao kuto-ka kwa Mataifa, naye akaagizawabatizwe ka-tika jina la Yesu. Tangu wakati huo na kue-ndelea, watu wa mataifa yote wangewezakupata uzima wa milele. Kutaniko lilikuwatayari kuhubiri habari njema kwa mapanana marefu.—Matendo 1:1–11:21.��������������

˛ Ni mambo gani yaliyotokea wakati wa Sikukuu yaPentekoste?˛ Adui waliwachukulia hatua gani wanafunzi waYesu kwa sababu ya kazi yao ya kuhubiri?˛ Watu wa mataifa yote walipata jinsi gani nafasi yakupata uzima wa milele?

22 Mitume Wahubiri kwa UjasiriKutaniko la Kikristo laongezeka licha ya mateso

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieliHoseaYoeli

AmosiObadia

YonaMika

NahumuHabakukiSefaniaHagai

ZekariaMalaki

MathayoMarkoLuka

YohanaMatendo ˘

Waroma1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefesoWafilipi

Wakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike

1 Timotheo2 Timotheo

TitoFilemoni

WaebraniaYakobo1Petro2Petro

1Yohana2Yohana3Yohana

YudaUfunuo

Page 26: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

60W.K.

BAADA ya kuwa Mkristo, Paulo alitanga-za kwa bidii habari njema kuhusu Ufal-

me wa Mungu. Mtu huyo aliyekuwa mpi-nzani alikumbana na upinzani mkali maranyingi. Mtume huyo mwenye bidii alisafirisehemu mbalimbali akihubiri habari njemaya Ufalme ambao utatimiza kusudi la awalila Mungu kwa wanadamu.

Katika safari yake ya kwanza ya kuhubirihuko Listra, Paulo alimponya mwanamumealiyekuwa kilema tangu kuzaliwa. Umatiulianza kupaaza sauti kwamba Paulo na Bar-naba, msafiri mwenzake ni miungu. Wa-naume hao wawili walijaribu sana kuwazuiawatu wasiwatolee dhabihu. Hata hivyo, baa-daye umati huohuo ulichochewa na aduiza Paulo, ukampiga kwa mawe na kumwa-cha akiwa mahututi. Paulo hakufa na baada-ye alirudi katika jiji hilohilo kuwaimarishawanafunzi kwa maneno ya kutia moyo.

Wakristo fulani Wayahudi walidai kwa-mba waamini wasio Wayahudi wanapa-swa kutimiza matakwa fulani ya Sheria yaMusa. Paulo alikwenda Yerusalemu kwa mi-tume na wanaume wazee ili kuwasilisha ta-tizo hilo. Baada ya kuyachunguza Maandikokwa makini na kwa mwongozo wa roho ta-katifu ya Mungu, wanaume hao waliyaa-ndikia makutaniko na kuyashauri yajiepu-she na ibada ya sanamu, kula damu nanyama zenye damu, na kuepuka uasherati.Amri hizo zilikuwa za “lazima,” hata hivyo,haikumaanisha kwamba walipaswa kufuataSheria ya Musa.—Mdo. 15:28, 29.

Katika safari yake ya pili ya kuhubiri, Pau-lo alienda Beroya, eneo ambalo leo liko Ugi-riki. Wayahudi waliokuwa wakiishi hukowalilipokea neno kwa hamu, wakiyachu-nguza Maandiko kila siku ili kuyathibitishamafundisho yake. Kwa mara nyingine tena,upinzani ukamfanya aondoke na kwendaAthene. Akiwa mbele ya Waathene wenyeelimu, Paulo alitoa hotuba yenye kuchocheakwelikweli. Leo tunaweza kumwiga Paulokwa kusema kwa busara, utambuzi, na ufa-saha tunapohubiri.

Baada ya safari yake ya tatu ya kuhubiri,Paulo alienda Yerusalemu. Alipoenda heka-luni, Wayahudi fulani walizusha ghasia, wa-kitaka kumuua. Askari-jeshi Waroma wakai-ngilia kati na kumhoji Paulo. Kwa kuwaalikuwa raia wa Roma, baadaye alijiteteambele ya Feliksi, gavana Mroma. Wayahudihawakuwa na uthibitisho wowote kuhusumashtaka yao dhidi ya Paulo. Ili kumzuia Fe-sto, aliyekuwa pia gavana Mroma, asimtiemikononi mwa Wayahudi, Paulo alisema:“Ninakata rufani kwa Kaisari!” Festo akaji-bu: “Utaenda kwa Kaisari.”—Mdo. 25:11, 12

Kisha Paulo akasafirishwa kwa meli hadiItalia ili akahukumiwe. Baada ya meli yaokuvunjika, alilazimika kukaa katika kisi-wa cha Malta wakati wa majira ya baridikali. Mwishowe alipofika Roma, alikaa kati-ka nyumba ya kukodi kwa miaka miwi-li. Hata ingawa alikuwa akilindwa na aska-ri, mtume huyo mwenye bidii aliendeleakuwahubiria wote waliomtembelea kuhusuUfalme wa Mungu.—Matendo 11:22–28:31.��������������

˛ Ni nini kilichotokea baada ya Paulo kumponyamtu aliyekuwa kilema jijini Listra?˛ Swali kuhusu kufuata Sheria ya Musa lilitatuli-waje?˛ Paulo alifika Roma jinsi gani, naye alifanya ninihuko?

23 Habari Njema YaeneaPaulo asafiri nchi kavu na baharini akihubiri

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa SulemaniIsayaYeremiaMaombolezoEzekieliDanieliHoseaYoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohana

˘ MatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo2 Timotheo

Page 27: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Paulo aandika barua akiwa gerezani Roma 61W.K.

27

KUTANIKO changa laKikristo lilikuwa na

kazi kubwa mbele yake. Li-ngetimiza sehemu muhi-mu katika kusudi la Yeho-va. Hata hivyo, baada yamuda usio mrefu Wakristohao wa karne ya kwanzawalishambuliwa. Je, wa-ngedumisha utimilifu waokwa Mungu wajapokabilimateso na hali nyingine ze-nye kuhatarisha uaminifuwao kutoka nje na ndani yakutaniko? Maandiko ya Ki-giriki ya Kikristo yana ba-rua 21 zenye kutia moyo nazenye shauri lililohitajiwa.

Barua 14, Waroma mpaka Waebrania,ziliandikwa na mtume Paulo. Barua hizozina majina ya wale walioandikiwa—iweni mtu binafsi au kutaniko fulani. Fikiriabaadhi ya mambo ambayo Paulo anazu-ngumzia katika barua zake.

Mashauri kuhusu maadili na mwe-nendo. Waasherati, wazinzi, na wanaote-nda dhambi nyingine nzito “hawataurithiufalme wa Mungu.” (Wagalatia 5:19-21;1 Wakorintho 6:9-11) Waabudu wa Mu-ngu kutoka mataifa yote wanapaswa kuwana umoja. (Waroma 2:11; Waefeso 4:1-6)Wanapaswa kuwasaidia kwa hiari waami-ni wenzao walio na uhitaji. (2 Wakorintho9:7) Paulo anasema: “Salini bila kuacha.”Kwa kweli, waabudu wanatiwa moyo ku-mmiminia Yehova mioyo yao katika sala.(1 Wathesalonike 5:17; 2 Wathesalonike3:1; Wafilipi 4:6, 7) Ili sala zinazotolewazisikiwe na Mungu, lazima zitolewe kwaimani.—Waebrania 11:6.

Ni nini kinachoweza kusaidia familiaziwe na furaha? Waume wanapaswa ku-wapenda wake zao kama miili yao we-nyewe. Wake wanapaswa kuwaheshimusana waume zao. Watoto wanapaswa ku-watii wazazi wao, kwa kuwa hilo linampe-ndeza Mungu. Wazazi wanapaswa kuwao-ngoza na kuwafundisha watoto wao kwaupendo, wakitumia kanuni za Mungu.—Waefeso 5:22–6:4; Wakolosai 3:18-21.

Wakristo wasaidiwa kuelewa kusu-di la Mungu. Sheria ya Musa ilikusudiwahasa kuwalinda na kuwaongoza Waisraelimpaka wakati ambapo Kristo angefika.(Wagalatia 3:24) Hata hivyo, Wakristo ha-wahitaji kushika Sheria hiyo ili ibada yaokwa Mungu ikubaliwe. Alipokuwa akiwaa-ndikia Waebrania, Wakristo waliokuwa naasili ya Kiyahudi, Paulo alieleza maana yaSheria na jinsi kusudi la Mungu linavyoti-mizwa katika Kristo. Paulo alieleza kwa-mba sehemu mbalimbali za Sheria hiyo

24 Paulo Ayaandikia MakutanikoBarua za Paulo zaliimarisha kutaniko la Kikristo

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

SefaniaHagai

ZekariaMalaki

MathayoMarkoLuka

YohanaMatendoWaroma ˘

1Wakorintho ˘

2Wakorintho ˘

Wagalatia ˘

Waefeso ˘

Wafilipi ˘

Wakolosai ˘

1Wathesalonike ˘

2Wathesalonike ˘

1Timotheo ˘

2Timotheo ˘

Tito ˘

Filemoni ˘

Waebrania ˘

Yakobo1Petro2Petro

1Yohana2Yohana3Yohana

YudaUfunuo

Barua Zilizoandikwa na PauloMnamoMwakawa 50-65W.K.

ROMAWaefesoWakolosaiFilemoniWafilipiWaebrania2 Timotheo

MAKEDONIA2 Wakorintho1 Timotheo

Tito (?)

KORINTHO1 Wathesalonike2 WathesalonikeWaroma

EFESO1 Wakorintho

ANTIOKIAWagalatia (?)

ITALIA

UGIRIKI GALATIA

MISRI

Filipi

Thesalonike

Kolosai

Yerusalemu

Sisili

Krete KiproB A H A R I Y A M E D I T E R A N I A

Mahali ambapo Paulo aliandikia barua zake(?) Hakuna uhakika kuhusu mahali alipoandikia

Page 28: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

61W.K. kabla ya 62 Yakobo, ndugu wa kambo wa Yesu, aandika barua yake

28

zilikuwa za kinabii. Kwa mfano, dhabihuya Yesu ilikusudiwa kuleta msamaha wadhambi, nayo iliwakilishwa na dhabihu zawanyama. (Waebrania 10:1-4) Kupitia kifocha Yesu, Mungu alifuta agano la Sheria,kwa kuwa halikuwa na kazi tena.—Wako-losai 2:13-17; Waebrania 8:13.

Maagizo kuhusu utaratibu wa ku-taniko. Wanaume wanaotaka kufikia ma-pendeleo kutanikoni wanapaswa kuwa namwenendo mzuri na kutimiza sifa za kiro-ho. (1 Timotheo 3:1-10, 12, 13; Tito 1:5-9)Waabudu wa Yehova Mungu wanapaswakukusanyika kwa ukawaida pamoja nawaamini wenzao ili kutiana moyo. (Wae-brania 10:24, 25) Mikutano ya ibada ina-paswa kuwa yenye kujenga na kuelimisha.—1 Wakorintho 14:26, 31.

Kufikia wakati ambapoalimwandikia Timotheo ba-rua ya pili, Paulo alikuwaamerudi Roma; alikuwa ge-rezani akisubiri hukumu.Ni watu wachache tu walio-jasiria kumtembelea. Pauloalijua kwamba ana wakatimfupi. Alisema: “Nimepi-

gana pigano zuri, nimekimbia mwendompaka mwisho, nimeishika imani.” (2 Ti-motheo 4:7) Yaelekea kwamba mudamfupi baadaye, Paulo aliuawa kwa sa-babu ya imani yake. Hata hivyo, baruaza mtume huyo zina mwongozo ambaowaabudu wa kweli wa Mungu wanafuatampaka leo.—Waroma; 1 Wakorintho; 2 Wakorintho; Wagala-tia; Waefeso; Wafilipi; Wakolosai; 1 Wathesalonike;2 Wathesalonike; 1 Timotheo; 2 Timotheo; Tito; Fi-lemoni; Waebrania.��������������

˛ Barua za Paulo zina mashauri gani kuhusu maa-dili na mwenendo?˛ Ni habari gani ambazo Paulo alitoa kuhusu kuti-mizwa kwa kusudi la Mungu kupitia Kristo?˛ Paulo alitoa maagizo gani kuhusu utaratibu wakutaniko?

YoeliAmosiObadiaYonaMikaNahumuHabakukiSefaniaHagaiZekariaMalakiMathayoMarkoLukaYohanaMatendo

˘ Waroma˘ 1Wakorintho˘ 2Wakorintho˘ Wagalatia˘ Waefeso˘ Wafilipi˘ Wakolosai˘ 1Wathesalonike˘ 2Wathesalonike˘ 1Timotheo˘ 2Timotheo˘ Tito˘ Filemoni˘ WaebraniaYakobo1Petro2Petro1Yohana2Yohana3YohanaYudaUfunuo

Baada ya Adamu na Hawa kutenda dhambi,Mungu alitumia lugha ya mfano alipomwambianyoka: “Nitaweka uadui kati yako na yulemwanamke na kati ya uzao wako na uzao wake.Yeye atakuponda kichwa nawe utamtia jerahakwenye kisigino.” (Mwanzo 3:15) Maandiko ya-namtambulisha Ibilisi kuwa “nyoka wa zamani.”(Ufunuo 12:9) Mkombozi au Uzao ulioahidiwa naMungu ulikuwa siri kwa karne nyingi, nao ume-kuwa ukifunuliwa hatua kwa hatua katika Biblia.

Miaka 2,000 hivi baada ya Adamu na Hawakutenda dhambi, Yehova alisema kwamba Uzaoulioahidiwa ungekuja kupitia ukoo wa Abrahamu.(Mwanzo 22:17, 18) Karne nyingi baadaye, Pauloalifunua kwamba Masihi, Yesu Kristo, ndiye sehe-mu ya msingi ya Uzao huo. (Wagalatia 3:16)Kulingana na Mwanzo 3:15, Yesu alipouawa, ni

kana kwamba alitiwa jeraha “kwenye kisigino.”Hata hivyo, Mungu alimfufua Yesu na ‘kumfanyahai katika roho.’—1 Petro 3:18.

Pia, Mungu alikusudia kwamba watu 144,000wawe sehemu ya pili ya uzao huo. (Wagalatia3:29; Ufunuo 14:1) Wanafufuliwa wakiwa namwili wa roho na kuwa warithi pamoja na Kristokatika Ufalme wa mbinguni.—Waroma 8:16, 17.

Akiwa Mfalme mwenye nguvu mbinguni, kari-buni Yesu atamwangamiza Ibilisi na uzao wake,yaani, wanadamu waovu na roho waovu wanao-mfuata Shetani. (Yohana 8:44; Waefeso 6:12)Chini ya utawala wa Yesu, wanadamu wote watii-fu wataishi kwa amani na furaha. Hata hivyo,mwishowe atamponda nyoka “kichwa,” na ku-mwangamiza kabisa asiwepo tena.—Waebrania2:14.

NI NANI ALIYE UZAO ULIOAHIDIWA?

Page 29: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

66Wayahudi waasi dhidi ya Roma Waroma waharibu Yerusalemu pamoja na hekalu lake 70 71W.K.

29

YAKOBO na Yuda walikuwa ndugu wa ka-mbo wa Yesu. Petro na Yohana waliku-

wa mitume wa Yesu. Wanaume hao wannewaliandika jumla ya barua saba katika Maa-ndiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kila moja ya ba-rua hizo ina jina la mwandikaji. Mashauriyaliyoongozwa na roho yaliyo katika baruahizo yalikusudiwa kuwasaidia Wakristo ku-dumisha utimilifu kwa Yehova na kuende-lea kuutazamia Ufalme wake.

Wakristo wanapaswa kuwa na ima-ni. Haitoshi tu kudai kwamba mtu ana ima-ni. Imani ya kweli huambatana na matendo.Yakobo aliandika: “Imani bila matendo ime-kufa.” (Yakobo 2:26) Mtu anapotenda kwaimani akiwa katika majaribu, anasitawishasifa ya uvumilivu. Ili kufanikiwa, Mkristoanahitaji kumwomba Mungu ampe heki-ma, akiwa na imani kwamba Mungu ata-mpa. Uvumilivu humfanya mtu akubaliwena Mungu. (Yakobo 1:2-6, 12) Mwabudu waMungu akidumisha utimilifu kwa imani, Ye-hova Mungu atajibu sala yake. Yakobo ase-ma: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribianinyi.”—Yakobo 4:8.

Mkristo anapaswa kuwa na imani yenyenguvu inayoweza kumsaidia kushinda vi-shawishi na kuepuka upotovu wa maadili.Kwa sababu ya upotovu wa maadili ulioku-wa umeenea, Yuda aliwahimiza waaminiwenzake ‘wafanye pigano kali kwa ajili yaimani.’—Yuda 3.

Dumisha mwenendo safi. Yehova hu-taka waabudu wake wawe watakatifu au safikatika kila njia. Petro aandika: “Ninyi we-nyewe pia iweni watakatifu katika mwene-ndo wenu wote, kwa sababu imeandikwa:‘Muwe watakatifu, kwa sababu mimi [Yeho-va] ni mtakatifu.’” (1 Petro 1:15, 16) Wa-kristo wamewekewa mfano wa kuiga. Petroasema: “Kristo aliteseka kwa ajili yenu, aki-waachia ninyi kielelezo ili mfuate hatua zake

kwa ukaribu.” (1 Petro 2:21) Ijapokuwa hue-nda Wakristo wakateseka kwa sababu wa-naishi kulingana na viwango vya Mungu,wanadumisha “dhamiri njema.” (1 Petro3:16, 17) Petro anawahimiza Wakristo wawena mwenendo na matendo matakatifu yaujitoaji-kimungu huku wakiingojea siku yahukumu ya Mungu na dunia mpya iliyoa-hidiwa ambamo “uadilifu utakaa.”—2 Petro3:11-13.

Wakristo wanapaswa kuwa na upe-ndo. Yohana aliandika: “Mungu ni upe-ndo.” Mtume huyo anasema kwambaMungu alionyesha upendowake mkuu kwa kumtumaYesu awe ‘dhabihu kwa ajiliya dhambi zetu.’ Kwa hiyobasi, Wakristo wanapaswakufanya nini? Yohana anaji-bu: “Wapendwa, ikiwa Mungu alitupendahivi, basi sisi wenyewe tuko chini ya waji-bu wa kupendana.” (1 Yohana 4:8-11) Njiamoja ya kuonyesha upendo kama huo nikwa kuwaonyesha ukarimu waamini wenze-tu.—3 Yohana 5-8.

Hata hivyo, waabudu wa Yehova wanawe-za kuonyesha jinsi gani kwamba wanampe-nda? Yohana anajibu: “Kumpenda Munguhumaanisha hivi, kwamba tuzishike amrizake; na bado amri zake si mzigo mzito.”(1 Yohana 5:3; 2 Yohana 6) Wale wanaomtiiMungu kwa njia hiyo wanahakikishiwa kwa-mba Mungu ataendelea kuwapenda huku‘wakitazamia uzima wa milele.’—Yuda 21.—Yakobo; 1 Petro; 2 Petro; 1 Yohana; 2 Yohana; 3 Yo-hana; Yuda.��������������

˛ Wakristo wanaweza kuonyesha imani kwa njiagani?˛ Mungu anataka waabudu wake wawe na mwene-ndo wa aina gani?˛ Mtu anaweza kuonyesha jinsi gani kwamba ana-mpenda Mungu kikweli?

25 Mashauri Kuhusu Imani,Mwenendo, na UpendoYakobo, Petro, Yohana, na Yuda, waandikabarua za kuwatia moyo waamini wenzao

“Mkaribieni Mungu,naye atawakaribianinyi.”—Yakobo 4:8

MwanzoKutoka

MamboyaWalawiHesabu

Kumbukumbu la ToratiYoshua

WaamuziRuthu

1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme

1MamboyaNyakati2MamboyaNyakati

EzraNehemia

EstaAyubuZaburiMethaliMhubiri

Wimbowa SulemaniIsaya

YeremiaMaombolezo

EzekieliDanieli

ZekariaMalaki

MathayoMarkoLuka

YohanaMatendoWaroma

1Wakorintho2Wakorintho

WagalatiaWaefesoWafilipi

Wakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike

1 Timotheo2 Timotheo

TitoFilemoni

WaebraniaYakobo ˘

1 Petro ˘

2 Petro ˘

1 Yohana ˘

2 Yohana ˘

3 Yohana ˘

Yuda ˘

Ufunuo

Page 30: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

71W.K.

Yohana aandika Ufunuomnamo 96

Kifo cha Yohana, mtume wa mwishomnamo 100W.K.

30

KITABU cha mwisho cha Biblia, Ufu-nuo, kinawapa wanadamu wote tu-

maini. Kitabu hicho kilichoandikwa namtume Yohana, kina maono mbalimbaliambayo upeo wake ni kutimizwa kwa kusu-di la Yehova.

Katika maono ya kwanza, Yesu aliyefufu-liwa anapongeza na kurekebisha makuta-niko kadhaa. Katika maono yanayofuata

tunaona kiti cha Ufalme cha Mungu,ambapo viumbe wa roho wanamsifu.

Huku kusudi la Mungu likizidi kuti-mizwa, Mwana-Kondoo, Yesu Kristo, apo-kea kitabu cha kukunjwa chenye mihu-ri saba. Anapofungua mihuri ya kwanzaminne, wapanda-farasi wa mfano wato-kea. Mpanda-farasi wa kwanza ni Yesuakiwa juu ya farasi mweupe naye amevi-shwa taji la kifalme. Kisha wapanda-farasijuu ya farasi wenye rangi mbalimbali, wa-naowakilisha vita, njaa, na tauni, mamboambayo yanatendeka katika siku za mwi-sho za mfumo huu wa mambo. Muhuri wasaba unapofunguliwa, tarumbeta saba zamfano zinapulizwa zikiashiria kutangazwakwa hukumu za Mungu. Kisha yafuata ma-pigo saba ya mfano, yanayowakilisha hasi-ra ya Mungu.

Ufalme wa Mungu, unaofananishwa na

mwana wa kiume aliyetoka kuzaliwa, wasi-mamishwa mbinguni. Vita vyatokea mbi-nguni, Shetani na malaika wake waovu wa-tupwa duniani. Sauti kubwa inasema: “Olewa dunia.” Ibilisi ana hasira kali, akijua anakipindi kifupi cha wakati.—Ufunuo 12:12.

Yohana amwona mwana-kondoo, Yesu,pamoja na wale 144,000 ambao wamecha-guliwa kati ya wanadamu, ‘watakaotawalawakiwa wafalme pamoja’ na Yesu. Hivyo,kitabu cha Ufunuo kinafunua kwamba se-hemu ya pili ya ule uzao inafanyizwa najumla ya watu 144,000.—Ufunuo 14:1; 20:6.

Watawala wa dunia wanakusanyika pa-moja kwa ajili ya Har–Magedoni, “vita vyaile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” Wana-pigana vita na yule anayeketi juu ya farasimweupe—Yesu, anayeyaongoza majeshi yambinguni. Watawala wote wa ulimwenguhuu wanaharibiwa. Shetani anafungwa,naye Yesu na wale 144,000 wanatawala juuya dunia kwa “miaka elfu.” Mwishoni mwaile miaka elfu, Shetani aharibiwa.—Ufunuo16:14; 20:4.

Utawala huo wa Kristo na watawala we-nzake utawatimizia nini wanadamu watii-fu? Yohana anaandika: “[Yehova] atafutakila chozi kutoka katika macho yao, nakifo hakitakuwapo tena, wala maombolezowala kilio wala maumivu hayatakuwapotena. Mambo ya zamani yamepitilia mba-li.” (Ufunuo 21:4) Kisha, dunia inakuwa pa-radiso!

Hivyo, kitabu cha Ufunuo kinakamilishaujumbe wa Biblia. Ufalme wa Kimasihi,utalitakasa jina la Yehova na kuitetea enziyake kuu milele!—Kitabu cha Ufunuo.��������������

˛ Wapanda-farasi wa mfano wanawakilisha nini?˛ Ni mambo gani ya ajabu yanayotokea huku kusu-di la Mungu likizidi kutimizwa?˛ Har–Magedoni ni nini, nayo itafanya nini?

26 Paradiso Yarudishwa!Kupitia Ufalme wa Kristo, Yehova alitakasa jina Lake,atetea enzi Yake kuu, na kuondolea mbali uovu

MwanzoKutokaMamboyaWalawiHesabuKumbukumbu la ToratiYoshuaWaamuziRuthu1 Samweli2 Samweli1Wafalme2Wafalme1MamboyaNyakati2MamboyaNyakatiEzraNehemiaEstaAyubuZaburiMethaliMhubiriWimbowa Sulemani

MathayoMarkoLukaYohanaMatendoWaroma1Wakorintho2WakorinthoWagalatiaWaefesoWafilipiWakolosai1Wathesalonike2Wathesalonike1 Timotheo2 TimotheoTitoFilemoniWaebraniaYakobo1Petro2Petro1Yohana2Yohana3YohanaYuda

˘ Ufunuo

Katika kitabu cha Ufunuo, dini zote za uwongo—yaani,dini zinazompinga Mungu wa kweli—kwa ujumla zina-tambulishwa kuwa “yule kahaba mkubwa.” Kahaba huyoanaitwa “Babiloni Mkubwa,” naye hufanya ukahaba naserikali za ulimwengu. Kitabu cha Ufunuo kinasema kwa-mba wakati uliowekwa na Yehova Mungu utakapofika,serikali hizo zitamshambulia kahaba huyo na kumharibu.—Ufunuo 17:1-5, 16, 17.

“BABILONI MKUBWA”

Page 31: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

Ujumbe wa BibliaM U H T A S A R I

1Yehova awaumba Adamu na Hawawakiwa na tumaini la kuishi milele katika

Paradiso. Shetani amchongea Mungu na ku-tilia shaka haki Yake ya kutawala. Adamu naHawa wajiunga na Shetani katika uasi,wajiletea dhambi na kifo waowenyewena wazaowao

2 Yehova awahukumuwaasi hao na kuahidi

Mkombozi, au Uzao,ambao utampondaShetani, na kubatilishamatokeo yote ya uasina dhambi

3 Yehova awaahidi Abrahamuna Daudi kwambawatakuwa

babu za Uzao, au Masihi, ambayeatatawala akiwaMfalme milele

4 Yehova awaongoza kwaroho manabii kutabiri

kwambaMasihi ataondoadhambi na kifo. Pamoja nawatawala wenzake, atatawalaakiwaMfalmewa UfalmewaMungu, ambao utamalizavita, magonjwa, hata kifo

5 Yehova amtumaMwanawakeduniani na kumtambulisha

kuwaMasihi. Yesu ahubiri kuhusuUfalmewaMungu na kutoa uhaiwake kuwa dhabihu. Kisha Yehovaamfufua akiwa kiumbewa roho

6 Yehova amtawaza Mwanawake kuwaMfalme mbinguni,

hatua hiyo ikitia alama mwanzowasiku za mwisho za mfumo huu wamambo. Yesu awaongoza wafuasi

wake duniani wanapohubiriUfalmewaMungu

duniani pote

7 Yehova amwagiza Mwanawake aanzekuitawala dunia. Ufalme huowazivunja-

vunja serikali zote mbovu, waleta Paradiso,na kuwasaidia wanadamu waaminifukufikia ukamilifu. Haki ya Yehova yakutawala yatetewa, na jina lakelatukuzwa milele

Page 32: Biblia - mickmimi.weebly.com · Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vi-tabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo. Bibliailitungwananani?Hiloniswaliambalolime-wasumbua

bm

-SW

17

04

21

BIBLIA

INAFUNDISHA

NINI Hasa?

Broshua hii inatoa muhtasari mfupi wenye kusisimua wa ujumbe uliokatika Biblia. Hata hivyo, kusudi lake si kueleza kirefu mambo ambayo Bibliainafundisha kuhusu kila jambo.

Kwa mfano, huenda ungependa kupata majibu ya Biblia kuhusu maswalikama haya: Je, kweli Mungu ananijali? Inakuwaje tunapokufa? Ninawezakupata furaha maishani jinsi gani?

Majibu ya maswali hayo na mengine yenye kusisimua yanawezakupatikana katika kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa naMashahidi wa Yehova. Kitabu hicho kimekusudiwa kuwasaidia watukujifunza Biblia hatua kwa hatua. Kujifunza kwa njia hiyo kunamsaidia mtukuunganisha mistari mbalimbali ya Biblia inayozungumzia habari fulanihususa.

UNGEPENDA KUJUA MENGI ZAIDI?

Unaweza kusoma au kuomba utembelewe au upakue chapisho hili kwenye tovuti yawww.jw.org/sw.

Au jaza ombi lililo hapa chini na utume kwenye anwani inayokufaa.Ili upate orodha kamili ya anwani zetu ulimwenguni pote, tazama www.jw.org/sw/mawasiliano.

� Tafadhali nitumie nakala ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?� Ningependa kujifunza Biblia bila malipo.

Lugha ������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������

Jina ����������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������

Anwani ���������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������

������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������

������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������

������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������������

Ili upate habari zaidi, tembelea Tovuti ya www.jw.org/sw,au wasiliana na Mashahidi wa Yehova.

s